Nyeti za siri zinapochafukwa

Nyeti za siri zinapochafukwa

Mji mzito sana huu

Sir buyer hakuimbiwa parapanda, sasa limezukwa jipya.

Nyeti lazima ziwe za siri, hata zikichafukwa hazianikwi upenuni, labda zioze na kutoa uvundo mkali, lakini bado unaweza kuziswafi na tindikali kisha ukazihifadhi kwenye jokofu lililogandama kipupwe cha nyuzi baridi centigrade hasi 100.

Mji mzito sana huu. Kuna tafauti ndogo sana kati ya hasidi na hashua, japo kinyume chake kina kima cha kipenyo
Kama pembe la moo halifichiki, basi usijifanye kwio mbuni kufutika medulla ardhini ili kujikinga na hadhira isikutie machoni.

Mji mzito kwelikweli

Nyeti za siri zimeshaanza kudoda, kila mtu anatamba na kikingio chake. Hivi kudoda na kuvuja vinashabihiana ama kibantu kina maingiliano? Kwasababu tundu na tobo vinafanana lakini havishabihiani.

Je, uwazi nao ni tundu au ni tobo? Ama ni kipenyo?

Kipenyo penye uwazi, mwanya? Hupenyeza panapopenyeka na waja hupenyezeana. Wengine hupenyana
Bado tu utajinasibu na nyeti za siri?

Hivi hizi ni fununu ama ni tetesi au ni minong'ono?

Penye fununu hufunuliwa, penye minong'ono hunong'onwa, penye tetesi je? Panatestiwaa.

Nyatunyatu huleta kimuhemuhe kama kilivyo kisebubu japo hiki ni kiroho papo. Sio kiroho paaa, hiyo itakuwa blinking news! Habari za kumweka mweka

Mma yana hulka moja; hayazuiliki. Unaweza kuyakinga lakini si kuyazuia lazima yatatafuta upenyo yapenye. Na hata kama utayakinga yana kima chake. Yakizidi kima yatapasua na kuvunja kingo, na madhara yatakuwa kwa wengine wengi.

Hebu tufanyeni kikowa na kulimaliza hili lisifutikwe mchagoni, ndimi hazitatulia na midomo haitapumbaa....! na ndimi zisipotulia mafikara yataundiwa uhalisia kisha midomo itaropoka ropo!

Wakulaumiwa atakuwa nani?

Lisemwalo lipo kama halipo haliwezi kusemwa asilani.
Master piece. Well written. Well thought.
 
Mji mzito sana huu

Sir buyer hakuimbiwa parapanda, sasa limezukwa jipya.

Nyeti lazima ziwe za siri, hata zikichafukwa hazianikwi upenuni, labda zioze na kutoa uvundo mkali, lakini bado unaweza kuziswafi na tindikali kisha ukazihifadhi kwenye jokofu lililogandama kipupwe cha nyuzi baridi centigrade hasi 100.

Mji mzito sana huu. Kuna tafauti ndogo sana kati ya hasidi na hashua, japo kinyume chake kina kima cha kipenyo
Kama pembe la moo halifichiki, basi usijifanye kwio mbuni kufutika medulla ardhini ili kujikinga na hadhira isikutie machoni.

Mji mzito kwelikweli

Nyeti za siri zimeshaanza kudoda, kila mtu anatamba na kikingio chake. Hivi kudoda na kuvuja vinashabihiana ama kibantu kina maingiliano? Kwasababu tundu na tobo vinafanana lakini havishabihiani.

Je, uwazi nao ni tundu au ni tobo? Ama ni kipenyo?

Kipenyo penye uwazi, mwanya? Hupenyeza panapopenyeka na waja hupenyezeana. Wengine hupenyana
Bado tu utajinasibu na nyeti za siri?

Hivi hizi ni fununu ama ni tetesi au ni minong'ono?

Penye fununu hufunuliwa, penye minong'ono hunong'onwa, penye tetesi je? Panatestiwaa.

Nyatunyatu huleta kimuhemuhe kama kilivyo kisebubu japo hiki ni kiroho papo. Sio kiroho paaa, hiyo itakuwa blinking news! Habari za kumweka mweka

Mma yana hulka moja; hayazuiliki. Unaweza kuyakinga lakini si kuyazuia lazima yatatafuta upenyo yapenye. Na hata kama utayakinga yana kima chake. Yakizidi kima yatapasua na kuvunja kingo, na madhara yatakuwa kwa wengine wengi.

Hebu tufanyeni kikowa na kulimaliza hili lisifutikwe mchagoni, ndimi hazitatulia na midomo haitapumbaa....! na ndimi zisipotulia mafikara yataundiwa uhalisia kisha midomo itaropoka ropo!

Wakulaumiwa atakuwa nani?

Lisemwalo lipo kama halipo haliwezi kusemwa asilani.
Mshana Jr

Sir Buyer = 7ya ?
 
Hivi kwanini post yangu inahusishwa na vitu ambavyo sijaviwaza kabisa.. Why so much hallucinations Mk54
Naomba sana kinachoendelea huko kwengine kisinasibishwe na andiko langu...[emoji2839][emoji2827]dokoadokoa na nyakuanyakua haijakoma[emoji19][emoji19][emoji19][emoji19]
Heee kumbe haijakoma kaka!! Mimi nilijua kuwa biashara ya viroba ilikoma pale serikali ilipokataza vifungashio vya plastiki!!
 
Heee kumbe haijakoma kaka!! Mimi nilijua kuwa biashara ya viroba ilikoma pale serikali ilipokataza vifungashio vya plastiki!!
Kuna mabaki na masalia tunayamalizia
 
  • Thanks
Reactions: Mj1
Hivi kwanini post yangu inahusishwa na vitu ambavyo sijaviwaza kabisa.. Why so much hallucinations Mk54
Naomba sana kinachoendelea huko kwengine kisinasibishwe na andiko langu...[emoji2839][emoji2827]dokoadokoa na nyakuanyakua haijakoma[emoji19][emoji19][emoji19][emoji19]
Mbona unapaki basi ?! [emoji23][emoji1787]

Umehisi nguvu wapinzani ni ya uadui ?!
 
Hebu tufanyeni kikowa na kulimaliza hili lisifutikwe mchagoni, ndimi hazitatulia na midomo haitapumbaa....! na ndimi zisipotulia mafikara yataundiwa uhalisia kisha midomo itaropoka ropo!
 
Hebu tufanyeni kikowa na kulimaliza hili lisifutikwe mchagoni, ndimi hazitatulia na midomo haitapumbaa....! na ndimi zisipotulia mafikara yataundiwa uhalisia kisha midomo itaropoka ropo!
Kwa lugha nyepesi umesema? Bado? Mbona hueleweki?
 
Hebu tufanyeni kikowa na kulimaliza hili lisifutikwe mchagoni, ndimi hazitatulia na midomo haitapumbaa....! na ndimi zisipotulia mafikara yataundiwa uhalisia kisha midomo itaropoka ropo!

Hebu tufanyeni kikowa na kulimaliza hili lisifutikwe mchagoni, ndimi hazitatulia na midomo haitapumbaa....! na ndimi zisipotulia mafikara yataundiwa uhalisia kisha midomo itaropoka ropo!
Kaka usemi wa mtu mzima akivuliwa nguo.... haukumbukwi tena.
Au ndio twaandaa maandalizi.......tuje kuita presi konferensi
 
Kaka usemi wa mtu mzima akivuliwa nguo.... haukumbukwi tena.
Au ndio twaandaa maandalizi.......tuje kuita presi konferensi
Nanukuu.... na ndimi zisipotulia mafikara yataundiwa uhalisia kisha midomo itaropoka ropo!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom