One Struggle, Many Fronts. Forward ever, Backward Never... Tumeamua kuangalia mbele!

One Struggle, Many Fronts. Forward ever, Backward Never... Tumeamua kuangalia mbele!

Zitto ndani ya ACT umejipa nafasi ya Kiongozi Mkuu na Mkiti wenu hana mamlska yoyote ni kama ceremonial figure tu.

Watu wamekufananisha na Ayatollah unayetaka kumiliki ACT kifalme huku ukigombea peke yako nafasi hiyo.

Unazungumziaje hilo?
 
Last edited by a moderator:
Zitto maswali haya ni mepesi kuliko Azma yako ya kuwarudishia wananchi uchumi wao ulioporwa na wanyonyaji wa nchi hii, tafadhali tunaomba majibu....................
 
Safi sana brother Zitto kwa kuweka msimamo wa Kisera, hicho ulichokifanya ndo jambo la msingi zaidi.

Hata hivyo ili hawa wenye kuuliza maswali ya dhihaka nafsi zao zitulie unaweza kutenga muda ukawajibu.

Kimsingi issues ndilo jambo la msingi, character assasination na adhominen attacks wanazotumia wenye chuki kali dhidi yako ni siasa nyepesi sana ambazo kesho na keshokutwa zinapeperushws na upepo mkali wa hoja kuntu.

Kusema kweli, umejitofautisha sana na wanasiasa wa kimatukio, waumini wa siasa za maji taka.

Ni dhahiri hoja za ACT kuhusu kumkomboa mnyonge, ni kama chemchem ya maji katika jangwa, wananchi wamekata tamaa, uchumi wa nchi haumnufaishi mwananchi ipasavyo, deni la nchi linazidi kupaa, ubora wa elimu unazidi kuwa duni, Rushwa imekithiri, Wananchi wenye ulemavu wa ngozi wanauawa. Kiufupi tunahitaji dira na mwelekeo thabiti. Na pia tunahitaji viongozi ambao tunaweza kuwaamini na hatimaye kwa imani hiyo tukawapa dhamana ya kuongoza mapambano.

UKIAMUA KUSAFIRI KWA NGUVU ZA MIGUU YAKO YAKO HATUA KWA HATUA HUWEZI KUJALI MATOPE YANAYOKURUKIA.

Hizi kashfa, matusi na kejeli za baadhi ya watu, inaitwa hate and love relationship, Unakipenda sana kitu mpaka sasa unaanza kukichukia!, au vice-versa sometimes.

Kwa hiyo Brother wewe komaa tu, wananchi wanawaeleweni sana. na I hope mtakuwa kimbilio la wanyonge
 
Zitto ndani ya ACT umejipa nafasi ya Kiongozi Mkuu na Mkiti wenu hana mamlska yoyote ni kama ceremonial figure tu.

Watu wamekufananisha na Ayatollah unayetaka kumiliki ACT kifalme huku ukigombea peke yako nafasi hiyo.

Unazungumziaje hilo?

Mkuu Molemo Mpaka ukamilifu wa Dahari utapata jibu la hilo swali lako maana michelemichele nimingi sana kwenye hilo swala
 
Last edited by a moderator:
Tumeweka dhamira yetu ya kuondoa utawala wa ccm. Mtu yeyote anayekuja muda huu kutukwepesha kutoka kwenye lengo letu hili, hakika ni adui wa Watanzania. Sisi tunasema uzi ule ule, mpaka ushindi!!
 
umetangaza Mali zako na source take he Mali za chama na source take je
 
Zitto hivi bado unafikiria baada ya kuapa kuifuta CUF pwani, unaweza ukachonganisha CDM na CUF?? kweli unadhani wewe pekee ndo unaakili, jiulize kwanini CUF iliunga mkono ufukuzwaji wako, they also know the whole story behind you and your malicious tectonic movements, AIDS like moves.
 
Zitto

Maneno na matendo yako ni tofauti kabisa. Unayoyazungumzia kuwa ndizo sababu za wewe kuunda chama cha ACT ni tofauti na tuhuma kubwa ulizokamatwa nazo ulipokuwa CHADEMA na kupelekea kufukuzwa kutoka chama hicho.

Katika andishi lako ukiwa na team yako ie. Kitila na Mwigamba kuhusu mapinduzi ndani ya CHADEMA kinyume cha katiba ya chama hakuna jambo hata moja kati ya hayo uliyoyaorodhesha hapo juu lilikuwa kwenye andiko lile. Je, huoni kuwa wewe ni mwongo? Je, kama kila leo unakuja na jipya ukiamini Watanzania ni wasahaulifu, huoni kuwa ACT na CCM ni sawa na mwanaume mrafi wa ufisadi wa mapenzi (CCM) na nyumba ndogo yake (ACT)? au gari na spare taili?

Kama unania ya ukombozi na hayo mayagoyombwe ya kuongeza mashambulizi ya utitili wa vyama vya siasa ukitetea hoja dhaifu ya kuwa wengi kushambulia chama kimoja ukijificha kwenye mwanvuli huo ambao bado unakutanaibaisha ulivyo na mawazo kuwa una akili kuliko wengine jambo ambalo sio kweli hata kidogo, unaweza kueleza hapa Watanzania tukuaminije kuwa ulikosa nafasi ya kuishambulia CCM ulipokuwa CHADEMA ilihali wakati chama kilikuwa kikipanga mashambulizi dhidi ya CCM wewe ulikuwa unakwepa unafanya yako Kigoma, CHADEMA ilipokuwa Ruvuma wewe ulikuwa Arusha n.k Na ilitokea mara nyingi hadi tuliokuwa wapenzi wa CHADEMA tukaumizwa na tabia yako hiyo ya kukwepa harakati za ukombozi. Je, huoni kuwa unadanganya kuwa ulikosa fursa ndani ya CHADEMA bali kuna ubinafsi ulio nao baada ya kujiswahibisha maadui wa Watanzania CCM? Ukawa unashindwa kuwashambulia kwenye mikutano ya hadhara.

Baada ya matukio ya mauaji ya Watanzania wenzetu huko Soweto kwenye mkutano wa CHADEMA na maeneo mengine ya Arusha haukushiriki kabisa majonzi na Wana-Arusha ulikula kona ukauenda Dar sawa na wana-CCM waliokuwa walioendelea kufanya kazi za kibunge huku Watanzania wakiangamizwa na mabomu yaliyoratibiwa na wapinzani wa CHADEMA. Je, na katika hilo CHADEMA walikuzuia kushiriki matanga ya kinyama. Hapo ni kwa ufupi sana.

Kwa kutumia sylogism ya kawaida tu, hata mtu mwenye akili ya kawaida atagundua kuwa kamwe wewe sio mkweli bali unaenda na media publicity kupotosha wasio na taarifa za ukweli kuhusu wewe kuwa wewe ndiye umefanyia kazi ya kuweka hadharani ufisadi wa CCM ilihali hakuna hoja hata moja uliyoianzisha ukaikamirisha.

Kama kuna eneo lisilo na ukweli kati ya hayo machache sana, tupe ukweli unaoujua wewe kuhusu hayo.
 
Ben;
visit the libraries there is a book Ujamaa or African socialism by Abdulharman Babu (check spelling); Nyerereism was based on African/Tanzanian characteristics. Not communism or the way you want to point.

Nyerere was a believer; he was Christian. Communists don't believe in God.
Nyerere invited scholars to challenge Azimio la Arusha (Arusha Declaration). Remember an example. Millionaire anaweza kuwa mjamaa? It was debated long time; Nyerere came back and said A millionaire can be Mjamaa.

if Zitto will try to improve that white paper we had; for motivation I think Zitto is a leader who can lead us(maybe); let us give him time; he is still a young man.

We are looking for the Messiah to rescue the country; most oppositions have failed us we should not disappoint those who are emerging; I see light on Zitto.
Azimio la Arusha doesn't say so brother. Nitafutie Billionea hata mmoja ambaye sio bepari au kabaila na ambaye hafanyiwi kazi. hapo nyuma nimeweka maana ya Ujamaa kama ilivyoelezwa na Azimio la Arusha..

Mimi nadhani tukielimishana vizuri ndio watu watakueleweni kuliko kutoa majibu ya Mkato kumuondoa mtu.. Ni wajibu wa Ben kuuliza ili afahamu hii ACT ina malengo gani na Taifa gani inataka kulijenga.
 
Zitto,

Chama chako kimejipambanua na Unyerere (Nyerereism) na kufuata misingi ya Azimio la Arusha ambao unaamini mgawanyo wa haki katika raslimali za taifa na pia unaruhusu umiliki wa mali kama nyumba,biashara n.k.

Je, unawezaje kufuata ujamaa wa kidemokrasia wakati huohuo ukijipambanua na Nyerereism ambayo msingi wake ni Ujamaa wa Kikomunisti usioamini katika umiliki wa mali kama nyumba zaidi ya moja na kumiliki biashara ukiwa Kiongozi wa umma?

Endapo kungekuwa na maswali ya aina hii, JF ingekuwa darasa haswa la kutoa elimu

Maana kwa swali kama hili ata vijana walioko sekondary wanapaswa wachukue karatasi na kuandika notes, big up Ben Saanane.
 
Last edited by a moderator:
Zitto zilikuja kauli za kukutuhumu kuwa ulianzisha chama ndani ya chama huoni kuwa umedhibitisha hili ulipoamia ACT na kupewa uongozi wa juu kwa muda mfupi? Unasema adui ni mmoja, huoni kuwa kuanzisha ACT inatupunguzia kura za kumwondoa CCM madarakani? Ni upinzani gani unajenga wa kubomoa upinzani na kuimarisha CCM? Unazungumziaje UKAWA na nguvu ya kuindoa CCM?
 
Naomba pia unijibu suali la Msingi kwani siku moja Juliana Shonza alipata kuandika kua mapato ya ACT anajua chanzo chake hivyo vijana wa ACT wasiseme chochote kile kwani atawalipua, je ni kweli Mwanachama wa CCM anaweza kuyafaham kwa ufasaha mapato ya ACT?

Sasa unategemea Zitto akujibu nini kwa swali la Juliana?kwani Zitto ndio Juliana?jamani tuwe tubafikiria mambo mengine.

Hivi Kapwela akisema Dj-kobo ni mpuuzi itakuwa sahihi mtu akurupuke huko akuulize eti Djkobo tuambue kwanini Kapwela kasema wewe ni mpuuzi?kweli?

Hilo swali ulipaswa umuulize Juliana na wala sio Zitto, kuhusu pesa za chama Zitto kasema yake kuwa ni michango ya wanachama.Hayo ya Juliana ulipaswa umuulize Juliana.
 
Zitto utarejeshe miiko ya uongozi kwa kuigiza orodha za mali zako? kama ili ulotia saini? wewe ni mjamaa aliyefaidika tayari una ubepari mashamba kila kona ya nchi, Huoni hizi danganya toto zitakukwama shingoni siku ile ikifika, sanduku la kura nje nje? UELEWA WA TZ LEO sio ule wa kujidanganyisha kama tetea
 
Asante kwa majibu yako, hata hivyo swali langu la kwanza hukunijibu. Niliuliza kwa nini mashabiki wako wengi ndani ya jukwaa hili ni manazi wa CCM?
Dah...hivi hili nalo swali?Zitto atachaguaji humu ndani nani wa kumshabikia?usichojua hakuna mshabiki wa CCM anayempenda Zitto wala Chadema.Bali kama anavyosemaga Ritz wanachochea kuni mbaki mnapigana wenyewe.Ndio furaha ya CCM.

Sasa kama kila mkienda kwa kupelekeshwa na ya CCM mtabaki mnagombana kila siku.Angalia hao CCM unaosema wanamsifia Zitto ilipofika hoja ya ESCROW haohao walikuwa wanamtukana humu.

Mpaka mtakapoweza kujisimamia na kutopelekeswa ata na vitu vya kitoto kama hivi ndipo mtaweza kusimama kama chama.
 
ZZK alieza hapa chanzo cha kipato cha chama kwanza kabla hamujaeleza kipato cha viongozi wa ACT, Kuanza kueleza chanzo cha mapato kwa viongozi wa chama bila kueleza chanzo cha mapato ya Chama ni ujinga na upuuzi ujue hili watanzania wameamka na kuelimika
 
fikirikwanza

Siasa ni mapambano. Siwezi kuacha mapambano. Sijawahi fanya usaliti wowote. kuitana majina hayo hakusaidii lolote zaidi ya kufurahisha ego zetu tu. ACT Wazalendo ina shabaha moja tu nayo ni kupambana na mfumo wa uchumi unaonyonya watanzania. Ku surrender mapambano hayo ndio usaliti. Tutaendelea kupambana

Zitto my insperational personality ever since. I wish I could believe you. Shida yangu nilikuamini sana, na unachosema sasa ni tofauti kabisa na watekelezaji wa chama chako wanavyofanya. Angalia kuanzia asubuhi hadi jioni wanapost nini mitandaoni na wanasema nini ni kutukana viongozi wa Chadema na Kuishambulia Chadema, angalia wanachama ambao wanajiunga na ACT 99% wanatoka Chadema. Hiki Chama chako umekianzisha kuwa confuse watanzania kipindi hiki muhimu cha uchaguzi? Na kwa maslahi ya nani? Ni kwa maslahi ya mabadiliko kweli?
 
Last edited by a moderator:



4. Sisi ACT Wazalendo tutachochea kuni kuwasha moto wa mapinduzi nchini kwa kuendesha siasa za masuala (issues). Tumeanza ziara yetu mkoa wa Ruvuma kwa sababu ni mkoa ambao wabunge wake wote ni CCM. Tutaweka nguvu sana maeneo hayo badala ya maeneo ambayo tayari vyama vingine vya upinzani vina nguvu. Sisi katika ACT wazalendo tunataka kuona uchumi unarudi kwa wananchi wenyewe badala ya uchumi kushikiliwa na watu wachache.



Zitto

Unamatatizo gani? au una umwa usahulifu?
why you don't practice what u preach?

ni Jana tu kwenye hot mix umesema unataka Ubunge kawe au Ubungo. Leo unasema kwenye upinzani ACT haihendi na haitaki kupambana na wapinzani, sasa ubunge kawe na Ubungo hiyo so vita umetangaza kiongozi mkuu we ACT dhidi ya CDM.

by the way kwa mini ukimbie kigoma kaskazini? au no kwasababu ya kura kupingua na madiwani kupungua sasa umeamua kuwakabidhi jumbo CCM.
 
Last edited by a moderator:
  • Thanks
Reactions: BAK
Sehemu ya kwanza ya swali lako nimeliuliza naona Mh. Zitto ameamua kunipotezea....

MwanajamiiOne, unatambua kuwa Zitto alisimamishwa Chadema na alikuwa afukuzwe uanachama takriban mwaka mmoja uliopita.Sasa kwa akili zako kubwa Mwanajamiione unataka kusema ulitegemea kuwa Zitto mwaka wote huo alikuwa amekaa tu anasubiri majaliwa ya mahakama ambayo mwisho wake ungekuwa June mwaka huu?please tusijidharirishe hivi.

Ni mtoto mdogo tu ndio atakayedhania kuwa Zitto mwaka mzima aliokuwa hatakiwi Chadema basi alikuwa amekaa, hana option na hana wazo mbadala, angekuwa ni mtu mjinga sana kama angefanya hivyo.
 
Swali kwa Zitto, Hoja ya Escrow ilikuwa yako au ya Kafulila? Maana nimesikiabukibeba utukufu wa hoja hiyo as if ni yako,

pili lini majina ya walioficha mabilion uswizi utawataja au bado wapelelezi wako binafsi wa Uk na uswizi hawajamaliza kazi.?

Shardole huku nyuma ulikuwa unatumia sana kichwa chako, sijui kimekupata nini Shardole.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom