Ole wenu CHADEMA!

Mzee Bob,

Maneno mengi unayosema hayana ubishi na ninaamini kijana JJ anahitaji watu kama wewe ili kuwa na giudance, maana hata hawa jamaa wa Mtandao pamoja na hela zao zote walizonazo, wanaelewa one thing very clear kuwa wasingeweza kuingia madarakani bila ya kuingia through CCM!, pamoja na vitisho vyao vyote kuwa wasingeshinda wangeingia Chadema, walijua wazi kuwa hawakuwa na ubavu wa kushinda nje ya CCM, sasa hivi chart yao imeshuka kwa sababu wananchi wajanja tayari wameshagundua kuwa hawana lolote, ni wale wale tu!

My point ni kwamba JJ sina uhakika kama ni kiongozi, lakini ninajua kuwa anayo skill muhimu ambayo inahitajika sana na upinzani bongo, nayo ni kwamba anaweza ku-communicate na wananchi, skill ambayo ni tatizo kubwa la mfanya biashara Free, sasa ni afadhali kuwa na kiongozi kama yeye ambaye angalau mnajua kuwa anaweza kuwaelimisha wananchi au wapiga kura, na pia anayeweza kuaminika na wapiga kura hata kama hana skills zingine hiyo moja inaweza ku-cover asizokuwa nazo, na the fact kwamba bado ni kijana!

Mzee Kimbembe,

(1). Acha hasira bro! tulia it is only politics halafu there is another day kesho, mimi niko hapa kama mwananchi yoyote yule anayeweza kuamua kuja hapa na kuijadili nchi yake, na kama tulivyosema toka BCS kuwa sio lazima wachangiaji wote tuwe wapinzani ndio demokracy iwe at work, HAPANA! Mimi ni mwananchi kama wewe na sio lazima niwepo hapa sasa kuwa muangalifu na maneno yako ya siasa za uchochoroni ambazo tumezisikia bongo for the last 44 years na hakuna lolote, kama una hasira kiasi hicho tafuta uongozi au nafasi ili ukatoe hasira zako, I got nothing to do na frustrations zako bro, kwa hiyo unapoandika andika kwa heshima kidogo, kumbuka kuwa wote tuko hapa kwa hiari!

(2). Umsema kwa nini wazee wa CCM, kina Kingunge na JM walikuwa wanamsakama Free, unajua nitarudia tena hili once and for all hawa wazee wawili they make their living kwa kuwashambulia kina Free politically, ni kazi ya JM kuuuwa upinzani kama ilivyo kazi ya makamu wa upinzani, unless hawaelewi wajibu wao kisiasa, halafu ninarudia tena kwenye vyama vyao hawa wazee na wengine they can say and do anything they want, ni matatizo ya vyama vyao sio taifa, kwa hiyo kama JM anasema ma-DC watafukuzwa au watanyongwa no body should lose a sleep ni matatizo ya ndani hayahusu taifa, kwa hiyo I could crae less what they do kwenye vyama vyao mpaka wakiingilia taifa!

(3). Kijana ngoja nikufahamishe, katika siasa za kila nchi kuna majina ambayo ni dominant na hata ufanye nini huwezi kukwepa ukweli, huwezi kuongelea Kenya bila Tom Mboya, huwezi kuongelea Zambia bila Vernon Mwanga, huwezi kuongelea Malawi bila Chiume, huwezi kuongelea Mozambique bila Gaubeza, sasa huwezi kuongelea siasa za bongo bila ya JM. Yes ninamuongelea maana influence yake katika siasa yetu ni kali kuliko unavyoafikiri, leo viongozi wote wa serikali na CCM, ni mawili either ni wa kambi ya JK au kambi ya JM, hakuna wa BM, hakuna wa Mwinyi, hakuna wa Mwalimu, hakuna wa Karume, I mean kwa huku bara! Sasa liking him or not haibadili ukweli na originally kambi ya JK imetokea kwa JM mpaka pale 1995 ndipo JK, RA, EL wakaanzisha Mtandao, lakin kwa kumuheshimu hata wakati wa uchaguzi at one point JK alimu-offer kumuachia one term ni kwa sababu ya kuelewa kuwa no matter what huyu mzee utakuta mkono wake na nchi haitawaliki bila ya kuwa naye sawa, huo ni ukweli Mwinyi aliukubali, Mwalimu aliukubali, BM na ujeuri wake wote aliukubali, na sasa JK ni yale yale, ndio maana Mtandao sasa hivi wanapigana sana yule mtoto wa JM kule NY, arudi ili aingie kwenye siasa kwa kuamini kuwa itamfanya huyu mzee aachie ngazi au ataweza kumshawishi aachie, sasa ukiamua kunichukia kwa sababu ninaishi kwa ukweli wa siasa ya bongo siwezi kukusaidia,

unajua ndugu yangu the man ni so influencial, yaani hata kuweka baraza kubwa la mawaziri ni ok yake tu ndiyo iliyoamua uamuzi wa mwisho bro! Sasa ukinichukia unanionea hiyo ndio siasa ya nchi yako, tena siasa ya mika 44 ya uhuru, sio chini ya mzungu! Ni chini ya wabongo kama wewe na mimi!

(3). CCM ilishinda kwa kura 80%, reaction ya viognozi wote wa upinzani ilikuwa kwamba wananchi ni wajinga, hawaelewi, I mean hata ukiiba kura huwezi kuiba 80%, halafu kama ni kweli wananchi hawamtaki JK, then wasingekuwa wanajazana kiasi tunchakiona kila anapopita bro!, huko NY bro ilikuwa mshike mshike pale ubalozini wananchi wanataka kumuona tu! Ndugu yangu sema mengine ila ya JK na wananchi asjie akakudanganya ntu, njo huku bongo uone anapoingia mahali uone wananchi wanavyopigania kumuona tu! Halafu jama unajua kama ana uchawi hata nje ya nchi, akingia mambo ni yale yale tu, I mean huo ni ukweli regardless ya uwezo wake kikazi ila kwa mvuto hakuna mfano bro!

Unjua kwa kumliaza kama kuchangia kwangu katika mada kunaashiria kuwa nimetumwa na CCM kuja kuandika, au itakuwa ni sababu ya wanaoona tofauti kufikiri kuwa njia ya kutoa hasira zao za kuitukana serikali ni kunirushia ujinga, ninasema HAPANA na nitawajibu kwa lugha ya fedhuli mno kwa sababu ninaiweza, mimi ni mwananchi kama wewe tena waya wa bongo ulishanifanya mpaka ni-risk maisha yangu na kuzamia meli za Wagiriki enzi zile za waya mkali, kwa hiyo kama unafikiri unaielewa hali ya bongo kuliko mimi bro, unajidanganya ila inafikia wakati inahitajika kuenda na wakati huku tukitafakati reality!

Shukrani!
 
Ukisoma vizuri maoni ya Mzee ES, utajua Tanzania ina watu wa fikra za namna gani, na utajua kwa nini hatuendelei. Viongozi wengi tulionao,, na wanasiasa wanaotamba sasa wana fikra za aina ya ES.

Binafsi simjui, lakini mawazo yake yanatosha kunieleza mtazamo wake. Bila shaka, kwa mawazo haya amewaharibu wengi. Sijui kama ni mzee au kijana. Kama ni mzee haoni mbali. Kama ni kijana, bado ana muda wa kujifunza. Akubali kufungua pazia machoni pake, akubali kuchungulia nje ya dirisha. Ataona mazuri mengi ambayo hakuyajua kabla!

Watanzania wanajua kilichotokea katika uchaguzi. Walijua kabla ya uchaguzi. Wanajua mfumo uliotumika. Hawakuwa na madaraka nao. Ni wafungwa. Ni watumwa wa siasa zao wenyewe.

Wanajua kilichowasambaza vigogo wote wa CCM nchi nzima katika wiki ya mwisho wa uchaguzi. Wanajua makada wa CCM waliofunzwa 'mbinu za kushinda uchaguzi' katika cha usalama wa taifa, mkakati uliosimamiwa na Mkapa, Malecela, Mangula na Bosi wa Usalama wa Taifa, mapema kabisa hata kabla ya mgombea kupatikana.

Bwana ES, kama ni mwana CCM, wenzake wanamficha mambo mengi. Au anayajua lakini anakufa nayo kwa sababu ana maslahi binafsi.

Anajua yaliyotokea Karagwe? Uhuni ambao haupaswi kuhusishwa na watu wanaojitambulisha kuwa ni waungwana wa kisiwa cha amani! Anajua Mzee Kahama alikuwa anasindikizwa na FFU kuwatembelea kina nani, na aiwa amebeba nini usiku wa kuamkia Desemba 14, 2005? Anajua mkakati wa kununua shahada na vituo feki vya kupigia kura?

Anajua kwamba vyama vingi, CHADEMAM kikiwamo, havikuwa na wawakilishi kila kituo, wakati CCm kilikuwa nao na kiba pesa ya ziada ya kuwapa hata wasio wake? Anajua kuwa katika kujumlisha matokeo ya vituo ndani ya kata, hakukuwa na wawakilishi wa chama?

Hakuhusika katika kufunzwa namna ya kuwapigia kura wasiojua kuandika au kusoma?

Hakujua matokeo ya ghiliba za Mkapa na dola nzima, kuwatisha ananchi kwamba wakichagua upinzani yatawapata makubwa? Anadhani vilipotea hivi hivi? Hajui nguvu ya maRC na maDC walioamrishwa na Mkapa, kwamba hatasubiri vikao kuwashughulikia iwapo watapitisha wagombea wapinzani?

Hakujua nguzu ya kipesa ya CCM na jinsi ilivyotumika kueneza propaganda mbovu za kichawi dhidi ya upinzani? Hakujua kwamba tangu Tanzania iwe huru hakuna mgombea urais aliyetangazwa kama Kikwete katika nchi nzima?

Hajui ghiliba zilizowapata watu kama Lwakatare hadi siku yenyewe ya kupiga kura?

Tukirejea kwa Mbowe, mze ES hakujua hadhi na uwezo wa CHADEMA kabla ya uongozi wa Mbowe? Hakujua udhaifu wa chama kimtandao na kimkakati - kwa sababu nyingi tu?

Anapuuza nguvu ya ubunifu na ufundi wa kampeni uliotumiwa na chama kidogo kama CHADEMA kukua na kuleta msisimko nchi nzima kiasi cha kutajwa kila kona na wana CCM - bila shaka kwa hofu? Anadhani hofi hiyo imekwisha?

Amefanya utafiti kujua maoni ya watanzania leo kuhusu CHADEMA? Amekwenda Ubungo, Kawe, Kibaha, Karagwe, Muleba, Hai, Vunjo, Bukoba Mjini, Muleba Kaskazini, Shinyanga Mjini, Songea Mjini, Mpanda Kati na kwingineko kujua kilichotokea?

Anajua kuwa ufafanuzi wa Mbowe kuhusu sera ya majimbo ndiyo unashika gumzo kichinichini sasa, baada ya watu kutafakari sasa? Na anajua moto utakaowaka?

Na kuhusu Kikwete. Mzee ES anajua kwamba huyu jamaa ni Machiavellian wa kutisha? Ampe muda.

Lakini zaidi, wengi tunasahau kwamba nchi yetu haina Usalama wa Taifa. Tuna usalama wa rais! Mambo mengi ya kipuuzi yanayofanywa na viongozi wetu dhidi ya wananchi wake yasingefanyika kama tungekuwa na usalama wa taifa. Tunahitaji kulitafakri hili.

Na tataizo jingine la mzee ES, anapenda - kama walivyo wengi ndani ya CCM, labda ikiwa ishara ya uchovu na kuishiwa - kujadili watu badala ya masuala. ndiyo maana anashindwa kuona suala katika hoja ya Sumaye.

Maskini ES, hajui kwamba Kikwete alijiandaa miaka 12 iliyopita, na amekuwa akinusa wanaotaka kuwania urais na kuwabomoa kupiia vyombo vya habari ambavyo pia amevitumia kwa muda wote huo bila watu kujua!

ES hakumbuki kashfa ya Sumaye kutumia milioni 500 katika ziara moja nje ya nchi (Marekani na Ulaya) miaka kama minne iliyopita? nani alimpangia ziara hiyo? nani alimpangia watu wa kuandamana nao? Nani aliwalipa posho? BIla shaka ES anajua wizara husika! Na nani alipeleka vielelezo kwenye gazeti la RAI? Anajua mchango wa gazeti hilo kwa JK?

Kama ES hajui mnyukano wa chini kwa chini ya JK na Sumaye kwa miaka kama mitano iliyopita, basi yu CCM nusu nusu!

Na sasa je, ES anajua kwamba JK amelinunua gazeti hilo kwa kuwekeza ndani ya Habari Corporation asilimia 70 kwa mgongo wa Rostam Aziz? Berlusconi mpya!!!

ES anajua jinsi CCM wanavyomalizana, si kisiasa tu bali hata kwa kutoana roho? mambo mengine ni very sensitive bwana, lakini vi vema kizazi hiki kijisafishe.

Kuhusu magazeti, ES ni wa kuogopwa. Pamoja na miaka 14 ya demokrasia - tunazungumzia diversity na plurality - mwenzetu anafikiria kufutia magazeti. Wanaojua, wanayatetea hata yale ya udaku. Yana mchango wake.

Na kama Watanzania wangejua umbumbu wao unaendelezwa na nini, ni haya magazeti ya udaku, yasiyoandika issue bali personalities, na wansiasa wanayapa mtaji ili yaendelee kuvuta hisia za wananchi, wao wavurunde wasiandikwe, ili wakifika wakati wa uchaguzi, wananchi wasiwe na ufahamu mkuvbwa wa masuala yanayoendelea, wasubiri kugawiwa fulana na kofia, na kutishwa kwamba wakichagua upinzani watakuwa kama Rwanda na Burundi!

Lakini magazeti makini yote yametekwa na JK sasa. Na sheria mbovu zinazotawala uandishi na uchapishaji nchini ndizo zinawamaliza kabisa waandishi, wanabaki kuogopa kushitakiwa...wanaufyata, wanaanza kujikomba ka watawala, nchi inaliwa!

Mdomo pekee uliobaki wa wananchi kusema mambo yao ni Tanzania Daima. Wanaliogopa Tanzania Daima ndi hao wanaomulikwa nalo. Huwezi kusoma uchambuzi wa gazeti hilo, hasa wa Jumapli, ukalibeza. labda kama upeo wako msomaji ni hivyo hivyo, hobela hobela!

Upeo mdogo wa Bwana ES nimeuona zaidi katika kujadili uhusiano wa Mbowe na viongozi wa CCM! Ana akili ka ya Mrema, ya kudhani mtu unayetofautiana naye kisera hupaswi kukaa naye, kufanya urafiki, kusaidiana naye katika masuala ya kifamilia hata kibiashara. Kizazi cha kina Mbowe kiko tofauti, kinajua mipaka hiyo. Wahafidhina wanazubaa, wanashangaa, na wanapotosha hata kwa mambo madogo.

kumbe ndiyo maana watu walishangaa kuona anamkumbatia Kikwete baada ya matokeo kutangazwa! Bado tuna nji ndefu.

Mwisho, akubali kwamba kilichoandikwa ni kweli. Kinamkera kwa sababu mpango wao umejulikana. Lakini kabla ya Mbowe CCM imewafanyia wengi uhuni huo. Kumbe hajui kwamba dhamira ya kwanza ya JK kummaliza Mbowe ilijadiliwa waziwazi Songea alikokuwa amealikwa kuwa mgeni rasmi siku ya Ukimwi duniani, Desemba 1, 2005? Sisi tunajua.

Hajui kwamba hata katika kikao cha juzi cha NEC - kwanza hata katika kamati ya maadili ya CCM - JK alianza kwa kukataa uwepo wa mtandano ndani ya CCM, akasema haya mambo yanasambazwa na wapinzani kina Mbowe ili CCM ionekane imegawanyika? Hajui? Sisi tunajua.

Hajui kwamba baadhi ya wajumbe wa NEC wamekerwa na maneno hayo, kwamba rais ajielekeze kwenye hoja ya mgawanyiko ka sababu upo, na kwamba Mbowe hahusiki? Sisi Tunajua.

ES hajui, kwa sababu nilizokwishataja hapo nyuma, kwamba JK anamwogopa Mbowe kisiasa? Hajui siasa zilizvyo? Hujuma kupitia vyombo vya habari, usalama wa "taifa", wakuu wa mikoa, na umafya wa kizamani dhidi ya upinzani kupitia tume ya uchaguzi vitaendelea kuwalinda wenye madaraka? Anadhani Watanzania hawataamka hata siku moja, bali wataendelea kuhatamiwa kama mayai?

Sisi hatudhani hivyo. Na hatuko wachache, wala dhaifu kiasi hicho. JK anajua. Ndiyo maana ananekana kujali, na hata kutumia baadhi ya mambo ya Mbowe (jambo linalokubalika kisiasa) kjijenga. Na huwezi kujijenga bila kubomoa washindani wako. Na katika Bara, hana mshindani zaidi ya Mbowe.

Tusisahau pia kwamba hata kama si lazima Mbowe awe rais, tunaweza kumtumia Mbowe kulijenga taifa. Kwanza aijenge CHADEMA kama taasisi halafu atumike kwa sababu yupo, na anataka. Hata kama tunataka kuwajenga wengine, kina JJ, Zitto, wewe na mimi na wengine, hatuwezi wala hatupaswi kufanya hivyo kwa kumbomoa Mbowe. Hiyo itakuwa ni mbinu ile ile, chafu ya CCM kupitia kwa watu wanyonge wa kuwaza, kutafakari na kuchambua.

Sisi hatutakubali kutumika
MAN
 
Kwanza kabisa I salute you Ansi
Umetoa mwelekeo mzima ambao mimi niliusema kwa kifupi lakini ujumbe huy Es aliupata kwamba what I meant and what I was telling you people .Es katika hoja zake kadhaa nilisha mjua kwamba si mwanasiasa wala si mzalendo kama anavyotaka tumuone pamoja na kuja hapa na habari zake nusunusu tu za ukweli anazikataa nayuko tayari kufa na mtu.Ansi umesema ukweli huyu jamaa ana mawazo ya kizamani na watu wake ni wa zamani kama JM ndiyo kila kukicha yeye na Malecela Malecela Malecela kama vile bila yeye hawezu kuishi .

Es nieweshe juu ya kijana wa Malecela wa US anafanay kazi gani kule ? Maana habari ninazo na ninashangaa sana unapo mlilia kuja kutuka kuchukua madaraka .Mnaifanya CCM kuwa na Kifalme mnapeana na mnadhani sisi Watanzanai tuko chini ya Mfalme CCM.Mnatuletea hatari kubwa kweney Nchi yetu sisi wazalendo .

Tanzania inaenda pabaya mno kwa ajili ya watu kama JM .Wamezeeka lakini wanataka tuu kufa na madaraka kwa upuuzi kama huo wa kukaa usiku kucha nakweney vikao wanalia na mgombea binafasi .Es hapendi kabisa wagombea binafsi maana kwa mawazo haya na vile takrima haipo basi unaweza usiwe Mbunge kama kweli wewe ni Mbunge maana mawazo yako ni ya siku za nyuma sana kwenye siasa za sasa .Kifo cha CCM cha haraka ni kuwa na Mgombea binafsi na Mbowe kuijenga Chadema imara .

Ansi mimi nataka nikuite Answer maana umesema ukweli ambao wengi wa wana forum hawaoni ama wana uona ila wanaogopa kumwabia ukweli huyu jamaa .Si vyema sana kulia na mtu hapa lakini ninakufa na wewe kwa kwua natakaa ku clear air kabla hujafua kila kitu kwa kutuuzia mawazo ya ukandamizaji .Magazet ya Mengi kuimba na JK hata akipiga chafya ndiyo ya maana lakini wale wasemao ukweli juu ya Serikali ya CCM nk unasema yafungiwe jamani ama kweli Siasa hizi .

Umewataja King makers wote wa Africa toka Nchi ambazo CCM inawashikaji huko na demokrasia yao ni ndoto kama ya Tanzania umeacha kuwataja wale wa Nchi za Demokrasia.Unataka sisi ama Magazeti yahoji Wabunge kupewa 40m maandishi yatafanya nini na kwa nini wewe kama ni mkweli una uchungu na kama kweli ni Mbunge usiulize huko Bungeni ama uende Maelezo uitishe wana habari na uanze kuongelea swala hili na wengine waanzie hapo ?? Huu ni unafiki , uzandiki na si uzalendo .

Kama wajua issues kibao ambazo zinamuumiza mtanzania una uhashidi kwa nini usiamue kusema wazi badala ya kuulinda mkate wako na utake waandishi wasema wakauawe maana kwa tabia hii naamini chini ya JM wako tayari kuua kuliko kusemewa ukweli .

Tubadilike tuweke maslahi ya Taifa mbele tuachane na akina JM ambao hawana nia ya kumkomboa Mtanzania na waoga wa mapinduzi ama mageuzi ya kweli .Najua hapa pana ukweli juu ya CCM yenu na Mbowe lakini tutasema na tunangoja kuona .

Hoja ya ushindi wa CCM ndugu Ansi umetaja maeneo machache tu lakini yako mengi ambayo CCM walicheza rafu .Arumeru Mashariki CCM walitaka kumuua Mgombea wa Chadema baada ya kumshinda kwa maoni Mgombea mwenzake ndani ya CCM lakini akanyimwa akaamua kuingia Chadema basi ikawa balaa .Kwa nini JM na kundi lako wewe mnafanay Siasa kuwa uhasama ? Hata kama anaishi kwa Siasa lazima mfikie hatua ya kuleta chuki na kujenga uadui miongoni mwa wananchi kisa njaa zenu na madaraka ?CCM ni wachafu wanatumia vibaya madaraka .Na nasema JK karibia ataanza kutumia vibaya vyombo vya dola maana hataweza ku deliver na watu watajenga hoja hapo atakuwa kama Mkapa.Ndiyo maana Mahita alisema ukweli wake na CCM wako kimya kumgusa maana wanajua anayajua mengi na kahakikisha wanapata Ushindi wa 80% leo mnapiga kelele jamani sisi si wajinga ila tuna angalia tu.Kumbuka Myahundi alishindwa kuning'iniza buyu la pesa langoni baada ya miaka 100 na CCM iko siku tutawafanyia kweli na kuwaburuza Mahakamani kw auovu huu .
 
vijana wa chadema punguzeni Munkari!!!

Ni kweli CCm ina makosa yake ya hapa na pale lakini kusema JK hakubaliki mfano Musoma je ni kweli?
Ila hata Chadema kama chama kina kasoro(ref wabunge wa viti maalumu na etc) zake tena zinatakiwa kurekebishwa mapema ili chama hicho kiimarike na kuweza ktuoa chagamato!!

Kitu cha maana ambacho wote tunakitaka ni kujadili mstakabari wa taifa letu bila upendelea au kuzidisha chumvi! au kuegema sana katika chama kimoja.

Anayetaka kuua upinzani inabidi yeye ndiye afe kwanza!!!
 
Mzee Mkira,

Bravo na ubarikiwe kwani bongo tunahitaji wananchi wanaoona mwanga au the light kama wewe,

Wazee wengne wawili huko juu,

Yote mliyosema ni NONESNSE, na ndio maana CCM itaendelea kushinda kwa 80%, maana viongozi wengi wa upinzani na wapambe wao wana mawazo kama yenu, Freeman mzee anayeogopwa na CCM akashindwa hata kumuweka mbunge wake kwenye jimbo aliloliacha HAI,

More power to you guys, CCM inamuogopa sana Freeman na Chadema, sasa mmesema mengi na kama nilivyosema ni NONESENSE, kwani hakuna hata hoja moja kwa ajili ya maendeleo ya nchi yetu zaidi tu ya hasira za mkizi, na kwa taarifa yenu huku hakuna wananchi wenye mawazo kama yenu huku bongo wananchi walishasahau kuhusu uchaguzi ila wanalia na uongozi mbovu kutoka vyama vyote viwili, yaani mmenikumbusha hasira za wale African Americans na wazungu,

sasa nyinyi mna hasira na waafrika wenzenu, tena wabongo wenzenu, hay ngoja tuisubiri hiyo siku mtakayo kuja "kuwaburuza mahakamani viongozi wenu waliochaguliwa kura za uchawi"!
 
Ansi umesema maneno mengi yana msingi mno .Es kuna wakati naingiwa na wasi wasi mzee na baadhi post zako .Ziko pro uzamani na ukandamizaji lakini nakuwa nakaa kimya maana ni mawazo yako na uhuru wako kusema utakalo.Lakini kwa kweli CCM kama kweli na mpango huu mchafu ni hatari kwa usalama wa Nchi.Mnaweza kutumia jeshi na usalama as Es has indicated lakini ukawa na mwisho mbaya.Kukaa vikao kote Dodoma na kuongelewa maamuzi ya Mahakama na kupanga kupeleka muswada mpya ili kuzima the move is too bad kwa Nchi na JK kama kweli anashiriki basi anatufanyia unafiki mkubwa .

Mbowe kama mnataka kummaliza kw auoga wa kuachia madaraka basi wananchi sisi ambao hatuna vyama tutasimama naye .Ndiyo nguvu yake itakuwa na Mungu wake .Lakini uongo wa CCM wa kuwayumbisha wananchi kila mara juu ya sera na matamshi kuyabadilisha na kuwatisha na hatimaye kuwaibia kura JM akiona kwamba CCM haina njia mbele ni mbaya zaidi na ni against human rights.Kama kweli JK ana uhakika na kila jambo lake na anajua anachofanya ni sahihi na Mbowe si tishio kwake basi yeye achape kazi tumpime kwa kazi zake .Najua amefunga ndoa na vyombo vya habari na mwisho wa ndoa zile huwa ni mbaya sana .Mambo muhimu hayasemwi sasa kupitia Media Tanzania Daima wanajaribu sana lakini bado iko kazi kubwa .

JK kama ana mvuto that means ana uwezo wa kuotowapa alicho ahidi na kushinda kura mwaka 2010 kama imani ya watu hapa bodini sawa sasa swala la ubabe na hata kutunyima haki ya sisi kusimama bila vyama unatoka wapi ?Kama kweli JK anashiriki hii dhambi kubwa itakuwa ni mbaya sana ila naonya kwamba kila mwanzo una mwisho wake .
 
Mzee Mugishagwe,

Kwanza heshima yako mkuu!

Now mimi sielewi what is the beef hapa? Unajua msipoangalia hapa ni kwamba mnaupanda kama mkenge wa US, ambako kuna mweusi anayeitwa Farrakhan, weusi wengiu wanaamini kuwa huyu jamaa ni very powerful na ati wazungu wanamuogopa, kumbe ni njama tu za wazungu baada ya kuona hakuna kiongozi mweusi powerful wameamua kumruhusu kueneza hatred zake wakijua kuwa ni mjinga lakini as long as weusi wanaamini kuwa ni powerful basi wanamuchia tu aendelee kuwadanganya wenziwe huku wao wakiendelea na maovu yao,

I am totaly lost na hii hadithi ya hili gazeti, ati CCM ilkaa kikao chini kupanga mikakati ya kummaliza Freeman? Guys please! Yaani JK mjinga kiasi hicho cha kwenda kukaa kikao na viongozi wengi anaojua hawamtaki ndani ya CCM na kukaa nao kuongelea mipango ya kummaliza Free! I mean kuwa na uchungu na nchi yetu ni lazima wote tuwe upinzani? What a joke! Great mawazo yangu ni yakizamani sasa haya ya kukaa kama wajinga ksusubiri siku ya kuwaburuza mahakamani viongozi waliochaguliwa kwa njia ya demokraisa ndio mawazo ya kisasa? I mean you guys are right kweli sina mawazo ya kisasa, lakini ninakataa kata kata kuwa JK anahitaji kukaaa kikao kizima cha CCM ku-plan mambo ya Free ni totally NONESENSE!

What JK na CCM wanafikiria kuhusu independent candidate, mimi ninatakiwa kufanya nini? au wewe na hao mashujaa wenzio kina ans na Kimbembe what can you do about it? Ninasema kiwenye kikao iliamuliwa kuwa watatunga sheria ya kuimaliza hiyo issue na gazeti lenu tukufu halikusema hayo, ambayo nilifikiri kuwa yatawekwa mbele ili wananchi wapige kelele au walijadili, NO! I mean kweli uchaguzi wa ZNZB ulikuwa na walakini, lakini sio wa bara hiyo hata watoto wadogo huku bongo huwezi kuwadanganya wananchi walimchagua JK hilo halina ubishi, yes kunaweza kuwa kulitokea matatizo hapa na pale, lakini ninakataa kuwa yalikuwa massive na nationally planned, hapana hao watakuwa viongozi wachache ambao walikuwa wanajaribu kujikomba kwa wakubwa, lakini kusema kuwa CCM waliiba kura 80% ni uongo! Ni uongo kwa sababu wananchi ambao hawakumchagua JK wasingepoteza muda wao kwenda kumuona kila anapokwenda.

Tanzania tuna matatizo ya uongozi kuanzia vyama vya upinzani, CCM, na serikali kwa ujumla, na pia tuna tatizo kubwa kuliko yote nalo ni wananchi wajinga wa siasa, me included! Na hii media ndio kabisaa inazidi kutadidimiza chini, sasa hiuzi hasira zenu sina uhakika kama ndio dawa ya haya matatizo! Sasa hivi bongo ninaomba muniambie ni gazeti gani ambalo linaandika bila influence ya hawa wanasiasa kuanzia wa upinzani mpaka CCM? Nitajieni gazeti moja tu ambalo liko huru?

Uchaguzi uliopita umewakatisha taama sana wananchi walikuwa wakitegemea mabadiliko, kwani umeonyesha wazi udhaifu wa upinzani, kule BCS tulijadili kwa kirefu hili na hata yule mzee mkali wa chadema kuliko nyinyi wote Msemakweli, alikubali kuwa kuna tatizo la wananchi kutoelewa what is going on! Hivi ni lini upinzani mtachukua responsibility na kufanya mambo tofauti badala ya kulaumu tuu CCM?

Uchaguzi uliopita lawama zote ni lazima ziwaangukie wenyewe upinzani, kwa sababu nilisema huko nyuma kuwa hii ilikuwa the best opportunity kwa upinzani kuchukua madaraka au kuingiza wabunge angalau 50%, hebu for once ongeleeni matatizo yenu ya upinzani, badala ya kuendelea kujidanganya kuhusu Free kuwa tishio kwa CCM, can you guys for once mbadili topic na kuongelea vyama vyenu vilivyo vibovu kama CCM, ndio maana hamuendi kokote! Halafu haya mawzo yenu ya kisasa mnashindwa vipi kuwashawishi wananchi wakawaelewa, badala yake kuleta ukali tu humu ambao hauwezi kubadili kitu chochote, haya mawazo ya kisasa mliyonayo yapelekeni upinzani mulete mabadiliko,

mimi ni mwanchama wa CCM, lakini sio mnazi! Na ninakubali kuwa chama changu kinamatatizo tena makubwa na sijawahi kukataa, so is vyama vyenuu vya upinzani kwani ni vibovu kuliko hata CCM, kazi kugombea rzuzuku tu toka CCM! Hela zote za kukodi Helikopta, lakini ilibidi baadhi ya wagombea ubunge wajitoe kwa kukosa hela kabisaaa! Tengenezeni vyama vyenu kwanza hii idea au ndoto kwamba mtapata madaraka na hivi vyama vibovu, haitatokea, ndio vyama vyenu ni vibovu mno,

tena Free angalau anasimama maana most of the time anatumia hela zake binafsi na ni lazima azirudishie kwa kula pamoja na CCM, hiyo ni common sense sihitaji kujua mambo yote aliyoandika mzee ANS, kulielewa hili!
 
Wana Chadema,

jamani sioni kabisa sababu yenu kuja juu kuhusu Mzee Es hali mtu huyu anawapa habari za ndani toka CCM. Habari ambazo hamuwezi kuzifahamu kama ni mbinu chafu lakini zimekubalika na ushindi kupatikana. Ikiwa kuna ushahidi wa oungo ambao utasaidia ushindi huwekwa. Mahakimu na mawakili hutengeneza mamillioni na majina yao sio kwa sababu wao ni wakweli ila wajuzi wa kuzua uongo kuufanya kweli. Siasa ni uwanja mchafu sana ni sawa na mpira usiokuwa na refa. Nadhani mnakumbuka kabla ya uchaguzi Zanzibar niliwatonya kuwa kuahirishwa kwa uchaguzi Zanzibar ilikuwa mbinu ya CCM kuweza kuweka nguvu yake yote huko Zanzibar na kuhakikisha ushindi. CUF, Chadema na vyama vingine vyote vilifahamu uchafuu huo lakini bado walishiriki badala ya kukataa kwa pamoja na kudai uchaguzi wa Zanzibar lazima ufanyike siku moja na ule wa Bara. Na ktk hoja hiyo nilisema ikiwa CCM itapita Zanzibar basi huku bara watateleza.

Ans kaeleza maelezo mengi sana yenye maana lakini kama mimi hapa nitasimamama kwa mapenzi ya CCM nitamwona mchawi tu. Kwa sababu inapofikia uchaguzi kila mbinu ya kuhakikisha ushindi ni muhimu hata kama mbinu hiyo imepuuza sheria. Sawa kabisa na kesi mahakamani ambapo waamuzi ni jury na ushahidi wote hutolewa kuwavuta hao jury.
Chadema walianza vizuri sana wakati Mbowe akiwa anatembea kwa miguu na kujichanganya na watu. Wengi waliolala walimkubali na hasa kutokana na lugha yake ambayo iliwalenga wengi sana. Nilitoa tahadhari kwamba Mbowe sio mkweli. Huyu mtu kutembea kwa miguu sii sababu kabisa ya kumfanya kuwa sawa na nyie kwani Mbowe aliwahi kuwa na BMW 7 series akiwa na umri wa miaka ishirini tu...anazipenda raha na starehe kama viongozi wengine wote walioko juu. Hakuwa mkweli ktk biashara zake kwa kuwanyanyasa wafanyakazi wake, malipo yao na hata wengine kuwaondoa kazi bila sheria ama imani ya kwamba bila wao Free asingekuwa pale aliposimama.. Mkanisema sana kwamba namuonea wivu na kadhalika, mara akaibuka na mashine pangaboi. Sura yake kamili ilipojitokeza mkazua hoja nyingine mpya kwamba Free alihitaji Ndege hii kwa sababu ya kufika mikoani.

Jamani, ikiwa mgombea urais ana wajumbe wake kila kona ya nchi kwa nini yeye aondoke na helkopta kujitangaza yeye badala ya kuwatangaza wahusika wa majimbo hayo?.Focus ya wananchi wote ilihama toka kwa wabunge na kumtazama Free kama msanii mashuhuri wa siasa. Na sababu kubwa ilikuwa Free alitaka ile popular vote na sio uchaguzi wa wabunge. He failed na Chadema lazima mtazame swala hili kwa makini kwani hata CUF ambao wamechezewa rafu kama nyie bado walikuwa mbele yenu.

CCM walihakikisha kila kichwa cha siasa kimekwenda kila mkoa na wilaya kutangaza majina ya wabunge wake na wakati mbinu mbaya zinatumika Mbowe alikuwa akitazama jarida lake. Mikutano mingi iliharibika kutokana na mbinu za CCM, yet haohao wapinzani hawakusimamisha madai yao ktk vyama vya kimataifa vya upigaji kura. Baadhi tu ya majimbo wameweka madai yao na kwa sababu hamna fedha, sheria haitasimama nanyi. Hii ndiyo demokrasia ya Ulaya tuliyoipokea, na msitake kujidanganya kwamba ktk ubepari kuna demokrasia ya Kijamaa yaani haki, ukweli na fare game. Kitu hicho hakuna na ndio maana wenzetu vyama vyao vya upinzani pia huwa na mbinu chafu.

Na kilichoshangaza zaidi baaya ya matokeo na Ushindi kwa JK kwa asilimia 80%, viongozi hawa hawa walimpongeza JK kwa ushindi hali majimbo karibu nusu yamepoteza kura za ukweli.

Hii inaashiria kwamba kila chama cha upinzani hakikuwa na moyo wa kushinda majimbo isipokuwa kiti cha Ikulu...Na mtanisamehe sana kusema kwamba Ikulu ni sehemu ya mwisho ambayo mlitakiwa kuiangalia.

Kwa hiyo nadhani mnatakiwa sana kuyasoma maelezo ya mzee ES with open mind kwani hata nyie bado mpo ndani kabatini -Chadema. Yote nje ya hapo ni upuuzi hali maneno ya Mzee ES yanaweza kuwasaidia sana. Leo hii mnafahamu uwezo wa JM ndani ya CCM na wachafu ya akina Rostam, manji, EN na wengine wote wanamtandano kwa maelezo ya mzee Es. Je, mnakumbuka kwamba mzee ES ndiye wa kwanza kutuletea habari za wanamtandao?... ama mmesahau kwa sababu leo hii ni kitu cha kawaida. Sio kwamba anayafurahia isipokuwa anawaeleza ukweli kwamba mbinu zao ni kali sana na haziwezi kuzimwa kwa maneno matupu na kunyoosheana vidole.
 
Wanabodi ,

Nimesoma mawazo ya watu wengi na kusema ukweli nimevutiwa sana na michango moto moto ya wajumbe lakini kitu kimoja muhimu ni lazima tujifunze kukubali kutokukubaliana na wakati huo let's attack the issue and not a person .

Suala la siasa za Tanzania ni suala gumu sana na linaitaji upembuzi yakinifu ili kufika katika kilele cha matatizo . Kwanza kabisa ningependa kumfahamisha Mzee ES kuwa mtu kuwa mbunge wa upinzani aimaanishi ya kuwa usiwe na marafiki toka kambi ya CCM au usisocialize nao ,na aimaanishi ya kuwa ni lazima upinge kila jambo linalofanywa na CCM , kwa hiyo Mbowe anayo haki ya kuwachagua marafiki anao wataka !

Mkandara umesema kwamba mbowe alikuwa na BMW7 series akiwa na mika ishirini tu, hivi unafahamu huyu bwana ametoka kwenye familia gani ? Mbowe kuwa na hilo gari katika huo umri sio jambo la kushangaza kabisa kwani baba yake alikuwa milionea tangu miaka ya nyuma sana.

Tunawalaumu sana upinzani bila ya kuangalia mambo wanayoyaface , kama kweli tunataka upinzani wa kweli ni lazima tu level playing field kwa kubadilisha vipengele vya katiba ambavyo vinaugandamiza upinzani . Pili CCM ni lazima irudishe mali ilizotaifisha toka kwa wananachi vitu kama uwanja wa jamhuri morogoro , Kirumba n.k hizi zote ni mali ya watanzania na sio CCM .

Mwisho kabisa kuna statement imetolewa na Mzee ES , Kusema ukweli it made me sick of my stomach .......Mzee ES labda utusaidie MADC ni viongozi wa chama au serikali ? na kama ni viongozi wa serikali then JM alitoa hiyo statement kama nani ? nI statement kama hizi zinanifanya ni conclude kuwa nchi yetu itaendelea kuwa nyuma tuu ! Statement aliyoitoa JM ilikuwa inatosha kumpeleka jela kwa kutaka kuharibu uchaguzi , ila kwa kuwa nchi yetu inaongozwa na vihiyo statement hiyo inaonekana sawa tuu.

MZEE ES ALISEMA
" kwa hiyo kama JM anasema ma-DC watafukuzwa au watanyongwa no body should lose a sleep ni matatizo ya ndani hayahusu taifa, kwa hiyo I could crae less what they do kwenye vyama vyao mpaka wakiingilia taifa " !
 
Unajua mzee uemeanza vizuri mpaka ulipoanza kutoa rangi yako,

(1). Halafu siku zote sina tatizo kuwaelimisha wananchi wasioelewa kama wewe na wenzako, ninasema hivi hili gazeti linadai kuwa Freeman ni tatizo la CCm mpaka wameamua kumkalia kikao namna ya kummaliza, halafu hawa wazee wa CCm wakatoka hapo wakashinda na Freeman majumbani kwao! Sasa jawabu hamna mmebakia maneno yale yale ya siasa tuliyoyazoea, ninasema tena kuwa siajawahi kuwaona kina Mrema, Lipumba, Mtikila, Mapesa, wakishinda majumbani kwa viongozi wa CCM! ni Freeman peke yake, WHY?

(2). Tumeambiwa CCM ni wabaya sana maana Kolimba, Mwaikambo, Malima, walipoanza tu kutaka kuwa tishio waliwaua, sasa kinachowashinda kummuua Freeman wanayeshinda naye, tena majumbani mwao ni nini? Freeman ana tofauti gani na hawa kina Kingunge mpaka awe tishio kwao?

Mzee Bob anasema ukweli kuwa Free hana tofauti yoyote na hawa viongozi wa CCM, tena yeye wafanyakazi wake huwapiga vibao, na kuwafukuza kama mbwa, na kuwatishia na bastola, Freeman ambaye maisha yake yote hucheka watu kuwa hawana kitu wanasota na yeye hasoti leo amekuwa kiongozi shupavu na mpaka wengine humu mnamlilia, ama kweli bongo tumejaa wajinga wengi!

Vijana Freeman ni mfanya biashara, sio mwanasiasa no matter what yeye anajali his bottom line na sasa hivi amegundua ujanja wa siasa kumpatia faida katika biuashara zake that is all, jamani huko majuu hivi ni kweli mzee Tom Delay anashinda na kina mama Pelosi, na kina Kennedy? Je kina Rush Limbaugh wanashinda na kina Dan Rather? Huu ustaarabu wa kina Freeman kushinda na wakina Chenge kila siku, halafu kina Chenge wakifika CCM wanakaa vikao kumjadili alivyo adui mkubwa wao, halafu wakitoka kwenye hivyo vikao wanaenda tena kushinda na Freeman, hivi mbona ndugu zangu mnachekesha! Maleclea au Kingunge wanaweza kuwa na urafiki na kiongozi wa upinzani toka lini? Hivi wa-Tanzania tutaamuka lini? Hata nyinyi mlioko nje pia ni mambumbu kama sisi tulioko bongo? Sasa atakayeiokoa hii bongo ni nani?

Yaani wewe Rufiji ndio bure kabisaa, yaani wewe unaamini mimi sielewi maana ya urafiki, na sielewi kuwa kiongozi anaweza kuwa rafiki na mtu yoyote! Unajua wengine kama hamna ya kuisaida nchi yetu ni afadhali mkanyamaza tu, badala ya kuingia na majina tofauti hoja hakuna!

Hebu atokee mmoja wenu aje na hoja za maana juu ya ubovu wa vyama vyenu vya upinzani, atueleze sasa wakati CCM inapanga mikakati ya kuummaliza Freeman nyinyi zaidi ya kulia kwenye haya magazeti mnafanya nini?
 
Mzee Es,
Huyu jamaa katokea wapi tena?...Rufiji!!!
Wee unafikia kuniuliza mimi kama naifahamu familia ya Mbowe?.. Labda nikwmbie kwa kifupi, mimi ndiye mwanzilishi, mbunifu wa Space 1900, kwanza tulikuwa Keys hotel tukahamia YMCA na baadaye Mbowe. Tukafungua tawi la club pale Moshi Hotel, New Africa na mwisho kabla sijaondoka Bongo - Valentino. Mikakati yangu ndiyo iliyowaangusha Bilibi ambao leo hii wanaitwa Clouds na wamefumka tena baada ya mimi kuondoka, tena basi hawa jamaa zangu wa karibu sana. It was all business.
Fedha za club na misheni town akiwa benki kuu ndizo zilimpa utajiri wa kwanza kabla ya urithi..Wee ulikuwa unaamfahamu mzee Mbowe ama unafanya kusimuliwa!
Kifupi maelezo yote ambayo tunazungumzia hapa ni kwa faida yenu Chadema. Haitaninyima usingizi kusikia wameshindwa tena kwa sababu ya watu kama nyie ambao hampendi kupima ukweli unaowagusa.
Mzee Es pamoja na machafu yote ya CCM kila siku yuko mstari wa mbele kuwafahamisheni yanayoendelea ndani kwake, badala ya nyie kuyachukua na kuyaweka mezani, mnayapuuza na kesho mtakuja lia tena.
Hivi kweli tujiulize wenyewe ikiwa kweli CCM wanataka kumuangusha Free kwa madongo yake inakuwaje watu hawa hawa walioweza kuwaua wengine washindwe kumuondoa Free ambaye hutembelea nyumba zao. Na huyu Free atakuwa mjinga kiasi gani kukaa karibu na marafiki wanafiki ambao wanataka kumwangusha hali akifahamu ya kwamba atakapo anguka yeye na Chadema mweleka vilevile!..I doesn't make sense! Unless mtupe sababu ya Free ku-hang up na hao watu ambao nyie mnaamini na kudai wanataka kumwangusha!
Nadhani patakuwa hakuna tena ubishi...
 
Wanabodi,

Mimi naomba kama alivyosema mmoja wetu hapo juu tuwe tuna attack issues na siyo mtu. Mzee ES, nadhani nyinyi ni wageni wa postings zake, kwa wale wanaomjua kama Mnyika(ingawa ni Chadema) wanajibu hoja. Kutofautiana naye ni jambo la kawaida kwa sababu mambo mengine anaambiwa, inawezekana akawa ameyapata lakini yakawa wrong. Rafiki yangu Mnyika anaita "umeteleza". Hii yote ni ktk kuijenga Tanzania yetu.

Tukielewa kwanini tunaandika hapa, basi hatutashambuliana, mimi ni mwana CCM na ni kiongozi, ila kama ES siyo yote yanayofanyika nayapenda, lakini kuna namna ya kuyabadili. Hasira should be the last thing in discussion.

Turudi kwenye topic. Mbowe, mimi binafsi sifahamiani na Mbowe, ndio maana siwezi kumjadili kwa undani, ila ninachojua Chadema katika vyama vya upinzani ndio chama bora kwa sasa, tatizo ni kuishinda CCM, CCm ina watu wenye hela na ni hao wanachagua viongozi, Chadema hawana watu kama hao. juhudi zenu za kuwaelimisha wananchi hazisaidii kama huwezi kutoa Milioni mia mbili kutenganeza barabara (Manji), wananchi wa kitanzania kamwe sio rahisi kuwaelemisha, wengi wana njaa na kuendekeza dhiki. Vyama vyote vya upinzani havina "tools" za kuwadanganya, Mpaka kizazi hiki kipite CCM itakuwa madarakani tu!, kwa maoni yangu mpaka 2025 bado tutakuwa madarakani.

Ukiondoa wananchi hata viongozi wenu ni matatizo, rejea postings za Mzee ES.

Kwahiyo haina maana kumshambulia mtu hapa, tulieni pangeni mikakati ya uchaguzi wa 2025.

Mnyika naomba tarehe yako ya kurudi, nitakutafuta mara tu ukifika. Najua nitakupataje.

FD
 
Habari kwamba CCM wanapanga kumbomoa Mbowe zinaweza kuwa za kweli. Lakini pamoja na kwamba watatumia mbinu inayodaiwa ilitumika kummaliza Sumaye, bado mimi naona iko ya pili na ambayo ni yenye ufanisi zaidi.

Na mimi naona kwamba CCM wamekwishaanza kumbomoa Mbowe, na upinzani kwa ujumla, kwa kutumia mbinu hii Nitaeleza.

FREE MEDIA wameandika kwamba: "CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimeanza mkakati wa siri wa kubomoa upinzani, na sasa imedhihirka kwamba mlengwa nambari wani ni Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe na chama chake"

Hii ni kweli kwa sababu tangu Rais Kikwete atinge pale Magogoni mpaka sasa hivi anatekeleza ILANI YA UCHAGUZI YA CUF NA PIA ILANI YA UCHAGUZI YA CHADEMA. Hili halihitaji maelezo. Sera zako zote zikishatekelezwa na CCM kitakachokutofautisha na CCM ni kitu gani? Hii ndiyo mbinu kubwa ninayoiona ikitumika sasa hivi. Mbinu zilizotumika kummaliza Sumaye hazipo hapa na wala sioni kama Sumaye amemalizika. Tofauti na propaganda za vyombo vya habari, bado anao wafuasi wengi ndani na nje ya CCM.

FREE MEDIA wameandika kwamba yuko mwana CCM anasema hivi: "Sisi tulikuwa tunamwona Mbowe kuwa ni mstaarabu, hana siasa za kubomoana; lakini baada ya hapo tuliona ameanza mambo ya Mrema ya kulipua mabomu.Sasa sisi tuko madarakani. Lazima atutambue."

Katika taifa ambako siasa ni biashara na uwekezaji kwa kutumia mtaji mkubwa kuanzia milioni 30 hadi milioni 100 kwa nafasi za Ubunge maneno kama hayo lazima kuyatarajia pale mtu anapokuwa amefanikiwa kuingia madarakani. Na hasa mtu huyu ataogopa ukweli na wasema kweli wote. Na kwa kuwa ana madaraka atafanya kila linalowezekana kuwamaliza wapinzani wake maana bila hivyo anaweza akapoteza nafasi yake na mtaji wake pia. Siongelei nafasi ya Uraisi, maani hilo ni suala tete! Lakini swali ni je: tunalazimika kuwatambua watu ambao waingia madarakani kwa kutumia nguvu ya pesa, lakini wasio na sifa za msingi kama viongozi wa watu, na hasa watu masikini kama walivyo watanzania?



FREE MEDIA wameandika kwamba: "Vyanzo vya habari vinasema macho ya watendaji wa CCM sasa yanaelekezwa kwa Mbowe kuliko kwa mwanasiasa yeyote wa upinzani, kwa kuwa ndiye anaonekana kuwa na hoja zenye mvuto mbele ya umma akilinganishwa na wapinzani wenzake."

Hili ni sawa kwa kuwa kiongozi ni mtu mwenye wafuasi na Mbowe anao wafuasi tena wafuasi ambao, sio "reflexive" kama ilivyo kwa CUF, bali wafuasi "reflective". Ni lazima CCM wamwogope.

FREE MEDIA wameandika kwamba kuna mwana CCM mwingine anasema kwamba "CCM mpya haitakuwa na simile juu ya Mbowe.Nakuhakikishia, baada ya miaka minne CHADEMA haitakuwa ile ile, wala Mbowe hatatamba tena."

Kwa mtindo wa kutekeleza sera za vyama mbadala ambao Rais Kikwete amekuja nao naweza kukubaliana na madai haya. Lakini kama Rais Kikwete ataendelea na baadhi ya sera mbovu alizo nazo sasa hivi sioni kama CHADEMA na Mbowe watakuwa wajinga kumezwa hivi hivi. Labda kama watakubali kuhongwa. Sera ya elimu ya juu ni mbovu, sera ya madini ni mbovu, sera ya ajira ni mbovu, sheria kadhaa za Bunge ni mbovu, katiba ni mbovu, na orodha inaendelea. Hata kama CHADEMA watakosa mwelekeo mbadala bado tutatafuta jukwaa mwafaka na kulitumia kupiga kelele mpaka Mungu apate habari kwamba Tanzania kuna sera mbovu na sheria mbovu!

FREE MEDIA wameandika kwamba: "CCM inadhamiria kumbomoa Mbowe kisiasa na kibiashara kupitia njia mbalimbali za propaganda na kisheria, na kwa kutumia vyombo vya habari. Uchunguzi unaonyesha kwamba hata sasa kazi hiyo imeanza, lakini inahitaji kuendelezwa kwa kasi hapo baadaye."

Hivi linawezekana maana tunaona kwamba tayari wamekwishaanza kutekeleza hili. Habari Corporation imenunuliwa kwa asilimia zaidi ya 50 na Rostam Aziz, mwanamtandao na personal friend wa Kikwete. Na kama tunavyojua magazeti kama Rai ni magazeti amabayo yanaitwa Opino Formers huko majuu. Mmiliki anapokwa ni nyani na habari inamhusu ngedere tunaweza kujua kitakachofuata. Sijua kama wataishia Habari Corporation au watendelea. TUnafuatilia kwa ukaribu. Ni dhambi kuua upinzani kisayansi namna hiyo.

FREE MEDIA wameandika kwamba:"Chama kinachoonekana kukua, hasa upande wa Bara, ni CHADEMA chini ya Mbowe, huku kikiwa na sera kuu mbili - ya majimbo na elimu - ambazo baada ya ufafanuzi wa Mbowe, zimekitofautisha na vyama vingine."

Hii ni sawa lakini sera ya elimu kwa kiasi fulani Kikwete amekwishaanza kuitekeleza. Ni CHADEMA wakiokuja na wazo la kuifanya DODOMA kuwa Mji Mkuu wa Sekta ya Elimu Tanzania. Sijaona kama sera ya majimbo wanaipenda CCM lakini ikishapigwa msasa nahofu nayo wataibeba.

Hata hivyo, bado kuna matumaini kwa CHADEMA. Kitu ambacho kinaweza kuusimamisha upinzani na kuibwaga CCM ni itikadi. Sasa hivi CCM hawana itikadi kamwe. Kwa sababu hii hawana dira. Na kutokana na ukosefu wa dira sera zinagongana. Kwa mfano ni ujinga kusema kwamba unamkopesha mtoto wa Tanzania pesa ajisomeshe halafu akimaliza unaanza kumkata mkopo huo, na hapo hapo ukatunga sheria ya mumkata PAYE mhitimu huyo huyo, na hapo hapo ukatunga sera ya kupambana na ukimwi bila kuona kwamba sera hii ya mwisho unahujumiwa na sera zile mbili za kwanza.

Hii ndiyo sababu tunasema Tanzania na hasa pale Mlimani waanzishe kitivo cha falsafa! Mafundi mchundo hawawezi kutengeneza itikadi wala sera za nchi! Tena falsafa ipewe kipaumbele katika sera ya elimu kama ilivyo kwa masoma kama vile Engineering na Medicine! We need more philosophers now than ever! Haya mambo ya aibu ya kuokota okota sera kutoka IMF na WB bila kuwa na uwezo wa kuzihakiki yatakomeshwa kwa njia hii.

Hata katibu mweneza wa CCM Mheshimiwa sana Ramadhani Omari Mapuri hajui maana ya itikadi wala haelewei tofauti kati ya mbnu na malengo. Nasema hivi kwa sababu naona kwamba hajui itikadi ya chama chake mpaka leo!

Kama kuna mtu anabisha juu ya hili aangalie anachokisema kuhusu siasa ya ujamaa na kujitegemea kwenye tovuti ya CCM

Angalia hapa: www.ccmtz.org/jarida/page21-23.htm ambapo kuna makala yenye kichwa cha maneno: Tumeachana na Siasa ya Ujamaa na Kujitegemea? La hasa! Ni aibu tupu!
 
Mzee JJ na Wenzako,

(1). Ninaomba minitajie gazeti moja tu, hapa bongo ambalo halina influence ya CCM au upinzani?

(2). JK kuwaharibu wagombea wa CCM, alitumia kikao gani cha CCM mpaka leo akiwa rais anahitaji vikao vya CCM kummaliza Free?

(3). Kingunge, Kinana, Malecela, Chenge, wanawza kuwa marafiki wa kiongozi wa upinzani bila ya sababu, ninaomba wewe useme kuwa inawezekana?
 
Bw. JJ, ningependa sana kufanya mahojiano na wewe na hatimaye kuyarusha kwenye podcast na kwenye bongoradio.com. Nina uhakika watu wengi wangependa kusikia maoni yako kuhusu mambo mbalimbali yahusuyo nchi yetu. Tafadhali wasiliana nami hapa mwanakijiji@journalist.com

KLH News - On the cutting edge of Tanzanian News.....online!!
 
J J Mnyika,
Ndugu yangu karibu sana tena ukiweza pitia kwangu.... usitie shaka bill juu yangu

Mengi umeeleza mazito na yenye maana isipokuwa nataka kukuuliza wewe! Hii habari ya kumbomoa Mbowe ni za kweli?

Ikiwa kweli, Je Chadema mmejiandaa vipi kama chama kwa sababu naona kuna maswala umetaka Mbowe mwenyewe ayajibu hali yanahitaji msimamo wa chama sio Mbowe. Zaidi ya hapo sina isipokuwa nashukuru sana kwamba umeonyesha tofauti kubwa iliyopo kati yako na viongozi wengine ambao wamejichimbia baada tu ya uchaguzi kuuguza madonda. Media coverage ni mbinu moja kubwa sana na inahitaji kufuatiliwa kila siku. Kusema kweli nimevutiwa sana na wewe pamoja na kwamba hatufahamiani lakini umenipa moyo..

Siwezi kudanganya hao CCM, Chadema, CUF sijui TLP n.k wote mmenikalia kushoto. Na sababu kubwa ni kwamba, vyama vyote havina tofauti. Wote mnainadi nchi - mikataba ya KUUZA NCHI badala ya mikataba ya KUFANYA BIASHARA. Hata masikini muuza nyanya anayo kila haki ya kuuza nyanya zake kwa mwenye fedha na sio haki ya kuuza shamba kuitwa ndio makubaliano ya biashara. Chadema pamoja na kwamba mnadai kuwa conservatives, UZAWA sio moja ya nguzo zenu, hii inawafanya kuondoa nguvu ya nani anatakiwa kuwa mmiliki na mrithi halili wa nchi yetu. Uzawa unakaribisha wageni kwa kuwapa nafasi ndani ya jumuiya yetu (uraia) na haki sawa ikiwa mgeni huyo atafuata na kuheshimu tamaduni zetu. Sikubaliani na mfumo ambao unatufanya sisi kuwa wageni wa kufuata na kulinda tamaduni za kigeni tukifikiria kwamba hadi ya mtu ni mali na uzungu. CCM wao ndani yao wamegawanyika..Conservative na Progressive kulingana na hoja iliyopo mezani mara nasikia kambi za mtandao n.k. Ujamaa na Kujitegemea ni barabara iliyoota magugu na haipitiki tena lakini bado ipo ktk ramani yao.

Mpango wenu Chadema wa majimbo, sikubaliani nao hata kidogo kwa sababu tatizo letu kubwa ni uwezo na nguvu ya hao ma DC na RC sio uongozi mzima wa nchi ama mikapa ya nchi. Kwa hiyo mabadiliko yanatakiwa ktk WATU - utawala na sio MIPAKA ya utawala. Nakubaliana na mabadiliko ya kuwepo na viongozi(Governors) badala ya watawala(RC) kwa hiyo hakuna haja ya kuunda serikali za majimbo kwani problem sio mipaka.

Mwisho, sikubaliani na mpango wa vyama vingi vya kisiasa kwa nchi maskini kama yetu. Bora vyama viwili vyenye tofauti zinazofahamika wazi kwa wananchi na kama kutakuwepo na wagombea binafsi basi lazima watofautiane na hivyo vyama. Nakubali pia chama kimoja kama hiyo ya kwanza haikubaliki lakini kiwe na kambi mbili tofauti -Conservatives/ Pogressive kisha nafasi ya wagombe Urais iwe wazi kwa wote. Ni bora kuwa na wagombea Urais kumi toka chama kimoja kuliko wagombea kumi toka vyama tofauti. Hii inaondoa nafasi za wale ambao ni kipenzi cha wananchi. Wagombea binafsi ndani ya mfumo huu tuliokuwa nao wa vyama vingi ni uzushi mtupu kwani CCM watazidi kuibuka washindi kila mwaka. Umoja ni nguvu, utengano siku zote huwa ni udhaifu. One man can't beat the system.

Deograsias,
Umesema kwamba CCM wamepania kuibomoa Chadema kwa sababu CCM wameiga sera za Chadema?...

Mshikaji sera sio ilani ya chama na hakuna sheria ambayo inakataza chama kutochukua sera fulani na ndio maana tunalo bunge kupitisha miswaada. Kwa kiswahili rahisi Vyama vyote vya kisiasa huwa na malengo sawa chini ya katiba ya nchi na hutofautiana kiitikadi. Kwa maana hii safari yao wote ni kutufikisha peponi lakini tofauti zao ni njia ama barabara gani wanazitumia. Hakuna sheria ya kusema ikiwa Chadema wanatumia gari basi CCM, CUF na vyama vinginevyo hawaruhusiwi kutumia gari. Watembee kwa mguu, wapande punda, baiskeli, mashua au ndege lakini sio gari. Laa hasha CCM wanaweza kutumia gari pia isipokuwa tofauti inakuja CCM hukodisha magari na kutoza nauli kubwa badala Chadema wanaotaka kununua hayo magari ya usafiri ili kupunguza gharama za usafiri kwa raia zake.

Still, bado naamini kwamba vyama vya upinzani havina mikakati bora. Kuamini kwamba shujaa ni yule ambaye haleti ushindi huku tukitumia mifano ya wale walioleta ushindi ktk azma yao (initial goal) haiwezi kutusaidia kitu.
 
Wanabodi ,

Kwanza kabisa ningependa kutumia nafasi hii tena kuifagilia bodi hii kwa michango moto moto na iliyoenda shule , na kwa mtazamo wangu kama kweli Viongozi wetu wangekuwa wana mitazamo kama ya wanabodi katika hii forum basi tungekuwa mbali .

Sitaki kujibu shutuma zilizoletwa juu yangu kwa sababu hakuna jambo lolote linaloweza kuwa gained by winning that argument , since we are living in a democratic society " i guess" then everyone is entitled to his opinion.

JJ ili upinzani uweze kushinda katika chaguzi zijazo ni lazima ubuni strategy zitakazopelekea kufikia malengo yao . Ni lazima wajaribu kuwafikia wananchi katika vipindi vyote, na sio kusubiri kipindi cha uchaguzi. Na kwa mtazamo moja ya vyombo muhimu ni Radio , ni lazima munzishe radio ambapo wanaanchi wataweza kuvoice up their opinion na wakati huo hiyo inaweza kutumika kama platform ya kuattack CCM.

Pia JJ ni lazima mhakikishe mnawaweka CCM kwenye defensive side wakati wote , kuna issue nyingi sana ambazo mlitakiwa mlitakiwa mzicounter attack lakini amfanyi hivyo ...kama wananchi kunyanga'nywa viwanja maeneo ya tegeta na kunduchi bila ya kueshimu sheria, masuala ya IPTL , Mikataba ya madini , Mahita kuwaita CUF majambazi hii issue ilitakiwa itumike vizuri kupoint out uozo wa viongozi wanaochaguliwa na CCM na sio kum attack mahita kama mahita . CCM iko so vulnerable katika issue nyingi lakini wapinzani awazitumii vizuri . Sasa kama auna platform kama radio uwezi kufanya hayo mambo. Mawaziri wengi wanazungumza tuu mambo lakini hakuna watu wa upinzani kujibu . Upinzani mara nyingi unakuwa dormant mpaka kipindi karibu na uchaguzi ndio unakuwa active.


JJ hata katika uchaguzi uliopita watu walifanya makosa sana , walitakiwa wamuattack JK as a person nadhani unaelewa nammanisha nini . Wapiga kura wengi especialy waumini wa dini wangebadili muelekeo but that is history anyway JJ mabadiliko yafanyike kama kweli tunataka upinzani wa kweli .

Mwisho, WAPINZANI ANZISHENI RADIO .
 
Rufiji,
ndugu yangu umeanza vizuri sana na unastahili pongezi kwa mchango wako. tatizo la sisi Wabongo lazima uwe na uwezo wa kupima hoja yako hadi tone la mwisho., sawa na mpishi ambaye lazima ahakikishe chunvi haikuzidi wala kuacha chuzi lina maji mengi.

Nakubaliana na wewe sana ulipotoa hoja ya radio na Mbowe anawafahamu vijana wote wazuri sana ktk habari na Utangazaji. Mbowe anawafahamu vijana wengi waliochipukiaktk uandishi wa magazeti na usanii. Free anawafahamu vijana wa rika lake na chini kuliko hata JK na kiongozi mwingine yeyote ndani ya CCM tena kwa ukaribu. lakini kibaya ni kwamba Free hatumii nafasi hiyo kwa manufaa ya chama isipokuwa hisia zake za kibinafsi. Mbowe ni mtu anayetaka umaarufu na kufuatwa yeye kama vile anavyowafuata yeye wale walioko juu yake. Mbowe anataka watu kama akina Mwanakijiji, Mzee Es wakaombe kazi kwake na hata siku moja Mbowe hawezi kumuomba Mwanakijiji awe mwakilishi wa Chadema ktk nchi za nje.

Matumizi ya ndege ya helikopta yalikuwa hayana maana kabisa zaidi ya umaarufu. hakuna hata sehemu moja aliyokwenda Mbowe ambayo magari hayawezi kufika. Uharaka wa kufika sehemu hizo haukuwepo kwani Tanzania nzima usafiri wa siku moja upo toka kila kona. Na uzuri wa msafara wa magari hasa bus kubwa la chama hupitia vituo vidogo muhimu.
Pili, Chadema inatakiwa kuyainua majina ya viongozi wa ndani ambao wanatyegemewa kushika uongozi kesho. leo hii ukimuondoa Mbowe hakuna jina lililobakia kama tishio zaidi ya Zitto na ndugu yetu JJ. hata hivyo hawa hawana nguvu kabisa na majina yao yapo magazetini tu, hakuna kiongozi Chadema anayeweza kwenda mikoani na kuwavutia watu kuhudhulia mkutano ama warsha. Yote haya yanatokana na kutowaanda watu kuwa kivutio cha wananchi. Media coverage ni muhimu sana hata iwe scandal maadamu jina la mhusika liwe ktk ndimi za wananchi.

Anayoyafanya Bush leo hii ni kutayarisha viongozi wa kesho na tayari majina yao yapo midomoni mwa watu. Wenzetu nchi za Ulaya, all politicians, wasanii wa Sinema na sanaa vyinginezo hutumia mbinu za kujitangaza ili kupandisha thamani sanaa zao pia kukuza majina yao. Mtakapo jenga majina ya viongozi wenu nje ya Mbowe, thamani ya Chadema kama chama itapanuka. Hivi sasa Chadema ni Mbowe, asiyempenda Mbowe basi hata Chadema haipendeki kama ilivyokuwa CUF na Seif Sharrif.

Mwisho ndugu Rufiji, samahani sana hoja yako ya mwisho kusema kweli ni tishio kubwa sana na Chadema wasiombe kujaribu mbinu kama hiyo. Mbinu hiyo ndiyo iliyowaangusha CUF na wao CUF wanaamini Chadema ni chama kilichoundwa kuivunja nguvu CUF kwa kutumia imani kama hizo. Kwa maana hiyo CUF na Chadema hawawezi kula sahani moja na kwamwe vyama hivyo haviwezi kuungana. Matokeo yake CCM anaendelea kupeta na marungu mtarushiana wenyewe.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom