Nyimbo kwa Waliopita JKT

Nyimbo kwa Waliopita JKT

Jkt ilikuwa poa sana, siku moja afande wetu katwambia twende Vibwende kupata machozi ya simba,halafu afande akazimika huko huko kwa babu ilikuwa kazi kumpepea. Pamoja na mapungufu yake,JKT ilikuwa safi. Shilingi ina pande mbili.

Naukumbuka wimbo wa; nampendapenda nani,yule pale. Basi wewe unakaa na yy anaimbisha disco mpaka saa 4.
 
Malela malela malela
Malela malela malela nakutafuta
Malela nasikia uko .........

Duu nakumbuka Mafinga JKT kwa afande Mlay na (twaisii) Afande Mirudi. Jamani there are a lot of good memories on JKT
RPC wa shinyanga Diwan Athmani kama umo humu unamkumbuka maafande wako Nusumungu, Mulembo, Msingwa, Rweikiza
 
hao machangudoa, mashoga, vibaka wangepelekwa jeshini hata sasa hutaamini wangerudi wamenyooka upuuzi wasingefanya.

Glory be to GOD
 
Kule kuzimu hakuna kombo, tungemkomboa Sokoine
Kule kuzimu hakuna Kombo tungemkomboa na Samora
Nalia eeh nalia mama, nalia Sokoine!

Nakumbuka saana Mlale JKT.....na maeneo muhimu, kama Lundipundipu, Masangu, Lusonga, Chipole etc!
Wapi Embakassy Uwanja wandege, shamba kubwa la mahindi, kupalilia miraba!
Mheshimiwa Sana Mbunge Janet Mhagama, kipindi hicho akiwa ametokea chuo cha Ualimu Korogwe!
Wapi Philipo Maendaenda!...!
 
hao machangudoa, mashoga, vibaka wangepelekwa jeshini hata sasa hutaamini wangerudi wamenyooka upuuzi wasingefanya.

Glory be to GOD
Wawapele mashoga ndio hawana mpango lkn machangu wanatutoa sana sie midomo zege
 
Niende Mafinga nibaki Makutu... (Mwimbishaji huku akibadili majina ya makambi - Ruvu, Buhemba, Mlale nk.) Makutu - Makutupora.

Yote Makambi makubwaaa!! (kiitikio)
Amri ya Jeshii hii inanichunguliaaa!!
Hata kama Nikijongoo oohh inanichunguliaa!!

Kwa wale wa Makutupora A coy watakumbuka

Kanadiani -- eeeee eeeee
Linaingia -- eeeee eeeee
na Gia Kubwa - eee eeeee

Kanadiani: Reference ni gari kubwa - A coy walikuwa wengi sana.

Na wale wa D Coy watakumbuka
Kindipundipu - eeee eeee
Kimevimbiwa - eee eeee
Hizo zabibu - eee eeee
Kupita Tossi -- (wote kimyaaa)
Kupita Burst -- Hakiwezi aaa aaaa Hakiweziiiii

key:
Kindipundipu: Ni jina na afande mmoja Private mnoko tulimbatiza - alikuwa mfupi na kitambi cha kwashakooo..... ha ha ha
Tossi: Kuwa na uwezo wa kuonja msosi kabla ya muda
Burst: Kurudia kuchukua msosi mara ya pili na zaidi.
 
Naukumbuka wimbo wa Malolasa nikiwa Mlale jkt mwaka 1987/1988
 
Malela malela malela
Malela malela malela nakutafuta
Malela nasikia uko .........

Duu nakumbuka Mafinga JKT kwa afande Mlay na (twaisii) Afande Mirudi. Jamani there are a lot of good memories on JKT
RPC wa shinyanga Diwan Athmani kama umo humu unamkumbuka maafande wako Nusumungu, Mulembo, Msingwa, Rweikiza

Mkuu, tulikuwa wote nini? Nakumbuka ire wimbo Kuruta na Kenge mzuri nani? Unajibu mzuri kenge. Ukisema mzuri kuruta utakula kibano.

Nakumbuka afande ndege, N yule referee Shayo.
 
Mkuu, tulikuwa wote nini? Nakumbuka ire wimbo Kuruta na Kenge mzuri nani? Unajibu mzuri kenge. Ukisema mzuri kuruta utakula kibano.

Nakumbuka afande ndege, N yule referee Shayo.
Ha ha haaa Afande referee Staff sajenti Shayo. duu umenikumbusha mbali. Na super koplo Thomas
 
Ukisikia anayesema JKT haikuwa na faida au alikuwa SELULE (mgonjwa asiyefanya kazi-waiukweli au uongo) au ***** aliyekataa kujifunza vilivyokuwa vinafundishwa kwa kujidhania ni WAMAANA KULIKO WENGINE WOTE WALIOKUWA WATIIFU NA KUJIFUNZA
 
Ikalosi mama kumbakumbaaa......Ikalosi mama kumbe yesaa....X 2
Ikalosi mtoto wa kwetuu mamaa --- eeeee chukua yotee....
 
Jeshini ilikuwa ni sehemu ya kufundisha utaifa na uzalendo. Vijana kutoka sehemu mbalimbali za nchi waliweza kukutana kambini na kubadilishana uzoefu. Kwa sasa mtoto anasoma shule ya msingi hadi....katika kata moja ambayo kuna kabila moja. Watanzania wategemee nini?
 
Back
Top Bottom