NYARAKA: Madudu mengine ya William Mhando ndani ya TANESCO

NYARAKA: Madudu mengine ya William Mhando ndani ya TANESCO

Inabidi serikali ikae chini ije na mpango kabambe kama walivyofanya South Africa chini ya tume ya upatinishi iliyoongozwa na Desmond Tutu ya kusahau yaliyopita na kuanza upya bila kufikiria mabaya ya nyuma, hivyo na sisi ifike mahala watu waape kiapo cha utii na once mtu atakapofanya kosa ni kuchukuliwa hatua tu hata kama ni mwanamtandao mwenzako.

Tatizo hizi kambi za kuweka viongozi ndio zinasababisha maana kila mtu ana watu wake kuanzia ngazi ya siasa mpaka kwa watendaji hivyo hata kama mtu ataharibu inachukuliwa poa. Tufike mahala mtu ukifanya kosa hata kama ni kambi moja unachukuliwa hatua kali

maana halisi ya mtandao au makundi ni kulindana
 
maana halisi ya mtandao au makundi ni kulindana

Wanatia hasira hawa jamaa, mbaya zaidi nchi yetu imefika pabaya, mtu anataka kukuumiza ukigundua tatizo uka-take action kama sehemu ya kutekeleza majukumu yako anakuchukulia kama adui wakati usingegundua ulikuwa umekwisha kwa utendaji kazi wako kuonekana upo below standard
 
Wabunge ambao tayari wameweka misimamo yao wazi kumtetea Mhando ni pamoja na Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Kabwe Zitto, Mbunge wa Simanjiro, Christopher ole Sendeka. Zitto ni Mwenyekiti wa Kamati ya Hesabu za Mashirika ya Umma, wakati Sendeka ni mjumbe katika Kamati ya Nishati na Madini.
Soma: Raia Mwema - Bosi wa TANESCO amtetea mkewe


Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma, Zitto Kabwe, naye ana msimamo kuwa Mhando ameonewa na wizara inaweza kujiokoa kwa kumrejesha ofisini kisha ufanywe uchunguzi maalumu utakaoendeshwa na Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali (CAG).
Soma:
Vita kubwa TANESCO

Kwa kweli Zitto aliyataka mwenyewe. Kwa hili naona ndiyo wamemmaliza. Labda awe na ngozi ya Lowassa.
 
Mhando bana, kuongea hawezi, kuongoza hawezi, yeye anachoweza ni kimoja tu, ufisadi!!
 
Inabidi serikali ikae chini ije na mpango kabambe kama walivyofanya South Africa chini ya tume ya upatinishi iliyoongozwa na Desmond Tutu ya kusahau yaliyopita na kuanza upya bila kufikiria mabaya ya nyuma, hivyo na sisi ifike mahala watu waape kiapo cha utii na once mtu atakapofanya kosa ni kuchukuliwa hatua tu hata kama ni mwanamtandao mwenzako.

Tatizo hizi kambi za kuweka viongozi ndio zinasababisha maana kila mtu ana watu wake kuanzia ngazi ya siasa mpaka kwa watendaji hivyo hata kama mtu ataharibu inachukuliwa poa. Tufike mahala mtu ukifanya kosa hata kama ni kambi moja unachukuliwa hatua kali

sikupaii mkuu
you mean tuanze upya tuwaache waliotuibia wandelee kuzifaidi siyo!!
what a good idea!

South Africa ilikuwa juu ya apartheid siyo wizi- tofautisha
 
Afadhari tunazidi kuamka na kuvijua vivuli vya wapuuzi wasio na huruma na Watanzania
 
Kwa upande wa kanisa analosali, hawatakaa wakubali ni mwizi simply bse alikuwa ni mtoa sadaka mzuri.
 
Kinachotia hasira zaidi ni kuwa tanesco inazidi kudidimia, wakichezea hela kuneemishana na huku wanaendeleza mgao wa siri.
 
Lakini mbona wakati Mhando bado yupo Tanesco hii issue haikuibuliwa? Inaibuliwa leo wakati ameshatimuliwa!

Alikuwa anogopwa au?......


Maelezo yako sio ya kweli.

Hii ishu ya Mhando kumpa mkewe zabuni ya stationery imeanza kuongelewa bungeni wakati Mhando bado anaitumikia Tanesco. Fuatilia mijadala ya hapa JF utaliona hilo. Mwanahalisi pia waliandika sana suala hili kabla hawajafungiwa
.
 
hii ndiyo tatizo ya mikataba kufanywa kuwa siri, ni watu wachache tu huwa wanayajua haya na huwa hawatoi siri mpaka wakosane, kumsema zitto mtakuwa manakosea, tungeanza na usalama wa taifa wetu wa taifa wetu,maana hii ni kazi yao wao 100%.....

Hivi wewe unajuwa kazi za Usalama wa Taifa au unataka kuropoka hapa? Zitto Kabwe he is History now, utaki unaacha.
 
Mimi bado nnaamini kuna sehemu Zitto atakuwa anahusika haiwezekana akawa anamtetea mtu kama huyu bila sababu!
 
Dah kaka sina mengi ila ufalme wa JF utukuzwe..hii ni aibu kinachouma watu hawa wanafukuzwa tu badala ya kufungwa awana adabu kabisa
 
Mhando ameonewa na wizara inaweza kujiokoa kwa kumrejesha ofisini kisha ufanywe uchunguzi maalumu utakaoendeshwa na Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali (CAG).
Mimi si mnafiki, ni wakati wa Zitto sasa kubeba kwa mikono miwili maneno yake na kipima uzito; na huyu ndie anaetaka urais
 
Tatizo ni nini hapo?
Yaani post zote hizo hujaona tatizo?

Sasa zitto katokea wapi hapa?.....

Zitto ni Mwenyekiti wa kamati ya mashirika ya umma, ambapo Tanesco ni mojawapo ya mashirika hayo. Alikuwa anamtetea Mhando kwamba hana mawaa,sasa mawaa ndio hayo hapo juu. Aje amtetee tena.
Hivi huwa hufuatilii mijadala hapa JF? Wake up
 
Back
Top Bottom