Million dollars
JF-Expert Member
- Jul 20, 2016
- 1,508
- 2,070
Shunie Unafeli
Sent from my iPhone using JamiiForums
Sent from my iPhone using JamiiForums
thanks mamy
[emoji8] [emoji8] [emoji8]Sehemu ya 21.
Adela ndiye alikuwa msichana pekee ambaye alifahamu kila kitu kilichokuwa kikiendelea kuhusiana na picha ambazo alikuwa amezipiga Monalisa na Richard.
Monalisa aliamua kumuonyesha Adela picha hizo huku akiwaficha Penina na Mary, hakutaka wafahamu lolote zaidi ya uhusiano wake na Richard tu.
“Kwanini nisiwaambie?” aliuliza Adela huku akionekana kushangazwa mno.
“Sitaki uwaambie lolote kuhusiana na hizi picha nilizozipiga,”alijibu Monalisa huku akimtazama kwa macho ya msisitizo Adela.
“Kuna kitu gani kinachoendelea kati yenu?”
“Hakuna.”
“Sasa kwanini hutaki niwaambie?”
“Nimeamua tu kwani picha ni zangu au za kwao?” “Una uhakika hakuna tatizo?”
“Ndiyo hakuna,” alijibu Monalisa.
Waliendelea kuzungumza wakati huo Penina na Mary hawakuwepo hostel, mpaka kufikia muda huo Adela hakujua ni nini kilichokuwa kikiendelea mpaka Monalisa aamue kuwaficha Penina na Mary na wakati wote walikuwa ni marafiki na kila jambo ambalo alikuwa akilifanya ilikuwa ni lazima awaambie, hilo lilizidi kumchanganya kichwa chake. ****
Siku iliyofuata ndiyo ilikuwa ile siku ambayo Evelyne alishindwa kuendelea kubaki darasani baada ya kumuona Richard akiwa ameingia, alishindwa kuyavumilia maumivu ambayo moyo wake tayari ulikuwa umshayapata, alimchukia mno Richard na hakutaka kuendelea kumtazama katika mboni za macho yake.
Alichoamua kukifanya ni kuondoka kabisa eneo hilo la chuo huku akiamini kwa kufanya hivyo angeweza kuyapooza maumivu na machungu ambayo moyo wake ulikuwa ukipitia..
Rafiki yake Happy hakuwa anafahamu lolote lile lililokuwa limetokea, alibaki katika wakati mgumu baada ya Evelyne kushindwa kumuelezea ni nini kilichokuwa kimetokea na kwa wakati huo aliamua kuondoka zake.
Alitamani sana kufahamu ni nini kilichokuwa kimetokea na mtu pekee ambaye aliamini angeweza kumueleza ukweli wa mambo yote hayo alikuwa ni Richard lakini na yeye alishindwa kumueleza ukweli, alibaki akiwa haelewi ni nini kilichokuwa kimetokea baada ya kumuona mpenzi wake akiwa ameondoka.
*
*
Je, nini kitaendelea?