NYARAKA: Madudu mengine ya William Mhando ndani ya TANESCO

NYARAKA: Madudu mengine ya William Mhando ndani ya TANESCO

Invisible

Robot
Joined
Feb 26, 2006
Posts
16,285
Reaction score
8,464
Wakuu,

Hivi kabla ya uteuzi wa ndugu Mhando hakukuwa na vetting? Inawezekanaje haya hayakubainika mapema?
Secret_Contact_pg1.jpg
Secret_Contact_pg2.jpg

Na baadae 2011 ikawa hivi:
Clara_2011_pg1.jpg
Clara_2011_pg2.jpg
Clara_2011_pg3.jpg
Clara_2011_pg4.jpg
 
Mkuu hii kaya iliyooza kuna wa kum-vet mwenzie kweli? Bila kuondoa huu mfumo tusahau kabisa maendeleo ambayo hayawezi kamwe kuletwa na akili zile zile zilizoyadunisha.

Natamani Uamsho, Ponda, na wanaharakati wengine focus yao kubwa ingekuwa kuwaunganisha watanzania wote dhidi ya upuuzi kama huu badala ya kujiangalia wao binafsi au makundi yao. Tuna safari ndefu mno.


PART II:

Chama cha Mapinduzi (CCM) kupitia Idara yake ya Habari na Uenezi kitaibuka soon kuipongeza Bodi ya Shirika la Umeme nchini (Tanesco) kwa kumsimamisha Mkurugenzi Mkuu kutokana na tuhuma mbali mbali.

Aidha, chama kitawaonya watendaji wengine wote wa taasisi za umma kutojihusisha na vitendo vilivyo kinyume na maadili ya kazi zao kwani sio sera ya chama wala ya serikali ya CCM.

Mwisho, chama kitawaomba watanzania wote kuwa watulivu wakati huu hatua stahiki dhidi ya "TUHUMA" hizo zikiendelea kuchukuliwa na mamlaka husika. Vilevile, kitawataka wanasiasa hususan wa upinzani na wanaharakati kutojitafutia umaarufu kwa kuzungumzia suala hili.

Itatolewa Leo,


Idara ya Habari na Uenezi, Makao Makuu.


Halafu, UWT, UVCCM, Wazee wa Mkoa wa Dar es Salaam, TAHLISO, na jumuiya nyingine za Chama zitatoa "press releases" kuunga mkono hatua hiyo. Kisha UVCCM wataomba kibali cha maandamano kuiunga mkono serikali halafu Jeshi la Polisi litayazuia kutokana na hali tete iliyopo nchini.

NA MCHEZO UTAKUWA UMEISHIA HAPO. Ha ha ha ha ha!
 
Lakini mbona wakati Mhando bado yupo Tanesco hii issue haikuibuliwa? Inaibuliwa leo wakati ameshatimuliwa!
Alikuwa anogopwa au?
 
haya hao wabunge kwenye ile kamati ya nishati na madini waliotaka mhando abaki na kwamba wakawa wanamtetea na wakawa mpaka na mpango wa kutoipitisha bajeti ya wizara ya nishati na madini wako wapi? naomba tuwataje hao wabunge hapa....WE SHOULD NAME AND SHAME THEM!!
 
Mwakamele huyu ndiyo Pedeshee Mwakamele ambaye sasa ni marehemu au huyu ni mwingine?
 
Ina maana hii ndiyo kampuni aliyoipa tender ya kusupply vifaa vya stationery kisha akasema siyo yake bali ni ya mkewe????
 
haya hao wabunge kwenye ile kamati ya nishati na madini waliotaka mhando abaki na kwamba wakawa wanamtetea na wakawa mpaka na mpango wa kutoipitisha bajeti ya wizara ya nishati na madini wako wapi? naomba tuwataje hao wabunge hapa....WE SHOULD NAME AND SHAME THEM!!
Zitto where u at?
 
Last edited by a moderator:
Kuna Mbunge mmoja namuona tuko pamoja naye hapa kwenye huu uzi, tufikishie salaam kwa Zitto Kabwe kwamba Janja yake ya Nyani tumeshambaini aendelee kuwadanganya Wasanii Wenzake wa Kigoma Leka Dutigite.

There are currently 79 users browsing this thread. (8 members and 71 guests)

 
Inabidi serikali ikae chini ije na mpango kabambe kama walivyofanya South Africa chini ya tume ya upatinishi iliyoongozwa na Desmond Tutu ya kusahau yaliyopita na kuanza upya bila kufikiria mabaya ya nyuma, hivyo na sisi ifike mahala watu waape kiapo cha utii na once mtu atakapofanya kosa ni kuchukuliwa hatua tu hata kama ni mwanamtandao mwenzako.

Tatizo hizi kambi za kuweka viongozi ndio zinasababisha maana kila mtu ana watu wake kuanzia ngazi ya siasa mpaka kwa watendaji hivyo hata kama mtu ataharibu inachukuliwa poa. Tufike mahala mtu ukifanya kosa hata kama ni kambi moja unachukuliwa hatua kali
 
Summary ya mchezo mzima iko hivi,

Mhando atatoa kiingilio cha 10Mil,

Kisha atatafuta wateja (Tanesco) na kuwapeleka kwenye kampuni ile. Mc Donald yeye atakua akipiga mzigo hapo kuhakikisha kazi inafanyika poa, huku Partner mwenza bwana Mhando akijificha nyuma yake.

Mapato watagawana 30% Mhando, 30% Mc Donald na 40% iliyobaki inabaki kwa kampuni.

Kwa wasiomjua Mc Donald ndio aliotapeliwa au kuchunwa na muigizaji wa Bongomovie aitwae Johari mtaji wa kuanzisha kampuni ya filam ambayo anaimiliki kwa ubia na msanii mwenzie Ray ya RJ Film. Johari alitoa mtaji, Ray akatoa idea
 
Back
Top Bottom