Nisamehe Mpenzi

Nisamehe Mpenzi

Sehemu ya 31.

“Siamini kama kweli Richard ameweza kunifanyia hivi, yani mapenzi yangu yote niliyompa bado amenisaliti ama kweli wanaume wabaya sana,” alisema Evelyne kwa sauti iliyoandamana na kilio.
“Kumbe kweli anatembea na Monalisa?” aliuliza Happy.

“Mwanzoni sikutaka kuamini niliposikia kuwa wanamahusiano, nilimuamini sana lakini katika hili siwezi tena kumuamini, ameuvunja uaminifu wangu kwake, namchukia sana,” alisema Evelyne.
Huo ulikuwa ni ukweli wenye kuuma mno tena mara zote alipomkumbuka mpenzi wake hakutaka kuamini, machozi yalikuwa yakimtoka. ****

Richard alizidi kuchanganyikiwa, kila alilokuwa akiliwaza kulifanya kama ishara ya kumuomba mpenzi wake msamaha aliona kama anakosea.

Alizidi kuwa katika wakati mgumu sana kipindi ambacho alikuwa akimuona Evelyne darasani, kuna muda alitamani kuzungumza naye kisha amuombe msamaha lakini Evelyne hakuwa tayari, alimchukia mno Richard tena chuki za waziwazi.

Hakuwa na njia nyingine ya kufanya zaidi ya kumfuata Happy na kuamua kuzungumza naye, alihitaji kumuomba msamaha Evelyne lakini aliamini ilikuwa ni vigumu sana kwa yeye kuweza kueleweka, alijua kuwa alifanya makosa sana kwa kumsaliti mpenzi wake lakini bado hakutaka kuamini kuwa huo ndiyo mwisho wa mapenzi yake kwa Evelyne.

“Najua nimemkosea sana Evelyne lakini tafadhali mwambie asinichukie moyo wangu bado unampenda,” alisema Richard huku akimtazama Happy kwa macho ya huruma.

“Richard hivi kwanini umeamua kumsaliti Evelyne?” aliuliza Happy.
“Sijui ata niseme nini? Nashindwa kujielezea Happy, nashindwa nimejikuta tu namsaliti,” alijibu Richard.

“Richard embu acha kunifanya mimi mtoto mdogo wakati picha zako za uchafu na huyo mchepuko wako nimeziona yani sikutegemea kama ungeweza kumfanyia ukatili huu rafiki yangu, Richard wewe ni mbaya sana unatembea na Monalisa?” aliuliza Happy.

“Hapana usiseme hivyo narudia tena moyo wangu bado unampenda Evelyne na ninahitaji anisamehe, najua ananichukia sana lakini tafadhali jaribu kuzungumza naye pengine anaweza akabadili mawazo yake,” alisema Richard.
 
Sehemu ya 35.

“Mimi Richard.”
“Nikusaidie nini?”
“Evelyne mpenzi wangu mbona hivyo?”
“Umesahau nini tena kwangu.”
“Sijasahau kitu ila naomba unisamehe mpenzi.”

“Nimeshakusamehe tangu siku ya kwanza uliyonipa maumivu ila kurudiana na wewe siwezi.”
“Kwanini?”

“Endelea na Monalisa nadhani yeye ndiye anayeweza kuliziba pengo langu kwako.”
Kila ujumbe aliyokuwa akitumiwa na Evelyne alipousoma ulizidi kumuumiza sana, alitamani mpenzi wake asahau mambo yote yaliyotokea kisha amsamehe lakini tukio hilo lilikuwa gumu mno kutokea.

Siku zilizidi kukatika huku moyo wa Evelyne ukiendelea kuhifadhi chuki kwa Richard, hakutaka kumsamehe kirahisi kama Richard alivyokuwa akihitaji.

Maisha ya chuo yaliendelea huku maelewano kati yake na Richard yakiwa bado sio mazuri, wafikia kipindi wakawa hawazungumzi lolote zaidi ya salamu ambayo muda mwingine haikuweza kujibiwa. Hilo lilizidi kumuumiza sana Richard, kila siku alikuwa ni mtu wa kulilia penzi la Evelyne bila mafanikio yoyote.

Moyo wake uliendelea kumpenda Evelyne lakini kwa upande mwingine penzi la Monalisa lilizidi kuwa kikwazo, alitamani kuwa mbali na msichana huyo lakini alionekana kuwa na nguvu kubwa ya kuendelea kuwa naye.

Kichwa chake kilizidi kutafakari mambo mengi sana juu ya msichana huyo ambaye alikuwa ndiye sumu ya penzi lake, alizikumbuka picha ambazo alikuwazo na ndizo zilizokuwa zikimfanya akose maamuzi ya kumpenda msichana mmoja.

Alichowaza kukifanya ni kumpigia simu Monalisa kisha akamwambia kuwa siku hiyo alihitaji kuonana naye kwani alikuwa ana mazungumzo naye ya umuhimu sana, alimwambia muda ambao alihitaji kuonana naye kisha wakapanga kukutana katika hoteli ya kifahari ya Golden Tulip.

muda wa kukutana ulipofika waliweza kukutana na kuyaanza mazungumzo yao.
“Sitaki niendelee kukudanganya.”
“Kwanini?”

“Umeulazimisha moyo wangu ukupende lakini hisia zangu hazipo kwako.”
“Una maanisha nini Richard?”
“Hisia zangu zipo kwa msichana mwingine, moyo wangu unampenda msichana mmoja tu na si mwingine bali ni Evelyne.”

“Richard umeshachelewa.”
“Kivipi?”
“Nina ujauzito wako Richard hivyo usijidanganye kuwa unaweza ukaniacha kirahisi.”
“Unasemaje?”
 
Sehemu ya 36.

“Nina ujauzito wako.”
Yalikuwa ni mazungumzo mafupi yaliyofanyika ndani ya chumba cha kifahari cha hoteli hiyo, Richard hakutaka kuamini aliposikia kuwa Monalisa alikuwa amebeba ujauzito wake, ilikuwa ni taarifa ya ghafla! ambayo ilimshtua sana, moyo wake haukumpenda hata kidogo msichana huyo na kwa wakati huo alikuwa tayari ameshaubeba ujauzito wake, hilo lilizidi kumchanganya.

“Umebebaje ujauzito lakini?” aliuliza Richard kwa ghadhabu.
“Kwani ukiingia unaingiaje inamaana umesahau jinsi ulivyokuwa umelala na mimi?” alijibu Monalisa.

Richard alishikwa na kigugumizi mara baada ya kusikia maneno hayo kutoka kwa msichana huyo, hakutaka kumuamini alihisi labda alikuwa akimdanganya ili asiweze kumuacha lakini kitu cha kushangaza Monalisa alipoona Richard hamuamini aliamua kutoa cheti cha majibu ya dakatri ambayo yalikuwa yakimuonyesha kweli kuwa ni mjamzito. ****

Mapenzi yaligeuka kuwa mwiba wa maumivu kwa upande wa Evelyne, licha ya moyo wake kumpenda Richard lakini mwanaume huyo tayari alikuwa ameshamsaliti, hilo liliendelea kuwa tukio lililozidi kumuumiza sana, alikosa raha ya maisha, alishindwa kusoma, ulimwengu wa mapenzi alichukia.

Maumivu ya kimapenzi hayakuishia kwa kusalitiwa tu bali alizidi kuumia mara baada ya kusikia kuwa Monalisa alikuwa amebeba ujauzito wa Richard na ujauzito huo ndiyo ulizidi kumfanya azidi kumchukia mwanaume huyo.
“Sidhani kama nitakuja kupenda tena katika maisha yangu,” alisema Evelyne huku akijiapiza.

“Usiusemee moyo huwezi kujua nini kitakachotokea baadae,” alisema Happy.
“Sijui Happy kama nitapenda tena moyo wangu unakidonda na sijui kama kitapona na hata kama kikipona bado kitaniachia jeraha la maisha,” alisema Evelyne huku machozi yakianza kumdondoka.

Kipindi ambacho moyo wa Evelyne uliweza kupata maumivu ya kimapenzi, alijikuta akiwa ni mpenzi wa kuperuzi mtandao wa kijamii wa Instagram, aliuamini mtandao huo na ndiyo ambao uliweza kumsahaulisha maumivu yote ya kimapenzi ambayo moyo wake ulikuwa umeyapata.
 
Sehemu ya 37.

Ndani ya mtandao huo wa Instagram katika kipindi asichokitarajia alikutana na mvulana aliyejulikana kwa jina la Fredick na kama utani alijikuta akianzisha urafiki na mwanaume huyo na baadae urafiki huo uliweza kuibua penzi kati yao.

Aliendelea na masomo yake ya chuo huku penzi hilo jipya likionekana kumbadilisha kwa kiasi fulani, hakuonekana kuwa mtu wa kuumizwa tena na mapenzi, moyo wake tayari ulikuwa umepata tumaini lingine, alimpenda sana Fedrick kwake mwanaume huyo alimuona kuwa sawa na malaika ambaye alikuja kipindi asichokitarajia. ****

Richard hakuwa tayari kuona Monalisa anaendelea kuubeba ujauzito, alichoamua kukifanya ni kumshauri autoe ujauzio huo lakini hilo lilikuwa ni jambo gumu mno kuweza kufanyika, Monalisa hakuwa tayari kufanya kitendo hicho.

Alizidi kuchanganyikiwa baada ya kusikia kuwa Evelyne alikuwa ameshampata mwanaume mwingine, hakutaka kuamini ilibidi atafute nafasi ya kuzungumza na msichana huyo ambaye moyo wake ulikuwa bado unampenda sana.
“Naomba uniache na maisha yangu,” alisema Evelyne.

“Siwezi kufanya hivyo hata mara moja nakupenda Evelyne,” alisema Richard.
“Upendo wako hauna faida tena kwangu.”
“Kwanini unasema hivyo kwanini unauumiza moyo wangu?”
“Siamini kama kweli ninauumiza moyo wako ila jaribu kuchunguza sababu ya maumivu yako.”

“Evelyne nataka urudi kuwa wangu.”
“Kwasasa haitawezekana kwasababu moyo wangu anaumiliki mwanaume mwingine.”
“Yupi.”
“Fredrick.”
“Hapana Evelyne, Hapana.”

“Huo ndiyo ukweli.”
“Nakupenda Evelyne.”
“Nilikupenda Richard,” alisema Evelyne kisha akaondoka eneo hilo.
*
*

Je, nini kitaendelea?
Usikose sehemu ijayo.
 
Sehemu ya 37.

Ndani ya mtandao huo wa Instagram katika kipindi asichokitarajia alikutana na mvulana aliyejulikana kwa jina la Fredick na kama utani alijikuta akianzisha urafiki na mwanaume huyo na baadae urafiki huo uliweza kuibua penzi kati yao.

Aliendelea na masomo yake ya chuo huku penzi hilo jipya likionekana kumbadilisha kwa kiasi fulani, hakuonekana kuwa mtu wa kuumizwa tena na mapenzi, moyo wake tayari ulikuwa umepata tumaini lingine, alimpenda sana Fedrick kwake mwanaume huyo alimuona kuwa sawa na malaika ambaye alikuja kipindi asichokitarajia. ****

Richard hakuwa tayari kuona Monalisa anaendelea kuubeba ujauzito, alichoamua kukifanya ni kumshauri autoe ujauzio huo lakini hilo lilikuwa ni jambo gumu mno kuweza kufanyika, Monalisa hakuwa tayari kufanya kitendo hicho.

Alizidi kuchanganyikiwa baada ya kusikia kuwa Evelyne alikuwa ameshampata mwanaume mwingine, hakutaka kuamini ilibidi atafute nafasi ya kuzungumza na msichana huyo ambaye moyo wake ulikuwa bado unampenda sana.
“Naomba uniache na maisha yangu,” alisema Evelyne.

“Siwezi kufanya hivyo hata mara moja nakupenda Evelyne,” alisema Richard.
“Upendo wako hauna faida tena kwangu.”
“Kwanini unasema hivyo kwanini unauumiza moyo wangu?”
“Siamini kama kweli ninauumiza moyo wako ila jaribu kuchunguza sababu ya maumivu yako.”

“Evelyne nataka urudi kuwa wangu.”
“Kwasasa haitawezekana kwasababu moyo wangu anaumiliki mwanaume mwingine.”
“Yupi.”
“Fredrick.”
“Hapana Evelyne, Hapana.”

“Huo ndiyo ukweli.”
“Nakupenda Evelyne.”
“Nilikupenda Richard,” alisema Evelyne kisha akaondoka eneo hilo.
*
*

Je, nini kitaendelea?
Usikose sehemu ijayo.
Hizi episode zinachinjwa na kuwa fupi, kama madamme mmoja tuliekuwa tukimuita madamme mchinjo kwenye wali maharage enzi hizo shulen
 
Sehemu ya 36.

“Nina ujauzito wako.”
Yalikuwa ni mazungumzo mafupi yaliyofanyika ndani ya chumba cha kifahari cha hoteli hiyo, Richard hakutaka kuamini aliposikia kuwa Monalisa alikuwa amebeba ujauzito wake, ilikuwa ni taarifa ya ghafla! ambayo ilimshtua sana, moyo wake haukumpenda hata kidogo msichana huyo na kwa wakati huo alikuwa tayari ameshaubeba ujauzito wake, hilo lilizidi kumchanganya.

“Umebebaje ujauzito lakini?” aliuliza Richard kwa ghadhabu.
“Kwani ukiingia unaingiaje inamaana umesahau jinsi ulivyokuwa umelala na mimi?” alijibu Monalisa.

Richard alishikwa na kigugumizi mara baada ya kusikia maneno hayo kutoka kwa msichana huyo, hakutaka kumuamini alihisi labda alikuwa akimdanganya ili asiweze kumuacha lakini kitu cha kushangaza Monalisa alipoona Richard hamuamini aliamua kutoa cheti cha majibu ya dakatri ambayo yalikuwa yakimuonyesha kweli kuwa ni mjamzito. ****

Mapenzi yaligeuka kuwa mwiba wa maumivu kwa upande wa Evelyne, licha ya moyo wake kumpenda Richard lakini mwanaume huyo tayari alikuwa ameshamsaliti, hilo liliendelea kuwa tukio lililozidi kumuumiza sana, alikosa raha ya maisha, alishindwa kusoma, ulimwengu wa mapenzi alichukia.

Maumivu ya kimapenzi hayakuishia kwa kusalitiwa tu bali alizidi kuumia mara baada ya kusikia kuwa Monalisa alikuwa amebeba ujauzito wa Richard na ujauzito huo ndiyo ulizidi kumfanya azidi kumchukia mwanaume huyo.
“Sidhani kama nitakuja kupenda tena katika maisha yangu,” alisema Evelyne huku akijiapiza.

“Usiusemee moyo huwezi kujua nini kitakachotokea baadae,” alisema Happy.
“Sijui Happy kama nitapenda tena moyo wangu unakidonda na sijui kama kitapona na hata kama kikipona bado kitaniachia jeraha la maisha,” alisema Evelyne huku machozi yakianza kumdondoka.

Kipindi ambacho moyo wa Evelyne uliweza kupata maumivu ya kimapenzi, alijikuta akiwa ni mpenzi wa kuperuzi mtandao wa kijamii wa Instagram, aliuamini mtandao huo na ndiyo ambao uliweza kumsahaulisha maumivu yote ya kimapenzi ambayo moyo wake ulikuwa umeyapata.
Monalisa king'ang'anizi kama ruba

the Legend☆
 
Mademu kama Monalisa Dawa yao ni kula 0713 huku unamtia makofi ya Chogo [emoji297]️🤬🤬🤬 Hatokufatafata tena, Naona dogo Richard analeta Urembo Mida ya kuwa serious


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Sehemu ya 38.

Moyo wa Evelyne ulihamisha mapenzi kutoka kwa Richard kwenda kwa mwanaume mwingine ambaye alikuwa ni Fredrick, hakutaka kusikia lolote kutoka kwa mwanaume huyo ambaye alizidi kuiteka akili yake, alimuona kuwa kama Malaika ambaye alishusha kwa ajili ya kumfariji kwa maumivu aliyokuwa ameyapata.

Mpaka kufikia kipindi hicho alikuwa bado hajaonana na Fredrick, aliishia kumuona kwenye mtandao wa Intagram na kuwasiliana naye kwenye simu, muda mwingine walikuwa wakitumiana picha WhatsApp.

Fredrick alikuwa akiishi Daresalaam maeneo ya Tabata Segerea lakini pia alikuwa ni mfanyakazi katika kampuni moja binafsi iliyokuwa ikijihusisha na mambo ya Bima.

Alizidi kuiteka akili ya Evelyne bila kujijua na kila siku penzi lao lilizidi kuota mizizi. Katika moyo wa Evelyne hakukuwa na nafasi ya mwanaume mwingine zaidi ya Fredrick mwanaume ambaye alitokea kumpenda bila kujua sababu.

“Nitakuona lini mpenzi?”
“Usijali utaniona tu.”
“Lini?”
“Wikiendi hii.”
“Kweli?”
“Ndiyo uhakika.”
“Nitafurahi bebi.”
“Hata mimi nitafurahi pia.”
“Kwanini?”

“Kwasababu nitakuona kiuhalisia, nitaushuhudia uzuri wako kwa macho lakini pia nitapata nafasi ya kukushika.”
“Nakupenda Fredick natamani hata kesho nikuone jamani.”
“Usijali tumuombe Mungu atufikishe salama Jumamosi hii tuonane.”
“Ameen.”

Walimaliza kuzungumza kwenye simu huku kila mmoja wao akionekana kutawaliwa na furaha kwa kuzungumza na mwenzake. Walipanga wikiendi ya wiki hiyo wakutane na ndiyo ilikuwa siku yao ya kwanza ambayo walikuwa wanaenda kuonana tangu walipoanzisha mahusiano yao ya kimapenzi mtandaoni.

Japo hawakuwahi kuonana lakini walipendana sana, walifarijiana, walishauriana, waliahidiana mambo mengi sana kama wapenzi. Picha za Fredrick alizomtumia Evelyne pamoja na sauti yake ya upole iliyosanjari na maneno yake ya faraja yalitosha kabisa kumteka Evelyne, kila alipokuwa akizitazama picha za mwanaume huyo aliona alikuwa na kila sababu ya kumpenda.
 
Sehemu ya 39.

“Kwahiyo Richard hana lake tena?” aliuliza Happy.
“Ndiyo naweza kusema hivyo,” alijibu Evelyne.
“Lakini kwanini umeshindwa kumsamehe huoni kama utakuwa umemuhukumu bure?” aliuliza Happy.

“Nimeshamsamehe lakini siwezi kurudiana naye,” alijibu Evelyne.
“Huyo Fredrick atakusaidia nini, kwanini usirudiane na Richard ambaye umetoka naye mbali na amekiri makosa yake?”
“Siwezi Happy.”

“Mapenzi ya mtandaoni hayadumu, huyo Fredrick atakuchezea mwisho wa siku akuache.”
“Siamini kama anaweza kunifanyia hivyo.”

“Kwani umeshaonana naye?”
“Hapana ila wikiendi hii nakwenda kuonana naye.”
“Unamjua?”
“Ndiyo amenitumia picha zake.”
“Unaamini vipi kuwa ndiyo yeye je, kama amekudanganya?”
“Ndiyo yeye nina uhakika.”
“Kuwa makini,” alisema Happy.

Licha ya mambo yote yaliyokuwa yametokea lakini bado Happy alitamani Evelyne arudiane na Richard, hakutaka kuona wawili hao wakitengana, mwanzoni alihisi labda zilikuwa ni hasira za Evelyne na mwisho wa siku zingeisha na kuweza kurudiana na mpenzi wake lakini hilo halikuweza kutokea. Evelyne alikuwa tayari ameanzisha mahusiano na mwanaume mwingine.

Hatimaye siku ya Jumamosi iliweza kufika, Fredrick alimpigia simu Evelyne na kumwambia kuwa siku hiyo walitakiwa kuonana nyumbani kwake, Evelyne hakutaka kuamini siku hiyo alikuwa anaenda kuonana na mwanaume aliyekuwa anampenda.

Hakutaka kupoteza muda alijiandaa haraka, alipomaliza kujiandaa safari ya kuelekea Tabata Segerea akaianza. Moyo wake ulikuwa na furaha muda wote kila alipomkumbuka Fredrick, katika mawazo yake aliunda taswira ya Fredrick ambaye alikuwa akizungumza. Mapigo ya moyo wake yalikuwa yanamuenda mbio, hakutaka kuamini hata kidogo kama alikuwa anaenda kukutana na mwanaume huyo.

Baada ya kupita dakika arobaini alikuwa tayari ameshafika Tabata Segerea, alimpigia simu Fredrick kumjulisha kuwa tayari alikuwa ameshafika, haikuchukua dakika chache Fredrick aliweza kufika, walipoonana kwa mara ya kwanza walikumbatiana, Evelyne hakuamini macho yake kama aliweza kumuona Fredrick mwanaume ambaye aliishia kumuona Instagram na kuzungumza naye kwenye simu. Ilikuwa ni zaidi ya furaha kwa wawili hao kuweza kukutana.
 
Sehemu ya 40.

Fredrick alimpeleka Evelyne nyumbani kwake alipokuwa anaishi, siku hiyo Evelyne kila kitu alichokuwa akikiona kwa Fredrick kiliweza kumshangaza, licha ya umri mdogo aliyokuwa nao mwanaume huyo lakini alikuwa tayari ameshajipanga kimaisha.

“Hapa ni kwako?” aliuliza Evelyne alipoingia nyumbani kwa Fredrick.
“Hapana ni kwako pia,” alijibu Fredrick huku akimtazama Evelyne ambaye kwa muda huo alikuwa akitazama samani zilizokuwa ndani ya nyumba hiyo.

Fredrick hakutaka kumuacha Evelyne aendelee kumuuliza maswali mengi kwa wakati huo, alichoamua kukifanya ni kumuuliza aina ya kinywaji ambacho alikuwa anatumia baada ya kuketi katika sofa.

“Unatumia Juisi, maziwa au soda?” aliuliza Fredrick huku akimtazama Evelyne.

“Niletee chochote,” alijibu Evelyne kwa sauti ya aibu.
“Ndiyo maana nikakutajia inabidi uchague kimoja wapo hapo,” alisema Fredrick.
“Ok basi niletee juisi.”
“Unapenda ya tunda gani?”

“Lolote lile mimi natumia,” alijibu Evelyne kisha Fredrick akaenda kumletea.
Evelyne hakutaka kuamini kama kweli mwanaume huyo alikuwa peke yake siku zote hizo, huo ulikuwa ni wasiwasi uliyoanza kumuingia mara baada ya kuyaona mazingira ya nyumba hiyo jinsi yalivyokuwa mazuri.

“Karibu,” alisema Fredrick baada ya kurudi, mikononi alikuwa amebeba glass mbili, moja ilikuwa ni ya juisi na nyingine ilikuwa ni ya maziwa. Alipomkaribia Evelyne alimpatia ile glass ya juisi halafu na yeye akaketi pembeni yake, mkononi alikuwa amebakiwa na glass ya maziwa.

Wakaanza kunywa taratibu huku wakitazamana kwa macho ya kuibianaibiana.

“Nikuulize kitu?” aliuliza Evelyne.
“Ndiyo niulize,” alijibu Fredrick.
“Kwani unaishi na nani hapa?”
“Mwenyewe.”
“Una uhakika?”
“Ndiyo.”
“Hauna mwanamke mwingine kweli?”
*
*
Je, nini kitaendelea?
 
Sehemu ya 40.

Fredrick alimpeleka Evelyne nyumbani kwake alipokuwa anaishi, siku hiyo Evelyne kila kitu alichokuwa akikiona kwa Fredrick kiliweza kumshangaza, licha ya umri mdogo aliyokuwa nao mwanaume huyo lakini alikuwa tayari ameshajipanga kimaisha.

“Hapa ni kwako?” aliuliza Evelyne alipoingia nyumbani kwa Fredrick.
“Hapana ni kwako pia,” alijibu Fredrick huku akimtazama Evelyne ambaye kwa muda huo alikuwa akitazama samani zilizokuwa ndani ya nyumba hiyo.

Fredrick hakutaka kumuacha Evelyne aendelee kumuuliza maswali mengi kwa wakati huo, alichoamua kukifanya ni kumuuliza aina ya kinywaji ambacho alikuwa anatumia baada ya kuketi katika sofa.

“Unatumia Juisi, maziwa au soda?” aliuliza Fredrick huku akimtazama Evelyne.

“Niletee chochote,” alijibu Evelyne kwa sauti ya aibu.
“Ndiyo maana nikakutajia inabidi uchague kimoja wapo hapo,” alisema Fredrick.
“Ok basi niletee juisi.”
“Unapenda ya tunda gani?”

“Lolote lile mimi natumia,” alijibu Evelyne kisha Fredrick akaenda kumletea.
Evelyne hakutaka kuamini kama kweli mwanaume huyo alikuwa peke yake siku zote hizo, huo ulikuwa ni wasiwasi uliyoanza kumuingia mara baada ya kuyaona mazingira ya nyumba hiyo jinsi yalivyokuwa mazuri.

“Karibu,” alisema Fredrick baada ya kurudi, mikononi alikuwa amebeba glass mbili, moja ilikuwa ni ya juisi na nyingine ilikuwa ni ya maziwa. Alipomkaribia Evelyne alimpatia ile glass ya juisi halafu na yeye akaketi pembeni yake, mkononi alikuwa amebakiwa na glass ya maziwa.

Wakaanza kunywa taratibu huku wakitazamana kwa macho ya kuibianaibiana.

“Nikuulize kitu?” aliuliza Evelyne.
“Ndiyo niulize,” alijibu Fredrick.
“Kwani unaishi na nani hapa?”
“Mwenyewe.”
“Una uhakika?”
“Ndiyo.”
“Hauna mwanamke mwingine kweli?”
*
*
Je, nini kitaendelea?
More episodes please:
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom