One Struggle, Many Fronts. Forward ever, Backward Never... Tumeamua kuangalia mbele!

One Struggle, Many Fronts. Forward ever, Backward Never... Tumeamua kuangalia mbele!

Zitto tangu uchaguzi mkuu wa 2010 uuishe kwa kweli alikuwa adimu sana katika mikutano ya chama, sijui hili atasemaje tangu m4c inaanza kwa kweli hakushiriki vya kutosha tena alipaswa kufanya kazi kubwa sana ya kukinadi chama kuliko hata Dr. Slaa, chama kilienda ;Lindi na Mtwara mapaka mauti yanamkuta mzee wa chadema yule wa shinyanga/mwanza zitto hakuwahi onekanaa huko kwa zaidi ya wiki 3, chama kikaenda morogoro mpaka muuza magazeti anauwa na polisi, zitto hayupo, chama kikaenda iringa mpaka mwangosi anauwa zitto hayupo, chama kikaenda arusha mpaka bomu linalipuka zitto hayupo hizo harakati zoote?? sasa utasema hizi zote ni coincidence kweli???

Lakini pia zikaja shutuma za yeye kuonekana kutumika na ccm na hata zikahususanishwa na kauli za wassira kuwa cdm itakuwa 2012, na kwa kweli tangu chama kimsimamishe zitto uanaachama 2013 mwishoni wassira hajasikika tena akisema ile kauli je hii nayo ni coincidence ya namana gani, zipo taarifa za kutumika 2010 kutoa siri za chama kwa ccm mpaka mwanaharisi likaanika na ushahidi wa mawasiliano ,kabla yake ilikuwa kila safari ya nje jk lazima mbebe zitto waende naye, asi if upinzania koote zito ndio kichwa, sasa sijui hata darasani alikuwa anapataga single digit au vipi...

...Kilichoudhi zaidi wakati wananchi wako busy kuidiscuss Elimu wanayopewa na M4C yeye ili kuwachanganya akaitisha waandishi wa habari na kuwatangazia "...nautaka uraisi kupitia CHADEMA" Bila shaka aliagizwa hivo na akina Wasira na Zoka ili kudivert attension ya raia kwenye elimu inayotolewa na M4C.
Swali: Lengo lako la kugombea urais bado lipo au ndo biashara na waliokutuma ilishakamilika?
 
Nadhani ule waraka wa chacha wangwe ndio jibu sahihi kwa swali lako, chadema siyo kama inakosa hela ya kupangisha ofisi ila asilimia kubwa ya pesa ya ruzuku inalipa madeni ya mtu mmoja anayekopesha bila hata Chama kuwekeana naye makubaliano ya riba then baadaye yeye ndio a najua sh ngap amekopesha na rib kiasi gani anatakiwa alipwe na Chama. Hvyo anza kuanza kuuliza chadema ndio uende kwa zito


Inachekesha sana, wengi humu wanamuuliza Zitto maswali waliyokuwa hawathubutu kuwauliza viongozi wao ndani ya CDM, na labda hadi sasa wanaogopa kufanya hivyo.

Mnauliza kuhusu mchanganuo wa mapato ya ACT, lakini sikuona mwana CDM aliyesapoti waraka uliokuwa unauliza maswali haya haya yaliyojaa humu ndani.

Waraka ulivyotoka wengi tuliwashauri CDM wa-calm down na ku-deal na mazuri ya waraka kiutu uzima na vijembe vya hapa na pale, na pale kina kitila walikoteleza wapotezee, lakini hot heads prevailed. Sasa ACT wanafanya walichoamini kwenye ule waraka imekuwa tatizo.

Imagine kama CDM wange-intergrate waraka kwenye siasa zake, na kuwaachia wapiga kelele nao waendelee, leo hii wangekuwa wanai-attack CCM on all fronts, kisera, na kwenye majukwaa pia.

Sasa hivi sehemu pekee CCM inatishwa na CDM ni kwenye majukwaa ya siasa, ambayo platform yake haipatikani kila siku, kwani huwezi kuitisha mkutano bila siku bila sababu,ndio maana sehemu pekee CDM inaweza kufight back against CCM ni wakati wa bunge, au kukitokea kashfa flani.

Waraka was CDM's biggest blunder, and missed opportunity, you could have punished Zitto and Team and bar him from party politics for a year or so, while internally digest waraka wao na kufanya nao kazi inakobidi.isingewapunguzia chochote.

Sasa inabidi mfanye kazi besides them, and i have yet to hear a CDM leader talk of "sera" for the past year or so.
 
mimi huwa nacheka sana...ati Ujamaa!? Nyerere alichemka na akatuletea umasikin ati leo zito mjamaa? wa wap kwanza wew.. mtu tajiri hivi ati mjamaa!!!!!! zito bwana anambwembwe sana
 
I think they are doing CDM a favor, i would not be surprised if a request came from CDM leaders, what their supporters are spewing in these threads about ACT is the worst i have seen CDM fall to.

They really need to get a grip and get back to CDM we used to know, the one that used to inspire millions of people in TZ to stand against CCM

Nakushauri uandike tu kwa Kiswahili mkuu.Unalazimishia kiingereza usichokijua.Sitakuwa nimekosea nikisema umeishia Form Four shule za Kata.

Samahani kama nimekuudhi..
 
Nakushauri uandike tu kwa Kiswahili mkuu.Unalazimishia kiingereza usichokijua.Sitakuwa nimekosea nikisema umeishia Form Four shule za Kata.

Samahani kama nimekuudhi..


Wala usijali, nimezoea kadhia ndogo ndogo kama hizi kutoka kwa pro CDM, hazijaanza leo. Kuhusu Elimu yangu hapa si mahala pake, ukitaka kufungua mada kuhusu elimu yangu fungua tukayaongee huko.
Now, let's get back to discussing issues at hand, enough about Kimweri.au vipi?
 
ACT Tanzania ndio ACT Wazalendo. Baada ya kufanya tafiti kwa wananchi ilionekana wananchi wanataka chama kitakachowarejeshea uzalendo kwa Taifa lao. Wananchi wengi walishauri iundwe Chama Cha Wazalendo. Hivyo tukaboresha jina letu kwa mujibu wa katiba yetu na kuitwa ACT Chama cha Wazalendo
Hili jibu ni jepesi sana, mlishauriwa muunde chama cha wazalendo au chama kinachoitwa wazalendo? Iwe chama au mtu huitaji kujiita mzalendo ni matendo yako yatakayopelekea watu wakuite mzalendo. Hebu onyesha ukomavu, mbona chama ulichofukuzwa ulisema hakuna demokrasia wakati hicho chama kinaitwa Chama cha Demokrasia na Maendeleo au waanzilishi wa chama hiki neno demokrasia hawakushauriwa na wananchi ndio maana hakunademokrasia kama mnavyodai?
 
Ndugu wana JF,

Kwa muda mrefu na hasa siku za hivi za karibuni kumekuwa na threads nyingi sana humu ndani kuhusu Zitto na kuhusu Chama cha ACT Wazalendo. Kumekuwa na tuhuma kwamba chama cha ACT Wazalendo kinashambulia vyama vingine vya upinzani hapa nchini. Napenda kusema mambo machache sana

Chama cha ACT Wazalendo ni chama cha siasa chenye mrengo wa kushoto na kinajitanabaisha na siasa ya Ujamaa iliyoasisiwa na Azimio la Arusha. Lengo letu ni kueneza siasa zetu zenye mrengo huo.

1. Chama cha ACT Wazalendo kwa sasa ni chama cha upinzani nchini. Kimekuja kuhuisha zaidi siasa za upinzani ili kuiondoa CCM madarakani. Chama cha ACT Wazalendo hakina lengo hata kidogo kuzorotesha upinzani nchini. Tofauti zetu tulizokuwa nazo katika chama tulichokuwamo wengine tumeshazifuta, tumepiga mstari na kutazama mbele.

Ndio maana hutasikia kiongozi hata mmoja wa ACT Wazalendo akihangaika na vyama vingine vya upinzani. Hata tukichokozwa namna gani tumefanya maamuzi kwamba hatutajibizana na chama kingine chochote cha upinzani hapa nchini. Tutapambana na chama tawala ili kubomoa mfumo wa uchumi unaonyonya wengi na kufaidisha wachache. Tutapigania uwajibikaji wa viongozi kwa wananchi. Tutapambana na ufisadi kwa nguvu zetu zote. Hizo ndizo kazi tulizo nazo.

2. Tunasisitiza, tunayo vita moja lakini una njia nyingi za kupigana dhidi ya adui. Huko tulipokuwa tulitofautiana mbinu hizo. Sasa tumepata jukwaa la kutumia mbinu hizo. Wenzetu watumie mbinu zao pia. Hatimaye kila mmoja alenge shabaha kwa adui mmoja. Tunasema One Struggle, Many Fronts

3. kuitana mamluki, wasaliti nk ni siasa za framing tu. Sio mara ya kwanza siasa hizi kutumika nchini katika kujaribu ku frame watu. Mwaka 1995 Mrema wa NCCR aliita CHADEMA chama cha mashushu kutoka Benki Kuu na kila mtu alimwamini. Leo Mrema yupo wapi na CHADEMA ipo wapi? Mwaka 2000 mpaka 2005 CUF ndio ilikuwa chama kikuu cha upinzani na kuidharau CHADEMA. Mwaka 2013 CHADEMA iliita CUF chama cha mashoga.

Miaka yote Mbatia amekuwa akiitwa pandikizi nk. Yote haya hayajazuia vyama hivi kufanya kazi pamoja hivi sasa. Ni vizuri sana wanasiasa kuweka akiba ya maneno. Hakuna sababu ya kutukanana na kuitana majina mabaya. Tunachohitaji ni kila mmoja kumlenga adui ili kumshinda. Tulishindwa kufanya kazi ndani ya moja, tunaweza kufanya kazi tukiwa majirani. Adui bado ni yule yule.

4. Sisi ACT Wazalendo tutachochea kuni kuwasha moto wa mapinduzi nchini kwa kuendesha siasa za masuala (issues). Tumeanza ziara yetu mkoa wa Ruvuma kwa sababu ni mkoa ambao wabunge wake wote ni CCM. Tutaweka nguvu sana maeneo hayo badala ya maeneo ambayo tayari vyama vingine vya upinzani vina nguvu. Sisi katika ACT wazalendo tunataka kuona uchumi unarudi kwa wananchi wenyewe badala ya uchumi kushikiliwa na watu wachache.


Tunataka kuona Miiko ya Uongozi inarudi ili kurejesha imani ya wananchi kwa viongozi wao. Tunataka kuona mfumo madhubuti wa uwajibikaji nchini. Hayo ndio mapambano yetu. Hayo ndio maelekezo yetu kwa wanachama wetu; Kupambana na adui mmoja tu - CCM.

Malengo ni mazuri nia ni mzuri lakini sina imani na njia munayotumia au munayotaka kutumia. Kupambana ukiwa jeshi la mtu mmoja ni ngumu lakini ukiunganisha nguvu na wapinzani wengine itakuwa njia mzuri zaidi. Binafsi naamini watanzania wengi wanataka mabadiliko na wamechoshwa na ccm lakini bado wanaichagua ccm kwakukosa imani na upinzani. Ushauri wangu ukiupenda chukua usipoupenda achananao """"Unganisha chama chako na ukawa ili kuongeza nguvu ya upinzani Tanzania"". Pia nikushauri usipende kujipa madaraka makubwa wewe bado mtoto kwenye siasa, naomba ufanye siasa madaraka yatakuja automatically. Ulichokifanya act kujipa madaraka makubwa ni utoto. Ulitakiwa uiongoze act ukiwa kama mwanachama wakawaida ili ukiongoze chama ukiwa mafichoni. Simaanishi nakulaumu huo ni mtazamo wangu. Kwasasa jambo jema kwako nikufanya muungano wa vyama ili tuiondoe ccm. Kubaki act ikifanya siasa kivyakevyake itatuaminisha kwamba wewe ni shushu wa ccm kitu ambacho binafsi sitaki kuamini. Kwasasa wewe ni kiongozi wa chama chako cha siasa hivyo ukipeleka wazo lakuungana na ukawa itakuwa safi sana ukizingatia mjadala wa wewe na cdm ulishafungwa, kwahiyo kwasasa unanafasi kubwa yakufanya kazi pamoja na cdm, cuf, nccr, na vyama vingine kila mmoja akitokea kwenye chama chake.

Ni ushauri tu Brother zitto.
 
mimi huwa nacheka sana...ati Ujamaa!? Nyerere alichemka na akatuletea umasikin ati leo zito mjamaa? wa wap kwanza wew.. mtu tajiri hivi ati mjamaa!!!!!! zito bwana anambwembwe sana
Kama sio kutafuta mass popularity ni wendawazimu karne hii kuongelea ujamaa, hasa ujamaa wa Tanzania ambao Dr, Mazrui aliuita "Nyerererism" kutokana na mfumo wake ambaa haukuwai tokea sehemu yeyote duniani.
 
Mie ninachofikiri zitto alileta thread hii ili ajue watu wanamuonaje kuhusu chama alichokianzisha kudhoofisha upinzani na madaraka aliyojitwalia.mie nimepitia comments za watu mbalimbali nikafanya tathmini na kugundua zaidi ya 90% hawakubaliani nawe hata kidogo hiyo 10% ni wale waganga njaa walio tayari kuikana kweli ili tu mkono uende kinywani. OMBA TO MH.ZZK UMEPOTOKA KWA KUSALITI HARAKATI ZA MAGEUZI KISA NJAA YA UMARUFU NA MADARAKA.
 
fikirikwanza

Siasa ni mapambano. Siwezi kuacha mapambano. Sijawahi fanya usaliti wowote. kuitana majina hayo hakusaidii lolote zaidi ya kufurahisha ego zetu tu. ACT Wazalendo ina shabaha moja tu nayo ni kupambana na mfumo wa uchumi unaonyonya watanzania. Ku surrender mapambano hayo ndio usaliti. Tutaendelea kupambana

Kamwe, Never hatuwezi kuiondoa ccm madarakani kwakuanzisha vyama kiholela. Tunahitaji kuunganisha nguvu za upinzani. Siasa sio kigodoro kwamba ukiweka taarabu mzuriiiii ndo utajaza watu kwenye unyago wako.
 
Last edited by a moderator:
zito unamawazo finyu ujafungua kujipambanunua kama kweli una dhamira ya dhati na hii nchi chama chako kingeweka kipaumbile kupambana na umaskini kupitia rasilimali na pato la taifa kama tunavyoomuona julius malema, wewe unajinasibu kupambanana na chadema siyo kiongozi wa kweli, kiongozi wa kweli atengenezi wafuasi anatengeneza viongozi km wewe mbowe alivyokutengeneza.
 
Ajitafakari! Kwa usaliti wake Kigoma bendera nyingi za ccm zinapepea. Huu ni uzaliti! Kwa kujua au kutojua anajaribu kuirudisha ccm madarakani (hasa jimboni/mkoani kwake)
 
Je hayo ya kweli!

Ndugu wana JF,

3. kuitana mamluki, wasaliti nk ni siasa za framing tu. Sio mara ya kwanza siasa hizi kutumika nchini katika kujaribu ku frame watu. Mwaka 1995 Mrema wa NCCR aliita CHADEMA chama cha mashushu kutoka Benki Kuu na kila mtu alimwamini. Leo Mrema yupo wapi na CHADEMA ipo wapi? Mwaka 2000 mpaka 2005 CUF ndio ilikuwa chama kikuu cha upinzani na kuidharau CHADEMA. Mwaka 2013 CHADEMA iliita CUF chama cha mashoga.


CC Kurugenzi ya Habari.
 
Last edited by a moderator:
Kaka Zitto Ukiwa Mwongo Usiwe Msahaulifu na Ukiwa Msahaulifu Usiwe Mwongo, Umekuwa Unatoa Kauli Tata Zenye Ukakasi.

Rejea kauli Zako Unazozitoa Zinatufanya Tukose Kukuamini Kwa kila Unachokifanya Sasa.

MAISHA MEMA
 
Zitto, swala la ujamaa hutaliweza kamwe! Wewe danganya wafuasi wako ila huo ndo ukweli!
 
Last edited by a moderator:
...but many uncoordinated fronts can lead to friendly-fires!!
 
Ndugu yangu Zitto! Nikihitaji nakala ya ilani na katiba vinapatikana wapi kwa huku Arusha? Au mna tovuti?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom