Niweke Mlango wa Nje? Inanitatiza sana

Niweke Mlango wa Nje? Inanitatiza sana

Mna jenga uswahilini sana na nyie, yaani unashindwa kupendezesha nyumba ukihofia vibaka.
Mimi huwa nashindwa kuwaelewa WaTz, yaani mtu anatafuta kiwanja cha bei rahisi halafu anaenda kujenga nyumba ina thamani ya zaidi ya 50m.
 
Nazungumzia Norway niliishi. CCTV zipo kwa sababu nyingi na siyo wizi tu. Naweza kusema bila shaka yoyote kuwa nchi kama Norway unaweza kuegesha mlango bila kufunga kwa ufunguo na ukaenda kazini na kurudi na kila kitu kikawa kiko salama. Watu hawana tabia ya wizi kama Bongo, hata simu kali kabisa ukidondosha unaweza kuipata (labda uwe na bahati mbaya iokotwe na mgeni mwizi). Magari yanalazwa nje na watu hawachomoi vioo au taa. NB: siyo kwamba hakuna wizi kabisa lakini inatokea mara chache chache hasa mateja wa madawa ya kulevya ndiyo wezi
Umeenda mbali sana, wizi ni hulka ya jamii husika, hapo visiwani tu Unguja zamani uilikuwa unalaza gari nje na asubuhi unalikuta halijaguswa! Siku hizi ukilaza gari nje ni pata potea.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom