Nyuma ya pazia Bunge live

Nyuma ya pazia Bunge live

Hapa sioni hoja yoyote ya msingi,uliyoitoa zaidi naona unatoa mapovu tu ma Mihemko yako ya kisiasasiasa!


Wanabodi,

Wote tunajua kuwa serikali imekuwa ikitafuta grounds mbalimbali za kuzuia kwanini bunge lisirushwe live.Hapo awali ilielezwa na waziri wa habari kuwa sababu kuu ni kubana matumizi ya serikali.Sababu nyingine iliyotajwa ni kuwa muda wa bunge uko sambamba na muda wa kufanya kazi hivyo watu wengi wanakuwa makazini.

Sababu hizo zilipingwa na wadau mbalimbali kwa hoja zenye mashiko lakini serikali haikusikia na mjadala wa hotuba ya Rais ukajadiliwa gizani. Wakati vikao vya bunge vinaenda kuanza, Kuna Taasisi iliamua kujitolea kulipa gharama ili bunge lirushwe live lakini sasa serikali imezuia vyombo vyote hata binafsi kurusha live muda wote kipindi cha bunge isipokuwa kipindi cha maswali na majibu. Hapa imeonekana hoja sio kubana matumizi. Pia hoja ya muda wa kazi iliisha juzi baada ya Rais kurushwa live ufunguzi wa daraja Kigamboni kwa kuwa ulikuwa muda wa kazi na watu hawakupaswa kuangalia kwa sababu walikuwa makazini.

Pamoja na kutafuta grounds mbalimbali ni sababu hizi pekee ambazo zinaweza kuingia akilini kwanini serikali haitaki bunge lirushwe live:

1.Wabunge wengi wa CCM kuwa na utamaduni wa kutowajibika bungeni, hii imepelekea wao kuwa watu wa "ndiyoo" hata kwa mambo yasiyo na faida kwa mtanzania, hata likiwa jambo la kipuuzi ilimradi limeletwa na serikali wao ni ndiyoo. Hii imepelekea kuishushia serikali na CCM heshima kwa wananchi.

2.Wabunge wengi wa CCM kutokuwa na hoja za maana za kuisimamia serikali, hii imetokana na wengi wao kubebwa bila kuwa na sifa. Hapa tunaona hata Dr anachangia kama mtoto wa darasa la pili (rejea kauli ya msigwa juu ya watu hawa kwa mkazo zaidi), hii inapelekea wao kupwaya na kuonekana wapinzani ndio husimamia serikali.

3.Uimara wa wabunge wa upinzani katika kujenga hoja, kuisimamia serikali na kutetea wananchi katika maswala yote.mfano halisi ni wakati wa sakata la ESCROW.

4.Wabunge na mawaziri wa CCM kulala bungeni hovyo, hili huwashushia heshima sana.

5.Spika na uongozi kuwaonea wapinzani bungeni.

Mambo hayo ukiyatafakari kwa makini utagundua ndio sababu pekee ambazo ni sensible na reasonable ambazo serikali inataka wananchi wasizione ili kulinda heshima na uhai wa chama. Sehemu kubwa ambayo upinzani umejijengea jina na heshima kwa wananchi ni bungeni, ndio maana serikali inataka kuminya mwanya huo. Sababu za kubana matumizi na muda wa kazi ni geresha tu, kwani zote zimeprove failure. Mwenye kuelewa ataelewa, wale wakushikiwa akili kutafuta uteuzi njooni mpambane huenda kesho ikawa zamu yenu.
 
Mwisho wa siku watasema bunge limekubaliana hata kama wengine wanapinga na hawataki tusikie hoja zinzotolewa kupinga jambo lolote
Naangalia habari sasa hivi hapa ITV kuhusu tukio la kusikitisha sana na la kizembe huko Dar es Salaam. kwenye pantoni la kwenda Kigamboni.
Msoma habari kasema kuwa mlango wa kivuko haukufungwa vizuri hivyo wakati kivuko kiko katikati ukafunguka na gari ikaserereka na kutumbukia baharini.
Dada mmoja msemaji wa TEMESA anaseema gari ilikuwa imesimama kwenye eneo la kuingilia kwenye kivuko na ndio ikaserereka na kutumbukia baharini.
Mtu wa timu ya uokozi anasema kuna kina kirefu sana hapo gari ilipodumbukia na wanatumia miwani na tochi za kawaida kuisaka huko chini ya bahari lakini hawawezi kuiona kutokana na matope na mawe.
Maelezo ya hawa watu watatu ni kuwa mtu wa TEMESA hatuwezi kumwamini wakati ndiye muhimu zaidi ya wote maana ndiyo anatoa offical statement.
Kwa maana hiyo ni bora kila kitu kikawekwa 'live' ili kila mtu aelewe kwa akili yake ili hata pale anapolipa hizo kodi ajue wanaozitumbua ni akina nani!
 
