One Struggle, Many Fronts. Forward ever, Backward Never... Tumeamua kuangalia mbele!

One Struggle, Many Fronts. Forward ever, Backward Never... Tumeamua kuangalia mbele!

Tumeweka dhamira yetu ya kuondoa utawala wa ccm. Mtu yeyote anayekuja muda huu kutukwepesha kutoka kwenye lengo letu hili, hakika ni adui wa Watanzania. Sisi tunasema uzi ule ule, mpaka ushindi!!
ni bora kutoiondoa kuliko kuiondoa na kuweka watu wanaofanana nayo.
 
kwa maneno yako ulisema UKAWA ni wasakatonge na kugawana madaraka... maneno yako yanaonyesha jinsi ulivyo mbali na vyama vingine vya upinzani je huo si usaliti ? sasa Watanzania wanapata nafasi ya kusoma rangi zako
 
Azimio la Arusha doesn't say so brother. Nitafutie Billionea hata mmoja ambaye sio bepari au kabaila na ambaye hafanyiwi kazi. hapo nyuma nimeweka maana ya Ujamaa kama ilivyoelezwa na Azimio la Arusha..

Mimi nadhani tukielimishana vizuri ndio watu watakueleweni kuliko kutoa majibu ya Mkato kumuondoa mtu.. Ni wajibu wa Ben kuuliza ili afahamu hii ACT ina malengo gani na Taifa gani inataka kulijenga.
tusubiri azimio la arusha lililohuishwa.
 
Mkuu Salary Slip are you serious? kweli kabisa

Unaongelea flexibility upi huo? Zitto hapa kaulizwa maswali ya msingi na kakimbia bila kuyajibu.

Hatuwezi kumpa mnafiki na msaliti muda wala fursa kwa sababu yeye Zitto na chama chake ACT wana nia ovu ya kudhoofisha upinzani

KATIBA ya ACT inasema mwanachama mpya atakaa miezi 6 bila uongozi lakini zitto ndani ya siku moja tayari ndie kiongozi mkuu wa chama

Ninachosema hizi ahadi za huyu bwana muda pekee ndio msema mkweli.Huwezi kudanganya watu wote muda wote.

Hii post yake ya leo ikiwezekana isevu alafu tutakuja kuitumia kama ushahidi siku zijazo.

Unajua huku kujieleza hadharani kwa Zitto ni sawa na kujitia kitanzi mwenyewe tofauti na kama angekaa kimya.

Kama hana dhamira ya dhati,basi anachokifanya kwa sasa ni sawa na kumwaga mchele kwenye kuku wengi.

Ukichunguza post yake hii ni kama mtu anaetaka kuanza ukurasa mpya baada ya kugundua kasoro zake ila tu anashindwa kuwa muwazi.

Mpaka Oktoba kuna muda wa kutosha kupima kauli na vitendo vyake.Kwa sasa haina haja ya kuangaika nae sana bali ni kumtazama tu.

Zitto hivi sasa ni kama msanii wa mziki aliechuja na sasa ana-fight kurudi katika kiwango chake hivyo ni lazima aandae nyimbo/single mpya za kuvutia upya mashabiki wake.

Tulieni wala msihangaike nae kwa sasa ila muda utatupa majibu tu.
 
Last edited by a moderator:
Swali zuri sana Mkuu , sio Tanzania ya leo pekee, ni ulimwengu mzima hakuna anayeubiri ujamaa sasa hivi. Na NWO ishatangazwa kitambo tuu sasa ni ujamaa upi ambao anaongelea. Dunia ipo katika Capitalism si socialism.

Ngoja nisubri atavyokujibu kwanza
UJAMAA FAILED.....ninakubaliana NA wewe hapo juu brother, Ndio maana Tanzania iko hapa tulipo. Ni jambo la kutoamini kama mtu bado anakuja ktk 21st century kuhubiri siasa ya ujamaa iliyofeli, sio hapa kwetu tu bali hata na nchi zingine zilizojaribu kuifuata. Where is Cuba? where is socialists Russians? Where is North Korea?

Kama utajibu kuwa zipo na zinaexist, nitakwambia kwamba if they would have followed something else besides Ujamaa wangekuwa mbali sana. China ambao leo wako hapo walipo kwasababu wamefanya major reforms ktk politics zao. So please STOP the BS, kuwadanganya watanzania kuwa utarudisha siasa ya Ujamaa ambayo imeprove failure.

Tanzania needs mixed Economy ambapo kila mtu atakuwa empowered to be who they wants to be, by creating opportunities for everyone to prosper kupitia Elimu, technology ya kisasa kwa kuruhusu competition within and outside the country.

Ningekupa lecture Mr ZZK but sina muda wa kufanya hivyo Sasa, but I hope you understand kile unachokifanya.
 
Zitto kete pekee muliyobaki nayo ni hicho chama chenu kujiunga na UKAWA nje ya hapo hakika hatutawatofautisha na ccm, haiwezekani leo wapinzani tumeungana halafu kaibuke kachama kakugawa kura zetu halafu tukachekee, vita yetu itakua ni UKAWA v/s CCM+ACT, hamuwez kututoa nje ya mstari sahh
 
Hiyo namba 4 yako ina lengo ovu, na haita-apply kwenye chama chako, vyama vingine vilianzishwa na watu safi ndio maana viling'ara, si hivyo kwa hiyo ACT yako.



Naona na wewe unatoa utabiri wako. Wakuite Nabii au sio?
 
ZZK katika mada zake hapo awali ukiwa CHADEMA miaka ya nyuma, alisema hivi wakati wa uchaguzi vya vipya huanzishwa kwa malengo ya kugawa kura, UMELITIMIZA HILO na malengo ya ACT ni kugawanya kura za upinzani, maana yake kazi kubwa ya ACT ni kusafisha njia ya CCM. YAANI ccm imebinafsisha jitihada za kuweka fitina kwa upinzani, sub contracted ZZK.

Umejitungia mtihani, kisha umejisahisha mwenyewe na very good ukajipa.

Safi sana.
 
fikirikwanza

Siasa ni mapambano. Siwezi kuacha mapambano. Sijawahi fanya usaliti wowote. kuitana majina hayo hakusaidii lolote zaidi ya kufurahisha ego zetu tu. ACT Wazalendo ina shabaha moja tu nayo ni kupambana na mfumo wa uchumi unaonyonya watanzania. Ku surrender mapambano hayo ndio usaliti. Tutaendelea kupambana

Wewe kila ukisema kesho yake unabadili, simply ni muongo hebu fikiria hili "Zitto anasema tayari nafasi zote zimeshajazwa fomu na zimerudishwa tayari na yeye hakujaza fomu za kugombea. Anasema wote wale waliosema amekwenda ACT ili awe kiongozi watakuwa wameumbuka" hapo ni EFM siku moja tu, BAADAYE YEYE NDO KIONGOZI MKUU wa ACT na mwenyekti yuko chini yake, SASA nani ameumbuka bwana mdogo? kwa hali hii kisiasa atakuamini Mwigulu, Mkumbo na Samson tuuu, Yule mama yeye anakuangalia na visenti vyako tu singida na ubunge hapati maana singida ni akili mtu tuuu.
 
shida yako ilikua ni kutaka uongozi CHADEMA, umepata ulichotaka huko ACT, mambo ya mifumo, ugawaji wa ardhi sijui elim na takataka zote haihitaji mashairi na ngonjera, hicho ndicho tunachokitaka wapinzani wote, ni mambo yanayowezekana lakn baada ya kushika dola, target yenu badala ya kuwa ccm muna i attack ukawa na hasa CHADEMA, dhambi ya kugawa kura za ukawa itawatafuna milele hakika, ukawa ndio tumaini pekee la kuitoa CCM madarakani
 
Kama kweli mkiyaishi hayo uliyoyanena, nadhani mtakuwa katika mstari nyoofu kama chama cha upinzani.

Tatizo kunavifaranga vilivyo chini ya KIONGOZI WA CHAMA kutwa nzima kuishambulia CHADEMA na CUF! Na hatujaona "Taswira ya chama" ukiwakemea na hapo ndipo mnapofungamanishwa na tuhuma za kuwa vibaraka wa "Jembe na Nyundo"

sasa unategemea Zitto aje humu kumkemea mwanachama mmoja mmoja?alichofanya kuandika "msimamo" wa chama ni sahihi, sasa yule atakayefuatisha taarifa au comment kutoka kwa kina pangupabichi wenye kuficha majina yao watakuwa wanafanya makosa wao.

La msingi itakuwa kama Zitto akikutwa anatenda kinyume na alichoandika hapa. Huwezi kuongoza kundi la maelfu wa watu na wote wakafuatisha unachosema bila kutoka nje ya mstari, ukiona unaongoza watu wa aina hiyo jua kuna problem hapo.Binadamu wako na free will.
 
Last edited by a moderator:
Kama kweli mkiyaishi hayo uliyoyanena, nadhani mtakuwa katika mstari nyoofu kama chama cha upinzani.

Tatizo kunavifaranga vilivyo chini ya KIONGOZI WA CHAMA kutwa nzima kuishambulia CHADEMA na CUF! Na hatujaona "Taswira ya chama" ukiwakemea na hapo ndipo mnapofungamanishwa na tuhuma za kuwa vibaraka wa "Jembe na Nyundo"

Yoyote atakaeishambia act na sisi vijana wa cama atutaeza vumilia tutashambulia tu kwani ndio sifa ya askari usisubiri idhini yoka kwa mkuu wakati unamuona adui yako alishaanza piga mengine yatafata japo mkuu hataki
 
Tumeainisha vizuri sana kwenye ilani yetu ya uchaguzi mwaka 2015 na tutafafanua zaidi kwenye Azimio la Arusha lililohuishwa. Moja ya sera zetu ni kukomesha kabisa uporaji wa ardhi nchini kwa kuhakikisha wananchi wanamilikishwa ardhi ya kilimo na ufugaji. Mashamba yote yaliyokuwa ya NAFCO yakabinafsishwa yatarejeshwa kwa wananchi na kugawiwa kwao kwa kilimo kwa mfumo wa outggrowers scheme.
ACT Wazalendo imeamua kusimama masuala yanayohusu wananchi. Naomba upate nakala ya ilani yetu uweze kujisomea
Zito usijivunjie heshima... mtu yeyote hawezi kuwapa support kwa hilo. Tunajua ya Zimbabwe - Leo utupe ardhi kwa utaalamu upi wa kilimo, utupe madini tuchimbe kwa jembe?? Siasa za ovyo sana hizo za Ujamaa
 
Zitto,

Chama chako kimejipambanua na Unyerere (Nyerereism) na kufuata misingi ya Azimio la Arusha ambao unaamini mgawanyo wa haki katika raslimali za taifa na pia unaruhusu umiliki wa mali kama nyumba,biashara n.k.

Je, unawezaje kufuata ujamaa wa kidemokrasia wakati huohuo ukijipambanua na Nyerereism ambayo msingi wake ni Ujamaa wa Kikomunisti usioamini katika umiliki wa mali kama nyumba zaidi ya moja na kumiliki biashara ukiwa Kiongozi wa umma?


Duh, watu mna maswali magumu.

In fact Ujamaa wa Nyerere hautekelezeki kwa uhalisia wa sasa wa dunia. It's too radical a step, labda wameamua kwenda kwa hatua.

Ingawa nisingependa wafike kwenye Ujamaa wa Nyerere, kwani kuna mambo mle yalikuwa ni makosa flani, na yeye mwenyewe Nyerere alikiri kuwa alifanya makosa, hakuna haja ya kurudia makosa wakati tumekuwa na miaka 50 ya kuyasoma mafundisho na practice ya ujamaa wa nyerere.Hata uchina alikojifunzia Nyerere na Cuba wamefanya updates za ujamaa wao.
 
Zitto,naamini chama chenu hakina nia ya dhati kuondoa duduwasha CCM kwa kuwa most of time mnaishambulia CHADEMA huku katibu mkuu akiapa kuwa atahakikisha anaiondoa CUF mikoa ya Pwani,pia kauli yako ya kuuita Umoja wa Katiba ya wananchi(UKAWA) kuwa ni wasaka tonge,sina imani na chama pamoja viongozi wake.
 
Naomba unijibu hili Zitto ACT kabla hujahamia wewe ilikwisha kuanzisha maofisi makubwa makubwa mikoa mingi ikiwamo Arusha mjini ofisi ambazo kwa hesabu ya kawaida kwa mfano ya pale Arusha mjini siyo chini ya Milioni moja kwa mwezi. Chama hiki kichanga chenye wanachama wachache kimetoa wapi fedha za kukodisha maofisi makubwa hivyo? Pia kabla hujahamia Chadema kule Kigoma ulitoa magari yako yakaanze kutumika kufanya kazi za ACT unataka kuniambia wewe ulikuwa moja ya wafadhili na waanzilishi wa ACT ukiwa bado ndani ya Chadema?

Fomu ya mali ya Zitto inaonesha ana gari moja tu!

Hivyo lawama zako zote zina hang kwenye ku-prove kuwa anamiliki hayo magari, baada ya hapo ndio uje kwenye hoja yako. Kama unashindwa kuprove beyond reasonable doubt kuwa Zitto anamiliki hayo magari mengi, ambayo kupitia kiapo cha chama chake amesema anamiliki gari moja tu!implying kuwa hamiliki haya magari unayosema, unaonaje chini ya hizi tuhuma ukaambatanisha na kadi za gari za umiliki wa hayo magari?au hata kum-tie Zitto na umiliki?

Kama unashindwa kufanya hivyo, kweli unategemea watu tukuchukulie serious?binafsi napenda kama tuhuma zinawekwa na mtu mwenye uelewa anaziweka na evidence, sio kuleta hadithi za nimesikia sehemu au kuleta picha Zitto amepanda gari flani, wangapi humu mnapanda na kuendesha magari sio ya kwenu?

nawasihi Bavicha muachane na hizi Siasa Uchwara, they are old, tiring and useless,mfike wakati mjitazame wapi mmekosea, mjirekebishe, mrudi kwa wananchi, mjenge nao hoja, huyu Zitto anawaambia amepigia mstari yote ya nyuma anaanza upya nyie bado mnamrudisha kule kule, hamuoni kuwa, ukiondoa tuhuma za usaliti this usaliti that, mmekosa hoja za kupambana nae?

Humu nimemuona Ben Saanane tu ameuliza swali la msingi na lenye kumchalenge Zitto kwenye hoja ya msingi.Katazame debate ya UK leadership, uone kama kuna mtu alikuwa napoteza muda kuongelea watu kule, watu walikuwa wanachallenge issues tu. Ifike wakati mjikite huko. By the time mnastuka hao ACT watakuwa wameimaria kwa kuwa wanawaambia wananchi kile wanataka kusikia, halafu mtawalaumu bure tu.
 
Last edited by a moderator:
Unaposema usaliti na uchonganishi weka ushahidi haiwezekan mtu yule yule kupewa kashafa zile zile watanzania wanaitaji kuaemewa sio kusikiliza hekaya kilasiku
 
Watoto wa cdm wanajitaidi sana kupiga vita act naamini hamtaweza hamuoni mshangao tu namna act ilivyoanza na sasa ilivyo mabadiliko makubwa sana imekusanya vijana wengi tu wenye kushambulia kama nyinyi tofauti na awali tulivyokua tunapata shida na page zote zinakua za cdm
Nyambafu mfikshieni mfalme mbowe
 
Back
Top Bottom