Nitamsaidiaje Anna?

Nitamsaidiaje Anna?

Hahahaa nimependa hapo kwenye sitaki maswali hahaa. Aiseee mtu akitaka nimgaye mazima aombe namba ya simu
Kuna kabinti flani nilikaombaga namba ya simu (sitaki maswali). Nikakabeep kakasevu namba yangu bhana...

Ikapita siku nne kimyakimya... siku ya tano nikakumbana na huu ujumbe "Sasa wewe mwanaume uliniomba namba kwa ajili ya nini???"

Hili swali lazima liingie kwenye waraka wa Bonny kwa ajili ya conclusion.
 
Wakati mwingine tunakwenda shule kupoteza tu muda,

Anna pamoja na kusoma kote huko anakuja kukubali hayo mambo sababu ya ufadhili? Anapewa fedha nyingi lakini anakosa akili ya kujiongeza. POLE YAKE
 
Habari za J3 wapendwa

Leo hii nimepata kesi ya Anna, Anna ni mtoto wa kwanza katika familia yao, baba yake ni mwalimu mkuu wa shule huko kwao mkoa ninauhifadhi. Anna alifaulu darasa la saba na kujiunga na shule ya secondary, majibu yake ya IV yalimwezesha kujiunga na form V.

Elimu ya Anna akiwa form V na VI elimu ya Anna haikuwa nyepesi, wakati huo wadogo zake wengine watatu walikuwa secondary, mzee alijitahidi kusaidia familia lakini mshahara wake haukukidhi mahitaji ya familia. Hali hii ilimfanya Anna awe na ari ya kutafuta kazi mara akimaliza masomo yake.

Anna ni binti mrembo sana na pia ni mzuri mwenye natural beauty. Mjini alifikia kwa shangazi yake, shangazi pamoja na Anna walihangaika kutafuta kazi na Anna alifanikiwa kuajiriwa katika kampuni moja, mshahara ukiwa 300,000 take home kwa mwezi. Kwa kweli katika zile pesa Anna alihakikisha anapeleka 200,000 kwa wazazi wake kila mwezi.

Kwa urembo wa Anna, ni wanaume wengi sana walimsumbua kwa urafiki, Anna alijikuta ameanguka katika penzi zito la boss wa kampuni yao, boss huyu kitu cha kwanza alichofanya ni kumpangishia Anna nyumba, alifanikiwa kumpatia guest wing ya mtu yenye chumba kimoja cha kulala jiko, choo na sebule, alimnunulia Anna usafiri, hivi vitu vilimshawishi Anna kuhama kutoka kwa shangazi yake.

Boss huyu alimkabidhi Anna 1000,000 kila mwisho wa mwezi, kwa pesa hizi Anna aliongeza msaada kidogo kwao, aliwapelekea 300,000 yote anayopata kutoka katika mshahara wake. Wadogo zake wote waliweza kusoma.

Tatizo ni kuwa, kibosile huyu kwanza halali kwa Anna, anakuja tu akitoka kazini, ikifika saa mbili usiku anaaga kuwahi kwake, hili linamfanya Anna abakie mpweke sana. La pili hafanyi kingine chochote Zaidi ya kumuingilia Anna kinyume cha maumbile, ameshamwambia kuwa anampenda sana mke wake na hawezi hata siku moja kumuomba hilo jambo hivyo sababu ya yeye kutafuta nyumba ndogo ni kupata mchezo huo.

Anna alijikuta mtegoni kwasababu kibosile alimuanzishia jambo hilo baada ya kuhama kutoka kwa shangazi, Anna aliogopa kurudi pia na yeye alitaka kujaribu hiyo kitu. Kwakweli Anna amechoshwa na mchezo huu, lakini anaogopa kumwacha akakosa ule msaada unaomwezesha kuishi mjini.

Jina la Anna ni lakubuni na ninaomba radhi kwa yeyote nitakaemkwaza kwa habari hii.

Aombe toba kwa MUNGU,aachane na mume wa mtu,ampende MUNGU kuliko kupenda fedha,ajifunze kusubiri mafanikio halali kama alivyovumilia kupata kiwango cha elimu aliyonayo, maelekezo mengine yatafuata.
 
Aombe toba kwa MUNGU,aachane na mume wa mtu,ampende MUNGU kuliko kupenda fedha,ajifunze kusubiri mafanikio halali kama alivyovumilia kupata kiwango cha elimu aliyonayo, maelekezo mengine yatafuata.
Asante sana mkuu.
 
Kuna future gani hapa na wazee wa shenzi kama hawa akimpata new form six leaver anakuacha kama kinyesi.
nmemaanisha kwamba sasa hv hawez kuondoka ghafla tu tatzo hakuna namna nyengne ya kukata ghafla huduma za mzee akusanye mafao yake kabisa asje akaachwa kwenye mataa na hana hata kumi
 
nmemaanisha kwamba sasa hv hawez kuondoka ghafla tu tatzo hakuna namna nyengne ya kukata ghafla huduma za mzee akusanye mafao yake kabisa asje akaachwa kwenye mataa na hana hata kumi
Kwa hiyo laki tatu kwa mwezi angepata chumba kule kwetu Kwamtogole na kumuomba Mungu ampatie mume mwema.
 
Back
Top Bottom