Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 152,998
- 453,945
Mtunzi Juma hiza Sehemu ya 01
Hali ya hewa ilikuwa shwari katika jiji la Daresalaam. Ndani ya chuo cha Usimamizi wa Fedha IFM kilichokuwepo maeneo ya Posta mtaa wa Shaaban Robert, msichana mrembo aliyejulikana kwa jina la Evelyne alionekana akitoka darasani huku akiwa anakimbia, machozi yalikuwa yakimdondoka kwa wakati huo.
“Evelyne! Evelyne! Evelyne,” ilisikika sauti ya msichana mwingine ambaye alikuwa akimfuata nyuma Evelyne baada ya kutoka darasani.
Evelyne aliongoza moja kwa moja mpaka kwenye kimbweta, alipofika hapo aliketi na kuanza kulia huku akiwa amejiinamia.
“Evelyne kuna nini mbona sikuelewi?” aliuliza msichana huyo aliyekuwa akimfuata nyuma Evelyne, alionekana kutoelewa chochote kilichokuwa kikiendelea kwa wakati huo.
“Hapana Happy siwezi kuendelea kuwa eneo hili acha niondoke zangu,” alisema Evelyne kwa sauti iliyoandamana na kilio cha kwikwi.
“Unaondoka unaenda wapi sasa na wakati darasani kuna kipindi?” aliuliza Happy huku akimtazama Evelyne ambaye aliendelea kulia muda wote huo.
“Narudi zangu nyumbani,” alijibu Evelyne.
“Unajua sikuelewi Evelyne,” alisema Happy lakini kabla ya Evelyne kumjibu lolote aliinuka na kuondoka eneo hilo la chuo, Happy alibaki akimtazama Evelyne huku asijue ni nini kilichokuwa kikiendelea.
Evelyne na Happy walikuwa ni marafiki wakubwa sana katika chuo hicho, walikuwa wakisaidiana mambo mengi sana, walishiriki kusaidiana katika masomo na hata katika mipango yao ya kimaisha pia walishirikishana.
Happy alikuwa akimfahamu vyema rafiki yake huyo tangu walipoanza kusoma katika chuo hicho mpaka kufikia mwaka waowa mwisho wa Digrii ambao ndiyo walikuwa wameubakiza. Walikuwa wakisomea Uhasibu.
Kila kitu kilichokuwa kikiendelea katika maisha ya Evelyne, Happy alikifahamu na kila kitu kilichokuwa kikiendelea katika maisha ya Happy, Evelyne naye alikifahamu, kwa kifupi walikuwa ni marafiki waliyoshibana.
Walikuwa wakiishi pamoja katika chumba kimoja walichokuwa wamepanga maeneo ya Kigamboni.
Hali ya hewa ilikuwa shwari katika jiji la Daresalaam. Ndani ya chuo cha Usimamizi wa Fedha IFM kilichokuwepo maeneo ya Posta mtaa wa Shaaban Robert, msichana mrembo aliyejulikana kwa jina la Evelyne alionekana akitoka darasani huku akiwa anakimbia, machozi yalikuwa yakimdondoka kwa wakati huo.
“Evelyne! Evelyne! Evelyne,” ilisikika sauti ya msichana mwingine ambaye alikuwa akimfuata nyuma Evelyne baada ya kutoka darasani.
Evelyne aliongoza moja kwa moja mpaka kwenye kimbweta, alipofika hapo aliketi na kuanza kulia huku akiwa amejiinamia.
“Evelyne kuna nini mbona sikuelewi?” aliuliza msichana huyo aliyekuwa akimfuata nyuma Evelyne, alionekana kutoelewa chochote kilichokuwa kikiendelea kwa wakati huo.
“Hapana Happy siwezi kuendelea kuwa eneo hili acha niondoke zangu,” alisema Evelyne kwa sauti iliyoandamana na kilio cha kwikwi.
“Unaondoka unaenda wapi sasa na wakati darasani kuna kipindi?” aliuliza Happy huku akimtazama Evelyne ambaye aliendelea kulia muda wote huo.
“Narudi zangu nyumbani,” alijibu Evelyne.
“Unajua sikuelewi Evelyne,” alisema Happy lakini kabla ya Evelyne kumjibu lolote aliinuka na kuondoka eneo hilo la chuo, Happy alibaki akimtazama Evelyne huku asijue ni nini kilichokuwa kikiendelea.
Evelyne na Happy walikuwa ni marafiki wakubwa sana katika chuo hicho, walikuwa wakisaidiana mambo mengi sana, walishiriki kusaidiana katika masomo na hata katika mipango yao ya kimaisha pia walishirikishana.
Happy alikuwa akimfahamu vyema rafiki yake huyo tangu walipoanza kusoma katika chuo hicho mpaka kufikia mwaka waowa mwisho wa Digrii ambao ndiyo walikuwa wameubakiza. Walikuwa wakisomea Uhasibu.
Kila kitu kilichokuwa kikiendelea katika maisha ya Evelyne, Happy alikifahamu na kila kitu kilichokuwa kikiendelea katika maisha ya Happy, Evelyne naye alikifahamu, kwa kifupi walikuwa ni marafiki waliyoshibana.
Walikuwa wakiishi pamoja katika chumba kimoja walichokuwa wamepanga maeneo ya Kigamboni.