One Struggle, Many Fronts. Forward ever, Backward Never... Tumeamua kuangalia mbele!

One Struggle, Many Fronts. Forward ever, Backward Never... Tumeamua kuangalia mbele!

Anasoma upepo unavuma kwa kasi gani na unatokea kusi au kaska.

ACT ni moja ya chama makini sana cha kupambana na CDM kwa hisani waliyopewa na CCM ndiyo maana kila siku wanavuna wanachama kutoka CDM.

Hongera Zitto mbunge uliyetimuliwa CDM kwa usaliti
 
Last edited by a moderator:
Mmejipanga nani agombee Urais mwaka huu?
Au ni kweli kua mnamuwekea nafasi Lowassa kama akitoswa CCM?
 
Chezeya Jamii Forums weye mpaka Serikali inaihofia imebidi kwenda kutengeneza muswaada wa kuidhoofisha.

Hapana cheza kabisa na jamiiforums, humu kila mtu ana first class, ndio maana wakina Makamba wanahangaika usiku na mchana kuifungia, humu ni hoja juu ya hoja hakuna kuangalia mtu usoni ni nondo tu.
 
Tunachohitaji ni kila mmoja kumlenga adui ili kumshinda. Tulishindwa kufanya kazi ndani ya moja, tunaweza kufanya kazi tukiwa majirani. Adui bado ni yule yule.


Mh. hapa.kidogo umeniacha tenge. Ni kweli kuwa unaamini katika utengano na si katika umoja? Maana kupambana na adui mkiwa wamoja ni sawa na kumuattack kwa kombora ambalo laweza kumsambaratisha kuliko kupambana naye kwa kila mmoja akirusha risasi yake kivyake.... what if risasi utakayoitupa wewe ikaishia kuparuza manyoya ya mkiani na ya jirani ikaishia kumjeruhi kucha.... ushindi utakuwepo kweli?

Saa nyingine ninawiwa kuamini kuwa umefanikiwa kupandikiza na kuimwagilia mbegu ya kilimo cha 'Divide and Rule' katika shamba la mfumo wa vyama vingi Tanzania.
 
Mmejipanga nani agombee Urais mwaka huu?
Au ni kweli kua mnamuwekea nafasi Lowassa kama akitoswa CCM?

Bavicha mbona mnauliza maswali ya kitoto?
 
Ndugu yangu Zitto , acha kutufanya watanzania wote wajinga na hatuoni mnachokifanya au hatusikii mnayoyaongea,

Ni juzi tu hapa Mwigamba kiongozi wa ACT alisema ACT itahakikisha inaifuta CUF Pwani sasa niambie je lengo la Mwigamba ni nini??

Ni majuzi tu hapa ulisema kuwa Ukawa ni wasaka tonge je lengo lako lilikuwa nini?

Ni lini wapi viongozi wa vyama vya upinzani umeishambulia ACT?
Alinda asante kwa kusema hili na pia kina mtu Anaitwa Mwl. Kaijage naye alikuja na thread yenye kusema ACT waibomoa ngome ya CHADEMA na leo hii Zitto anasema wamekuja kuongeza nguvu ya upinzani..... Hatuelewi....
 
Last edited by a moderator:
Mh. hapa.kidogo umeniacha tenge. Ni kweli kuwa unaamini katika utengano na si katika umoja? Maana kupambana na adui mkiwa wamoja ni sawa na kumuattack kwa kombora ambalo laweza kumsambaratisha kuliko kupambana naye kwa kila mmoja akirusha risasi yake kivyake.... what if risasi utakayoitupa wewe ikaishia kuparuza manyoya ya mkiani na ya jirani ikaishia kumjeruhi kucha.... ushindi utakuwepo kweli?

Saa nyingine ninawiwa kuamini kuwa umefanikiwa kupandikiza na kuimwagilia mbegu ya kilimo cha 'Divide and Rule' katika shamba la mfumo wa vyama vingi Tanzania.

Tatizo kuna vyama vya upinzani wabinafsi sana mfano.chadema na ndio maana UKAWA itavunjikamwezi wa nane maana Chadema wana lazimisha kutoa Rais..na chadema hawataki kuungana na chama cha wazalendo ACT chini ya Dr Zitto kabwe kijana makini.
 
Tatizo kuna vyama vya upinzani wabinafsi sana mfano.chadema na ndio maana UKAWA itavunjikamwezi wa nane maana Chadema wana lazimisha kutoa Rais..na chadema hawataki kuungana na chama cha wazalendo ACT chini ya Dr Zitto kabwe kijana makini.

Mtabiri wa vifo vya upinzani anayeaminika huko CCM ni Wassira tu.Yeye alitabiri kabisa CHADEMA kitakufa 2012.

Sasa naona na wewe umeibuka na Ramli chonganishi
 
fikirikwanza

Siasa ni mapambano. Siwezi kuacha mapambano. Sijawahi fanya usaliti wowote. kuitana majina hayo hakusaidii lolote zaidi ya kufurahisha ego zetu tu. ACT Wazalendo ina shabaha moja tu nayo ni kupambana na mfumo wa uchumi unaonyonya watanzania. Ku surrender mapambano hayo ndio usaliti. Tutaendelea kupambana
Maelezo na malengo mazuri. Kauli yako hata hivyo ni tofauti na maandiko ya Mwl Kaijage hapartment JF! Pengine anza kwa kumwelimisha makusudio haya ya chama.
 
wadau tuwe na heshima kiasi na tujali mtu kama Zitto kuacha mambo yake akajibu hoja za watu hapa hata kama tunachuki vipi ila Zitto ni jina kubwa na anaheshima yake katika taifa letu viongozi wangapi tumeona wanajibu hoja hapa??
kwahiyo kwa kijana kama huyu kujitolea kuongea nasi hapa tuulize maswali ya msingi na si kebehi na kusambaza chuki
Zitto keep it up bro kama unavyosema mwenyewe watu waweke akiba ya maneno
 
Kati ya watu niliyowaani ni wewe na siyo kama mwanasiasa bali kama kiongozi, mpaka sasa haya yanatokea na skendo zako zote za usaliti sitakuamini tena nimekufuatialia sana Zitto lakini nimepoteza tumaini kwako wewe ni kigeugeu sana kaka usimamii kauli zako na wewe unawahi kusahau wakati rekodi zako zipo. Vizuri siasa ya Ujamaa naipenda sana ila ACT hapana, by the way you will never be a President of our State, Mwisho kwa nini nafasi ya kiongozi mkuu haikutangazwa kama zingine na wewe ukapewa kama shuka? yapi majukumu ya m/kiti kama wewe umejirundukia madaraka ya kifalme?
 
Waiten na hao wenye saccos yenu muwaulze matumiz ya ruzuku km hamjaitwa wotemamluki ha ha haa ZZK anafaa kuwa ktk chama chenye misingi ya uwaz
 
Zitto,

Chama chako kimejipambanua na Unyerere (Nyerereism) na kufuata misingi ya Azimio la Arusha ambao unaamini mgawanyo wa haki katika raslimali za taifa na pia unaruhusu umiliki wa mali kama nyumba,biashara n.k.

Je, unawezaje kufuata ujamaa wa kidemokrasia wakati huohuo ukijipambanua na Nyerereism ambayo msingi wake ni Ujamaa wa Kikomunisti usioamini katika umiliki wa mali kama nyumba zaidi ya moja na kumiliki biashara ukiwa Kiongozi wa umma?

Ben;
visit the libraries there is a book Ujamaa or African socialism by Abdulharman Babu (check spelling); Nyerereism was based on African/Tanzanian characteristics. Not communism or the way you want to point.

Nyerere was a believer; he was Christian. Communists don't believe in God.
Nyerere invited scholars to challenge Azimio la Arusha (Arusha Declaration). Remember an example. Millionaire anaweza kuwa mjamaa? It was debated long time; Nyerere came back and said A millionaire can be Mjamaa.

if Zitto will try to improve that white paper we had; for motivation I think Zitto is a leader who can lead us(maybe); let us give him time; he is still a young man.

We are looking for the Messiah to rescue the country; most oppositions have failed us we should not disappoint those who are emerging; I see light on Zitto.
 
Am sure atarudi kujibu maswali haya otherwise sioni kwa nini ameanzisha hii thread.

Lengo lake ni kutufahamisha juu ya ACT Wazaa leo na lazima alitimize hilo kama ana nia ya kupata wafuasi.
 
Zito nikikutazama hata machoni sioni dhamira yako ya kweli kwamba umelenga kuifuta ccm!! Mana ulipo shutumiwa na cdm kwamba umeanzisha chama na hutakiwi tena cdm, walahi hukutaka hata kuomba msamaha wala kujieleza, ulileta dharau, kipi leo kitufanye tukuamini kua sio msaliti
 
Mtani wangu huwa mimi huwa nakukubali,lakini kitendo chako cha kuanzisha chama ukiwa ndani ya chama kingine hapo uliniboa sana!p

Pa tabia yako ya kupenda KUJIKWEZA mfano jana kwenye kipindi cha HOTMIX unasema heti umeiangusha serikali mara 2 kitu ambacho ni uongo kwani ktk hiyo kamati ya PAC hukufanya kazi peke yako. Ulikuwa na wabunge wengine ambao mlishirikiana kwa pamoja,pia uliwahi kusema kuwa unawafahamu wote walioficha pesa USWISS na kwamba upo tayari kuwataja, lakini mpaka umetoka bungeni umeshindwa kufanya hivyo na kupoteza imani kwa watu waliokuamini kama mimi
 
Zitto,

Kiongozi naomba ufafanuzi wa maneno yako haya
Kwa muda mrefu na hasa siku za hivi za karibuni kumekuwa na threads nyingi sana humu ndani kuhusu Zitto na kuhusu Chama cha ACT Wazalendo. Kumekuwa na tuhuma kwamba chama cha ACT Wazalendo kinashambulia vyama vingine vya upinzani hapa nchini. Napenda kusema mambo machache sana

Chama cha ACT Wazalendo ni chama cha siasa chenye mrengo wa kushoto na kinajitanabaisha na siasa ya Ujamaa iliyoasisiwa na Azimio la Arusha. Lengo letu ni kueneza siasa zetu zenye mrengo huo.
Sasa tunanze na kifungu kimoja kimoja, maana naposoma Azimio la Arusha linasema hivi:-

SIASA YA UJAMAA

(a) Hakuna Unyonyaji:
Nchi yenye Ujamaa kamili ni nchi ya wafanyakazi: hainaubepari wala ukabaila. Haina tabaka mbili za watu: tabaka ya chini ya watu wanaoishi kwa kufanya kazi, na tabaka ya juu ya watu wanaoishi kwa kufanyiwa kazi. Katika nchi ya Ujamaa kamili mtu hamnyonyi mtu, bali kila awezaye kufanya kazihufanya kazi, na kila mfanyakazi hupata pato la haki kwa kazi aifanyayo na wala mapato ya wafanyakazi mbali mbali hayapitani mno.

Katika nchi ya Ujamaa kamili watu peke yao ambao huishikwa jasho la wenzao, na ni haki yao kuishi kwa jasho la wenzao ni watoto wadogo, wazee wasiojiweza, vilema na wale ambao kwa muda, Jumuiya imeshindwa kuwapatia kazi yoyote yakujipatia riziki kwa nguvu zao wenyewe. Nchi yetu ni nchi ya Wakulima na Wafanyakazi, lakini sii nchi ya Ujamaa kamili. Ina misingi ya ubepari na ukabaila na vishawishi vyake. Misingi hii ya ubepari na ukabaila yawezaikapanuka na kuenea.

Hadi kufikia hapo ACT inakubaliana kwa kiasi gani na dhana hiyo kwamba hakuna UBEPARI wala UKABAILA. Kwa maana hiyo misingi ya UBepari ni ipi na UKabaila ni ipi katika Tanzania ya leo.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom