NJAA YAJA: Dear Mr. President, On a Serious Note...

NJAA YAJA: Dear Mr. President, On a Serious Note...

No Mwanakijiji, Serikali haijaamka. Imegeuka ubavu wa pili. Si umesikia sasa mkakati wa kulima mazao si kwa ajili ya Chakula bali kwa ajili ya ethanol ili kuanza kujipatia nishati ya mafuta kwa unafuu au kushibisha "mabosi" ambao wanataka kukataa mafuta ya miamba ile waanze kuvuna mafuta ya mahindi?
 
Ndugu zangu, kuna uwezekano mkubwa kwamba itakapofika kiangazi mwaka huu, Taifa letu linaweza kujikuta kwenye upungufu mkubwa wa chakula ambao siyo tu unatishia maisha ya watu wetu bali pia unashusha hadhi na utu wa mwanadamu. Hakuna kitu kinachomdhalilisha mwanadamu na kuweza kumfanya awe mtu kama njaa.

Ni njaa ndiyo inayoweza kumfanya mtu aukane urithi wake wa kwanza kama alivyofanya Esau na ni njaa ambayo ilikuwa inatumika tangu enzi za kale kama silaha ya mwisho ya vita ambayo inalazimisha watu kusalimu amri.

Tanzania tutakabiliwa na njaa ambayo chanzo chake si ukame. Mara nyingi (kama siyo zote) njaa husababishwa na ukame na vita. Hata hivyo njaa ambayo naweza kuiangalia toka mbali na inayosogelea kama simba anyatiaye haitokani na mambo hayo bali makubwa mawili.

a. Kupanda kwa bei ya chakula duniani.
Habari za leo ni kuwa bei ya chakula duniani imepanda kwa haraka kuliko wakati wowote ule na hivyo kusababisha ugumu wa kupatikana kwa chakula. Yaliyotokea Haiti na Misri siku chache zilizopita ni dalili ya ubaya wa hali hiyo. Kwa wale walioko Dar au maeneo yenye masoko ya kudumu na kwenye mialo mbalimbali kanda ya ziwa wanaweza kutusaidia kutuambia kama kumeanza kutokea mabadiliko yanayoonekana ya bei ya chakula siku hizi chache zilizopita.

b. Mvua ya masika.
Hata hivyo naamini kwa upande wa Tanzania kitakachosababisha njaa sana ni hii mvua ambayo imeharibu mashamba na mazao ya watu kiasi kwamba baadhi ya maeneo ambayo kwa kawaida yana chakula cha kutosha yanaweza kujikuta yanahamia mwaka huu. Kama mpunga wa Kyela utakuwa umeathirika kama Dr. Mwakyembe alivyosema kwenye mahojiano yake nami kuna uwezekano kuwa Mwaka huu bei ya Mchele nayo itapanda na hivyo kufanya nafaka hiyo ianze kuwa adimu na kupatikana kwa wachache.

Maeneo ambayo mchele ndiyo chakula kikuu na pia zao la biashara watajikuta wanakabiliwa na upungufu wa fedha za kununulia hata vitu vingine na hivyo kusubiri chakula cha misaada.

Kwa vile tunajua haya yote na ziada; tufanye nini ili tujiandae na njaa ijayo?

Kwanza natoa shukurani kwako Mzee MJJ kutukumbusha hili swala la njaa wakati wengi wetu macho namsikio yako kwenye ufisadi....hali inayo kuja ni ngumu someni hii link hapa chini

http://news.bbc.co.uk/1/hi/world/7432583.stm#map
http://news.bbc.co.uk/1/hi/talking_point/7434509.stm

Nakubaliana nawe katika ile thread yako 14022 -Kupanga ni Kuchagua.
turudishe nguvu zetu kwenye kilimo maana hali ni mbaya sana inakuja,kama vile zamani mashuleni watu walikuwa wakijitosheleza kwa mboga.

Leo na mungu apishe mbali ikitokea njaa hakuna wa kuweza kutusaidia. nchi ambazo walikuwa wakizalisha mazao ya chakula kwa wingi kama vile Canada Marekani Argentina .n.k.... wanazalisha mazao kwa ajili ya biofuels.

Tunakuja mwishowe kuishia na ma GM chakula na sasa hivi hawa jamaa MONSANTO wanachukulia haya matizo ya njaa kwa faida yao.....soma link hii chini


http://www.nytimes.com/2008/06/05/b...r=rssuserland&emc=rss&oref=slogin&oref=slogin

Mungu tunaomba utuepushie na janga la njaa.....AMEN
 
Mwanatanu..unajua kuna wakati nafikiri Mungu akiingalia Tanzania anatikisa kichwa kwa masikitiko na kuuliwa "niwape nini watu hawa"?
 
Mwanatanu..unajua kuna wakati nafikiri Mungu akiingalia Tanzania anatikisa kichwa kwa masikitiko na kuuliwa "niwape nini watu hawa"?

Nchi nyingi zilizoendelea wana tabia ya kurithina,yaani mkulima basi familia yake itakuwa wakulima. Sisi Tanzania JKN alikipa kipa umbele kilimo ndio maana tuna mbwana shamba in surplus tofauti na hizi serikali za Mwinyi,Mkapa na JK wao wameshupalia madini wakati hatuna madini engineer wa kutosha sidhani kama wanafika hata 30 nchi nzima.

Na wakulima wengi sasa waliobaki ni older generation hawa new generation wote wamekimbilia dar kupiga madebe na kuuza vitu toka China au wengine kufungua maduka. Na hii imetokana haswa na mambo makuu mawili,kwanza hawa vijana wengi(watoto wa wakulima) wamekosa mwelekeo, kwa kuwa serikali zote baada ya JKN zimekuja na kubomoa ile nguzo alizotuachia..kilimo na viwanda. Pili kwa vile sisi watanzania tuna hulka ya uvivu na tamaa ya mapato ya haraka haraka ndio hii new generation ya vijana haiko tena vijijini imekuja mjini.

Naomba sana wabunge wetu waanze kurudisha ile mentality ya watu kupenda kilimo wakumbuke enzi zile za mzee JKN aliposema badala ya kupanda maua barazani kwenu pandeni chakula...wengi walimlaumu lakini nia yake kubwa ni kutujengea mentality ya kuwa kilimo ni muhimu.

Nakumbuka enzi za late 80's ilikuwa ni mtindo wa watu wakati wa weekend watu wanaenda kwenye vi bustani vyao vya mboga na household nyingi walikuwa wana vi poultry farm vyao vidogo.....yote hayo hamna tena kila mtu sasa anataka kwenda China na Dubai......kilimo chetu,viwanda vyetu ....KUFA KABISA.

MKJJ kuna swali lingine linatisha ni hili la GM food kama tujuavyo viongozi wetu walivyokuwa taahira naogopa wanaweza kukubali hii GM seeds bongo maanake jirani zetu Uganda wameshaanza kuipigia ngoma ndogo ndogo.
http://news.bbc.co.uk/1/hi/world/africa/7428789.stm

Na nakutahadharisha JK...ufisadi au haya madini hayataweza kukuangusha lakini ole wako usiombe njaa hiyo itakuangusha na utaburutwa barabarani hapo ndipo mtajua kuwa Watanzania sio wapole kama mnvyodhani.
 
Unajua tatizo ni kuwa kilimo ni sekta duni.. kwa watu wengine kilimo kimegeuka kuwa kitu cha fedheha na kazi ya kutweza. Sababu kubwa ni kuwa bado ni kilimo cha kuhenyeka. Kwa baadhi ya watu kuwa mkulima ni sawa na kutokuwa msomi n.k Leo hii sijui ni wahitimu wangapi wa Sokoine University ambao ni wakulima wa mashamba yao wenyewe na jinsi gani wametumia kilimo chao kuwa mfano?

Je maeneo yanayozunguka Sokoine yamenufaika kwa kiasi gani na elimu inayotolewa kwenye Chuo hicho? Tuna vyuo vya Kilimo Uyole, na taasisi kadhaa za utafiti wa mazao n.k Tuna ardhi yenye rutuba, maji kibao (kuliko nchi yoyote ya Afrika) n.k Kwanini tuje kufa njaa wakati nchi kama Israeli iliyoko jangwani ndani ya miaka 50 wameweza kugeuza jangwa kuwa chanzo cha chakula cha kujitosheleza tu?
 
Unajua tatizo ni kuwa kilimo ni sekta duni.. kwa watu wengine kilimo kimegeuka kuwa kitu cha fedheha na kazi ya kutweza. Sababu kubwa ni kuwa bado ni kilimo cha kuhenyeka. Kwa baadhi ya watu kuwa mkulima ni sawa na kutokuwa msomi n.k Leo hii sijui ni wahitimu wangapi wa Sokoine University ambao ni wakulima wa mashamba yao wenyewe na jinsi gani wametumia kilimo chao kuwa mfano?

Mkuu mwanakijiji, kuna hoja moja ambayo serikali haijaiweka sawa for all these yrs (Masoko). Mimi nikiwa kama mtoto wa mkulima. Kilimo kimekuwa a very dissapointing career in the last two decades especially in the big four regions ( Rukwa, Mbeya, Iringa na Ruvuma). Tatizo kubwa likiwa ni soko kwani wakulima wa maeneo haya hulima mazao ya chakula kwa matumizi yao na kibiashara. Wakati serikali ikitamba majukwaani kupiga marufuku mazao ya chakula kuuzwa nje huwa hata hawafikirii wakulima watatokaje? Mimi katika kukua kwangu all the biggest achievements alizopata mzee wangu kupitia kilimo ilikuwa ni kuuza mazao aliyoyalima nje hasa Zambia, malawi na DRC. (directly or indirectly).

Nimewahi kuandika humu kwamba katika historia ya nchi hii end of 2007 pembejeo zilipanda bei to an extent ya mfuko wa mbolea kuwa expensive zaidi ya baiskeli. Imagine 70-80,000 (Ukiangalia mtandaoni same product ni $9 - $15). Bado kuna mbegu, labour, capital ambavyo vyoote serikali huwa haisemi chochote bali inapokuja kwenye mavuno ndio wanajifanya kuweka ban kuuza nje. Lazima tuelewe zile ile theory ya demand na supply itaendelea kuplay no matter what. Sasa kama gunia la maharagwe ni sh.50,000 Tanzania and just accross the border (100km away) ni 120,000 kwa nini watu wasipeleke huko??? Maana ni business.

Hivyo basi kutoakana na theory ya mtaji na faida kuonekana haiko practical kwenye kilimo hata sisi watoto wa wakulima hatuko tayari kujishughulisha na shughuli hiyo. It is hectic and demanding - I have been there, I am there and I know it.

It is very dissapointing kuona kwamba mkulima anayelima around ekari 20 - 50 ana maisha mabovu kulika vijifisadi vinavyotumika kwa mabepari kwa mshahara wa $300 kwa mwezi. Lakini ndio hali halisi na si kwamba hao wakulima ni wajinga but the system can't just let them in. They know what a better life is and are always thinking of getting there..

Mkulima wa kweli ni tofauti na kada nyingine yeyote akipata hela jambo la kwanza ni maandalizi ya kulima the next yr na ikiwezekana bigger than the previous. Lakini huwa inakuwa unrealistic kutokana na kupanda bei za pembejeo mwaka hadi mwaka na masoko yaliyobanwa.

Sasa basi serikali iache longolongo kama kweli ina nia njema na taifa hili kuhusu chakula. Sera madhubuti na practicable ziwekwe mfano masoko ya uhakika, kuregister wakulima woote na kumonitor statistics, kuweka ruzuku kwenye pembejeo na kuhakikisha zinawafikia walengwa ( I can see someone screaming out there kwamba hilo tayari linafanywa, lakini ni kiini macho - In short haipo), Kuziempower zile research centers za kilimo kama enzi za mwalimu (Hivi mnajua kuwa eneo la kilimo mpaka mid 90's lilkuwa na PhD's nyingi kuliko fani yoyote ile?). Kukomesha ufisadi (maana hii fani imekuwa more attractive), Kuboresha shule, zahanati na miundombinu ya vijijini hasa maeneo yanayolimwa hayo mazao ya chakula, kutoa hata ikiwezekana ruzuku ya unafuu wa ada shuleni kwa watoto wa wakulima, kutoa motisha kwa wakulima (Mwalimu used to do this kwenye vijiji vya ujamaa - Mnakumbuka kijiji bora cha ujamaa - Isansa).

Kuna hili alilolizungumzia mwkjj la kuiboresha sekta hiyo na ikiwezekana kuelevate its status naomba tuendelee kudebate on that.
 
Nimechukua nafasi kuwaandikia e-mail waziri wa kilimo inabidi tukumbushane ingawaje hawa viongozi wetu ukiwatumia barua wanakuwa na hisia mbaya....ati unawafundisha kazi yaani hawako tayari kabisa kusikiliza maoni na kero ya waajiri wao ambao ni sisi wananchi.

to
swasira@parliament.go.tz,
ddavid@parliament.go.tz
cc

info@raiamwema.co.tz,
tzdaima@freemedia.co.tz,
editor@thecitizen.co.tz
date 5 Jun 2008 15:26
subject KILIO CHA WANANCHI
mailed-by googlemail.com

Mheshimiwa Waziri Wassira,
Mheshimiwa Naibu Waziri Mathayo.

Mimi kama mwananchi wa nchi yetu hii tukufu yenye neema Tanzania nakerekwa na hili balaa ya njaa ambayo inatabiriwa kuwa inakuja.
Naombeni kwa taadhima mtueleweshe michakato yenu kama wizara mnafanya nini ili tuweze kuepukana na hili balaa ya njaa maana itakuwa aibu kwetu sisi kama nchi,yenye watu milliono 56 tukategemea msaada wa chakula kutoka nje,ni aibu na ni aibu zaidi ikiwa bajeti yetu tunategemea wafadhili na sasa chakula.

Napenda kuchukua nafasi vilevile kuwakaribisha mkasoma maoni mengi tu kuhusiana na swala hili la njaa kutoka kwa Watanzania waliko pande zote za dunia.Hii ni hapa link

https://www.jamiiforums.com/showthread.php?t=12051

https://www.jamiiforums.com/showthread.php?t=14022

Nitashukuru sana kama mtachukua nafasi mkasoma hayo maoni ya watanzania wazalendo .
Asanteni sana
MUNGU IBARIKI NCHI YETU TANZANIA

Nilishawahi kutoa maoni kuhusu kijiji chetu cha londoni kilichoko Manyoni...sasa hivi kjiji hicho kina wachimbaji wengi wadogo wa dhahabu ambao wamekata miti sana...nikawaandikia wahusika waje waone miti inavyokatwa kwa ajili ya migodi na nikatoa maoni kuwa walazimishwe wenye migodi wapande mbono pale wanapokata miti ili isiwe ikawa jangwa lakini paka leo hakuna majibu wala lilofanyika.Mvua ikinyesha kidogo kunatokea mmomonyoko wa ardhi utaastajabu
 
Mwanatanu.. that is what I call action.. na miye naikopy na kuirusha kwa wakulu wengine na kesho naanza kampeni ya kuwapigia simu wabunge.. inatosha kuzungumza... it is about time we should take action..
 
a. Kupanda kwa bei ya chakula duniani.
Habari za leo ni kuwa bei ya chakula duniani imepanda kwa haraka kuliko wakati wowote ule na hivyo kusababisha ugumu wa kupatikana kwa chakula. Yaliyotokea Haiti na Misri siku chache zilizopita ni dalili ya ubaya wa hali hiyo. Kwa wale walioko Dar au maeneo yenye masoko ya kudumu na kwenye mialo mbalimbali kanda ya ziwa wanaweza kutusaidia kutuambia kama kumeanza kutokea mabadiliko yanayoonekana ya bei ya chakula siku hizi chache zilizopita.Kwa vile tunajua haya yote na ziada; tufanye nini ili tujiandae na njaa ijayo?
Naomba kutofautia na wewe hapa. Watu watakaopata shida ni wale wenye kutaka chakula ambacho kimekubalika duniani kama mahindi, mchele, maharage na vitu kama hivyo.
Kama tukirejea kwenye vyakula vyetu vya asili, Viazi vya aina kadhaa, mihogo, mboga nyigi tu, nyama za aina kibao, hatutakuwa na neno.
Ni mtazamo tu.
unless hali ya hewa iwe mbaya.
 
Serikali kupambana na upungufu wa chakula

2008-06-07 21:46:50
Na Radio One Habari

Serikali imewahakikishia wananchi kuwa imejiandaa vya kutosha kukabiliana na changamoto ya tishio la upungufu wa chakula ambao unaikabili dunia hivi sasa.

Akizungumza na wazee wa mji wa Shinyanga Makamu wa Rais Dakta Ali Mohammed Shein amewaambia wazee hao walioonesha wasiwasi wa kuwepo kwa tishio la njaa nchini kuwa serikali imeliona tishio hilo na hatua zimeanza kuchukuliwa.

Makamu wa Rais amesema nchi haijafikia hatua za kukosa chakula japo kuna baadhi ya wilaya zina upungufu lakini pia ziko wilaya zenye ziada ya chakula.

Amesema pamoja na hatua hizo ambazo alizitaja kuwa ni za muda mfupi lakini ili kujitosheleza kwa chakula serikali inaendelea na utekelezji wa mkakati wake wa kuimarisha kilimo mkakati ambao umetilia mkazo kilimo cha umwagiliaji.

Wakati huo huo wananchi wa miji ya Shinyanga na Kahama ambayo inatarajia kufaidika na mradi mkubwa wa maji safi kutoka Ziwa Victoria wametakiwa kuwa na subiri kwani si muda mrefu maji yataanza kupatikana hivyo kukidhi kiu yao ya miaka mingi ya kujipatia huduma za uhakika za maji safi na salama.

My Take:

Wilaya zenye upungufu wa chakula zitakuwa na tatizo la njaa!
 
Mzee Mwanakijiji,

Tanzania leadership is in full use of Viagra, hence Viagra Policies!
 
Tuendelee kupiga kelele tutafika tu....

Watanzania tutafakari kwa makini kulima jatropha na miwa badala ya chakula

2008-06-14 09:54:48 (Nipashe)
Na Adam Fungamwango

Katika miaka ya karibuni kumekuwa na kampeni maalum ya kuhimiza kilimo cha jatropha na miwa ikielezwa kuwa miaka si mingi ijayo, nchi iweze kuzalisha nishati mbadala ambayo itaifanya nchi kujinasua kwenye mtego wa kutegemea mafuta ya petroli ambayo kwa sasa yanapanda bei kila kukicha.

Imekuwa ikisema kuwa, uzalishaji wa nishati mbadala utasaidia sana kupunguza utegemezi wa nishati ya mafuta ya petroli, ikiwa pamoja na kuisaidia nchi kuingiza fedha za kigeni kwa ziada ambayo itazalishwa na kuuzwa nchi za nje.

Wakati kampeni hizo za kuhimiza upatikanaji wa nishati hiyo ambayo hasa inasemwa kuwa inapatikana kwa wingi katika miti ya mibono- jatropha, miwa na mahindi ambayo wakulima wanatakiwa kulima kwa wingi ili nishati hiyo iweze kupatikana kutokana na mazao hayo.

Wazo la kuwa na nishati mbadala ni zuri sana kama litaangaliwa kijuujuu kwa sababu litaondoa utegemezi wa nishati ya mafuta toka nje ambayo imekuwa ikilalamikiwa sana kuwa inachukua sehemu kubwa ya mapato ya nje.

Lakini ukitafakari kwa makini kuhusu utekelezaji wa mpango huo inaonekana kuwa unahitaji kufikiri kwa makini zaidi badala ya kuuvamia kwa kasi.

Hii ni kutokana na ukweli kuwa kwa sasa, inasemwa kuwa huko Mbarali na Kapunga mkoani Mbeya, eneo hilo lilikuwa linasifika sana kwa kilimo cha mpunga kilichokuwa kinafanywa na Shirika la Chakula na Kilimo (NAFCO) wakati huo, ambapo ilikuwa neema kubwa ya chakula.

Uzalishaji wa mpunga ulikuwa na mchango mkubwa wa kuihakikishia nchi inakuwa na chakula cha kutosha na ziada kuuzwa nje.

Pia wakulima wadogowadogo waliokuwa wakiishi na kulima kuzunguka mashamba ya shirika hilo, walikuwa wakinufaika na uwepo wa mradi huo katika eneo hilo.

Zao la mpunga liliwahikikishia kuwa wananchi hao wanakuwa na chakula cha kutosha, ikiwa pamoja na ziada kuuzwa kwa wahitaji. Lilikuwa ni zao la chakula na biashara.

Kwa sasa inasemwa kuwa, mwekezaji aliyeuziwa shamba hilo ameamua kulima jatropha kwa kile kinachosemwa kuwa jitihada za kuhakikisha kuwa nchi inakuwa na nishati mbadala.

Hii maana yake ni kuwa eneo hilo ambalo lilikuwa limefanyiwa upembuzi yakinifu kwa miaka mingi, likafanyiwa majaribio ya kilimo hicho na kuonekana kuwa linafaa na kuihakikishia nchi kuwa inanufaika tangu mavuno yanapovunwa mwaka hadi mwaka, lakini sasa kwa makusudi kabisa linasitishwa kilimo hicho na maji yote ya asili yanayopatikana katika eneo hilo yanatumika kuoteshea mimea ya jatropha ambayo itamnufaisha mwekezaji na labda kikundi cha watu wachache tu.

Wakulima wadogowadogo waliokuwa wakiishi na kutegemea eneo hilo, ni kwamba mipango yao inavurugika kabisa na maisha yao na vizazi vyao kuwa rehani.

Ina maana kuwa uzalishaji mkubwa wa chakula uliokuwa unafanyika katika eneo hilo, sasa hautafanyika na itachukua muda mrefu kulipata eneo jingine likazalisha kama hapo hilo kwa umwagiliaji.

Wakati hayo yanasikika, lakini kuna taarifa nyingine kuwa makampuni makubwa ya nje, tayari yamekuwa yakipitapita na kununua mapande makubwa ya ardhi katika wilaya karibu zote za mkoa wa Pwani, ikiwemo wilaya ya Rufiji ambayo ina raslimali nyingi muhimu za uoto wa asili.

Baadhi ya vijiji vimekuwa vikiuza ardhi inayofikia hata ekari 20,000 hadi 50,000 kwa dhamira ya kulima kilimo cha miwa ili kuzalisha nishati mbadala.

Imekuwa ikisemwa kuwa upatikanaji wa ardhi kubwa itakayolimwa miwa hiyo, ndiyo itakayoamua kiwanda kijengwe wapi na uzalishaji uanze.

Kitu cha msingi cha kuelewa ni kuwa, ulimaji wa mashamba hayo ni dhahiri miti mingi itakatwa na hivyo kuyaharibu mazingira na uoto wa asili ambao utakuwa na athari kubwa kwa muda mrefu.

Wakati hayo yakifanyika, haijaelezwa kama umefanyika upembuzi yakinifu wa mazingira (EIA), ili kuona kuwa uanzishwaji wa miradi hiyo hautakuwa na madhara mengine au utawiana vipi na hali halisi ya kilimo, mkusanyiko wa watu, miradi mingine, shule, hospitali, ajira, kodi na mengine Tena basi, ifahamike kuwa uchukuaji wa ardhi hiyo utasababisha upungufu wa ardhi ambao sina hakika kama umefanyiwa tathimini ya kutosha kuhusu mahitaji ya ardhi ya vijiji hivyo katika muda mfupi na muda mrefu ujao.

Ukweli uko bayana kuwa, sasa hivi inasemwa kuwa bei ya mazao ya jatropha na miwa inatangazwa kuwa iko juu sana na kuwa kivutio cha kuwashawishi wakulima walime mazao hayo.

Lakini tuna hakika gani kuwa, baada ya muda fulani, bei hiyo ikafanywa kuwa ni kiini macho au njama fulani kuwa baada ya kulima kwa wingi mazao hayo, ikashushwa ghafla na kujikuta hakuna namna zaidi ya kuuza mazao hayo kwa bei yoyote ile hata ya chini namna gani kuwa hakutakuwa na ujanja wa kujitoa katika mtego huo kwa wakati huo.

Isitoshe, hali ya sasa ni kwamba dunia yote inahitaji sana chakula na Umoja wa Mataifa umetangaza tishio la njaa na kwamba kama kweli taifa letu litazalisha chakula kwa wingi, ni kwamba kuna uhakika mkubwa wa soko hapa nchini na nje ya nchi.

Ni dhahiri kuwa nchi yetu bado haijajitolsjeleza kwa chakula na hatua zozote za kuzalisha chakula kwa wingi,zingefaa kuungwa mkono kwa nguvu zote.

Kuhusu nishati,kama kweli taifa limetambua kuwa nishati mbadala ni muhimu sana,kwa nini tunaendelea na utafutaji wa mafuta katika maeneo mbalimbali nchini?

Ni vyema basi tusitishe shughuli za utafutaji wa mafuta hayo ili tutilie mkazo uzalishaji wa nishati mbadala.

Tunatakiwa kuwa makini sana katika kupokea kila aina ya ushauri na fikra mpya toka nje.

Hivi kweli nishati mbadala itayozalishwa hapa nchini itaweza kushindana na zile za mataifa mengine?

Kwa hakika, kama tutafanya mzaha maeneo yetu yatahodhiwa na wageni au yatazalishwa mazao ambayo hatuyahitaji.Tuwe makini na kufunguka macho.
 
Editorial ya "The Guardian"

Tanzania`s security lies in food self-sufficiency

2008-06-14 09:33:40
By Editor

The world is currently experiencing an unprecedented food shortage and a crippling fuel crisis.

This development has brought a lot of crisis in both the poor and developed countries.

Recently, the world has seen food riots that have caused political crisis in several countries.

And, even more perplexing, there have been fuel riots in Europe.

These occurrences have painted a gloomy picture of the economic future of poor countries, Tanzania included.

However, the mood in Tanzania is of not to give in, but more or less an optimistic one.

This explains Finance minister Mustafa Mkulo`s upbeat posture when he announced in his Budget Speech that the economy will grow by 7.8 percent in 2008, 8.1 per cent in 2009, 8.8 per cent in 2010 and 9.2 percent in 2011.

Moreover, the minister said that by mid-next year, inflation will be kept below 7.0%.

Although it needs a lot of courage to accept the minister`s forecasts, given the above-mentioned challenges, we think it is proper for Tanzania to adopt the path of hope, at the same time adopting appropriate policies and approaches.

We suggest that Tanzania takes a more serious look on agriculture, especially in the area of food self-sufficiency, and for the immediate future, the establishment of a solid internal food supply network, both as a way of boosting local trade, but also of ensuring the improvement of food security.

The recent global occurrences have sent a clear message to us that our security lies in food self-sufficiency.

In the past, we got used to receiving a lot of food aid in times of crisis or making huge food imports.

However, the signs of the times indicate, not in soft terms, that such days are long gone, perhaps for good.

Time might come when we won`t be able to get food in the international market even if we shall have the money to do so.

The only solution is to strengthen local capacity to produce food, such that we may also be able to sell the surplus to other countries, because from now onwards, food supply is going to be a lucrative business.

We have to invest in food production far more than on, say, biofuel, because it is only sufficient food that is going to ensure the security and freedom of this country in the long run.

Parallel with the introduction and application of food security policies, having all weather roads all around the country should go hand in hand with improving yields to raise output.

Even now, we have several upcountry regions which always have surplus food but are not connected to the national paved road network.

Increased agricultural production is sustainable when a country has a wide and durable road network.

We therefore urge the government not only to go on building and rehabilitating the country\'s roads, but to be visibly seen to be doing so by the wananchi.

The volatile international trade system brought about by the fuel and food crisis compels us to ensure having adequate strategic food reserves; and taking radical action in the belief that the future of this country-and the achievement of other economic, social and political goals-lies in food-self sufficiency.
 
Heshima mbele wakuu. Hii maneno naona imekuwa kimya kwa muda mpaka naona Asha Rose naye kaja kuwakumbusha wakuu kule bungeni kuwa kweli kuna njaa na lazima tujipange. Sisi kwa sasa mwendo mbele ni kwenye mazao ya "Biofuel" (correct me if am wrong) pia juzijuzi tu hapa ilisemekena kuwa tumeruhusu kuuzwa kwa chakula Kenya..... Hivi kweli kuna waliosema kuna SGS na vitu kama hivyo lakini mimi hilo inakuwa ngumu sana kuamini kwamba serikali yetu ina mikakati imara ya kukabiliana na baa hili la njaa!! Tuzingatie kuwa nchi kama India wameshaanza kukata export ya mazao kama mchele!!

Haya MWananchi la leo limesema:
Dk Migiro aitahadharisha Tanzania kuhusu chakula Na Ramadhan Semtawa, Dodoma

NAIBU Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa (UN), Dk Asha Rose Migiro, ametahadharisha kwamba kupanda kwa bei ya vyakula duniani ni kengele ya kuamsha Tanzania kuanza kuweka mikakati madhubuti ya uzalishaji wa chakula cha kutosha nchini.

Akizungumza kwa umakini na utulivu, huku akishangaliwa mara kwa mara, alisema Tanzania inapaswa kulichukulia ongezeko la bei ya vyakula duniani kama fundisho na kuanza kuweka mikakati ya kuzalisha chakula cha kutosha.

"Nimesimama hapa kama Mtanzania mwenzenu, nikiwakumbusha kwamba bunge lina kazi kubwa katika kusaidia maendeleo ya nchi. Licha ya kujadili bajeti za serikali, saidieni utekelezaji wa Malengo ya Milenia," alisema DkMigiro na kuongeza:


''Sasa hivi kuna kupanda kwa bei ya vyakula duniani, hii ni kengele ya kutuamsha usingizini, lazima tuongeze uzalishaji na kuweka chakula katika maghala.''

Alisema moja ya malengo ya milemia ni kupunguza� idadi ya watu wanaokabiliwa na njaa ifikapo mwaka 2015.

Dk Migiro ambaye aliongozana na watendaji mbalimbali wa UN nchini, akiwamo Mwakilishi Mkaazi, Oscar Fenandez, alisema Bunge lina nafasi kubwa kusaidia ukuaji wa sekta ya kilimo kwa kushirikiana na serikali.

Alifafanua kwamba, sekta ya kilimo haiwezi kukuzwa na serikali peke yake, bali hata kwa kuishirikisha sekta binafsi ambayo inapaswa kushiriki kikamilifu katika uzalishaji.

Naibu Katibu Mkuu huyo wa UN wa kwanza mwanamke na� wa kwanza kutoka Afrika, alisema changamoto nyingine kwa Tanzania ni kuhakikisha kwamba kunakuwepo upatikanaji nishati endelevu.

Kuhusu mipango ya UN na nafasi ya Tanzania katika ushiriki, alitaka Bunge liusaidie umoja huo katika mpango wake wa kuunganisha shughuli za� mashirika yake katika jengo moja (One UN).

Alisema Tanzania ni miongoni mwa nchi nane ambazo zimefanikiwa kuingia katika mpango huo, hivyo aliishukuru Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) kwa kukubali kusaidia jengo ambalo litatumika na mashirika yote ya UN.

Akitoa shukrani kwa niaba ya Bunge, Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Kepten John Chiligati alisema wabunge na serikali watajitahidi kutekeleza ushauri aliotoa Migiro na kuahidi kwamba serikali itashiriki kikamilifu kufanikisha mpango wa upatikanaji wa jengo la UN nchini.

Habari kutoka:
www.mwananchi.co.tz leo 23 Jul 2008
 
Asante.. hivi karibuni tumeuza tani laki moja kwa Kenya.. halafu baadaye mwaka huu tutaagiza tani laki moja...
 
Asante.. hivi karibuni tumeuza tani laki moja kwa Kenya.. halafu baadaye mwaka huu tutaagiza tani laki moja...

Mkuu MMM, sio baadae tutaagiza, tayari tumeshajua tunatakiwa kuagiza manake wenyewe tayari tunajua kuwa tulichoonacho hakitatutosha Mkuu wangu!!! Hebu angalia waziri wa Chakula anatuambia nini kupitia Bunge!!

Hebu angalia hii:
1. Although data zinasema kati ya 2004 - 2006 kilimo kimekuwa kinadumaa (angalia asilimia ya ongezeko yutaona inashuka) Waziri anasema kilimo kinategemewa kupanda bila kutuletea data halisi!!
2. Je ongezeko la chakula analolitegema ameandalia vitu kama ongfezeko la watu, ongezeko la soko la mauzo nchi za nje (hii ni crissis ya dunia na sio Tz pekee)
3. Nimeangalia statistics za vitendea kazi kutuka kwenye jembe la mkono mpaka matrekta nimebaki nimeduwaa manake duh, kukuza uchumi (sekta ya kilimo) kwa asilimia 20 ukizingatia rationality ya vitendea kazi mtu unabaki unajiuliza kama Mheshimiwa Mbunge wa CUF pale kwenye last para alivyosema!!!
4. Na hili la waziri kuliambia Bunge kuwa wamesitisha uuzwaji wa chakula nje na Raisi kuruhusu wakati wa ziara yake mkoani Tanga nalo mbona ni mauzauza tu.............

Mungu Ibariki Tanzania na watu wake!!!

Serikali yafuta kodi ya uagizaji mahindi nje

na Irene Mark, Dodoma


WAZIRI wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Stephen Wasira, amesema serikali imefuta kodi ya uingizaji wa mahindi kutoka nje.

Waziri Wasira alisema hayo jana bungeni wakati akisoma hotuba ya makadirio na mapato ya bajeti ya wizara hiyo kwa mwaka huu wa fedha.

Wasira alisema lengo la kufuta kodi hiyo ni kuongeza upatikanaji wa chakula na kuleta unafuu wa bei.

Alisema kutokana na kuondolewa kwa kodi hiyo, tani 300,000 za nafaka zenye nafuu ya kodi, zilitarajiwa kuingizwa nchi katika kipindi cha Januari hadi Mei mwaka huu.

Waziri huyo pia alisema ili kilimo kiweze kutoa mchango unaotakiwa katika vita dhidi ya umaskini, kinapaswa kukua kwa zaidi ya asilimia 10 kwa mwaka.

Hata hivyo alisema licha ya ukuaji mdogo wa sekta hiyo, bado inachangia kwa zaidi ya asilimia 95 ya chakula kinachopatikana nchini na kudhibiti kwa kiwango kikubwa mfumuko wa bei.

Kuhusu kupanda kwa bei za mazao ya chakula duniani na upungufu uliojitokeza, waziri huyo alisema ni fursa kwa Tanzania kuongeza uzalishaji wa chakula kwa matumizi ya nchi na kuuza ziada nje ya nchi.

“Kutokana na hatua za muda mfupi zitakazochukuliwa, matarajio ya uzalishaji wa chakula ni kufikia tani milioni 11.579 kwa mwaka 2008/09 ikilinganishwa na tani milioni 10.782 mwaka jana.

“Mahitaji ya chakula kwa mwaka huu wa fedha yanakisiwa kufika tani milioni 10.34 hivyo taifa linategemewa kujitosheleza kwa chakula kwa takriban asilimia 104,” alisema Wasira.

Kuhusu zana za kilimo, waziri huyo alisema tathmini iliyofanywa na ofisi yake juu ya matumizi na mahitaji ya zana hizo imebaini kuwepo kwa majembe ya mkononi milioni 14; yanayokokotwa na wanyamakazi ni 585,000; maksai ni milioni 1.3 na matrekta 7,200.

Hata hivyo alikiri kuwa kasi ya ukuaji wa sekta ya kilimo nchini inazorota, ambapo mwaka 2004 kilikua kwa asilimia 5.9; mwaka 2005 kiliongezeka kwa asilimia 4.3; mwaka 2006 asilimia 3.8 na mwaka jana kilikua kwa asilimia 4.0.

Pia waziri huyo alisema Mei mwaka huu, serikali ilisitisha uuzaji wa mazao yote ya chakula kutokana na kutokuwepo kwa akiba ya kutosha ya chakula hadi hali itakapokuwa nzuri.

Pamoja na usitishwaji huo, hivi karibuni akiwa mkoani Tanga katika ziara ya siku tisa, Rais Jakaya Kikwete aliruhusu uuzaji wa mahindi nchini Kenya.

Waziri huyo aliliomba Bunge kupitisha bajeti ya sh 113,737,050,400 kwa ajili ya wizara hiyo.

Kati ya fedha hizo, sh 93,704,218,000 ni kwa ajili ya matumizi ya kawaida na sh 20,032,832,400 zitatumika kwa shughuli za maendeleo.

Katika hatua nyingine, kambi ya upinzani bungeni, imetahadharisha kuhusu udumavu katika sekta ya kilimo kwamba ni hatari kwa usalama wa nchi.

Msemaji mkuu wa kambi ya upinzani bungeni, Salim Hemed Khamisi, alisema udumavu huo unaonyesha wazi kuwa kamwe Serikali ya Awamu ya Nne iliyoingia madarakani kwa ahadi ya kukuza kilimo kwa asilimia 20, imeshindwa kutimia.

“Katika nchi yetu ambayo watu wake wanategemea kilimo kujiendeleza, ukuaji duni wa sekta hii inayochangia kwa kiasi kikubwa pato la taifa, ni hatari kwa usalama wa nchi.

“Kwa hali hii ni wazi kwamba Tanzania haiwezi kufikia malengo ya MKUKUTA ya kuwa na kilimo endelevu kinachokua kwa asilimia 8-10 ili kufikia ukuaji wa uchumi kwa asilimia 6-8 ifikapo mwaka 2010.

“Ni wazi kuwa ilani ya CCM iliyoahidi kukuza kilimo kwa asilimia 20 ilikuwa ya kilaghai ama ya kusadikika…wachumi waliobobea wanasema ukuaji wa kasi hiyo haujapata kutokea katika nchi yoyote duniani,” alisema Khamis, ambaye pia ni Mbunge wa Chambani, (CUF).

Courtesy:
http://www.freemedia.co.tz/daima/2008/7/23/habari5.php
 
Hapa nilipo mwaka jana mida kama hii nilinunua gunia la mpunga elfu 15, leo hii ni elfu 35 tena kwa kumbembeleza mkulima.
 
From: , Science and Development Network, More from this Affiliate
Published August 6, 2008 08:49 AM
Kenyan courts consider terminating biofuel plans

The Kenyan courts are considering halting the first stage of a US$370 million biofuel project that aims to replace up to 20,000 hectares of coastal grassland with irrigated fields of sugarcane.

A judicial review of the project, based at the Tana River Delta on the northern Kenyan coast, was granted last month (11 July) after a campaign from environmental groups such as Nature Kenya and the East Africa Wildlife Society,and nomadic cattle-farming groups.

The project is intended to generate electricity - up to 34 megawatts a day at its peak - from sugar refining and up to 20 million litres of ethanol fuel annually from molasses.


ADVERTISEMENT



The Tana River Development Authority, under the Ministry for Regional Development, and Kenya's biggest sugar miller, Mumias, are partners in the project.

The National Environmental Management Authority (NEMA) approved the first stage of the three-stage project on 19 June this year, with only 500 hectares of farmland affected in this first stage, according to Ruth Musembi, communications manager at NEMA.

NEMA commissioned agroforestry researcher David Mungai, from the University of Nairobi, to carry out an environmental impact assessment of the project in September 2007. Mungai found negative environmental impacts could be mitigated using the best available practices and strict compliance with the national regulations.

Proponents of the project say it will reduce fuel prices, lower foreign exchange losses from importing 200,000 tonnes of sugar annually, create 20,000 jobs and put biofuel-powered cars on Kenyan roads.

But conservationists such as Paul Matiku of Nature Kenya say the lack of project design documents - required by Kenyan environmental law - has been a critical omission in the assessment process.

A report commissioned by Nature Kenya in May found that developers' plans overestimated profits, ignored fees for water use and pollution from the sugarcane plant, and disregarded the loss of income from wildlife tourism.

"We cannot just start messing around with the wetland because we need biofuel and sugar," Kenyan peace prize Nobel laureate and environmentalist Wangari Maathai said, according to Engineering News.

Hellen Omondi, high court judge in the town of Malindi, is currently reviewing the decision-making process of government departments such as the Tana and Athi River Development Authority, the Tana River County Council, the Lands and Water Resources Management Authority, and NEMA.

Mumias sugar company has also been ordered to submit its documentation to the court. No deadline has been set for the court's decision.
 
UNITED REPUBLIC OF TANZANIA

Telephone: 255-22-2114512, 2116898
E-mail: press@ikulu.go.tz
Fax: 255-22-2113425


PRESIDENT’S OFFICE,
THE STATE HOUSE,
P.O. BOX 9120,
DAR ES SALAAM.
Tanzania.



TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Na Mwandishi Maalum, Micheweni, Pemba

Rais Jakaya Mrisho Kikwete amesema kuwa hakuna Mtanzania yoyote atakayekufa kwa njaa kutokana na uhaba wa chakula unaotabiriwa kutokea nchini kutokana na uhaba wa mvua katika mikoa kadhaa nchini.

Amesema kuwa Serikali yake itachukua kila hatua inayostahili kuhakikisha kuwa wananchi wanaendelea kupata chakula kama kawaida, hata kama ukitokea uhaba wa chakula kama inavyobashiriwa.

Rais Kikwete ametoa uhakikisho huo wa kupatikana kwa chakula leo, Januari 20, 2009, katika mikutano yake mitatu tofauti katika siku ya kwanza ya ziara yake ya siku sita kutembelea mikoa ya Tanzania Visiwani.


Rais Kikwete ameanzia ziara yake Kisiwani Pemba wakati alipowasili kwenye Uwanja wa Ndege wa Karume, Mkoa wa Kusini Pemba, na kupokelewa na mamia ya wananchi wakiwamo wana-CCM, wakiongozwa na Waziri Kiongozi wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ), Shamsi Vuai Nahodha.

Katika tukio la kwanza la ziara hiyo, ikiwa ni sehemu ya ziara zake katika mikoa yote ya Tanzania, Rais Kikwete ameweka jiwe la msingi la Nyumba ya Kufikia Wageni ya Serikali ya SMZ katika Wilaya ya Micheweni, zamani ikiitwa Wilaya ya Konde, Mkoa wa Kaskazini Pemba.

Akizungumza na wananchi baada ya kuwa ameweka jiwe la msingi katika ujenzi wa Nyumba hiyo, Rais kikwete ameonya kuwa Tanzania inatabiriwa kuwa Tanzania itakabiliwa na uhaba wa chakuka kutokana na kushindwa kunyesha kwa mvua, kama ilivyo kawaida, katika mikoa mbali mbali.

Mikoa ya Tanzania Bara ya Pwani na Kaskazini Mashariki pamoja na ile ya Tanzania Visiwani haikupata mvua ya vuli mwishoni mwa mwaka uliopita. Mikoa ya Lindi na Mtwara ambayo hupata mvua ndefu nayo haipati mvua ya kutosha wakati kuna habari kuwa mvua katika baadhi ya mikoa ya kati ukiwamo Dodoma tayari imekatika.

Rais amesema kuwa hata kama Tanzania itakumbwa na uhaba wa chakula, bado hakuna mtu ambaye atakufa na njaa kwa sababu Serikali yake imejipanga vizuri kutimiza
wajibu wake kuhakikisha kuwa hakuna Mtanzania anayekufa kwa njaa.

“Tutakuwa na upungufu wa chakula, lakini hakuna atakayekufa kwa njaa. Serikali zetu mbili zitashirikiana kuhakikisha kuwa kila Mtanzania anapata chakula,” amesema Rais kwenye mkutano huo.

Rais Kikwete pia amewaambia wananchi wa Micheweni kuwa kwa maana ya wananchi kupatiwa huduma za jamii, Pemba iko mbele sana ya maeneo yote ya Tanzania Bara ikiwa ni pamoja na huduma ya maji, huduma ya elimu, barabara, afya.

Rais Kikwete ameeleza ukweli huo baada ya Sheha wa eneo la Micheweni kuwa amethibitisha kuwa wananchi wa eneo hilo hawana tatizo kupata huduma hizo. “Maji tunayo, barabara zipo, zahanati zipo, shule tunazo za kila rangi, tatizo letu ni kwamba hatuna fedha za matumizi,” amesema Sheha wa eneo hilo.

Baada ya kuwa amesikia hayo, Rais amesema: “Kule Bara ndio kwanza tunajaribu kufikisha huduma za afya karibu na wananchi, ndio tunajenga shule za sekondari, tunaendelea na ujenzi wa barabara za lami ambazo nyie mnazo…”

Kuhusu malaria, Rais Kikwete amesema kuwa wakati Tanzania Bara inaendelea kuhangaika kupunguza ugonjwa huo, upande wa Pemba dawa za malaria sasa hazina wagonjwa. “Sisi Bara sasa tunajaribu kuiga hili kupitia ule mradi mkubwa wa afya wa miaka 10.”

Rais Kikwete pia amekagua Bonde la Kilimo cha Umwagiliaji Maji katika Kijiji cha Saninga Tumbe, ambako amepata maelezo ya mradi. Kesho, Rais Kikwete anaendelea na ziara yake kwa kutembelea Mkoa wa Kusini Pemba.
 
Huyu huyu aliwahi kutwambia kwamba' "Hakuna mtoto wa maskini Tanzania atakayekosa elimu ya juu" na ukweli kuhusu yanayojiri pale UDSM unapingana na kauli yake hiyo. Hivyo hili pia inaweza kabisa kuwa ni kujiosha tu machoni mwa Watanzania.
 
Back
Top Bottom