Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,400
- 465,165
- Thread starter
- #81
Sehemu ya 31.
“Siamini kama kweli Richard ameweza kunifanyia hivi, yani mapenzi yangu yote niliyompa bado amenisaliti ama kweli wanaume wabaya sana,” alisema Evelyne kwa sauti iliyoandamana na kilio.
“Kumbe kweli anatembea na Monalisa?” aliuliza Happy.
“Mwanzoni sikutaka kuamini niliposikia kuwa wanamahusiano, nilimuamini sana lakini katika hili siwezi tena kumuamini, ameuvunja uaminifu wangu kwake, namchukia sana,” alisema Evelyne.
Huo ulikuwa ni ukweli wenye kuuma mno tena mara zote alipomkumbuka mpenzi wake hakutaka kuamini, machozi yalikuwa yakimtoka. ****
Richard alizidi kuchanganyikiwa, kila alilokuwa akiliwaza kulifanya kama ishara ya kumuomba mpenzi wake msamaha aliona kama anakosea.
Alizidi kuwa katika wakati mgumu sana kipindi ambacho alikuwa akimuona Evelyne darasani, kuna muda alitamani kuzungumza naye kisha amuombe msamaha lakini Evelyne hakuwa tayari, alimchukia mno Richard tena chuki za waziwazi.
Hakuwa na njia nyingine ya kufanya zaidi ya kumfuata Happy na kuamua kuzungumza naye, alihitaji kumuomba msamaha Evelyne lakini aliamini ilikuwa ni vigumu sana kwa yeye kuweza kueleweka, alijua kuwa alifanya makosa sana kwa kumsaliti mpenzi wake lakini bado hakutaka kuamini kuwa huo ndiyo mwisho wa mapenzi yake kwa Evelyne.
“Najua nimemkosea sana Evelyne lakini tafadhali mwambie asinichukie moyo wangu bado unampenda,” alisema Richard huku akimtazama Happy kwa macho ya huruma.
“Richard hivi kwanini umeamua kumsaliti Evelyne?” aliuliza Happy.
“Sijui ata niseme nini? Nashindwa kujielezea Happy, nashindwa nimejikuta tu namsaliti,” alijibu Richard.
“Richard embu acha kunifanya mimi mtoto mdogo wakati picha zako za uchafu na huyo mchepuko wako nimeziona yani sikutegemea kama ungeweza kumfanyia ukatili huu rafiki yangu, Richard wewe ni mbaya sana unatembea na Monalisa?” aliuliza Happy.
“Hapana usiseme hivyo narudia tena moyo wangu bado unampenda Evelyne na ninahitaji anisamehe, najua ananichukia sana lakini tafadhali jaribu kuzungumza naye pengine anaweza akabadili mawazo yake,” alisema Richard.
“Siamini kama kweli Richard ameweza kunifanyia hivi, yani mapenzi yangu yote niliyompa bado amenisaliti ama kweli wanaume wabaya sana,” alisema Evelyne kwa sauti iliyoandamana na kilio.
“Kumbe kweli anatembea na Monalisa?” aliuliza Happy.
“Mwanzoni sikutaka kuamini niliposikia kuwa wanamahusiano, nilimuamini sana lakini katika hili siwezi tena kumuamini, ameuvunja uaminifu wangu kwake, namchukia sana,” alisema Evelyne.
Huo ulikuwa ni ukweli wenye kuuma mno tena mara zote alipomkumbuka mpenzi wake hakutaka kuamini, machozi yalikuwa yakimtoka. ****
Richard alizidi kuchanganyikiwa, kila alilokuwa akiliwaza kulifanya kama ishara ya kumuomba mpenzi wake msamaha aliona kama anakosea.
Alizidi kuwa katika wakati mgumu sana kipindi ambacho alikuwa akimuona Evelyne darasani, kuna muda alitamani kuzungumza naye kisha amuombe msamaha lakini Evelyne hakuwa tayari, alimchukia mno Richard tena chuki za waziwazi.
Hakuwa na njia nyingine ya kufanya zaidi ya kumfuata Happy na kuamua kuzungumza naye, alihitaji kumuomba msamaha Evelyne lakini aliamini ilikuwa ni vigumu sana kwa yeye kuweza kueleweka, alijua kuwa alifanya makosa sana kwa kumsaliti mpenzi wake lakini bado hakutaka kuamini kuwa huo ndiyo mwisho wa mapenzi yake kwa Evelyne.
“Najua nimemkosea sana Evelyne lakini tafadhali mwambie asinichukie moyo wangu bado unampenda,” alisema Richard huku akimtazama Happy kwa macho ya huruma.
“Richard hivi kwanini umeamua kumsaliti Evelyne?” aliuliza Happy.
“Sijui ata niseme nini? Nashindwa kujielezea Happy, nashindwa nimejikuta tu namsaliti,” alijibu Richard.
“Richard embu acha kunifanya mimi mtoto mdogo wakati picha zako za uchafu na huyo mchepuko wako nimeziona yani sikutegemea kama ungeweza kumfanyia ukatili huu rafiki yangu, Richard wewe ni mbaya sana unatembea na Monalisa?” aliuliza Happy.
“Hapana usiseme hivyo narudia tena moyo wangu bado unampenda Evelyne na ninahitaji anisamehe, najua ananichukia sana lakini tafadhali jaribu kuzungumza naye pengine anaweza akabadili mawazo yake,” alisema Richard.