Padri Kitima: Unafiki na kusifia kila jambo ili kupata vyeo kutaliua Taifa

Tuwache siasa za udini pembeni tuangalie uhalisia.

Naomba tumsikilize huyu mtumishi wa Mungu tuna cha kujifunza juu ya ustawi wa maisha yetu kama watanzania.
 
Naona masheh wameamua Rasmi kupambana na warumi!!!

Vuguvugu lilianza pale masheh walipoamua kuwaaachia masheh waliotuhumiwa kwa ugaidi!!

Juzi mmoja kasema wazi Kuwa mapadri zaidi ya hamsini wameuawa Lakini VYOMBO vya habari havitangazi!

Leo kuna kesi kadhaa za ulawiti!!


Samiah mama YANGU nakuonya !!!Acha kupambana na Hawa WATU!we Tulia coz waliyemuamini akapewa kutawala aliharibu Sana!wanamaumivu walipoteza utawala pale mtu wao alipo itwa na MUNGU!Wana uchungu Sana!!!


Wakiamua huwezi washinda can masheh BADO hawajatengeneza Taasisi imara ya kutawala Dunia kama wao!!

"Rasimu ya Warioba irudi mezani SASA iwe katiba mpya"
 
Chawa wataanza kumparua Padre sasa hivi bila kupima uzito wa ujumbe wake.
Alikuwa wap enzi za mwendazake akat masifio yalifika Hadi juu ya kitu Cha enzi
Et mh Mungu pumbavu mwambie kitima atulie
 
Huu ugonjwa wa uchawa wa viongozi aliotuletea magu unaliteketeza taifa.

Kabla yake ilikua serikali ya ccm, alipoingia ikawa ya magu sio ccm tena, sasa hivi imehamia mama samia sio ccm tena

Sent from my Infinix X624B using JamiiForums mobile app
 
Mwambie maoni yake ni mazuri Ila aanzie ndani kwake kwanza maana Mapadri wamekuwa wanalawiti watoto na wengine wanauwawa kiutata sana.
Nasema uongo ndugu zanguuuu
 
Wakati Azory Gwanda na Ben saanane wanatoweka mbona hawakusema haya?Magufuli alikuwa anafunga watu hovyohovyo anawapoteza,anawabambikizia watu kesi,anapora fedha za watu viongozi wetu wa dini walikuwa kimya!

Viongozi wetu wa dini mseme kila nyakati,hata zile nyakati za hatari.
Labda umemfahamu leo padre
 
Wakati Azory Gwanda na Ben saanane wanatoweka mbona hawakusema haya?Magufuli alikuwa anafunga watu hovyohovyo anawapoteza,anawabambikizia watu kesi,anapora fedha za watu viongozi wetu wa dini walikuwa kimya!

Viongozi wetu wa dini mseme kila nyakati,hata zile nyakati za hatari.
Rudi kwenye mada usichanganye mafaili kukwepa ukweli!!!
 
Rais Samia, kama anataka uongozi wake uwe na tija kubwa, ni lazima awaondoe wanafiki wote ndani ya Serikali yake.

Ndani ya Serikali wamejaa watu wanafiki. Watu watoa rushwa ya sifa. Sifa wanazozitoa kwa Rais kw kila kitu, hata zisipostahili, ni rushwa ya sifa kwa Rais.

Kiongozi yeyote ana haki ya kusifiwa anapofanya jambo jema la pekee, lakini kumsifia Rais kwa kila kitu, tena kwa baadhi ya mambo ambayo ni ya kawaida kabisa au hata kwa yale ambayo yamefanyika vibaya, ni unafiki, ujinga, uwendawazimu, na rushwa kwa kiongozi anayesifiwa, na njia ya kumpofusha mtawala.

Hongera sana Baba Kitima, kwa kuunena ukweli.
 
Padri yupo sahihi...lakini kwa nini hakutuyasikia haya kipindi cha JPM,ilifika hatua hadi anapewa mic kanisani ahutubie.....huku wakina Pengo wakimtaka Makonda awe raisi wa awamu ya Sita.
Ni kweli Padri Kitima yupo sahihi,"Unafiki wa kisiasa unaondelea miongoni mwa watanzania,utaliangamiza taifa"
nafikiri umeanza kumjua jana
 
Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), Padre Charles Kitima ametahadharisha unafiki wa kisiasa unaoendelea miongoni mwa Watanzania kwa sasa kwa kupenda kusifia kila jambo kuwa utaliua taifa.

Amesema tabia hiyo inaendelea kupata mashiko nchini kutokana na upeo mdogo wa watu kushindwa kujua misingi ya haki za binadamu na badala yake wanatanguliza maslahi yao binafsi mbele .

Akizungumza leo Dar es Salaam, Septemba 30, 2022 katika kongamano la viongozi wa dini zote linaloangazia haki za binadamu nchini, kiongozi huyo amesema tabia hiyo iliyojengeka isipokomeshwa ni wazi mahusiano mazuri miongoni mwa Watanzania yanaenda kupotea.

"Unafiki unaharibu nchi, unafiki wa kisiasa uliopo miongoni mwa Watanzania kupenda kusifia viongozi ili tu kujipendekeza wapate vyeo unaenda kuliua Taifa na tatizo hili linaendelea kwa sababu watu hawajui misingi ya haki za binadamu," amesema Padri Kitima

Kiongozi huyo wa kiroho amesema hata kujitoa kwenye mahakama ya haki iliyopo Arusha na kuwahamisha wananchi kutoka Loliondo kwenda Handeni mkoani Tanga ni uvunjivu wa haki za binadamu.

"Kwa sababu nchi imeridhia mikataba mbalimbali ya kimataifa inayohusu haki za binadamu," amesema

Amesema wao kama viongozi wa dini baada ya kuona tabia hiyo hususan miaka mitano iliyopita, mwaka 2020 walianza kuandika kitabu Cha elimu ya haki za binadamu kwa lengo la kuanza kutoka elimu watu wote.

"Haki za binadamu haziombwi, zinapiganiwa, dini ni kiungo muhimu na tumeona tufanye hivi na tunatarajia kuwafikia viongozi 16,000 nchi nzima na kushuka kwa Watanzania wote," amesema

Chanzo: Mwananchi
Ifike mahali sasa viongozi wawe wanatuma maombi ya kazi, interview ifanywe na wananchi hadharani na wapangiwe kazi na kusimamiwa na hata kufukuzwa na wananchi, hii teuanateuana inatuumiza sana
 
Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), Padre Charles Kitima ametahadharisha unafiki wa kisiasa unaoendelea miongoni mwa Watanzania kwa sasa kwa kupenda kusifia kila jambo kuwa utaliua taifa.

Amesema tabia hiyo inaendelea kupata mashiko nchini kutokana na upeo mdogo wa watu kushindwa kujua misingi ya haki za binadamu na badala yake wanatanguliza maslahi yao binafsi mbele .

Akizungumza leo Dar es Salaam, Septemba 30, 2022 katika kongamano la viongozi wa dini zote linaloangazia haki za binadamu nchini, kiongozi huyo amesema tabia hiyo iliyojengeka isipokomeshwa ni wazi mahusiano mazuri miongoni mwa Watanzania yanaenda kupotea.

"Unafiki unaharibu nchi, unafiki wa kisiasa uliopo miongoni mwa Watanzania kupenda kusifia viongozi ili tu kujipendekeza wapate vyeo unaenda kuliua Taifa na tatizo hili linaendelea kwa sababu watu hawajui misingi ya haki za binadamu," amesema Padri Kitima

Kiongozi huyo wa kiroho amesema hata kujitoa kwenye mahakama ya haki iliyopo Arusha na kuwahamisha wananchi kutoka Loliondo kwenda Handeni mkoani Tanga ni uvunjivu wa haki za binadamu.

"Kwa sababu nchi imeridhia mikataba mbalimbali ya kimataifa inayohusu haki za binadamu," amesema

Amesema wao kama viongozi wa dini baada ya kuona tabia hiyo hususan miaka mitano iliyopita, mwaka 2020 walianza kuandika kitabu Cha elimu ya haki za binadamu kwa lengo la kuanza kutoka elimu watu wote.

"Haki za binadamu haziombwi, zinapiganiwa, dini ni kiungo muhimu na tumeona tufanye hivi na tunatarajia kuwafikia viongozi 16,000 nchi nzima na kushuka kwa Watanzania wote," amesema

Chanzo: Mwananchi
Yeye na Kanisa lake pia ni Wanafiki. Wakati wa Mwendazake ambaye ndiye mwanzilishi wa hii tabia hawakudiliki kusema kitu. Sana sana walimsifia.

Kwenye hili siliungi mkono Kanisa.
 
Back
Top Bottom