Nisamehe Mpenzi

Nisamehe Mpenzi

Sehemu ya 51.

Baada ya masaa kadhaa kupita, hatimaye majibu yaliweza kutolewa na daktari, kutokana na ajali aliyoipata Fredrick ilimsababishia matatizo katika kizazi chake pamoja na mshtuko aliyoupata ulimpelekea kupooza hivyo katika maisha yake angeshindwa kuamka na kufanya shughuli zake kama ilivyokuwa kawaida na badala yake maisha yake yalibadilika na kuwa ni ya kitandani.

Fredrick alikuwa amelala kitandani, uso wake ulikuwa umetawaliwa na furaha, alizidi kuonekana kuyafurahia maisha yake.

Alimtazama mke wake ambaye machozi yalikuwa yakimdondoka kwa muda huo, Evelyne kila alipokuwa akimtazama mume wake jinsi alivyokuwa amelala kitandani alihisi maumivu makali mno ndani ya moyo wake.

Alimpenda sana mume wake, hakutaka kumuona akiendelea kuteseka, alipanga kufanya kila awezalo ili aweze kuyaokoa maisha yake lakini alipoyakumbuka majibu ya daktari kuwa asingeweza kupona, alizidi kuumia mno.

Hakuna maumivu makali kama kumuona yule umpendae akiteseka kwa ugonjwa katika dunia hii, ni zaidi ya maumivu makali mno.

Machozi yaliendelea kumbubujika Evelyne pale hospitalini, hakutaka kuamini kama mume wake alikuwa amepooza na kibaya zaidi alipoteza uwezo wa kupata mtoto. Hilo liliendelea kumuumiza sana moyo wake.

Ilikuwa imepita miezi kadhaa tangu walipofunga ndoa yao, kabla ya kufika hata mwaka tayari ndoa hiyo ilikuwa imeingiwa na tatizo.

Ndugu wa mume wake walipozipata taarifa za ajali hiyo hawakutaka kuelewa chochote, waliamini ilikuwa ni ajali ya kupangwa na ilisababishwa na Evelyne ambaye walidai alizitamani mali za ndugu yao.
 
Sehemu ya 52.

Mwanzo wa maneno na vitisho vikaanzia hapo, hakukuwa kuna ndugu upande wa mume aliyekuwa upande wa Evelyne, wote walimchukia.

Kuna muda Evelyne alikuwa akikufuru Mungu, alihisi kuonewa, hakutaka kuamini kama yeye ndiye alikuwa binadamu mwenye makosa mengi zaidi hapa duniani mpaka akafikia hatua ya kupewa matatizo hayo.

"Usilie mke wangu, usilie futa machozi yako," alisema Fredrick.
"Nashindwa kufanya hivyo mume wangu," alijibu Evelyne huku machozi yakiendelea kumdondoka.

Alipokuwa akiendelea kumtazama mume wake pale kitandani machozi yalizidi kumbubujika tu, kila kitu kilibadilika katika maisha yake, alipowakumbuka ndugu wa mume wake alizidi kujisikia vibaya mno, alijua fika hawakumpenda, walimtenga hivyo kila kitu alichokuwa akikifanya kilionekana kuwa kibaya.

Aliamua kuwapigia simu wazazi wake na kuwaeleza kila kitu kilichokuwa kikiendelea, alihitaji msaada wao lakini walionekana kuchukizwa na taarifa hizo, hawakutaka kuona akiendelea kuteseka wakati bado walikuwa hai.

Maamuzi ambayo waliamua kuyachukua ni kumuhitaji binti yao arudi nyumbani haraka iwezekanavyo.

"Naomba upande basi kesho uwe umeshafika hapa nyumbani," alisema baba yake kwa sauti ya ukali.

"Nitaondokaje baba halafu nitamuacha Mume wangu na nani?" Aliuliza Evelyne.
"Muache na ndugu zake wewe rudi zako nyumbani," alijibu baba yake kwa msisitizo.

"Hapana baba bado itakuwa ni vigumu kwani nitahitajika pia kazini," alisema Evelyne.

Yalikuwa ni mazungumzo mafupi ambayo yalihitajika utekelezaji wa haraka sana lakini Evelyne hakutaka kukubaliana nayo. Hakutaka kuona akiondoka na kumuacha mume wake akiendelea kuteseka kitandani.

Alikumbuka siku yao ya harusi jinsi alivyokula kiapo mbele za watu na kuahidi kuishi naye katika shida na raha, aliamini katika kipindi hicho kilikuwa ni cha shida hivyo hakuwa na jinsi ya kufanya ilibidi amvumilie mume wake.
 
Sehemu ya 53.

Rafiki yake Happy hakumtupa mkono katika kipindi hicho, alikuwa na yeye bega kwa bega katika kila hali, alionyesha msaada mkubwa sana.

Alipokuwa akimuona Evelyne akiteseka na mume wake hospitalini alimuonea huruma sana, alizidi kumfariji kwa maneno ya matumaini ambayo yalizidi kumpa nguvu. Ndoto yake kubwa aliamini siku moja mume wake angeweza kuinuka kitandani na maisha yakaendelea lakini hilo lilikuwa ni jambo lisilowezekana.

Siku ziliendelea kukatika huku Fredrick na yeye akizidi kuteseka hospitalini, alianza kupoteza matumaini ya kuishi baada ya afya yake kuanza kudhoofika, aliamini ule ndiyo ulikuwa mwisho wa maisha yake, mwisho wenye mateso makali mno.

"Hapana usijiwazie kifo, huwezi kufa mume wangu," alisema Evelyne.
"Angalia ninavyoteseka hapa kitandani mke wangu, madaktari wameshindwa kunitibu hivi unafikiri nitapona kweli?"aliuliza Fredrick huku machozi yakimbubujika.

"Hapana huwezi kufa," alisema Evelyne.
Yalikuwa ni maneno machache lakini aliamua kuishi ndani yake, hakutaka kumpoteza Fredrick, alichoamua kukifanya ni kuanza kuhangaikia matibabu yake.

Madaktari walimshauri ampeleke mume wake nchini India katika hospital ya Apollo iliyokuwepo nchini humo kwani huko ndipo palipokuwa na uwezekano mkubwa wa mume wake kutibiwa na kupona kabisa.

Alipoambiwa hivyo hakutaka kupoteza muda, alianza kupanga mipango wa kumsafirisha mume wake nchini humo na baada ya kufanyiwa matibabu iligundulika kuwa Fredrick asingeweza kupona.

Hilo lilizidi kumuumiza sana, hakutaka kuamini maneno hayo hata kidogo.
Aliporudi nchini Tanzania bado aliendelea kuhangaika na mume wake.

Ilifikia wakati akaanza kuwaamini wachungaji, alipokuwa akisikia palikuwa na mchungaji ambaye aliweza kumuombea kilema kisha akapona aliamua kwenda, kila kanisa alilokuwa akienda kwa ajili ya maombi ya mume wake hakuna miujiza iliyoweza kutendeka.
**
 
Sehemu ya 54.

Richard alifahamu kila kitu kilichokuwa kikiendelea katika maisha ya Evelyne, alimpenda mno msichana huyo, kutokana na hali aliyokuwa nayo aliamini ulikuwa ndiyo muda wake muafaka wa yeye kujitokeza kwa mara nyingine, hakutaka kumuomba msamaha ila alichoamua kukifanya ni kurudi kama rafiki ambaye aliguswa na matatizo yaliyompata Evelyne katika ndoa yake.

Alijitoa katika kila hali na mali, hakutaka kuonekana adui kwa msichana huyo, kila alilokuwa akilifanya alilifanya kwa kuonyesha moyo wa msaada.

Baada ya kupita miezi miwili Fredrick aliweza kupoteza maisha, kilikuwa ni kifo ambacho kilimuacha Evelyne na maumivu makali mno, ndugu zake Fredrick waliamua kumshtaki Evelyne polisi na kisha wakamfungulia kesi ya mauaji, ilikuwa ni kesi nzito ambayo ilimuweka Evelyne na hatia ya mauaji lakini kutokana na uwezo wa kifedha aliyokuwa nao Richard alihakikisha anapigana mpaka anafanikiwa kumuweka huru Evelyne.

Richard alimuomba msamaha Evelyne na kumuahidi kuwa muaminifu katika maisha yake yote. Evelyne hakuwa na kipingamizi chochote, aliamua kumsamehe Richard kisha mapenzi yao yakarudi kuwa kama zamani.

Walifanikiwa kufunga ndoa na baada ya mwaka mmoja kupita walifanikiwa kupata mtoto wa kiume, alikuwa ni mtoto mzuri sana, aliyekuwa na afya njema. Evelyne aliamua kumpa jina la Fredrick ikiwa ni kama kumbukumbu ya kumuenzi mwanaume huyo huko alipo.

Maisha yao yalizidi kutawaliwa na furaha huku mtoto wao akiendelea kukuwa vizuri bila matatizo yoyote.
*
*

MWISHO.

Mwisho wa simulizi hii ndiyo mwanzo wa simulizi nyingine nzuri ya maisha.
 
Sehemu ya 54.

Richard alifahamu kila kitu kilichokuwa kikiendelea katika maisha ya Evelyne, alimpenda mno msichana huyo, kutokana na hali aliyokuwa nayo aliamini ulikuwa ndiyo muda wake muafaka wa yeye kujitokeza kwa mara nyingine, hakutaka kumuomba msamaha ila alichoamua kukifanya ni kurudi kama rafiki ambaye aliguswa na matatizo yaliyompata Evelyne katika ndoa yake.

Alijitoa katika kila hali na mali, hakutaka kuonekana adui kwa msichana huyo, kila alilokuwa akilifanya alilifanya kwa kuonyesha moyo wa msaada.

Baada ya kupita miezi miwili Fredrick aliweza kupoteza maisha, kilikuwa ni kifo ambacho kilimuacha Evelyne na maumivu makali mno, ndugu zake Fredrick waliamua kumshtaki Evelyne polisi na kisha wakamfungulia kesi ya mauaji, ilikuwa ni kesi nzito ambayo ilimuweka Evelyne na hatia ya mauaji lakini kutokana na uwezo wa kifedha aliyokuwa nao Richard alihakikisha anapigana mpaka anafanikiwa kumuweka huru Evelyne.

Richard alimuomba msamaha Evelyne na kumuahidi kuwa muaminifu katika maisha yake yote. Evelyne hakuwa na kipingamizi chochote, aliamua kumsamehe Richard kisha mapenzi yao yakarudi kuwa kama zamani.

Walifanikiwa kufunga ndoa na baada ya mwaka mmoja kupita walifanikiwa kupata mtoto wa kiume, alikuwa ni mtoto mzuri sana, aliyekuwa na afya njema. Evelyne aliamua kumpa jina la Fredrick ikiwa ni kama kumbukumbu ya kumuenzi mwanaume huyo huko alipo.

Maisha yao yalizidi kutawaliwa na furaha huku mtoto wao akiendelea kukuwa vizuri bila matatizo yoyote.
*
*

MWISHO.

Mwisho wa simulizi hii ndiyo mwanzo wa simulizi nyingine nzuri ya maisha.

Simple like that Mwisho mzuri


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Sehemu ya 51.

Baada ya masaa kadhaa kupita, hatimaye majibu yaliweza kutolewa na daktari, kutokana na ajali aliyoipata Fredrick ilimsababishia matatizo katika kizazi chake pamoja na mshtuko aliyoupata ulimpelekea kupooza hivyo katika maisha yake angeshindwa kuamka na kufanya shughuli zake kama ilivyokuwa kawaida na badala yake maisha yake yalibadilika na kuwa ni ya kitandani.

Fredrick alikuwa amelala kitandani, uso wake ulikuwa umetawaliwa na furaha, alizidi kuonekana kuyafurahia maisha yake.

Alimtazama mke wake ambaye machozi yalikuwa yakimdondoka kwa muda huo, Evelyne kila alipokuwa akimtazama mume wake jinsi alivyokuwa amelala kitandani alihisi maumivu makali mno ndani ya moyo wake.

Alimpenda sana mume wake, hakutaka kumuona akiendelea kuteseka, alipanga kufanya kila awezalo ili aweze kuyaokoa maisha yake lakini alipoyakumbuka majibu ya daktari kuwa asingeweza kupona, alizidi kuumia mno.

Hakuna maumivu makali kama kumuona yule umpendae akiteseka kwa ugonjwa katika dunia hii, ni zaidi ya maumivu makali mno.

Machozi yaliendelea kumbubujika Evelyne pale hospitalini, hakutaka kuamini kama mume wake alikuwa amepooza na kibaya zaidi alipoteza uwezo wa kupata mtoto. Hilo liliendelea kumuumiza sana moyo wake.

Ilikuwa imepita miezi kadhaa tangu walipofunga ndoa yao, kabla ya kufika hata mwaka tayari ndoa hiyo ilikuwa imeingiwa na tatizo.

Ndugu wa mume wake walipozipata taarifa za ajali hiyo hawakutaka kuelewa chochote, waliamini ilikuwa ni ajali ya kupangwa na ilisababishwa na Evelyne ambaye walidai alizitamani mali za ndugu yao.
Dah maskini, Fredrick amenisikitisha[emoji22] jamaa ni gentleman sana

the Legend☆
 
Sehemu ya 54.

Richard alifahamu kila kitu kilichokuwa kikiendelea katika maisha ya Evelyne, alimpenda mno msichana huyo, kutokana na hali aliyokuwa nayo aliamini ulikuwa ndiyo muda wake muafaka wa yeye kujitokeza kwa mara nyingine, hakutaka kumuomba msamaha ila alichoamua kukifanya ni kurudi kama rafiki ambaye aliguswa na matatizo yaliyompata Evelyne katika ndoa yake.

Alijitoa katika kila hali na mali, hakutaka kuonekana adui kwa msichana huyo, kila alilokuwa akilifanya alilifanya kwa kuonyesha moyo wa msaada.

Baada ya kupita miezi miwili Fredrick aliweza kupoteza maisha, kilikuwa ni kifo ambacho kilimuacha Evelyne na maumivu makali mno, ndugu zake Fredrick waliamua kumshtaki Evelyne polisi na kisha wakamfungulia kesi ya mauaji, ilikuwa ni kesi nzito ambayo ilimuweka Evelyne na hatia ya mauaji lakini kutokana na uwezo wa kifedha aliyokuwa nao Richard alihakikisha anapigana mpaka anafanikiwa kumuweka huru Evelyne.

Richard alimuomba msamaha Evelyne na kumuahidi kuwa muaminifu katika maisha yake yote. Evelyne hakuwa na kipingamizi chochote, aliamua kumsamehe Richard kisha mapenzi yao yakarudi kuwa kama zamani.

Walifanikiwa kufunga ndoa na baada ya mwaka mmoja kupita walifanikiwa kupata mtoto wa kiume, alikuwa ni mtoto mzuri sana, aliyekuwa na afya njema. Evelyne aliamua kumpa jina la Fredrick ikiwa ni kama kumbukumbu ya kumuenzi mwanaume huyo huko alipo.

Maisha yao yalizidi kutawaliwa na furaha huku mtoto wao akiendelea kukuwa vizuri bila matatizo yoyote.
*
*

MWISHO.

Mwisho wa simulizi hii ndiyo mwanzo wa simulizi nyingine nzuri ya maisha.
Mwisho mzuri kwa Richard, ila Fredrick kanisikitisha sana.
Asante Shunie

the Legend☆
 
Sehemu ya 54.

Richard alifahamu kila kitu kilichokuwa kikiendelea katika maisha ya Evelyne, alimpenda mno msichana huyo, kutokana na hali aliyokuwa nayo aliamini ulikuwa ndiyo muda wake muafaka wa yeye kujitokeza kwa mara nyingine, hakutaka kumuomba msamaha ila alichoamua kukifanya ni kurudi kama rafiki ambaye aliguswa na matatizo yaliyompata Evelyne katika ndoa yake.

Alijitoa katika kila hali na mali, hakutaka kuonekana adui kwa msichana huyo, kila alilokuwa akilifanya alilifanya kwa kuonyesha moyo wa msaada.

Baada ya kupita miezi miwili Fredrick aliweza kupoteza maisha, kilikuwa ni kifo ambacho kilimuacha Evelyne na maumivu makali mno, ndugu zake Fredrick waliamua kumshtaki Evelyne polisi na kisha wakamfungulia kesi ya mauaji, ilikuwa ni kesi nzito ambayo ilimuweka Evelyne na hatia ya mauaji lakini kutokana na uwezo wa kifedha aliyokuwa nao Richard alihakikisha anapigana mpaka anafanikiwa kumuweka huru Evelyne.

Richard alimuomba msamaha Evelyne na kumuahidi kuwa muaminifu katika maisha yake yote. Evelyne hakuwa na kipingamizi chochote, aliamua kumsamehe Richard kisha mapenzi yao yakarudi kuwa kama zamani.

Walifanikiwa kufunga ndoa na baada ya mwaka mmoja kupita walifanikiwa kupata mtoto wa kiume, alikuwa ni mtoto mzuri sana, aliyekuwa na afya njema. Evelyne aliamua kumpa jina la Fredrick ikiwa ni kama kumbukumbu ya kumuenzi mwanaume huyo huko alipo.

Maisha yao yalizidi kutawaliwa na furaha huku mtoto wao akiendelea kukuwa vizuri bila matatizo yoyote.
*
*

MWISHO.

Mwisho wa simulizi hii ndiyo mwanzo wa simulizi nyingine nzuri ya maisha.
Shukrani Shunie, God bless you mama.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kabisa mkuu. Hapo ndo huwa tunapofeli. Binafsi always huwa namshkuru sana Mungu kwa kunifanya nsiwe mwanaume wa kutawaliwa na mihemko, especially ya abdallah kichwa wazi, otherwise yaliyomkuta Richard yangekua yashanikuta zamani sana. Kina Monalisa vivuruge wako wengi sana

the Legend☆
Aah..wap..
msalimie shunie...

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom