Nisamehe Mpenzi

Nisamehe Mpenzi

Hahhaha kwani mkuu umelazimishwa mpaka uimalize
Bibie nakushauri uwe unatupia EPISODE moja baada nusu saa unatupia nyingine

Ila kwa mtindo huu wengi watakua wanaishia njiani.

ni ushauri tu.
 
Hii story inafundisha sana! Sisi wanaume kukataa Free Pussy ni kazi ngumu saana


Sent from my iPhone using JamiiForums
Kabisa mkuu. Hapo ndo huwa tunapofeli. Binafsi always huwa namshkuru sana Mungu kwa kunifanya nsiwe mwanaume wa kutawaliwa na mihemko, especially ya abdallah kichwa wazi, otherwise yaliyomkuta Richard yangekua yashanikuta zamani sana. Kina Monalisa vivuruge wako wengi sana

the Legend☆
 
Bibie nakushauri uwe unatupia EPISODE moja baada nusu saa unatupia nyingine

Ila kwa mtindo huu wengi watakua wanaishia njiani.

ni ushauri tu.
Unayeishia njiani ni ww mkuu kwa anayependa story hawezi kuongea hivyo wengine wanalalamika ni fupi we jisomee unavyoweza usiwasemee wengine
 
Kabisa mkuu. Hapo ndo huwa tunapofeli. Binafsi always huwa namshkuru sana Mungu kwa kunifanya nsiwe mwanaume wa kutawaliwa na mihemko, especially ya abdallah kichwa wazi, otherwise yaliyomkuta Richard yangekua yashanikuta zamani sana. Kina Monalisa vivuruge wako wengi sana

the Legend☆
Sema kweli jamani
 
Sehemu ya 45.

Mwezi wa kwanza ulikatika huku wanachuo wakiendelea kujiandaa na mitihani yao, mwezi wa pili nao ukakatika, hatimaye wiki ya kwanza ya mitihani ikaanza. Wanachuo wakaanza kuifanya mitihani yao ambayo iliwachukua takribani mwezi mzima kuweza kuimaliza.

Ilikuwa ni furaha kwa kila mwanachuo kuweza kumaliza salama mitihani hiyo, kila mwanachuo alimshukuru Mwenyezi Mungu kutokana na hatua waliyokuwa wameifikia. Kama kawaida pia hawakuacha kupongezana, sherehe mbalimbali ziliandaliwa kama ishara ya kupongezana kwa kufanikiwa kumaliza masomo yao salama.

Wiki moja baadaye Richard aliamua kumueleza ukweli Monalisa juu ya taarifa alizozisikia kuhusu ujauzito huo kuwa haukuwa ni wake, alipokuwa akimueleza hayo macho yake yalikuwa yakitoa machozi. Alishindwa kuyavumilia maumivu ambayo moyo wake ulikuwa ukipitia.

Monalisa alibaki kinywa wazi baada ya kusikia maneno hayo kutoka kwa Richard, hakutaka kuamini kama alifahamu kila kitu kilichokuwa kikiendelea, siri ambayo aliamini ilikuwa ni vigumu kufichuka kwa wakati huo ilikuwa tayari imeshafichuka.

Swali ambalo alianza kujiuliza ni rafiki yake gani ambaye alimgeuka na kumueleza Richard kila kitu, hakupata jibu hata alipoamua kumuuliza Richard hakuwa tayari kumuweka wazi. Hilo lilizidi kumshangaza sana, alichanganyikiwa, hakutaka kuamini kama alikuwa ameshagundulika.

“Sidhani kama nitakuwa ninanafasi ya kuendelea kuwa na wewe, naomba huu ndiyo uwe mwisho wetu, umeniharibia mahusiano yangu vya kutosha, please naomba uniache, niache Mona na maisha yangu,” alisema Richard kwa sauti ya uchungu, machozi yalikuwa yakimbubujika.

“Hapana Richard usiseme hivyo, nakupenda, nakupenda tena sana na ndiyo maana nimefanya yote haya kwasababu yako, sikutaka nikupoteze kirahisi kiasi hiki. Richard ni kweli huu ujauzito sio wako lakini naomba unisamehe bado naamini nina nafasi ya kufanya kitu kwa ajili yako,” alisema Monalisa.
 
Sehemu ya 46.

Kila alipokuwa akimtazama Richard alivyokuwa akilia mbele yake alijisikia vibaya mno, alimkosea sana, alimfanyia kila aina ya uhuni, alimchanganya na wanaume wengi sana ambao alikuwa akitembea nao kwa ajili ya kuwachuna, hakuwa na mapenzi ya dhati, huo ndiyo ulikuwa ukweli lakini alipogundua kuwa siri hiyo ilifichuka alizidi kujisikia vibaya.

Hakuwa na kitu kingine cha kufanya zaidi ya kumuomba msamaha na kumuahidi kufanya kitu kwa ajili yake, licha ya mambo yote aliyokuwa ambayo alikuwa amemfanyia lakini hakutaka kuona akimpoteza mwanaume huyo, aliendelea kuushikilia msimamo wa kumpenda zaidi kila kitu katika dunia hii.

Richard alipomuona Monalisa mbele yake pamoja na maneno ambayo alikuwa akiyazungumza yalizidi kuweka katika wakati wa hasira, alimuona kuwa adui mkubwa sana wa maisha yake, alimchukia mno.

“Sijui nikuambie nini mpenzi?”
“Usiniambie kitu, sitaki kusikia lolote kutoka kwako ni bora uendelee kukaa kimya.”

“Hapana Richard usiseme hivyo utazidi kuumiza moyo wangu.”
“Mona kwa uliyonifanyia inatosha, nashindwa kuvumilia, moyo wangu haukuhitaji.”

“Richard hunipendi?”
“Ndiyo sikupendi Mona,” alijibu Richard.
Monalisa alizidi kuchanganyikiwa baada ya kuyasikia majibu hayo, hakutaka kukubaliana na ukweli wa kile kilichokuwa kimetokea.

Alijitahidi sana kumbembeleza, muda mwingine alikuwa akimlilia lakini yote hayo bado hayakuweza kuwa sababu iliyomfanya Richard akubali kuendelea kuwa naye.
 
Sehemu ya 47.

Alimpenda sana mwanaume huyo, alitamani kumuona kila wakati akiwa naye. Baada ya kuona Richard ameshindwa kumsamehe uamuzi aliyoamua kuuchukua ni kuutoa, aliamini ujauzito huo ndiyo ulikuwa sababu ya yeye kuchukiwa na Richard. Hakutaka kupoteza muda haraka alipanga mipango ya kuutoa ujauzito huo na hatimaye aliweza kufanikiwa kuutoa salama.

Furaha ilizidi kumtawala, aliamini huo ndiyo ulikuwa muda wake muafaka wa kuweza kumuomba msamaha Richard kisha akaweza kumsamehe, hilo lilikuwa ni jambo gumu mno kwa Richard kuweza kutokea licha ya msichana huyo kuwa ni mzuri. ****

Baada ya kupita miezi kadhaa hatimaye Evelyne pamoja na Happy walifanikiwa kupata kazi katika moja ya kampuni iliyokuwa ikiwalipa wazuri.

Richard na yeye kutokana na utajiri aliyokuwanao baba yake aliweza kuachiwa kampuni aweze kuiongoza. Kwa upande wa Monalisa pamoja na marafiki zake na wao pia walifanikiwa kupata kazi katika moja ya kampuni hapa mjini. ****

Fredrick aliamua kujitambulisha kwa wazazi wake Evelyne pamoja na kumtambulisha mpenzi wake, hakutaka kufanya utani hata mara moja, baada ya kufuata taratibu zote aliamua kumvalisha pete ya uchumba na baadae kufunga naye ndoa kabisa.

Evelyne hakuamini kama aliweza kupata mwanaume ambaye alimpenda na kumthamini kiasi kile, alizidi kumpenda sana mwanaume huyo ambaye kila kitu alichokuwa akikifanya hapa duniani alikifanya kwa sababu ya mapenzi yake.

Taarifa hizo za Evelyne kuolewa na Fredrick ziliweza kumfikia Richard, alipoambiwa kwa mara ya kwanza mapigo ya moyo wake yalimuenda mbio, hakutaka kuamini, alihisi kutaniwa.

Alibaki katika simanzi baada ya kuthibitisha ukweli wa taarifa hizo, zilizidi kumuumiza mno moyo wake.

Kila alipomkumbuka Evelyne wakati alipokuwa ofisini machozi yalikuwa yakimbubujika muda wote, taswira ya msichana huyo ikajijenga upya akilini mwake, alishindwa kufanya kazi kabisa siku hiyo.
 
Sehemu ya 48.

Hisia za mapenzi bado ziliendelea kumuumiza, kichwa chake kilikataa kabisa kumsahau Evelyne.
Muonekano wake mzuri uliendelea kuwatesa wasichana waliyokuwa katika kampuni yake hiyo, wote walimtetemekea.

Kama kulikuwa kuna uwezekano wa kutokea walau siku moja kila moyo wa msichana katika kampuni hiyo kusema chochote, hakika sauti za maombi ya kumuhitaji Richard ndiyo zingesikika ndani ya ofisi nzima, hakukuwa na msichana ambaye alipomuona Richard moyo wake haukuacha kushtuka, ulimuhitaji mno mwanaume huyo.

Kama kawaida maneno na mabifu ya chinichini hayakuacha kuwepo kwa wasichana hao, walijikuta wakiingia katika ugomvi na chuki kila wakati, sababu ikiwa ni Richard.

Msichana aliyepata bahati ya kutolewa lunch na Richard aliitumia nafasi hiyo katika kuwaumiza roho wafanyakazi wenzake, hilo lilizidi kutengeneza chuki kati yao.

Licha ya kuwepo na mambo yote hayo ofisini lakini hakukuwa na msichana aliyebahatika kuumiliki moyo wa Richard, kila siku waliishia kumpelekea zawadi na mialiko mingi ambayo haikuweza kuzaa matunda yoyote.

"Ni Mzuri ndiyo tena anavutia mno ila sijakuelewa kwani nini unachokitaka hasa kwa Boss?" Aliuliza msichana mmoja.
"Sijui niseme nini, sijui nianzie wapi kukuelezea ila kwa kifupi nampenda sana, natamani siku moja ajue ni jinsi gani moyo wangu unavyomuhitaji," alijibu msichana mwingine ambaye alizungumza kwa hisia.

Kitendo cha wasichana kuamini siku moja kufanikiwa kulimiliki penzi la Richard kilibaki kuwa ndoto, ulikuwa ni ukweli uliyowaumiza mno.

Maisha ya Richard yalikuwa mazuri kwa upande wake lakini upande mwingine alijiona kukosa bahati, licha ya kuwa alifanikiwa kununua nyumba maeneo ya Mbezi, kumiliki pesa, kutembelea gari la kifahari lakini tukio la kumpoteza Evelyne kilimuacha na pigo kubwa mno.
 
Sehemu ya 49.

Alifahamu kwa wakati huo msichana huyo alikuwa ni mke wa mtu lakini bado alijipa matumaini ya kuwa naye siku moja, moyoni hakutaka kukubaliana na ukweli, alijiapiza kufanya lolote ili aweze kulirudisha penzi lake.

"Nitatumia kila nilichonacho, kama ni pesa, nguvu hata kwa kumwaga damu ilimradi urudi kwangu, sikubali na siwezi kuvumilia maumivu na mateso haya ninayoyapata katika moyo wangu," alijisemea Richard alipokuwa nyumbani kwake, wakati huo alikuwa akiitazama picha ya Evelyne kwenye simu. Ilizidi kumuumiza mno.

Alijitahidi kuvumilia, kuficha kwa kipindi kirefu lakini kuna muda uzalendo ulimshinda. Akatamani kuwaeleza wazazi wake ukweli kwani katika kipindi hicho tayari walishaanza kumuuliza kuhusu mipango yake ya kufunga ndoa na Evelyne.

Alihisi kuchanganyikiwa kila alipokuwa akiulizwa kuhusu Evelyne, wazazi wake hawakufahamu kilichokuwa kimetokea hivyo walionekana kumuhitaji sana msichana huyo.

Baada ya kuona wazazi wake wamezidi kumsumbua sana kuhusu suala hilo la kumuoa Evelyne ilibidi awaeleze ukweli wa kilichotokea kati yake na msichana huyo ambaye kwa wakati huo alikuwa ni mke wa mtu, zilikuwa ni taarifa zilizowashtua wazazi wake, hawakutaka kuamini walichokuwa wakiambiwa.

"Umefanya ujinga gani mwanangu?" Aliuliza Mama yake, hakuishia kuuliza swali tu isipokuwa alianza kumlaumu kwa kosa alilokuwa amelifanya hata kwa upande wa baba yake Mzee Gombanila na yeye alimlaumu pia.

Richard alipoona lawama zimezidi kuwa nyingi aliamua kuondoka nyumbani kwao, alipokuwa barabarani kichwa chake bado kilitawaliwa na mawazo mengi sana, hakujua ni kwa jinsi gani angeweza kuyatatua. Kuna kipindi alijikuta akilipa faini kwa kosa la uzembe wake mwenyewe barabarani.

Licha ya kuwa na maisha mazuri, kutamaniwa na wasichana lukuki lakini alipokumbuka yaliyomtokea katika maisha ya kimahusiano hakutaka kumkabidhi msichana mwingine moyo wake, aliogopa mno.
 
Sehemu ya 48.

Hisia za mapenzi bado ziliendelea kumuumiza, kichwa chake kilikataa kabisa kumsahau Evelyne.
Muonekano wake mzuri uliendelea kuwatesa wasichana waliyokuwa katika kampuni yake hiyo, wote walimtetemekea.

Kama kulikuwa kuna uwezekano wa kutokea walau siku moja kila moyo wa msichana katika kampuni hiyo kusema chochote, hakika sauti za maombi ya kumuhitaji Richard ndiyo zingesikika ndani ya ofisi nzima, hakukuwa na msichana ambaye alipomuona Richard moyo wake haukuacha kushtuka, ulimuhitaji mno mwanaume huyo.

Kama kawaida maneno na mabifu ya chinichini hayakuacha kuwepo kwa wasichana hao, walijikuta wakiingia katika ugomvi na chuki kila wakati, sababu ikiwa ni Richard.

Msichana aliyepata bahati ya kutolewa lunch na Richard aliitumia nafasi hiyo katika kuwaumiza roho wafanyakazi wenzake, hilo lilizidi kutengeneza chuki kati yao.

Licha ya kuwepo na mambo yote hayo ofisini lakini hakukuwa na msichana aliyebahatika kuumiliki moyo wa Richard, kila siku waliishia kumpelekea zawadi na mialiko mingi ambayo haikuweza kuzaa matunda yoyote.

"Ni Mzuri ndiyo tena anavutia mno ila sijakuelewa kwani nini unachokitaka hasa kwa Boss?" Aliuliza msichana mmoja.
"Sijui niseme nini, sijui nianzie wapi kukuelezea ila kwa kifupi nampenda sana, natamani siku moja ajue ni jinsi gani moyo wangu unavyomuhitaji," alijibu msichana mwingine ambaye alizungumza kwa hisia.

Kitendo cha wasichana kuamini siku moja kufanikiwa kulimiliki penzi la Richard kilibaki kuwa ndoto, ulikuwa ni ukweli uliyowaumiza mno.

Maisha ya Richard yalikuwa mazuri kwa upande wake lakini upande mwingine alijiona kukosa bahati, licha ya kuwa alifanikiwa kununua nyumba maeneo ya Mbezi, kumiliki pesa, kutembelea gari la kifahari lakini tukio la kumpoteza Evelyne kilimuacha na pigo kubwa mno.

huwezi kunikusanyia zote kwenye PDF Moja
 
Sehemu ya 50.

Fredrick na Evelyne walizidi kuyafurahia maisha ya ndoa yao, kila wakati furaha iliendelea kushika hatamu, baada ya kupita miezi miwili, siku moja majira ya jioni Fredrick alipokuwa akirudi nyumbani kwake Tabata, alipata ajali mbaya sana maeneo ya Ubungo mataa, gari yake ndogo aina ya Toyota Harrier lenye rangi nyeusi liligongana uso kwa uso na lori.

Ilikuwa ni ajali mbaya sana ambayo kila mtu aliyeishuhudia hakutaka kuamini kama angeweza kupona mtu.

Mwili wa Fredrick haukuweza kutambuliwa kwa haraka kutokana na damu zilizokuwa zimetapakaa kila sehemu, wasamaria waliyojitokeza wakamsaidia kumtoa ndani ya gari hiyo iliyokuwa imebondekabondeka na kupoteza umbo lake la kawaida, walijitahidi kadri ya uwezo wao na hatimaye walifanikiwa kumtoa lakini alikuwa amepoteza fahamu.

Baada ya kupita dakika kadhaa polisi waliweza kufika eneo la tukio, kama ilivyokuwa kawaida yao walianza kuwatawanyisha watu, walihitaji kuona usalama wa eneo hilo ukiendelea kuwepo.

Wakati polisi wakiendelea kufanya kazi yao ghafla! Ving'ora vya gari la kubebea wagonjwa (Ambulance) viliweza kusikika na ndani ya dakika chache liliweza kufika eneo la ajali kisha wakamchukua Fredrick ambaye alikuwa katika hali mbaya sana.

Walipomfikisha hospitali taratibu za kuyaokoa maisha yake zilianza kufanyika, wakati huo Evelyne alishapigiwa simu na kwa wakati huo alikuwa njiani akielekea katika hospitali ya Muhimbili, alipofika alionekana kuchanganyikiwa, hakuamini kama Fredrick alikuwa amepata ajali na kwa wakati huo alikuwa katika chumba cha upasuaji akiendelea kupatiwa matibabu.
*
*
Je, nini kitaendelea
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom