One Struggle, Many Fronts. Forward ever, Backward Never... Tumeamua kuangalia mbele!

One Struggle, Many Fronts. Forward ever, Backward Never... Tumeamua kuangalia mbele!

mirisho pm;


Kuhusu majimbo hayo, ni mambo tu. Maombi yanakubaliwa na kukataliwa. Ungesubiri kuona maamuzi yangu nipo uweze kutoa maoni yako.

Kwamba sijawahi kuionya CCM kuishambulia CHADEMA nadhani ni propaganda tu. Maisha yangu yote napambana na CCM ndani na nje ya Bunge. Wao kunisifia ni divide and rule.

Mara ngapi viongozi wa CHADEMA wanasifiwa na mawaziri wa CCM? Hata humu JF imeandikwa mara kadhaa pale mawaziri wa ccm wanapowasifia baadhi ya wabunge wa CHADEMA. Ni kawaida hiyo kwenye siasa.

Mara nyingi sana nimetoa matamko makali kulaani uvunjifu wa amani nchini na ugandamizaji dhidi ya upinzani nchini. Mara kadhaa nimeadhibiwa na CCM nimesimishwa ubunge, kamati ya POAC ilivunjwa, niliswekwa ndani kwenye uchaguzi Kigoma Mjini nk.

Hatupimi umakini wa viongozi wa upinzani kwa kuwekwa ndani na polisi, kama ni hivyo leo DP ingekuwa chama kikubwa kuliko vyote nchini
 
Last edited by a moderator:
Cha muhimu wana-upinzani ni kuishawishi ACT kujiunga na UKAWA ili kuwa na kauli moja yenye nguvu.
 
Hongera kwa uamuzi wako! Nina maswali mawili tu,

1. kwa nini mashabiki wako wengi waliomo humu ni manazi wa CCM, huoni inakutia doa?

2. Vijana wengi wa ACT waliomo kwenye jukwaa hili wamekuwa wakiishambulia chadema, mfano ACT yachukua wanachama wa chadema. Pamoja na yote haya, hatujasikia kauli ya chama juu ya hili. Houni hili bandiko lako haliwiani na kile kinachoendelea kivitendo?

Tumeshaonya wanachama wetu wote kutoshambulia chama chochote cha upinzani. Walikuwa wanachokozwa na wao kujibu mapigo. Hata hivyo haina tija na tumeamua kuwa hata tukichokozwa tunasema " tumeshapiga mstari. Forward ever backward never". Hatutachokozeka tena. Kazi yetu kueneza Sera za ACT Wazalendo
 
Kama hujawahi kufanya usaliti wowote ilikuwaje December 2012 ukaanzisha thread hapa jamvini ya kuwaomba radhi wanachama wa CHADEMA na kuahidi mwaka mpya wa 2013 kubadilika na kuongeza ushirikiano na viongozi wenzio ili kuhakikisha mshikamano ndani ya CHADEMA?

Je, ile radhi ambayo ulikuwa unawaomba wanachama wa CHADEMA ilihusiana na kitu/vitu gani ulichokifanya/ulivyovifanya kama mwanachama na kiongozi wa CHADEMA kilichokusukuma/vilivyokusukuma mpaka uanzishe uzi kama ule!? Bahati mbaya sana uzi ule ulifutwa bila sababu zozote zile za msingi.

Swali la nyongeza ule uzi ulitaka wewe ufutwe au ulifutwa na wamiliki wa JF? Kama ni wewe ulitaka ufutwe ni kwa sababu zipi hukutaka ule uzi uendelee kuwepo hapa jamvini?

Siasa ni mapambano. Siwezi kuacha mapambano. Sijawahi fanya usaliti wowote. kuitana majina hayo hakusaidii lolote zaidi ya kufurahisha ego zetu tu. ACT Wazalendo ina shabaha moja tu nayo ni kupambana na mfumo wa uchumi unaonyonya watanzania. Ku surrender mapambano hayo ndio usaliti. Tutaendelea kupambana
 
Tumeshaonya wanachama wetu wote kutoshambulia chama chochote cha upinzani. Walikuwa wanachokozwa na wao kujibu mapigo. Hata hivyo haina tija na tumeamua kuwa hata tukichokozwa tunasema " tumeshapiga mstari. Forward ever backward never". Hatutachokozeka tena. Kazi yetu kueneza Sera za ACT Wazalendo

cc mwl Kaijage Naamini utaheshimu tamko la Kiongozi wa Chama.
 
Last edited by a moderator:
Tumeainisha vizuri sana kwenye ilani yetu ya uchaguzi mwaka 2015 na tutafafanua zaidi kwenye Azimio la Arusha lililohuishwa. Moja ya sera zetu ni kukomesha kabisa uporaji wa ardhi nchini kwa kuhakikisha wananchi wanamilikishwa ardhi ya kilimo na ufugaji. Mashamba yote yaliyokuwa ya NAFCO yakabinafsishwa yatarejeshwa kwa wananchi na kugawiwa kwao kwa kilimo kwa mfumo wa outggrowers scheme.
ACT Wazalendo imeamua kusimama masuala yanayohusu wananchi. Naomba upate nakala ya ilani yetu uweze kujisomea

Ndugu Zitto Katiba ya ACT ninayo Soft Copy naipitia kila siku,tungependa muweke ilani yenu online nayo tuipate kuiona na kuangalia ipo vipi au kama ipo weka link tuidownload.
 
Last edited by a moderator:
Zitto nini chanzo cha mapato ya Chama cha ACT maana ninajua hampati ruzuku.

Ni kweli hatupati ruzuku. Kama ilivyo vyama vingine vyote vilipokuwa vinaanza havikuwa na ruzuku lakini vilikuwa vinaendeshwa mpaka kukomaa na kuanza kupata ruzuku. Tunapita njia hizo hizo ambazo wenzetu walipita. Tunapita kuomba kuomba na tuna mikakati ya dhati ya wanachama wetu kuchangia. Tunaendeshwa na thumni thumni za wanachama. ACT Wazalendo ni moto wa pumba, ina wanachama na wapenzi wengi sana nchi nzima. Ndio maana Mkutano Mkuu wetu ulijaa kutoka kila kona ya nchi. Vyama vingi sana vilitumia miaka mingi sana kufikia hali hii ambayo ACT Wazalendo ilifikia. Imani ya wananchi ni kubwa sana na hivyo wanachangia sana kwa wanyonge wenzao.

Tumeweka utaratibu wa kuweka vyanzo vyetu vya mapato wazi na kukaguliwa na CAG. Tutaweka kwenye tovuti ya chama
 
To be honest mkuu Zitto, ACT lengo lenu ni kuuangamiza upinzani, hususani CDM.

Japo unapretend umechora mstrari na kuanza upya, lakini ukweli ni kwamba unachuki ya dhahiru na chama upichotoka. Nilifuatilia majadiliano yako jana, especially ulipotamka...tumesajiri wanachama 200 moshi, jimbo linaloongozwa na CDM...

Vijana wako wa mtandaoni hawaji na habari ya kupokea wanachama wapya toka vyama vingine,, ni CDM tu!

Ulikua na bright future ya siasa za nchi hii siku zijazo, lakini umajiharibia kwa tamaa zako, wewe mwenyewe kimoyomoyo unalijua hili, japo unajikaza kisabuni.

Mwisho, achana ja tabia ya kujikweza sana, jana unaoungelea kuingusha serikali mara mbili, really? Hivi kwenye ESCROW ni kitu gani kipya ulichofanya, kusoma ripoti bungeni?
 
Tumeshaonya wanachama wetu wote kutoshambulia chama chochote cha upinzani. Walikuwa wanachokozwa na wao kujibu mapigo. Hata hivyo haina tija na tumeamua kuwa hata tukichokozwa tunasema " tumeshapiga mstari. Forward ever backward never". Hatutachokozeka tena. Kazi yetu kueneza Sera za ACT Wazalendo

* hivi ni mbinu gani uliotumia ndani ya siku saba za uanachama wako mpaka ukapata nafasi ya juu kabisa katika chama!??

* Unazungumziaje swala la kuanzisha ACT wakati ukiwa bado chadema!??

* Kwa kipindi kifupi cha uhai wa chama chenu tumeona matumizi makubwa ya fedha kulinganisha hata na vyama mlivyoikuta kama saut ya umma au nld, je ni nani mfadhiri mkuu wa chama ukizingatia hamjaanza kupata ruzuku toka serikalini!??


Ni hayo tu ndugu mbunge mstaafu, yanatusuumbua sana huku mtaani kwetu!!!! nadhani utasaidia kutujibu...
 
Kwa uelekeo wa ukuaji wa Demokrasia katika Taifa letu tunahitaji vyama vyenye mtazamo wa kizalendo , tusubiri tuone kazi ya ACT ni nini tuwasikilize na tuwapime na hatuna sababu ya kuitana wasaliti bila ushahidi eti kwa kua tumeaminishwa hivyo na viongozi wetu wa vyama
 
Tumeainisha vizuri sana kwenye ilani yetu ya uchaguzi mwaka 2015 na tutafafanua zaidi kwenye Azimio la Arusha lililohuishwa. Moja ya sera zetu ni kukomesha kabisa uporaji wa ardhi nchini kwa kuhakikisha wananchi wanamilikishwa ardhi ya kilimo na ufugaji. Mashamba yote yaliyokuwa ya NAFCO yakabinafsishwa yatarejeshwa kwa wananchi na kugawiwa kwao kwa kilimo kwa mfumo wa outggrowers scheme.
ACT Wazalendo imeamua kusimama masuala yanayohusu wananchi. Naomba upate nakala ya ilani yetu uweze kujisomea

Zitto,

Chama chako kimejipambanua na Unyerere (Nyerereism) na kufuata misingi ya Azimio la Arusha ambao unaamini mgawanyo wa haki katika raslimali za taifa na pia unaruhusu umiliki wa mali kama nyumba,biashara n.k.

Je, unawezaje kufuata ujamaa wa kidemokrasia wakati huohuo ukijipambanua na Nyerereism ambayo msingi wake ni Ujamaa wa Kikomunisti usioamini katika umiliki wa mali kama nyumba zaidi ya moja na kumiliki biashara ukiwa Kiongozi wa umma?
 
Last edited by a moderator:
Ndugu Zitto nasubiri kwa hamu majibu ya swali no. 6 pg 1...

Pia nina swali la nyongeza.. Uliwahi kutamka "Msiwaamini wanasiasa" Naomba ufafanuzi wa hiyo kauli na pia ni kwa vipi tukuamini leo wewe hali ulishawahi kututaadhlisha juu kuamini wanasiasa..
 
Last edited by a moderator:
Kaka zito napenda kukupongeza sana kwa uamuzi huo wakuanzisha Chama kipya acha waongee kwani hao ni mashabiki tu endelea kupiga kazi. Hopefully watakuja kukuelewa mwisho wasiku. Mwenyezi Mungu akubariki na Chama chako kipya
 
Back
Top Bottom