Aya sista wala usijaliJamani vumilieni tu ninapozitoa mwenyewe anatuma hivyohivyo
Usijari mama.Jamani vumilieni tu ninapozitoa mwenyewe anatuma hivyohivyo
Asante Prisoner tubarikiwe sote Ameen [emoji120][emoji120][emoji120][emoji120]Usijari mama.
Hata hivyo, naomba niseme asante sana kwa moyo uliokuwa nao. Ubarikiwe Shunie
Sent using Jamii Forums mobile app
Amen.Asante Prisoner tubarikiwe sote Ameen [emoji120][emoji120][emoji120][emoji120]
Shunie unantengaa jamani, sikujua kama umeiendelezaSehemu ya 41.
“Atokee wapi wakati tayari nipo na wewe.”
“Fredrick niambie ukweli usinidanganye.”
“Niamini upo peke yako katika moyo wangu,” alisema Fredrick.
Kila maneno aliyokuwa akiyasema Fredrick yalizidi kumteka Evelyne, alijikuta akikosa la kusema, alibaki akimtazama mwanaume huyo ambaye alitofautiana mambo mengi sana na Richard. ****
Monalisa hakuishia kumpenda Richard pale chuoni, kila mwanaume mwenye pesa na muonekano mzuri ambaye alijitokeza mbele yake alikuwa akianzisha mahusiano naye na hiyo ndiyo ilikuwa tabia yake. Hakukuwa na watu waliyokuwa wakifahamu hilo zaidi ya marafiki zake Penina, Adela pamoja na Mary.
Tabia yake hiyo ya kuwachanganya wanaume ndiyo iliyosababisha mpaka akapata mimba ambayo hakuwa anamfahamu baba halisi, hakuwa na njia nyingine ya kufanya zaidi ya msingizia mimba hiyo Richard mwanaume ambaye tayari alikuwa ameshafanya naye mapenzi.
Richard baada ya kupewa taarifa hizo za ujauzito hakutaka kukataa, alikubali huku akiamini ulikuwa ni ujauzito wake.
Hakutaka kuamini kama kweli alikuwa amempa ujauzito msichana huyo ambaye moyo wake haukumpenda, alizidi kujilaumu mno baada ya kukumbuka kuwa msichana huyo ndiye alikuwa sababu ya kumgombanisha na mpenzi wake na kwa wakati huo tayari alikuwa ameanzisha mahusiano na mwanaume mwingine.
Tukio hilo bado liliendelea kumuumiza sana moyo wake, hakutaka kuamini kile kilichokuwa kimetokea, alihisi alikuwa katika ndoto lakini haikuwa hivyo, kila kitu kilichokuwa kimetokea ndiyo ulikuwa ukweli halisi.
Alitamani kuwaeleza ukweli wazazi wake kwa kile kilichokuwa kimetokea kuhusu Monalisa mpaka kufikia hatua ya kumpa ujauzito lakini alipokumbuka maswali ambayo angeweza kuulizwa na Mama yake kuhusu Evelyne alighairi kufanya hivyo.
Alipokuwa akimuona Monalisa chuoni moyo wake ulizidi kumchukia, alimuona kuwa msichana aliyeyaharibu mahusiano yake na mpenzi wake, kitu kibaya zaidi alikuwa ameubeba ujauzito wake na hilo ndilo lilizidi kumchanganya akili yake bila kujua kuwa alisingiziwa ujauzito huo haukuwa ni wake.
Daah, sijui nini kitatokea. Richard alibugi sana kukubali kutembea na Monalisa, angebaki na msimamo wake yote yasingetokea. Asante ShunieSehemu ya 44.
“Jamaa karuka mkoja kakanyaga mavi,” alisema mwanachuo mmoja.
“Hili ndilo tatizo letu sisi wanaume hatuwezi kutulia na mwanaume mmoja,” alisema mwanachuo mwingine.
Hakukuwa na kitu kilichokuwa kikiwakasirisha watu kama kusikia kuwa msichana huyo aliyelisambaratisha penzi la Evelyne alikuwa amebeba ujauzito.
Baada ya kuzisikia taarifa hizo Happy na yeye alianza kumchukia Richard, hakutaka kuzungumza naye, aliamua kuwa upande wa rafiki yake na kuanzia siku hiyo alimuunga mkono kwa uamuzi aliyokuwa ameuchukua wa kuanzisha mahusiano na Fredrick.
Alifahamu ni maumivu kiasi gani aliyokuwa ameyapata hivyo kwa uamuzi aliyokuwa ameuchukua aliamini uliweza kumpunguzia maumivu hayo.
“Yaani pamoja na uchafu aliyoufanya ameona haitoshi ameamua bora ampe ujauzito kabisa,” alisema Happy.
“Wanaume ndivyo walivyo hawaridhiki,” alisema Evelyne.
“Nimemchukia sana.”
“Sio wewe tu hata mimi sitaki kuzungumza naye,” alisema Evelyne.
Mpaka kufikia hapo hakukuwa na mtu aliyefahamu ni nini kilichokuwa kikiendelea, wanachuo walimchukia sana Richard kwa ujinga aliyokuwa ameufanya wa kumsaliti mpenzi wake.
Ilikuwa imebakia miezi miwili ili waweze kufanya mitihani ya kumaliza degree yao, kila mwanachuo alionekana kuwa bize na kusoma kwa ajili ya kujiandaa na mitihani hiyo.
Kwa upande wa Richard hali ilikuwa tofauti, alijitahidi kujisomea lakini badala ya kuelewa alichokuwa akikisoma ndiyo kwanza mawazo yake yalikuwa yakitafakari ukweli aliyoelezwa na Adela kuhusu ujauzito wa Monalisa.
Alihisi kuchanganyikiwa kila alipokuwa akiyakumbuka maneno ya Adela, alitumia pesa nyingi mno kwa ajili ya Monalisa, hakutaka kuamini kama msichana huyo aliyedai kuwa anaujauzito wake hakuwa muaminifu, alishiriki mapenzi na wanaume wengi na mpaka kufikia wakati huo ujauzito haukuwa ni wake.
Hilo liliendelea kumuumiza sana moyo wake, alijiona kuwa mwanaume mwenye mikosi kila kukicha.
*
*
Je, nini kitaendelea?
Daah, sijui nini kitatokea. Richard alibugi sana kukubali kutembea na Monalisa, angebaki na msimamo wake yote yasingetokea. Asante Shunie
the Legend☆