Synthesizer
Platinum Member
- Feb 15, 2010
- 14,176
- 25,919
Huko nyuma niliwahi kupendekeza kwamba ni vema Raisi Samia ajitoe kuwa mgombea Uraisi na kumwachia Polepole apambane na Lissu, kwa sababu uwepo wa Samia katika nafasi yake unaleta migongano mikubwa ambayo pia inatishia kuanzushwa uhasama kati ya Tanzania bara na Visiwani.
Baada ya barua ya Polepole ya kujiuzulu sio raisi Polepole akawa mgombea mbadala wa Samia, na huenda hata CCM wakamvua unanachama wa CCM kwa kile watakachoita utovu wa nidhamu.
Hivyo basi, kama Polepole ana uchungu na nchi hii katika suala la uongozi, ushauri wangi ni kwamba asijiuzulu na kukaa nyumbani. Anapaswa aunge mkono juhudi zinazofanya na Chadema au ACT wazalendo kuwa na mfumo wa kuuwajibisha uongozi, hata kama uongozi huo utaendelea kuwa wa CCM, pamoja na ubovu wao. Ikiwezekana aombe kuteuliwa kuwa mgombea uraisi wa mojawapo wa vyama hivi, kukiwa na maridhiano Chadema warudishwe kwenye kushiriki uchaguzi Mkuu.
Kwa hali ya hewa ya siasa nchini na mambo yalivyo ndani ya CCM, Polepole anaweza kuwa na mchango mkubwa sana katika kupata kura za watu ambao wako ndani ya CCM lakini wanakerwa sana na mambo yanayoendelea ndani ya chama hicho. Polepole anaweza kuleta "mafuriko ya watu yasiyozuiliwa kwa mikono" kama ilivyokuwa kwa Lowasa.
Ideally, kama Samia hataki kujitoa, basi tuwapambanishe Samia na Polepole kwenye kinyang'aniro cha uraisi na tuone Watanzania wataamua vipi.
Baada ya barua ya Polepole ya kujiuzulu sio raisi Polepole akawa mgombea mbadala wa Samia, na huenda hata CCM wakamvua unanachama wa CCM kwa kile watakachoita utovu wa nidhamu.
Hivyo basi, kama Polepole ana uchungu na nchi hii katika suala la uongozi, ushauri wangi ni kwamba asijiuzulu na kukaa nyumbani. Anapaswa aunge mkono juhudi zinazofanya na Chadema au ACT wazalendo kuwa na mfumo wa kuuwajibisha uongozi, hata kama uongozi huo utaendelea kuwa wa CCM, pamoja na ubovu wao. Ikiwezekana aombe kuteuliwa kuwa mgombea uraisi wa mojawapo wa vyama hivi, kukiwa na maridhiano Chadema warudishwe kwenye kushiriki uchaguzi Mkuu.
Kwa hali ya hewa ya siasa nchini na mambo yalivyo ndani ya CCM, Polepole anaweza kuwa na mchango mkubwa sana katika kupata kura za watu ambao wako ndani ya CCM lakini wanakerwa sana na mambo yanayoendelea ndani ya chama hicho. Polepole anaweza kuleta "mafuriko ya watu yasiyozuiliwa kwa mikono" kama ilivyokuwa kwa Lowasa.
Ideally, kama Samia hataki kujitoa, basi tuwapambanishe Samia na Polepole kwenye kinyang'aniro cha uraisi na tuone Watanzania wataamua vipi.