Kuhusu majimbo hayo, ni mambo tu. Maombi yanakubaliwa na kukataliwa. Ungesubiri kuona maamuzi yangu nipo uweze kutoa maoni yako.
Kwamba sijawahi kuionya CCM kuishambulia CHADEMA nadhani ni propaganda tu. Maisha yangu yote napambana na CCM ndani na nje ya Bunge. Wao kunisifia ni divide and rule.
Mara ngapi viongozi wa CHADEMA wanasifiwa na mawaziri wa CCM? Hata humu JF imeandikwa mara kadhaa pale mawaziri wa ccm wanapowasifia baadhi ya wabunge wa CHADEMA. Ni kawaida hiyo kwenye siasa.
Mara nyingi sana nimetoa matamko makali kulaani uvunjifu wa amani nchini na ugandamizaji dhidi ya upinzani nchini. Mara kadhaa nimeadhibiwa na CCM nimesimishwa ubunge, kamati ya POAC ilivunjwa, niliswekwa ndani kwenye uchaguzi Kigoma Mjini nk.
Hatupimi umakini wa viongozi wa upinzani kwa kuwekwa ndani na polisi, kama ni hivyo leo DP ingekuwa chama kikubwa kuliko vyote nchini
Kama malengo yenu ni haya kwa nini msijiunge na UKAWA? Katibu mkuu wenu alisikika akisema chama chenu kitaisambaratisha CUF mikoa ya Pwani, huoni kama ulichoandika juu ni kujikosha tu? kwamba lengo lenu ni kupambana na upinzani
Hivi ulipotoa lile tamko la kulaani viongozi wa CDM walipopigwa mabomu na risasi pale soweto ulikuwa una shida gani Ulikuwa huna taarifa za kutosha,ulikuwa na hang over au?Je umewahi jutia hata in private?Kuhusu majimbo hayo, ni mambo tu. Maombi yanakubaliwa na kukataliwa. Ungesubiri kuona maamuzi yangu nipo uweze kutoa maoni yako. Kwamba sijawahi kuionya CCM kuishambulia CHADEMA nadhani ni propaganda tu. Maisha yangu yote napambana na CCM ndani na nje ya Bunge. Wao kunisifia ni divide and rule. Mara ngapi viongozi wa CHADEMA wanasifiwa na mawaziri wa CCM? Hata humu JF imeandikwa mara kadhaa pale mawaziri wa ccm wanapowasifia baadhi ya wabunge wa CHADEMA. Ni kawaida hiyo kwenye siasa. Mara nyingi sana nimetoa matamko makali kulaani uvunjifu wa amani nchini na ugandamizaji dhidi ya upinzani nchini. Mara kadhaa nimeadhibiwa na CCM nimesimishwa ubunge, kamati ya POAC ilivunjwa, niliswekwa ndani kwenye uchaguzi Kigoma Mjini nk. Hatupimi umakini wa viongozi wa upinzani kwa kuwekwa ndani na polisi, kama ni hivyo leo DP ingekuwa chama kikubwa kuliko vyote nchini
Haha..ndio nyie mnajibunia misemo waganga waliochepuka ndio wanaitisha viungo vya albino badala ya kukubali ukweli kuwa uganga ni uchawi na uchawi siku zote lazima kuwepo na uchawi ndio maana wapo watu wanakwenda kwa hao hao waganga kuponywa na haohao kuwadhuru wengine.Ukomunist na ujamaa ni km ndama na ng`ombe...sasa km unataka kusema ndama anaweza kuwa mwana simba.Utakuwa una shida sana.Mkajipange bhana.ujamaa hauna usasa.uchina wenyewe bado wanahangaika kuweza beba vyote wakati raia wanataka uhuru wa fikra zaidi.Ujamaa unajificha ktk ufanyiwa hujuma kuliko kufanya mambo yanayaowezekana na uhuru wa fikraUjamaa wa Nyerere ni ukomunisti na ujamaa wa ACT ni ujamaa wa kisasa ambao unaamini demokrasia
Naomba unijibu hili Zitto ACT kabla hujahamia wewe ilikwisha kuanzisha maofisi makubwa makubwa mikoa mingi ikiwamo Arusha mjini ofisi ambazo kwa hesabu ya kawaida kwa mfano ya pale Arusha mjini siyo chini ya Milioni moja kwa mwezi. Chama hiki kichanga chenye wanachama wachache kimetoa wapi fedha za kukodisha maofisi makubwa hivyo? Pia kabla hujahamia Chadema kule Kigoma ulitoa magari yako yakaanze kutumika kufanya kazi za ACT unataka kuniambia wewe ulikuwa moja ya wafadhili na waanzilishi wa ACT ukiwa bado ndani ya Chadema?
Ninachokiona hapa ni kuwa,tuna tatizo kubwa sana la kukosekana "flexibilty" miongoni mwa viongozi wa vyama vya upinzani kwa upande mmoja na sisi mashabiki wa vyama vya siasa kwa upande mwingine.Kukosekana huku kwa flexibility miongoni mwa wanasiasa wetu ndio kuliko changia umoja kama huu wa UKAWA tulionao leo hii kuchelewa kupatikana.
Hata hivyo,nawapongeza viongozi wa vyama vya upinzani waliogundua tatizo hili la flexibility na kuli-overcome kwa kukaa pamoja na kuanzisha UKAWA.
Hivyo basi,na sisi mashabiki na wapenzi wa vyama vya siasa tunapaswa ku-exercise flexibiliy,lakini kwa tahadhari kubwa,ili tuifikie ile nchi ya ahadi tunayoililia kila kukicha.
Japo wanasiasa hawaaminiki,flexibility katika kufikia maridhiano/makubaliano ni jambo la muhimu sana kwa mafanikio yoyote ya kisiasa ila tu maridhiano/makubaliano hayo yasiwe ya kukurupuka na yafanywe kwa tahadhari.
Tutoe nafasi kuwapima ACT kwani muda pekee ndio msemakweli then flexibility "inaweza" kuchukua nafasi yake.
Note:Kipimo cha muda pekee bila flexibilty ya pande zote ni bure.
Kwa hiyo unataka kusema kuwa ACT ilianzishwa na Zitto pale alipokoipeleka CHADEMA Mahakamani as a plan B incase akishindwa kesi ?