NJAA YAJA: Dear Mr. President, On a Serious Note...

NJAA YAJA: Dear Mr. President, On a Serious Note...

Huyu huyu aliwahi kutwambia kwamba' "Hakuna mtoto wa maskini Tanzania atakayekosa elimu ya juu" na ukweli kuhusu yanayojiri pale UDSM unapingana na kauli yake hiyo. Hivyo hili pia inaweza kabisa kuwa ni kujiosha tu machoni mwa Watanzania.
Kama taratibu zitafuatwa ni kweli hakutakuwa na mtoto wa maskini ambae atakosa elimu ya juu. Walengwa katika hili wanakosa nafasi hiyo kutokana na baadhi ya watu kujivisha nafasi hiyo ili kupata njia mtelemko ya kupata elimu hiyo ya juu.
 
Date::3/2/2009
Tishio la njaa: Tanzania haina Sera ya Taifa ya Chakula
Na Lugano Uli Mbwina
Mwananchi

WAKATI serikali inakiri kukabiliwa na upungufu mkubwa wa chakula katika mikoa zaidi ya 10, imefahamika kuwa mpaka sasa hakuna Sera ya Taifa ya Hifadhi ya chakula inayofahamika, isipokuwa rasimu ya sera ya 2005 ambayo imepitwa na wakati.

Taarifa hiyo imepatikana katika mkutano wa kitaifa wa kujadili tishio la uhaba wa chakula linaloikabili Tanzania pamoja na nchi nyingine zinazoendelea duniani kote.

Mkutano huo wa siku moja uliofanyika katika ofisi za Taasisi ya Utafiti,Uchumi na Jamii (ESRF) jiini Dar es salaam, pamoja na kushirikisha wataalam wa chakula nchini, ulisimamiwa na wataalam wawili kutoka Taasisi ya Kimataifa ya Chakula, Sera na Utafiti yenye makao makuu jijini Washington, Marekani.

Katika baadhi ya mapendekezo ya kuinusuru nchi hii katika janga la uhaba wa chakula, wataalamu hao, Teunis van Rheenen na Suresh Babu, walipendekeza kuanzishwa kitengo mahsusi kwa ajili ya kukusanya taarifa za hali ya chakula nchini.

Kwa kuwa taasisi yao iko mbioni kuanzishwa kituo cha kimataifa cha habari za chakula kwa njia ya inteneti, habari toka Tanzania zitakuwa na nafasi katika kituo hicho na pia Tanzania itakuwa na uwezo wa kupata taarifa za hali ya chakula kutoka sehemu mbalimbali duniani kwa kutumia mtandao wa kituo hicho, kwa mujibu wa wataalamu hao.

Hata hivyo, kinyume na ilivyotegemewa, wadau muhimu katika sekta ya chakula nchini ambao walialikwa, hawakuhudhuria isipokuwa kiasi cha wajumbe kiasi cha wajumbe watano kati ya 20 waliokuwa katika orodha ya waalikwa.

Wengi wa waliokosekana katika mkutano huu ni kutoka wizara za serikali zinazohusika na masuala ya chakula na hifadhi ya chakula.


Pamoja na kukosekana kwa sera ya chakula, mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo (FAO) aliyejitambulisha kwa jina la Sussane alishauri kuwa huu ni wakati mwafaka kuirejea rasimu hiyo ya chakula kwa lengo la kuirekebisha kwa kuwa imepitwa na wakati.

Mkutano huo unafanyika siku moja baada ya Rais Jakaya Kikwete kuwatangazia wananchi kuwa taifa limebakiwa na akiba kidogo ya chakula na kutoa tahadhari kwa wananchi kutumia kwa makini akiba yao.

Hata hiyo kwa mujibu wa majadilano ya mkutano huo, ilifahamika kuwa idara za serikali zinazohusika na hifadhi ya chakula nchini hazina taarifa na takwimu sahihi kwa sababu wakati mwingi hutumia takwimu zilizopitwa na wakati.

Pia ilifahamika kuwa wakati mwingine kutokana na kukosekana kwa sera ya chakula kitaifa, baadhi ya takwimu ambazo si sahihi hutumika ili kukidhi matakwa ya kisiasa.
 
Tangu Aprili 15 mwaka jana nilipaza sauti yangu pweke kuliamsha taifa kuhusu njaa ijayo. Leo hii, habari zote ambazo nimefuatilia zinaonesha kuwa njaa yaja mapema zaidi na taifa halijajiandaa na kama kawaida watawala wetu wameshaandaa barua zao za kuomba kwa wakwe misaada ya chakula na hivyo kuendeleza kujenga utajiri wao.
 
Why tuwe na njaa? Sielewi kabisa...
swali zuri sana hili.yale yale ya graduates wa SUA badala ya kwenda kuhimiza kilimo bora na chenye tija vijijini wanajazana benki kuwa ma loan office na ma teller...halafu unazindua mkakati wa KILIMO KWANZA.....!!!! najutaaa kuwa mtanzania
 
Mwanatanu..unajua kuna wakati nafikiri Mungu akiingalia Tanzania anatikisa kichwa kwa masikitiko na kuuliwa "niwape nini watu hawa"?

MMM maneno haya yamenitia uchungu sana...we dont deserve all these shits...kweli Tanzania ya leo tunalia njaa kweli ,wako wapi viongozi??
 
akiba ya chakula tanzania ipo tena kubwa sana, jamani hadi muambiwe kila kitu ?

chakula kipo, na kama hakipo, basi mnafaa kulaumiwa nyinyi mnaolalamika ! Hamtaki kwenda kwenye mashamba kazi kwenye intaneti 24/7, mara ya mwisho Mnyika alikataa kata kata ushauri wangu wa kwenda shambani instead akaenda kwa wamachinga.

Kila mmoja humu anaweza kulima hekari 20 kutokana na uwepo wako humu ( kuna baadhi wanalala humu humu) hao nadhani wanaweza kuzalisha zaidi ! kama akina mwafrika wa kike !

mkuu sijaelewa sehemu hiyo niliyopigia mstari naomba muongozo
 
suala la njaa ni kweli linakuja na lilishaanza kuonekana...ukiacha mvua ambazo zimeharibu mazao, kuna sehemu nyingi mvua hazikuwepo kabisa mwaka huu na wakulima walipanda kusibilia mvua za mwezi wa3 ambazo zilipita lashlasha tu....hali ya hewa imebadilika sana inabidi suala la kilimo cha umwagiliaji lipewe msisitizo mkubwa na wakulima wabadilike sasa...
 
Hata hivyo njaa ambayo naweza kuiangalia toka mbali na inayosogelea kama simba anyatiaye haitokani na mambo hayo bali makubwa mawili.

a. Kupanda kwa bei ya chakula duniani.
Habari za leo ni kuwa bei ya chakula duniani imepanda kwa haraka kuliko wakati wowote ule na hivyo kusababisha ugumu wa kupatikana kwa chakula. Yaliyotokea Haiti na Misri siku chache zilizopita ni dalili ya ubaya wa hali hiyo. Kwa wale walioko Dar au maeneo yenye masoko ya kudumu na kwenye mialo mbalimbali kanda ya ziwa wanaweza kutusaidia kutuambia kama kumeanza kutokea mabadiliko yanayoonekana ya bei ya chakula siku hizi chache zilizopita.

b. Mvua ya masika.
Hata hivyo naamini kwa upande wa Tanzania kitakachosababisha njaa sana ni hii mvua ambayo imeharibu mashamba na mazao ya watu kiasi kwamba baadhi ya maeneo ambayo kwa kawaida yana chakula cha kutosha yanaweza kujikuta yanahamia mwaka huu. Kama mpunga wa Kyela utakuwa umeathirika kama Dr. Mwakyembe alivyosema kwenye mahojiano yake nami kuna uwezekano kuwa Mwaka huu bei ya Mchele nayo itapanda na hivyo kufanya nafaka hiyo ianze kuwa adimu na kupatikana kwa wachache.

Kwa vile tunajua haya yote na ziada; tufanye nini ili tujiandae na njaa ijayo?

c. ElNino inakuja Mikoa 16 / 21 Tanzania kuanzia mwezi ujao.
(Source:The Guardian 6, August 2009) Hapa napo sijui tumejiandaa?
 
Sisi tunapenda kuishi kwa bahati na kwa kudra; kitu kinachoitwa "kujiandaa" kinafanywa kwa kibaba sana. Matokeo yake huwa tunalipa gharama kubwa kweli.
 
Kama tuna serikali kubwa namna hii, yenye waziri, naibu waziri, katibu mkuu, mkurugenzi wa wizara na maofisa kibao wa wizara husika wanafanya nini? Kweli hawa ni mzigo kwa walipa kodi.
 
Kama tuna serikali kubwa namna hii, yenye waziri, naibu waziri, katibu mkuu, mkurugenzi wa wizara na maofisa kibao wa wizara husika wanafanya nini? Kweli hawa ni mzigo kwa walipa kodi.

Na tukitoa Mawaziri kumi tu katika Baraza lao basi hatutakuwa na njaa asilani
 
Bajameni habari ndo hiyo na lisemwalo lipo ka halipo basi li njiani. Zaidi wana JF erimisheni umma kuweka akiba kwa wakati mgumu usemwao. Mie sishangi kwa hili yawezekana unabii unatimia. Tusiwe ngedere aliye juu ya mti ikishangilia kuungua kwa msitu akali yumo humo. Zaidi ni kuwashawishi washauri na wataalamu kusimama katika nafasi zao ili kulinusuru Taifa letu ktk balaa hili. Maana kama tunaweza kuwashawishi watu fufani kugombea nyadhifa mbalimbali na ikawa si zaidi kwa hili??????
 
Bajameni habari ndo hiyo na lisemwalo lipo ka halipo basi li njiani. Zaidi wana JF erimisheni umma kuweka akiba kwa wakati mgumu usemwao. Mie sishangi kwa hili yawezekana unabii unatimia. Tusiwe ngedere aliye juu ya mti ikishangilia kuungua kwa msitu akali yumo humo. Zaidi ni kuwashawishi washauri na wataalamu kusimama katika nafasi zao ili kulinusuru Taifa letu ktk balaa hili. Maana kama tunaweza kuwashawishi watu fufani kugombea nyadhifa mbalimbali na ikawa si zaidi kwa hili??????

Kwa sasa hivi kwa kweli tumechelewa; kilichobakia ni kuanza kuandika barua za kuomba misaada ya chakula kutoka kwa "wakwe".
 
Kwa watanzania tulioaangalia taarifa maalum Iiyokusanywa na ITV kuhusu kukabiliwa na njaa kali kwa wilaya arubaini ,...tulipatwa na simanzi sana ,....kuona watu live wanaokula uji wa magome ya ubuyu baada ya siku mbili.....luona watu wanaokula ma gongo huko mtwara na kwingineko,...ni kama vile nchi haina serikali...

Najiuliza kuwa wilaya 40 zinapokumwa na njaa ya ajabu ..... ni robo ya nchi....najiuliza kweli viongozi wetu wanasubiri kula chakula mezani na kusaza wakati watu wanakufa,ndo maana nyerere alisemaga kuwa IKULU NI MATESO.....kwa mtu makini hatapata uzingizi kwa hali ya sasa ya nchi......maneo mengi watu wamehama wameacha makazi yao wanaenda kuhemea vyakula...hata uchaguzi msichangae ...watu maeneo hayo kushindwa kushiriki au wagombea kupita bila kupingwa ....watu wana njaaa!!

Hapo ndipo tunapojiuliza ...umakini wa serikali hii...ya JK..ni mtihani pia kwa pinda ...waziri mkuu...tunampima...kwani mwenzake lowassa pamoja na yote lakini katika hili he was firm...na hakusita kupigana "kavu kavu "na wakuu wa wilaya kwa ajili ya hili...na ilikuwa mwaka 2006..kulikuwa na njaa na walijitahidi kuagiza mahindi mapema ....na mbegu...safari hii imekuwaje....JK UMEISHIWA NGUVU HATA YA KULISHA WANANCHI WAKO WANAKUFA.....////?????...ni kiapo chako cha kwanza kabisa ....

NAOMBA WALIONGALIA KILE KIPINDI MMWAGE HISIA ZENU HAPA..LABDA WATASIKIA!!
 
Mkuu;

Niliangalia hicho kipindi maalumu, I felt like crying . . . .

Nikaumia zaidi na kujilaumu kwamba wakati mimi nakula na kusaza, kuna watu wanakufa. I wish they were close nisaidie ninapoweza.

naibu Waziri wa kilimo anulizwa, anadai chakula kipo inatakiwa wakifuate katika maghala na kuwa labda hawana fedha za usafiri . . . . Grrrrrrrr I was shocked to hear that.

Then sijui chakula cha msaada ni kilo 10+ kg kwa kaya. I wonder kitawachukua muda gani kabla ya kwisha.

Tanzania hii yenye neema watu wanakula mizizi kweli . . . something is wrong in this country.

The question is: What is wrong and what can be done to bring positive changes?
 
Mkuu;

Niliangalia hicho kipindi maalumu, I felt like crying . . . .

Nikaumia zaidi na kujilaumu kwamba wakati mimi nakula na kusaza, kuna watu wanakufa. I wish they were close nisaidie ninapoweza.

naibu Waziri wa kilimo anulizwa, anadai chakula kipo inatakiwa wakifuate katika maghala na kuwa labda hawana fedha za usafiri . . . . Grrrrrrrr I was shocked to hear that.

Then sijui chakula cha msaada ni kilo 10+ kg kwa kaya. I wonder kitawachukua muda gani kabla ya kwisha.

Tanzania hii yenye neema watu wanakula mizizi kweli . . . something is wrong in this country.

The question is: What is wrong and what can be done to bring positive changes?

......IT WAS very sad wale kinamama na watoto wanavyolia......tunaishi karne ya mawe .leo hiii ..pesa za kuiba benki kuu zipo lakini kutoa bilioni kadhaa kununua mahindi ya msaada marekani inashindika ....nini mahindi hata soko la ndani lina mihogo mingi tu ambayo kibinaadamu ni bora kuliko kuona wenzetu wanakula mizizi......ni dhambi!!!!!!!!!
 
Habari hizi zina sikitisha sana mbona mkuu lakini ujatueleza sababu zenyewe kamili amna mvua huko au la? yaani na sababu zingine za hiyo njaa zaidi ya uzembe wa serikali ambao unajulikana.
 
Watu walikuwa busy na uchaguzi, muda wote priority ilikuwa uchaguzi wa serikali za mitaa sasa uchaguzi umekwisha tusubiri wapongezane halafu ndo waangalie sasa matatizo ya wananchi. Any way hii ndio tanzania
 
Back
Top Bottom