kazi gani na viwanda mmeuza na walionunua wamegeuza godown .

Hujaomba kazi kwa Dangote?

Hujaomba kazi kwenye kampuni zaidi ya 20 za gas?

Wageni wamejazana Tanzania kwa fursa zilizokuwepo za kazi za kila aina lakini hamzioni.

Sishangai kwanini huzioni kwani time ya watu kufanya kazi wewe unataka kutazama bunge.

Kalagabaho.
 
Bunge kuonyeshwa au kutokuonyeshwa live, kunawapunguzia nini Wabunge jukumu lao la kuishauri na kuisimamia Serikali?

Wakae ndani humo humo waisimamie Serikali kwa hoja zenye mashiko sio fitina fitina na uchochezi tu, baadhi Wabunge wanataka kugeuza Bunge kama ukumbi wa kufanya siasa ili kujipatia umaarufu mwepesi mwepesi huku wakionekana live.

Sasa tuone kama Bunge lisiporushwa live watatueleza walikwenda Bungeni kuonekana live, au walikwenda kuwasilisha hoja za msingi juu ya matatizo ya wananchi na kuisimamia Serikali kuhakikisha inawajibika?
mkuu kuwa muelewa. hapa hatuongelei UWAJIBIKAJI WA WABUNGE bali tunaongelea WANANCHI KUNYIMWA TAARIFA KUTOKA KWA WAWAKILISHI WAWAKILISHI (WABUNGE) WAO. umeelewa sasa? kama hujaelewa uliza.
 
Rais kufungua bunge live,waziri mkuu kuhutubia bunge live,mawaziri kuhutubia bunge live,mawaziri kujibu maswali live ila "wabunge kujadili hotuba ya Rais,waziri mkuu na bajeti za wizara gizani"
Hii maana yake nini?uhuni tu
Africa kawaida kabisa!aibu,wenzetu wanapiga hatua mbele sisi tunapiga hatua kurudi nyuma!
 
Tunakoelekea ili kumpa "kick" Rais wao Magufuli itaamuriwa au utapitishwa utaratibu wa kuhakikisha hakuna platform yoyote ambayo wote wanaomkosoa "mfalme" au wanopingana na maamuzi ya serikali wataitumia!!

Mfano inawezekana ukaja wakati hata JF itapigwa marufuku kuruhusu aidha kuchapa maoni mbadala pinzani ya bajeti kuu au ya wizara flani kama ambavyo mara nyingi imekuwa ikifanyika miaka ya nyuma.

Inawezekana kabisa pia huko mbeleni ikaja ikatolewa amri au maagizo ya electronic na publishing media yoyote kupigwa marufuku kumpa airtime au page mbunge au mtu yeyote aliye kinyume na mtazamo wa viongozi wa serikali kutoa maoni yake!!

Mpaka sasa kuna kila dalili kuwa magazeti au vituo vya TV au Redio ambavyo vina uelekeo wa kumkosoa Magufuli au serikali yake vitapigwa kufuli!!

Naona kabisa kwa upande wa magazeti ya mfano wa MwanaHalisi, Mtanzania, Tanzania Daima, Dira ya Mtanzania, MwanaHabari na mengine ya namna hiyo yakiwekwa kifungoni au kufutwa kabisa kumfuata Mawio!!

Huyu jamaa (Magufuli) si mvumilivu, ni mtu wa visasi, si mkweli na ana kila dalili za chembechembe ambazo kama hatadhibitiwa zitageuka kuwa cheche za udikteta!!

Na tayari anajitengenezea au anatengenezewa mazingira ya kutodhibitiwa na mazingira yenyewe ndiyo haya sasa; dhibiti bunge, fungia magazeti au futa kabisa, tunga sheria kandamizi nk...

Kwa sababu ukiicheki hii ishu ya bunge live broadcasting inavyoepukwa na serikali, mtu mwenye akili timamu hawezi kuelewa ni nini kipo nyuma ya pazia zaidi ya haya 100%!!

Twendeni tu tutaona huko mbeleni....
 
Mimi namshangaa Magu anachoogopa ni nii? Kama anasema tumuombee sisi watanzania huku anatuwekea ukungu kwenye mambo yanayotuhusu si muelewi vile!
Fanyeni kazi, maana wenzenu muda huo wanakuwa kazini.
 
Kwa kumtaja msigwa kwenye uzi wako umeharibu kila kitu cjuu kama kuna chiz yyte akaendelea kumsikiliza huyu pungutwo
 
Bunge kuonyeshwa au kutokuonyeshwa live, kunawapunguzia nini Wabunge jukumu lao la kuishauri na kuisimamia Serikali?

Wakae ndani humo humo waisimamie Serikali kwa hoja zenye mashiko sio fitina fitina na uchochezi tu, baadhi Wabunge wanataka kugeuza Bunge kama ukumbi wa kufanya siasa ili kujipatia umaarufu mwepesi mwepesi huku wakionekana live.

Sasa tuone kama Bunge lisiporushwa live watatueleza walikwenda Bungeni kuonekana live, au walikwenda kuwasilisha hoja za msingi juu ya matatizo ya wananchi na kuisimamia Serikali kuhakikisha inawajibika?
Utajuaje kama amekuwasilisha vyema. Huu si ndio mwanzo wa kuongopeana
 
Watafanya kazi kwa adabu kama wapo kwenye kamati.
Wabunge wa upinzani huchangia kwa kukosa adabu pale matangazo yanaporushwa papo. Wakati mwingine hutaka bunge lisitishwe kusubiri hitilafu irekebishwe ili mtu wao aongee na kutukana. Ilifanyika hivyo kwenye Bunge la katiba wakati Tundu Lisu akichangia.
Natamfaham muda wa wapinzani kuhutubia papo kwenye Tv ni kipindi cha bunge nje ya hapo ni nadra sana. Wanahaki ya kulia
Inaonyesha mawazo yako yameishia kuwakomoa wapinzani badala ya kuboresha ufanisi.
 
Naangalia habari sasa hivi hapa ITV kuhusu tukio la kusikitisha sana na la kizembe huko Dar es Salaam. kwenye pantoni la kwenda Kigamboni.
Msoma habari kasema kuwa mlango wa kivuko haukufungwa vizuri hivyo wakati kivuko kiko katikati ukafunguka na gari ikaserereka na kutumbukia baharini.
Dada mmoja msemaji wa TEMESA anaseema gari ilikuwa imesimama kwenye eneo la kuingilia kwenye kivuko na ndio ikaserereka na kutumbukia baharini.
Mtu wa timu ya uokozi anasema kuna kina kirefu sana hapo gari ilipodumbukia na wanatumia miwani na tochi za kawaida kuisaka huko chini ya bahari lakini hawawezi kuiona kutokana na matope na mawe.
Maelezo ya hawa watu watatu ni kuwa mtu wa TEMESA hatuwezi kumwamini wakati ndiye muhimu zaidi ya wote maana ndiyo anatoa offical statement.
Kwa maana hiyo ni bora kila kitu kikawekwa 'live' ili kila mtu aelewe kwa akili yake ili hata pale anapolipa hizo kodi ajue wanaozitumbua ni akina nani!
Kweli kaka
 
Mi namshauri Rais aruhusu au aamrishe bunge lionyeshwe live. Kwa sababu sera zake ni kidhibiti wizi na ufisadi, bunge kutoonyeshwa live ni sawa na mtu kusema kuwa unahitaji nuru kisha taa ya kukuwezesha hiyo nuru unaifunika isiangaze!
Katika kipindi hiki tungependa bunge liwe live ili ufisadi wote na uzembe wote uonekane kwa wote ili tujue kama wezi wote wanatumbuliwa? Dunia hii ya sasa si kipindi cha kunyimana haki ya kupata habari. Serikali iliangalie vyema, isiogope wala kuona aibu madhaifu ya waliopita yakiwekwa hadharani, yaonekane yote mabaya na mazuri.
 
Back
Top Bottom