SteveMollel
JF-Expert Member
- Jul 12, 2015
- 8,432
- 23,753
- Thread starter
- #121
*NYUMA YAKO (MSIMU WA PILI) -- 26*
*Simulizi za series*
ILIPOISHIA
“Hata nami ningependa kwenda huko kabla ya kukoma kwa maisha yangu!” Vio akasema kwa furaha. Wakakumbatiana tena na tena. Walikuwa na furaha sana, waliona sasa wameshaukwaa.
Lakini pasipo kujua, Jack Pyong alikuwa amesimama mahali akiwatazama, moyo wake ukiwa unavuja damu.
“Vio,” Jack akaita kwa kunong’ona. “Nimekukosea nini?” akauliza kana kwamba Vio yu pembeni yake kisha akajikongoja taratibu kulifuata gari.
ENDELEA
Alipolifikia hakufanya kitu bali akaendelea kutazama mpaka pale aliposhtukiwa. Vio alibumbuwaa kumwona Jack, na kwa kiasi fulani akahofu, lakini kwa upande wa Gotham kwake ilikuwa kinyume, ni kama vile alikuwa anatarajia ujio wa Jack kwani hakuwa anahofu wala kuhenya, alimtazama Jack kisha akampuuza.
“Vio,” Jack akaita na kuuliza, “nimekukosea nini wewe?”
Mashavu yake yakafunikwa na machozi, alikuwa anang’ata meno kwa uchungu. Kidogo Vio akabanwa na haya.
Lakini kadiri muda ulivyokuwa unaenda, Jack akawa anapatwa na hasira. Akajikuta akitaka kumdaka Vio na kumwadhibu kadiri awezavyo lakini Gotham akammudu mwanaume huyo na kumkandika makonde kadhaa kabla ya kumwacha hapo akiwa anavuja damu na hajielewi.
Uso wa Jack ulikuwa unavuja damu, jicho lake moja limevimba na tumbo lake linauma haswa kwa kukandikwa ngumi! Lakini Jack hakuwa anaumizwa sana na hayo majeraha bali kutendwa kwake na Vio.
Huko kulimuuma kusipokuwa na mithili. Alihisi moyo wake unasinyaa kwanguvu kumimina damu.
“Kwanini Vio?”
Alijikunyata akiwa gizani.
**
Saa mbili asubuhi …
“Nyanyuka twende!” alisema bwana Charles Smith akimtazama Miss Danielle, bwana huyo aliyekuwa amevalia suti nyeusi iliyobana mwili wake mwembamba.
Alikuwa ni mwanasheria wa Danielle. Punde alikuwa ametoka kuongea na inspekta James Peak na kaufikiana kulipeleka shauri hilo mahakamani, mahali ambapo mteja wake atapata haki yake.
Basi Danielle akanyanyuka na kuongozana na bwana Charles mpaka kwenye gari na kutimka toka kituoni. Mwanamke huyo alikuwa amejikunyata akiwa amemezwa na mawazo.
“Usijali, miss,” Charles akamtoa hofu. “Ni kesi ndogo sana isiyo na ushahidi. Tutakapoenda mahakamani haitachukua muda kuimaliza na kuifutilia mbali!”
Na zaidi bwana huyo akapendekeza waweke fidia ya juu kwa serikali kwa kumpotezea muda mteja wake na pia kumchafulia taswira yake mbele ya jamii.
“Unaonaje?” akauliza bwana Charles akitabasamu.
“Ni sawa,” akajibu Danielle kisha akanyamaza asiongeze jambo, basi safari yao ikawa kimya kwa muda.
Bwana Charles hakujua nini ambacho kinamtatiza Danielle kichwani. Alimwona mwanamke huyo akiwa ametulia kupita kiasi na kwakuwa hakutaka kumtibua akaamua naye kuufunga mdomo wake.
Walipotembea kwa muda fulani Danielle akamuuliza bwana Charles kuhusu ile fidia aliyokuwa ameisema awali, anadhani itakuwa ni kiasi gani? Hapo bwana huyu akapata kujua angalu kile ambacho kilikuwa kinakatiza kwenye ubongo wa huyu mwanamke.
Alitabasamu akimwangalia.
“Inaweza ikawa pesa kubwa sana, inategemea na wewe utakuwa unahitaji kiasi gani.”
Danielle akafikiria kidogo, ni kama vile alipata wazo jema, alifyatua miguu yake aliyokuwa ameikunyata akamwangalia bwana Charles na kumuuliza,
“Una uhakika tunaweza kushinda hii kesi?”
Bwana Charles akatikisa kichwa. “Sijaona ugumu wake, miss. Nimeshahangaika na kesi kubwa na ngumu kuliko hii … huko kote nikatoka salama!”
Kauli hiyo ikapandikiza mmea ndani ya moyo wa Danielle.
Kuna kitu alifikiria na kwa namna moja kikaukimbiza moyo wake.
**
Saa moja jioni …
“Unaweza ukapumzika sasa,” alisema Marshall akiwa anamfunika Jack shuka.
Jack alikuwa na macho mekundu ila la kulia likiwa jekundu zaidi. Uso wake ulikuwa umevilia damu na kuzibwa na bandeji baadhi ya sehemu. Alikuwa amechoka lakini pia ameumizwa. Majeraha ya mwili waweza kuyatia dawa, vipi ya mapenzi?
Marshall alikuwa anafahamu kile ambacho Jack alikuwa anapitia. Alikuwa anafahamu namna gani ambavyo mwanaume huyo alikuwa akimpenda Vio, kwa moyo wake wote, ilikuwa ni ngumu kuukubali ukweli kwamba mwanamke huyo alikuwa akimdanganya.
Ukweli ulikuwa mchungu kuukubali kuumeza.
“Jack, yapasa uache jambo hili lipite sasa,” alisema Marshall aliyekuwa ameketi pembeni ya Jack. Alikuwa akimtazama rafikiye kwa imani.
“Kuendelea kulibeba hili hakutaleta lolote jema zaidi ya maumivu. Sawa, Jack?”
Jack alikuwa akitazama kingo ya kitanda kwa fikira. Macho yake yalikuwa yanadondosha machozi. Machozi na damu.
Alimtazama Marshall kisha akamuuliza, “Ulikuwa unayafahamu haya, Tony, sio?”
Marshall akashusha pumzi ndefu puani. “Jack, si muda mzuri wa kuongelea haya.”
“Ulikuwa unafahamu, sio?” Jack akakazia swali lake. Alikuwa anamtazama Marshall kwa macho yake mekundu.
“Kwanini haukuniambia muda wote huo, Tony?”
“Jack, sikutaka kukuumiza.”
“Mbona sasa naumia?”
“Samahani, Jack. Nilitaka nilimalize jambo hili kwa mikono yangu, ni kwamba nimekawia.”
“Tony, siku zote ulikuwa unajua Vio ananizunguka lakini ukanyamaza. Umeniumiza.”
“Najua, Jack. Nisamehe sana.”
Jack akarudisha macho yake kwenye kingo ya kitanda akiendelea kuwaza.
“Kumbe ndo’ mana alikuwa anataka uondoke karibu na mimi. Ndo’ maana alikuwa hataki kuja kukuona. Kwanini sikuyajua yote haya mapema? Kwanini nilikuwa mpofu kiasi hiki?”
Marshall akamsihi Jack aachane na fikra hizo kwani zitazidi kumuumiza, lakini kidogo kwa Jack swala hilo likawa gumu, alishindwa kunyamaza, moyo ulikuwa unamuuma sana.
Mwishowe akamwomba Marshall akamletee kinywaji kikali ili apate kunywa kujipumbaza, mwanzoni Jack akawa mgumu kutimiza agizo hilo lakini alipokuja kuona kwamba pengine litakuwa ni tiba ya muda kwa Jack, akaamua kwenda zake kumfuatia.
Baada ya dakika kadhaa akawa amerejea akiwa amebebelea chupa kubwa ya vodka, akammiminia Jack glasi kadhaa na haikuchukua muda Jack akajikuta akielemewa na kichwa, akalala.
Marshall akamfunika vema shuka kisha akamtakia usiku mwema. Akiwa hapo pembeni ya Jack, akafikiria kumhusu Vio, akafikiria kuhusu Gotham.
Aliona watu hao wanastahili kuadhibiwa. Haiwezekani waishi maisha kwa furaha tele ingali wamemuumiza rafiki yake, tena pasipo huruma!
Kila ngumi iliyomgusa Jack, itarudi mara tatu yake. Aliapa kwenye hilo.
**
“Mbona umekawia sana?” Katie alimuuliza Marshall punde baada ya mwanaume huyo kuingia ndani. Ulikuwa ni usiku wa saa tano sasa.
“Kulikuwa kuna mambo kadhaa ambayo nisingeweza kuyaacha,” Marshall akamwambia Katie na kisha akambusu mwanamke huyo kwenye lips zake.
“Vipi lakini? Unaendelea vema?”
Katie akatabasamu.
“Nipo sawa maana upo hapa!”
Wakakumbatiana kisha Marshall akambeba mwanamke huyo juu juu mpaka kochini alipomlaza.
“Nilikukumbuka kweli,” akasema Katie. “Nilijihisi mpweke sana, siku nyingine usiwe unaniacha kwa muda hivyo Marshall.”
“Basi nimeshafika, kuna tatizo?”
Wakatazama kwa mapenzi na kupeana mabusu. Wakafurahia haswa muda wao.
Lakini wakiwa hawana hili wala lile, hawakuwa wanajua kwamba hawapo wenyewe. Nje ya kuta kulikuwa kumepaki magari manne, na bwana James Peak akiwa na maajenti wengine wa FBI pamoja na polisi walikuwa wapo maeneo ya karibu wakitazama kila kinachoendelea. Walikuwa wameshazigira eneo zima wakisubiria amri tu.
Katika hali ya kushtua, bunduki ikalia kwanguvu na risasi ikafyatuka kumfuata Marshall! Kufumba na kufumbua, risasi iyo ikatoboa kochi pembeni kidogo ya bega la mwanaume huyo.
“Amka Katie! Kimbia!” Marshall akafoka akimnyanyua Katie, mambo yalikuwa yamekwisha haribika, lakini wasifike mbali, risasi zikarushwa kwa fujo sana na tatu zikazama ndani ya mwili wa Katie!
**
*Simulizi za series*
ILIPOISHIA
“Hata nami ningependa kwenda huko kabla ya kukoma kwa maisha yangu!” Vio akasema kwa furaha. Wakakumbatiana tena na tena. Walikuwa na furaha sana, waliona sasa wameshaukwaa.
Lakini pasipo kujua, Jack Pyong alikuwa amesimama mahali akiwatazama, moyo wake ukiwa unavuja damu.
“Vio,” Jack akaita kwa kunong’ona. “Nimekukosea nini?” akauliza kana kwamba Vio yu pembeni yake kisha akajikongoja taratibu kulifuata gari.
ENDELEA
Alipolifikia hakufanya kitu bali akaendelea kutazama mpaka pale aliposhtukiwa. Vio alibumbuwaa kumwona Jack, na kwa kiasi fulani akahofu, lakini kwa upande wa Gotham kwake ilikuwa kinyume, ni kama vile alikuwa anatarajia ujio wa Jack kwani hakuwa anahofu wala kuhenya, alimtazama Jack kisha akampuuza.
“Vio,” Jack akaita na kuuliza, “nimekukosea nini wewe?”
Mashavu yake yakafunikwa na machozi, alikuwa anang’ata meno kwa uchungu. Kidogo Vio akabanwa na haya.
Lakini kadiri muda ulivyokuwa unaenda, Jack akawa anapatwa na hasira. Akajikuta akitaka kumdaka Vio na kumwadhibu kadiri awezavyo lakini Gotham akammudu mwanaume huyo na kumkandika makonde kadhaa kabla ya kumwacha hapo akiwa anavuja damu na hajielewi.
Uso wa Jack ulikuwa unavuja damu, jicho lake moja limevimba na tumbo lake linauma haswa kwa kukandikwa ngumi! Lakini Jack hakuwa anaumizwa sana na hayo majeraha bali kutendwa kwake na Vio.
Huko kulimuuma kusipokuwa na mithili. Alihisi moyo wake unasinyaa kwanguvu kumimina damu.
“Kwanini Vio?”
Alijikunyata akiwa gizani.
**
Saa mbili asubuhi …
“Nyanyuka twende!” alisema bwana Charles Smith akimtazama Miss Danielle, bwana huyo aliyekuwa amevalia suti nyeusi iliyobana mwili wake mwembamba.
Alikuwa ni mwanasheria wa Danielle. Punde alikuwa ametoka kuongea na inspekta James Peak na kaufikiana kulipeleka shauri hilo mahakamani, mahali ambapo mteja wake atapata haki yake.
Basi Danielle akanyanyuka na kuongozana na bwana Charles mpaka kwenye gari na kutimka toka kituoni. Mwanamke huyo alikuwa amejikunyata akiwa amemezwa na mawazo.
“Usijali, miss,” Charles akamtoa hofu. “Ni kesi ndogo sana isiyo na ushahidi. Tutakapoenda mahakamani haitachukua muda kuimaliza na kuifutilia mbali!”
Na zaidi bwana huyo akapendekeza waweke fidia ya juu kwa serikali kwa kumpotezea muda mteja wake na pia kumchafulia taswira yake mbele ya jamii.
“Unaonaje?” akauliza bwana Charles akitabasamu.
“Ni sawa,” akajibu Danielle kisha akanyamaza asiongeze jambo, basi safari yao ikawa kimya kwa muda.
Bwana Charles hakujua nini ambacho kinamtatiza Danielle kichwani. Alimwona mwanamke huyo akiwa ametulia kupita kiasi na kwakuwa hakutaka kumtibua akaamua naye kuufunga mdomo wake.
Walipotembea kwa muda fulani Danielle akamuuliza bwana Charles kuhusu ile fidia aliyokuwa ameisema awali, anadhani itakuwa ni kiasi gani? Hapo bwana huyu akapata kujua angalu kile ambacho kilikuwa kinakatiza kwenye ubongo wa huyu mwanamke.
Alitabasamu akimwangalia.
“Inaweza ikawa pesa kubwa sana, inategemea na wewe utakuwa unahitaji kiasi gani.”
Danielle akafikiria kidogo, ni kama vile alipata wazo jema, alifyatua miguu yake aliyokuwa ameikunyata akamwangalia bwana Charles na kumuuliza,
“Una uhakika tunaweza kushinda hii kesi?”
Bwana Charles akatikisa kichwa. “Sijaona ugumu wake, miss. Nimeshahangaika na kesi kubwa na ngumu kuliko hii … huko kote nikatoka salama!”
Kauli hiyo ikapandikiza mmea ndani ya moyo wa Danielle.
Kuna kitu alifikiria na kwa namna moja kikaukimbiza moyo wake.
**
Saa moja jioni …
“Unaweza ukapumzika sasa,” alisema Marshall akiwa anamfunika Jack shuka.
Jack alikuwa na macho mekundu ila la kulia likiwa jekundu zaidi. Uso wake ulikuwa umevilia damu na kuzibwa na bandeji baadhi ya sehemu. Alikuwa amechoka lakini pia ameumizwa. Majeraha ya mwili waweza kuyatia dawa, vipi ya mapenzi?
Marshall alikuwa anafahamu kile ambacho Jack alikuwa anapitia. Alikuwa anafahamu namna gani ambavyo mwanaume huyo alikuwa akimpenda Vio, kwa moyo wake wote, ilikuwa ni ngumu kuukubali ukweli kwamba mwanamke huyo alikuwa akimdanganya.
Ukweli ulikuwa mchungu kuukubali kuumeza.
“Jack, yapasa uache jambo hili lipite sasa,” alisema Marshall aliyekuwa ameketi pembeni ya Jack. Alikuwa akimtazama rafikiye kwa imani.
“Kuendelea kulibeba hili hakutaleta lolote jema zaidi ya maumivu. Sawa, Jack?”
Jack alikuwa akitazama kingo ya kitanda kwa fikira. Macho yake yalikuwa yanadondosha machozi. Machozi na damu.
Alimtazama Marshall kisha akamuuliza, “Ulikuwa unayafahamu haya, Tony, sio?”
Marshall akashusha pumzi ndefu puani. “Jack, si muda mzuri wa kuongelea haya.”
“Ulikuwa unafahamu, sio?” Jack akakazia swali lake. Alikuwa anamtazama Marshall kwa macho yake mekundu.
“Kwanini haukuniambia muda wote huo, Tony?”
“Jack, sikutaka kukuumiza.”
“Mbona sasa naumia?”
“Samahani, Jack. Nilitaka nilimalize jambo hili kwa mikono yangu, ni kwamba nimekawia.”
“Tony, siku zote ulikuwa unajua Vio ananizunguka lakini ukanyamaza. Umeniumiza.”
“Najua, Jack. Nisamehe sana.”
Jack akarudisha macho yake kwenye kingo ya kitanda akiendelea kuwaza.
“Kumbe ndo’ mana alikuwa anataka uondoke karibu na mimi. Ndo’ maana alikuwa hataki kuja kukuona. Kwanini sikuyajua yote haya mapema? Kwanini nilikuwa mpofu kiasi hiki?”
Marshall akamsihi Jack aachane na fikra hizo kwani zitazidi kumuumiza, lakini kidogo kwa Jack swala hilo likawa gumu, alishindwa kunyamaza, moyo ulikuwa unamuuma sana.
Mwishowe akamwomba Marshall akamletee kinywaji kikali ili apate kunywa kujipumbaza, mwanzoni Jack akawa mgumu kutimiza agizo hilo lakini alipokuja kuona kwamba pengine litakuwa ni tiba ya muda kwa Jack, akaamua kwenda zake kumfuatia.
Baada ya dakika kadhaa akawa amerejea akiwa amebebelea chupa kubwa ya vodka, akammiminia Jack glasi kadhaa na haikuchukua muda Jack akajikuta akielemewa na kichwa, akalala.
Marshall akamfunika vema shuka kisha akamtakia usiku mwema. Akiwa hapo pembeni ya Jack, akafikiria kumhusu Vio, akafikiria kuhusu Gotham.
Aliona watu hao wanastahili kuadhibiwa. Haiwezekani waishi maisha kwa furaha tele ingali wamemuumiza rafiki yake, tena pasipo huruma!
Kila ngumi iliyomgusa Jack, itarudi mara tatu yake. Aliapa kwenye hilo.
**
“Mbona umekawia sana?” Katie alimuuliza Marshall punde baada ya mwanaume huyo kuingia ndani. Ulikuwa ni usiku wa saa tano sasa.
“Kulikuwa kuna mambo kadhaa ambayo nisingeweza kuyaacha,” Marshall akamwambia Katie na kisha akambusu mwanamke huyo kwenye lips zake.
“Vipi lakini? Unaendelea vema?”
Katie akatabasamu.
“Nipo sawa maana upo hapa!”
Wakakumbatiana kisha Marshall akambeba mwanamke huyo juu juu mpaka kochini alipomlaza.
“Nilikukumbuka kweli,” akasema Katie. “Nilijihisi mpweke sana, siku nyingine usiwe unaniacha kwa muda hivyo Marshall.”
“Basi nimeshafika, kuna tatizo?”
Wakatazama kwa mapenzi na kupeana mabusu. Wakafurahia haswa muda wao.
Lakini wakiwa hawana hili wala lile, hawakuwa wanajua kwamba hawapo wenyewe. Nje ya kuta kulikuwa kumepaki magari manne, na bwana James Peak akiwa na maajenti wengine wa FBI pamoja na polisi walikuwa wapo maeneo ya karibu wakitazama kila kinachoendelea. Walikuwa wameshazigira eneo zima wakisubiria amri tu.
Katika hali ya kushtua, bunduki ikalia kwanguvu na risasi ikafyatuka kumfuata Marshall! Kufumba na kufumbua, risasi iyo ikatoboa kochi pembeni kidogo ya bega la mwanaume huyo.
“Amka Katie! Kimbia!” Marshall akafoka akimnyanyua Katie, mambo yalikuwa yamekwisha haribika, lakini wasifike mbali, risasi zikarushwa kwa fujo sana na tatu zikazama ndani ya mwili wa Katie!
**