Nini maana ya Professor na Doctor(PhD)?

Nini maana ya Professor na Doctor(PhD)?

professor niliwahi kusikia ni yule ambae amefanya utafiti UNIQUE sana juu ya jambo fulani, ambalo halikuwahi kufanywa hapo nyuma sana

Na amevumbua jambo ambalo lililkuwa likisumbua sana watu kwa kulifanyia utafiti wa kina

mi najua kidoogo hivyo kuhusu Professor

Hapana. Hakuna kipya Dunia mkuu mengi yanarudiwa rudiwa tu.
Ukishafika hatua ya dhahada ya PhD kinachoendelea kwako ni kuwa mtunzi wa vijarida ukichambua mambo critical zaidi na pia kama ukawa mwandishi wa vitabu alafu board ya ma professor inavipitia sio mara moja nadhani kuna muda furani hivi then unatunukiwa u professor.
Kumbuka PhD inasomewa
Ila professor unatunukiwa
 
Doctor utamkuta anapiga watu sindano kwa zahanati.
Professor ni kame vile maji marefu yaani mganga wa jadi.
Kwa ujumla prof na doctor wote ni waganga sema mmoja anatibu vidonda mwingine anatoa majini
Umewaweza
 
Nimekuelewa, but kinachonitatiza nimetolea mfano Obama ana PHD lakini sikuwahi kusikia au kusoma akiitwa Doctor.

Utofauti upo wapi?
Ni ulimbukeni wetu waAfrika, weupe hawana hii tabia wanatumia tu majina yao..sisi PhD holder usipoanza na dr. anaweza kukumaindi as if ndo jina lake
 
point of interruption unaweza kuwa na masters ukiwa huna PhD na bado ukawa proffessor.
PhD ndio mtaaluma kuliko proffessor.Proffessor ni kufundisha chuo kikuu muda flani na ukaandika research paper nyingi.
Kuwa na PhD sio lazima ufundishe.
Kuna udr wa heshima ila hakuna uproffessor wa heshima lazima ushike chaki
Hii siyo kwa Africa, maybe United States
 
Habari zenu wadau wa JF.

Hivi Ni vigezo gani hutumika mpaka mtu aitwe Proffesor au Doctor.Doctor ninayemzungumzia ni yule mwenye PHD sio hospitali.

Nimeuliza hivi kwa sababu, Tanzania mtu yeyote mwenye shahada ya uzamivu huitwa Doctor(Dr).

Lakini nimesoma biography ya Barrack Obama na Hillary Clinton na nikagundua wamesoma mpaka level ya PHD lakini sijawahi kusikia wanaitwa Doctor tofauti na hapa kwetu.

Mfano rais wetu John Pombe Magufuli ana PHD anaitwa Doctor.Obama pia ana PHD na aliwahi kufundisha Chuo kikuu ila sikuwahi kusikia akiitwa Doctor au Proffesor.

Hii imekaaje ndugu wa JF naomba kuelimishwa.

Waswahili wanapenda sifa,,naweza kusema "kipofu kaona" ndio cc waswahili.
 
Hahaha kwahiyo uprofessor ni tafiti siyo PhD au nakuelewa ndivyo sivyo?! Au ndiyo doctorate degree?! Hivyo PhD holder ni sawa kujiita professor au Doctor?!
PhD ni kigezo no1 then hivyo vya publications n.k hufuata, fuatilia replies zangu huko juu nilimweleza mleta mada tofauti zake.
 
Ila kwa Tanzania ni ulimbukeni wa elimu. Mfano mzuri angalia hata kwenye vyuo vyetu hususani Udsm, wanajiona ni special sana. Mwengine ukimsalimia pasipo kumuita doctor au Prof. haitiki.
Hizo ni tabia binafsi za mtu, hazihusiani na elimu yake. Watu wa hivi kila mahala wapo.
 
Ninachojua Obama hakuwa na PhD, na pia kuna kipindi aliitwa profesa akiwa mwalimu chuo kikuu cha Chicago. Akiwa nje ya hapo hakujiita/ hakuitwa profesa.
 
Swali niliokuwa najiuliza mfano Obama alikuwa na PHD lakini sikuwahi kuona au kusikia jina lake likianzia Dr kama ilivyo kwa Kikwete,Magufuli etc, ambao majina yao yanaanzaga na Dr
Angel Markel waziri mkuu wa ujerumani ana PhD na Ni profesa Lakini hupenda tu kuitwa Agel Markel huku kwetu nchi za kiafrika mbwembwe nyingi.
 
Uzi huu unafurahisha sana. Kiufupi kama walivyosema wengine PhD unasomea kwa wengi na kwa wachache ziko zile za heshima (wanasiasa au watu waliofanya jambo fulani na chuo kuwa tambua). huu uPhD kawaida ukisha pewa wewe ni Dokta popote pale ulipo hivyo haijalishi unafanya nini na wengi huitwa kwa sifa hiyo labda chuo kilichokutunuku kikunyang'anye hiyo degree.
Professor ni ngazi inayo ashiria umahiri katika jambo fulani na hutolewa na vyuo vikuu kwa walimu wao waliotimiza sifa fulani (machapisho, ugunduzi) lakini kuna nchi kama Poland nasikia unaweza kupewa uprofessor nje ya chuo kwa mfano watafiti na hii inamuwezesha kusimamia wanafunzi wa utafiti. Hapa juzi juzi wengi tulishangaa Kikwete kupewa Uprofessor na chuo cha kilimo huko china hivyo hiyo ni aina nyingine ya uprofessor huko china.
Tunajiitaje-hiyo hutegemea utamaduni wa mahali fulani. Kuna ambao huwa rasmi kabisa na inakubalika kuwa kwa heshima yake lazima utangulize Dr. au Prof. na huko ujerumani wapo hata Prof. Dr. Dr. Fulani. Na wengine kama USA wanapotezea lakini wao Uprofessor wanautumia ukiwa unafanya kazi chuoni na ukitoka unakoma. Hivyo Condoleeza Rice ingawa alikuwa Professor alipoingia kwenye siasa akabaki kuwa Dr. Rice. Wengi wakiwa vyuo pia huitwa kwa majina yao au Dr so and so, lakini kwenye official communication mara nyingi unatumia full title.
Hapa Tz "utamaduni wetu" ambao hauna msingi wa kisheria au kitaaluma ukishatunikiwa cheo cha Prof. basi utakufa nacho. Sasa ukiwa nje ya chuo au umeretire jiulize wewe ni professor wa wapi-hapo hakuna jibu. Nimeshaona Barmaid akipigwa vibao kisa hakutanguliza uProfesa alipomuita huyo profesa fulani. Labda waliotangulia huko UDSM watajibu na sasa hii kitu imeenea. Bahati mbaya haikuishia kwa hawa maprofessor bali huko kwa ma injinia nako imeshika uzi na sasa imekuwa utamaduni Eng. Fulani mwana wa Daraja.

Mbaya ni pale wasio na hizo sifa wanapojipachika: Huko upande wa Afya binadamu na mifugo kuna madoctor hata hujui wametoka wapi (huu si utamaduni mzuri).
PhD na Uprofessor: Kuna nchi ambazo kuwa professor sio lazima uwe na PhD na hata hapa kwetu zamani ilikwa hivyo. Lakini baadae wakatokea wajanja wakasema kama huna PhD basi uprofessor utausikia kwenye bomba kwa hiyo karibu vyuo vyetu vingi kama si vyote unatakiwa uopoe PhD halafu ndio usake uprofessor. Nchi nyingi ushindani wa kazi inafanya waombaji wengi wa kazi vyuoni wawe na PhD hivyo wengi wa maprofessor sasa ni PhD (and the like) holders. Kwa vyuo ambavyo vinaweka kipaumbele kwenye utafiti bila PhD kazi hakuna.
Mimi haya madegree na mavyeo hayanipi tabu sana ukiacha hawa wanaotaka kuendelea kuitwa Professor wakati hawafanyi kazi vyuoni (retired, resigned etc).
 
Tofauti yetu na nchi zingine nikwamba sisi hao wanaojiita Madocter na maprofesser
Hawajawahi tengeneza hata mshumaa au tuspic kazi yao kuandika vitabu ambavyo hata watoto wao hawasomi kazi kubwa wanayofanya wanafungua Gest na bar

Lakini wenzetu ni wangunduzi wa vitu vingi Sana kwahyo hata akiitwa Professor hanashuda na hata asipo itwa hakuna shida
Mtu mmoja nikamuita Dk. Pale kazini kidogo anipige kwa nini namuita Dk. Wakati yeye ni Professor
Yaani wanadhani Dili halafu wakistafu unawaonea huruma mtaani huku
 
Nakuonesha hizo PhD haziwasaidii angalia hapa mapovu yanavowatoka kutetea utadhani ni dili sana
Mm nadhani maisha ni zaid ya PhD
Maana kama una hizo zote na unamiaka zaid ya 45 na bado ukawa unaishi maisha yaleyale saa nyingine hata kukaaa unakaa kwenye nyumba ya taasisi maana yake wew ni Ziro PhD
 
Habari zenu wadau wa JF.

Hivi Ni vigezo gani hutumika mpaka mtu aitwe Proffesor au Doctor.Doctor ninayemzungumzia ni yule mwenye PHD sio hospitali.

Nimeuliza hivi kwa sababu, Tanzania mtu yeyote mwenye shahada ya uzamivu huitwa Doctor(Dr).

Lakini nimesoma biography ya Barrack Obama na Hillary Clinton na nikagundua wamesoma mpaka level ya PHD lakini sijawahi kusikia wanaitwa Doctor tofauti na hapa kwetu.

Mfano rais wetu John Pombe Magufuli ana PHD anaitwa Doctor.Obama pia ana PHD na aliwahi kufundisha Chuo kikuu ila sikuwahi kusikia akiitwa Doctor au Proffesor.

Hii imekaaje ndugu wa JF naomba kuelimishwa.
hizo ni level za juu zaidi za upumbavu, ukifika level hizo unakuwa kama bamia iliyokomaa haifai kwa matumizi.
 
Sasa mbona dr JP anaonekana kama uwezo wake ni wa bachelor?
Nyerere alitunukuwa PhD nyingi tu za heshima na vyuo mbalimbali lkn sikuwahi msikia akiitwa doctor Nyerere. Hii doctor kwa viongozi ilipamba moto sana enzi za Kikwete tena ilipambishwa moto na watu wa chama tawala, hao si unajua tena kwa kusifia mtu akiwa Ikuku unaweza dhani ktk nchi hakuna anayeweza kuja kuongoza zaidi yake. Katika harakati za uchaguzi fulani kulikuwa na professor Lipumba, Doctor Slaa na ndugu Kikwete. Kuvuta mfanano wa wagombea zikapekuliwa degree za kutunukiwa za Kikwete ghafla zikaanza kupaishwa naye akaanza kuitwa doctor Kikwete. Ameondoka Ikulu hii Doctor naona kama inasahaulika ktk kum-address. Wamarekani hawahitaji hiyo sifa kuonekana kiongozi anajua ndo maana akina Obama wahawakuhitaji kuitwa madoctor
 
Back
Top Bottom