Nisamehe Mpenzi

Nisamehe Mpenzi

Sehemu ya 16.

Alichokuwa akikifikiria katika kichwa chake kwa wakati huo ni jinsi gani angeweza kumuumiza Evelyne, alifahamu fika alikuwa akimpenda sana Richard na hakutaka kusikia kitu chochote kuhusu mpenzi wake huyo.

“This will be the end of your love for Richard,” (Huu ndiyo utakuwa mwisho wako wa kumpenda Richard,) alijisemea Monalisa maneno aliyoyasindikiza na tusi zito.

Aliichukua simu yake kisha akaiwasha, kitu cha kwanza aliingia katika sehemu ya kuhifadhi picha na video, alianza kutabasamu baada ya kuziona picha alizokuwa amejipiga akiwa pamoja na Richard kitandani, wakati huo Richard alikuwa amelala, hakuishia hapo pia aliamua kuingia katika sehemu ya video na hapo aliweza kuitazama video aliyoirekodi kipindi alipokuwa amelala na Richard, wote walikuwa uchi wa mnyama.

Aliamini kwa asilimia kubwa ni lazima video ile pamoja na zile picha alizopiga na Richard kitandani ni lazima zingeweza kuyasambaratisha mapenzi ya wawili hao.
“Your dangerous,” (Wewe ni hatari.)
“I told you that I can’t never fail,” (Nilikuambia kuwa kamwe siwezi kushindwa.)

“So what you are going to do?” (Kwahiyo nini unakwenda kukifanya?)
“I must make sure I destroyed this love,” (Lazima nihakikishe naliangamiza penzi hili.)

“About those photos and videos Richard has he seen?” (kuhusu hizo picha na video Richard ameziona?)
“Everything I did in secret so they did not know anything,” (Kila kitu nilikifanya kwa siri hivyo hajui lolote.)

Yalikuwa ni mazungumzo kati ya Monalisa na Adela, wakati huo Monalisa alikuwa akimuonyesha picha na video aliyojirekodi kipindi alipokuwa amelala na Richard. Adela alishikwa na butwaa baada ya kuziona picha hizo pamoja na video iliyokuwa ikimuonyesha Monalisa akiwa juu ya kifua cha Richard.
 
Sehemu ya 17.

“Itabidi uzifiche maana italeta picha mbaya endapo kila mtu akaziona,” alisema Adela huku akionekana kuogopa.
“Siogopi lolote ila ninachokitaka kuona nilichokipanga kinatimia,” alisema Monalisa.

“Unamaanisha nini?” aliuliza Adela. “Nitamtumia hizi picha pamoja na hii video WhatsApp.” “Nani?”.
“Evelyne.”

“Ataumia sana.”
“Nataka aumie zaidi yangu, nimeteseka sana katika kumpata Richard na huu ndiyo utakuwa mwanzo wa moyo wake kupokea maumivu ya kimapenzi,” alisema Monalisa huku akionekana kutokujali lolote.

Alidhamiria kufanya kila aliwezalo ilimradi afanikiwe kuliangamiza penzi hilo ambalo hakupendezewa nalo hata kidogo, alitamani yeye ndiye awe mpenzi wa Richard hivyo kwake kufanya lolote kwa ajili ya penzi hilo bila kujali maumivu ambayo angeweza kuyasababisha kwa Evelyne.

Hakutaka kupoteza muda alichoamua kukifanya usiku wa siku hiyo aliamua kuwasha data kweye simu yake kisha akaingia WhatsApp, alianza kuitafuta namba ya Evelyne ambayo alikuwa ameisevu kwa jina la “Vomiting” (Matapishi.) alipoliona jina hilo alilibonyeza kisha akaingia moja kwa moja katika uwanja wa kuandika ujumbe na kutuma chohote na kama alivyokuwa amepanga alianza kumtumia zile picha pamoja na video ambayo ilikuwa ikimuonyesha yeye akiwa kitandani pamoja na Richard.

Hakuishia hapo baada ya kumaliza kumtumia aliamua kuandika maneno machache ambayo pia alimtumia Evelyne, maneno hayo yalisomeka kwa herufi kubwa “YOUR HUSBAND.” (MUME WAKO.) ****

Richard alikuwa chumbani kwake huku akionekana kutokuwa sawa kabisa, hakutaka kuamini kwa kile kilichokuwa kimetokea siku hiyo alipokuwa hotelini.

Kichwani kwake mawazo ya Monalisa ndiyo yalikuwa yamemtawala, alikumbuka kila kitu kilichokuwa kimetokea lakini hakutaka kuamini hata kidogo, kuna muda alihisi labda alikuwa katika ndoto lakini haikuwa hivyo, alizidi kuchanganyikiwa baada ya kukumbuka kuwa simu yake aliichukua msichana huyo na kukimbia nayo.

Muda mwingine alimkumbuka mpenzi wake Evelyne, aliamini kwa vyovyote ni lazima alikuwa akimtafuta na kwa muda huo simu yake alikuwa nayo Monalisa.
 
Sehemu ya 18.

“Mungu wangu sijui Monalisa akipokea atamuambia nini?” alijiuliza swali hili katika mawazo yake.
Hakufahamu ni nini alichokuwa amedhamiria kukifanya Monalisa, alibaki katika hali ya sintofahamu huku asijue nini alitakiwa kukifanya kwa wakati huo.

Wakati akiendelea kuwaza mambo yote hayo lilimjia wazo kichwani, lilikuwa ni wazo la kumtafuta Evelyne kwa njia yoyote ili aweze kuzungumza naye, alipokumbuka umbali uliyokuwepo kati ya Mikocheni na Kigamboni alighairi kuchukua maamuzi hayo.

Alikumbuka kuwa Evelyne alikuwa akijulikana na Mama yake na alikuwa akipenda kuwasiliana naye mara kwa mara, hakutaka siku hiyo iweze kupita bila ya kuzungumza naye. Alichoamua kukifanya ni kwenda kumuomba Mama yake simu kisha akampigia, simu ya Evelyne ilikuwa ikiita bila ya kupokelewa. “Mbona hapokei simu ni nini kimemkuta?” alijiuliza Richard baada ya kumpigia simu Evelyne zaidi ya mara tatu bila kupokelewa.

Hakutaka kukata tamaa, aliendelea kupiga huku akitegemea kuna muda Evelyne angeweza kuipokea simu hiyo lakini tukio hilo halikuweza kutokea. ****
“Punguza wasiwasi Richard yuko salama.”
“Nitapunguzaje na wakati hapokei simu yangu.”
“Labda yupo mbali na simu yake.”
“Sio rahisi.”

“Sasa unahisi atakuwa wapi?”
“Embu ngoja nijaribu kumpigia tena,” alisema Evelyne kisha akaamua kuipiga simu ya Richard kwa mara nyingine tena, safari hii simu ilikuwa haipatikani, akahisi labda mtandao ulikuwa unasumbua hivyo akarudia kupiga tena huku akijaribu kuzunguka huku na kule mule chumbani lakini majibu yalikuwa ni yaleyale.
“Hapatikani,” alisema kwa sauti ya unyonge.

“Hapatikani?” aliuliza Happy kwa mshangao.
“Ndiyo,” alijibu Evelyne kisha akakaa chini, nguvu zilikuwa zimeanza kumuishia kwa wakati huo.
“Mbona alikuwa anapatikana lakini?” “Mimi sijui ni nini kilichomkuta Richard wangu jamani.”

“Embu ngoja nijaribu na mimi kumpigia,” alisema Happy kisha akaichukua simu yake halafu akampigia Richard, hakukuwa na jibu lingine alilojibiwa kwa wakati huo zaidi ya kuisikia sauti ya msichana ikimuambia “ Mtumiaji wa simu unayempigia kwa sasa hapatikani, tafadhili jaribu tena baadae.
*
*
Je, nini kitaendelea?
Usikose toleo lijalo.
 
Sehemu ya 04.

Monalisa ndiye msichana ambaye alionekana kumpenda zaidi Richard kuliko wasichana wengine pale chuoni, licha ya Richard kumkatalia ombi lake la kuwa wapenzi lakini bado hakutaka kukubali hilo, aliamini kwa vyovyote iwezekanavyo ni lazima mvulana huyo angefanikiwa kummiliki.

Kuna kipindi kichwani mwake yalimjia mawazo ya jinsi ambavyo alivyofanikiwa kumpata Richard kisha wakawa wanayafurahia mapenzi yao katika ufukwe wa bahari ya Hindi, alizidi kulifurahia hilo katika moyo wake maradufu na hata pale mawazo hayo yalipomtoka kichwani alionekana kukasirika mno, hakutaka kuamini kama kweli alikuwa akiwaza kwa wakati huo.

Moyo wa mapenzi ukazidi kumuendesha vilivyo, alikuwa amezama katika dimbwi la mapenzi ya Richard mvulana ambaye na yeye moyo wake ulikuwa umekufa umeoza kimapenzi na msichana mwingine chuoni hapo.

“Kwanini Richard anashindwa kunikubalia hivi inamaana sina uzuri wa kumvutia au?” aliuliza Monalisa huku akiwatizama wale mashoga zake watatu walipokuwa hostel.

“Sio kwamba humvutii isipokuwa Richard ameshatekwa na Evelyne,” alijibu msichana mmoja huku akionekana kuwa bize na simu yake.

“Sitaki kumsikia huyo mpumbavu tena nitamkomesha mwanaharamu yule,” alisema Monalisa huku akionekana kuchukia mno baada ya kulisikia jina la Evelyne likitajwa na rafiki yake huyo aliyejukana kwa jina la Penina.

“Shoga yangu mimi nimeshachoka kumfuatilia huyo Richard kwani hakuna wavulana wengine hapa chuo kwani yeye nani?” aliuliza Mary.

“Jamani Richard ni Handsome mimi mwenyewe bado sijaona mvulana anayemfikia kwa uzuri hapa chuoni,” alisema Adela msichana aliyeikamilisha hesabu yao pale ndani, walikuwa wanne.
“Lakini lazima nitampata tu,” alisema Monalisa huku akijiapiza kumpata kwa vyovyote iwezekanavyo.

“Utatumia njia gani?” aliuliza Mary huku akimtazama Monalisa.
“Nitajua tu lakini lazima nimpate, nitahakikisha Richard anakuwa mali yangu,” alisema Monalisa.
Nimeishia hapa.
Ngoja niweke alama.

The Hate U Give, Little Infants F's Everyone.
 
Sehemu ya 18.

“Mungu wangu sijui Monalisa akipokea atamuambia nini?” alijiuliza swali hili katika mawazo yake.
Hakufahamu ni nini alichokuwa amedhamiria kukifanya Monalisa, alibaki katika hali ya sintofahamu huku asijue nini alitakiwa kukifanya kwa wakati huo.

Wakati akiendelea kuwaza mambo yote hayo lilimjia wazo kichwani, lilikuwa ni wazo la kumtafuta Evelyne kwa njia yoyote ili aweze kuzungumza naye, alipokumbuka umbali uliyokuwepo kati ya Mikocheni na Kigamboni alighairi kuchukua maamuzi hayo.

Alikumbuka kuwa Evelyne alikuwa akijulikana na Mama yake na alikuwa akipenda kuwasiliana naye mara kwa mara, hakutaka siku hiyo iweze kupita bila ya kuzungumza naye. Alichoamua kukifanya ni kwenda kumuomba Mama yake simu kisha akampigia, simu ya Evelyne ilikuwa ikiita bila ya kupokelewa. “Mbona hapokei simu ni nini kimemkuta?” alijiuliza Richard baada ya kumpigia simu Evelyne zaidi ya mara tatu bila kupokelewa.

Hakutaka kukata tamaa, aliendelea kupiga huku akitegemea kuna muda Evelyne angeweza kuipokea simu hiyo lakini tukio hilo halikuweza kutokea. ****
“Punguza wasiwasi Richard yuko salama.”
“Nitapunguzaje na wakati hapokei simu yangu.”
“Labda yupo mbali na simu yake.”
“Sio rahisi.”

“Sasa unahisi atakuwa wapi?”
“Embu ngoja nijaribu kumpigia tena,” alisema Evelyne kisha akaamua kuipiga simu ya Richard kwa mara nyingine tena, safari hii simu ilikuwa haipatikani, akahisi labda mtandao ulikuwa unasumbua hivyo akarudia kupiga tena huku akijaribu kuzunguka huku na kule mule chumbani lakini majibu yalikuwa ni yaleyale.
“Hapatikani,” alisema kwa sauti ya unyonge.

“Hapatikani?” aliuliza Happy kwa mshangao.
“Ndiyo,” alijibu Evelyne kisha akakaa chini, nguvu zilikuwa zimeanza kumuishia kwa wakati huo.
“Mbona alikuwa anapatikana lakini?” “Mimi sijui ni nini kilichomkuta Richard wangu jamani.”

“Embu ngoja nijaribu na mimi kumpigia,” alisema Happy kisha akaichukua simu yake halafu akampigia Richard, hakukuwa na jibu lingine alilojibiwa kwa wakati huo zaidi ya kuisikia sauti ya msichana ikimuambia “ Mtumiaji wa simu unayempigia kwa sasa hapatikani, tafadhili jaribu tena baadae.
*
*
Je, nini kitaendelea?
Usikose toleo lijalo.
Ukiweka muendelezo wa hii love story, naomba unitag tafadhar.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom