Mkuu
Zitto naona umekuja na kauli mbiu nzuri yaani hiyo kauli ya Dr. Nkrumah kwamba foward ever backward never. Hii ni kauli ya kiungwana zaidi.
Haina haja ya kulumbana na mtu ama kuanza kukisema chama chako cha zamani. Nakumbuka siku uliyoitisha mkutano wa waandishi wa habari pale Serena watu hasa wa CHADEMA walihamanika wakidhani utaenda kuichafua. Katika kuhamanika huko, ikabidi Naibu Katibu Mkuu kuitisha mkutano na wandishi wa habari pale makao makuu harakaharaka ili kugawa waandishi na matokeo yake akaishia kuongelea habari za maji jimbo la Ubungo. Kitu ambacho angeweza kukiongelea kwenye mkutano wa hadhara huko Bonyokwa.
Katika siasa za Tanzania ni watu wengi wameitwa wasaliti, hakuna mwanasiasa ambaye hajaitwa msaliti. Marando aliwahi kuitwa msaliti, Mrema aliwahi kuitwa msaliti, Maalim Seff aliwahi kuitwa msaliti, Dr. Slaa aliwahi kuitwa msaliti, nk. Hivyo neno usaliti kwa mwansiasa wa Tanzania ninkama fashion vile; leo utakuwa shujaa mkitofautiana na wenzako tayari unaitwa msaliti.
Kazana na kuimarisha chama chako ila hili la kuacha kugombea ubunge Kigoma Kasikazini na kutaka (kuombwa) kugombea Kawe, Segerea, Kahama, nk naona halijakaa sawa. Litafakari kwa makini.