One Struggle, Many Fronts. Forward ever, Backward Never... Tumeamua kuangalia mbele!

One Struggle, Many Fronts. Forward ever, Backward Never... Tumeamua kuangalia mbele!

Naomba pia unijibu suali la Msingi kwani siku moja Juliana Shonza alipata kuandika kua mapato ya ACT anajua chanzo chake hivyo vijana wa ACT wasiseme chochote kile kwani atawalipua, je ni kweli Mwanachama wa CCM anaweza kuyafaham kwa ufasaha mapato ya ACT?
 
Sawa mkuu, lakini challenges bado ni kubwa, msitegemee kuona mabadiliko kwa usiku mmoja.
 
Zitto;

Mkuu umejibu vizuri, lakini kusema kuwa hampimi umakini wa Upinzani kwa kuwekwa ndani utakuwa umefumbia macho siasa za Africa ama hutaki kuamini kinachoendelea, na hapo sitaki kusema lolote, DP ni chama cha mtu mmoja na hakijawahi kwenda public, REV. anafanya siasa za ki intellectual ndio maana anawakera wakubwa wenzake lakini uraiani haonekani..is the man of his kind....Respect to him.

Mkuunakuhakikishia kuwa mtakapojipambanua kuwa kweli nyie ni wapinzani na mnataka kubomoa mahekalu ya CCM ndio utakumbuka huu uzi hapa JF....Unless isiwe Africa ninayoijua mimi
Kuhusu majimbo na kwamba ningesubiri ndio nitoe maoni yangu ni kuto utendea haki ubongo wangu, na hivyo kutilia mashaka mkakati wenu kama chama dhidi ya wapinzani wenzenu.

Out of the topic but valid, mmesema mtaweka wagombea nchi nzima, swali, pesa mtatoa wapi, vipo vyama vinapata ruzuku ya hadi milioni 69 lakini haviwezi kufanya hivyo, nyie fedha mtapata wapi ikizingatiwa mmezungukwa na wanaharakati wa wakawaida wengine hata kazi za kueleweka hawana?

Ni hayo tu mkuu Zitto# All the best.
 
Last edited by a moderator:
Lengo langu na wenzangu siku zote limekuwa hilo. Kama tumekoseshwa jukwaa la kupambana, njia nzuri ni kutafuta jukwaa lingine. Tunapambana kupitia ACT Wazalendo

Ha ha ha.. Yaani jibu lako lime-sum up nia ovu mlio nayo kwa kushirikiana na ccm.. Kwa hiyo njia nzuri ya kuisaidia ccm ni kuvuruga upinzani na kutengeneza chama kingine kwa minajili ya kugawanya kura za upinzani..! Kwangu mimi wewe ni msaliti wa mageuzi na mbinafsi..
 
Tumeshaonya wanachama wetu wote kutoshambulia chama chochote cha upinzani. Walikuwa wanachokozwa na wao kujibu mapigo. Hata hivyo haina tija na tumeamua kuwa hata tukichokozwa tunasema " tumeshapiga mstari. Forward ever backward never". Hatutachokozeka tena. Kazi yetu kueneza Sera za ACT Wazalendo

Asante kwa majibu yako, hata hivyo swali langu la kwanza hukunijibu. Niliuliza kwa nini mashabiki wako wengi ndani ya jukwaa hili ni manazi wa CCM?
 
Naomba tutulie na tuulize maswala ya msingi kwani, katika siasa tunatakiwa kua na mitazamo tofauti yenye lengo moja baadae
 
Nikupongeze mkuu zitto kwa kutenga muda wako na kuja hapa jukwaani, hii inaonyesha kuwa unaijali jf na members wake wote, HONGERA KWA UAMUZI HUU.
kupitia uzi huu naamini baadhi yetu tutajifunza mengi hasa ukiendelea kujibu baadhi ya maswali ya wana jukwaa
 
Zitto hiyo slogan yako ya many fronts, one struggle kutoka kwa Baba wa Africa Nkwame Nkurumah inapingana mbali sana na struggle za chama chako ACT, chama chako pamoja na wafuasi wako kazi yao kuu ni kupambana na CHADEMA na sio CCM,

Mnachokisema na mchatotenda ni tofauti kabisa, mjejidhatiti kupambana na upinzani CHADEMA lakini kwa bahati mbaya sana mmeshachelewa, mnajifanya mnapigania uwazi na uwajibikaji as if CHADEMA hawapiganii hivyo hizo zana!

Shame to you all traitors.
 
Last edited by a moderator:
ACT Tanzania ndio ACT Wazalendo. Baada ya kufanya tafiti kwa wananchi ilionekana wananchi wanataka chama kitakachowarejeshea uzalendo kwa Taifa lao. Wananchi wengi walishauri iundwe Chama Cha Wazalendo. Hivyo tukaboresha jina letu kwa mujibu wa katiba yetu na kuitwa ACT Chama cha Wazalendo

Wazalendo - perfect and sounds well; discard ACT.
Wazalendo goes well with Charisma
 
Zitto mbona nimapema sana wewe kuingia nakupewa madaraka makubwa je ule usemi wa kua ulikua unaanzisha chama ndani ya chama si ndio imetimia? Mbili mapato makubwa ya ACT ni yapi?
 
Sina hamu na vyama vya upinzani tena na wanasiasa vijana kama wewe. Zitto sina hata cha kukuambia kwa kuchangia kutucheleweshea maendeleo kwa kuitoa CCM madarakani. Kipindi niko Buly kuna mashine moja chini ya mgodi tuliibatiza jina Zitto Kabwe lakini naamini kila mtu anajuta kukuamini,anyway tumehamishia matumaini kwa Lowassa ili ndoto zako zitimie.
 
Zitto mbona nimapema sana wewe kuingia nakupewa madaraka makubwa je ule usemi wa kua ulikua unaanzisha chama ndani ya chama si ndio imetimia? Mbili mapato makubwa ya ACT ni yapi?

Mbowe alipewa madaraka kipindi gani?
 
Swali kwa Zitto, Hoja ya Escrow ilikuwa yako au ya Kafulila? Maana nimesikiabukibeba utukufu wa hoja hiyo as if ni yako,

pili lini majina ya walioficha mabilion uswizi utawataja au bado wapelelezi wako binafsi wa Uk na uswizi hawajamaliza kazi.?
 
Last edited by a moderator:
Kwenye cheo cha kiongozi wa Chama uligombea peke yako, lakini wakati uko CDM ulishawahi kutangaza kugombea cheo cha KUB huku ukijua kiongozi wako wa Chama nae yuko bungeni, huoni kama hizo ni dalili za mtu mpenda madaraka?
 
Tutaweka ilani yetu kwenye tovuti ndani ya siku chache

Shukrani,nitasupport chama chenye ilani ya kumuondolea mzigo mwananchi na kukipigia kampeni sehemu yeyote endapo kitaondoa kodi kero zisizokuwa na kichwa wala miguu kama kitashika madaraka.

Kodi Kero hizo ni:-

1.Service Charges za Umeme za kila mwezi,Kulipa EWURA na REA.

2.Kulipia Road License(TLB) kila mwaka na hapo hapo unakatwa fedha ya kuchangia barabara ukinunua mafuta,hapo hapo serikali imeshapata kodi kwenye hayo mafuta.

3.Kulipia Fire Extinguisher kuanzia Sh 10,00/= na kuendelea inategemea na cc ya gari bila kupewa mtungi huo uliolipia.

4.Bima ya Gari ipunguzwe hii Third Party ni Kubwa Mno.

5.Kuwe na Limit ya Kuchangia Kodi kwa mtu kama ilivyo USA,Ukilipa kodi ikazidi kiwango unarudishiwa ile iliyozidi,Huku kwetu Unakatwa PAYE,Unakatwa VAT(indirect) hapo hapo ukiagiza kitu nje hakuna unafuhu hata kidogo yaani mmachinga asiyelipa kodi na mfanyakazi anayekatwa PAYE kila mwezi wakiagiza magari wote wanakatwa kodi sawa wakati mfanyakazi ameshachangiaa PAYE nyingi na hana msamaha wowote.

N.B Serikali ina vyanzo vingi vya mapato kutoka kwenye mali asili(Misitu,Bahari,Madini,Gesi),Sisemi kwamba serikali isikusanye kodi kwa mwananchi la hasha bali iondoe kodi kero.
 
Back
Top Bottom