Nini maana ya Professor na Doctor(PhD)?

Nini maana ya Professor na Doctor(PhD)?

Professor J. & the late Prof. majimalefu !

Hapo mnawekaje ?
 
professors saa ingine wanawaita senior teachers of university.
PhD ni Shahada ya Uzamivu, yaani mtu anabobea au kuzamia katika Kaeneo fulani kidogo kataaluma take na wanaitwa madaktari wa falsafa. Uprofesa ni daraja la juu la wanataaluma, kuanzia mhadhiri mzaidizi, hadi profesa. Na vyeo hivyo vinapanda kwa kusomea na kufanya machapisho kwenye majarida ya kisayansi
 
Obama hajasoma level ya Ph.D, ila technically ni Juris Doctor kwa sababu ana degree ya sheria. Degree ya Sheria Marekani ni Juris Doctor (J.D)Kwa hiyo angependa maujiko angejiita Dr. Obama.

Nchi kama Marekani, si ma doctor wote wana Ph.D. Kunda ma doctor wengine wana Ed.D (Doctor of Education) au Psy.D (Doctor of Psychology)

Jamii zilizoendelea kielimu, kama mtu hayupo katika kazi za kufundisha au research, kujiita Dr. inaonekana ulimbukeni.

Watu kama Waziri wa Ulinzi wa zamani wa Marekani Robert Gates, ana Ph.D, lakini alikuwa anaitwa tu Defense Secretary, Robert Gates. Kwa sababu mtu kuwa na doctorate si kitu cha ajabu.

Watu wengine ambao wana Ph.D lakini mara nyingi husikii wakiitwa "Dr" ni Condoleeza Rice na Susan Rice.

Kuhusu tofauti ya Dr na Professor, inategemea na mfumo wa nchi.

Kwa Marekani, Professor ni mtu anayefundisha chuo Kikuu tu. Nakumbuka wakati naanza chuo, kuna Professor mmoja tulimuita Dr., tukifikiri ni Dr., akatusahihisha kwamba yeye hajafanya doctorate degree yake bado, kwa hiyo tusimuite Dr. yeye ni Profesa tu.

Lakini kwa Tanzania, nilivyoona, ni kwamba, U Profesa ni cheo fulani, kwa hiyo kuna watu wengi wenye doctorate zao ni ma Doctor so and so, lakini hawajafikia cheo cha u Profesa.
Umeliweka vizuri sana mkuu! Bravo! Kwa kuongezea kibongo ukishakuwa na PHD ili uwe Prof kuna number of research and publications unatakiwa uwe nazo na kwa chuo baada ya kuwa na phd unakuwa associate prof then prof. Pia kuna honorary phd ndio zile za JK na Marehemu Mengi...uwe una mchango fulani katika jamii...hizi ni phd za heshma na sio za kusoma.
 
Swali niliokuwa najiuliza mfano Obama alikuwa na PHD lakini sikuwahi kuona au kusikia jina lake likianzia Dr kama ilivyo kwa Kikwete,Magufuli etc, ambao majina yao yanaanzaga na Dr
note: kikwete alitunuikiwa tu Udaktari wa heshima (honourable doctor) kama alivyotunukiwa Kanye West.
 
Nyerere alitunukuwa PhD nyingi tu za heshima na vyuo mbalimbali lkn sikuwahi msikia akiitwa doctor Nyerere. Hii doctor kwa viongozi ilipamba moto sana enzi za Kikwete tena ilipambishwa moto na watu wa chama tawala, hao si unajua tena kwa kusifia mtu akiwa Ikuku unaweza dhani ktk nchi hakuna anayeweza kuja kuongoza zaidi yake. Katika harakati za uchaguzi fulani kulikuwa na professor Lipumba, Doctor Slaa na ndugu Kikwete. Kuvuta mfanano wa wagombea zikapekuliwa degree za kutunukiwa za Kikwete ghafla zikaanza kupaishwa naye akaanza kuitwa doctor Kikwete. Ameondoka Ikulu hii Doctor naona kama inasahaulika ktk kum-address. Wamarekani hawahitaji hiyo sifa kuonekana kiongozi anajua ndo maana akina Obama wahawakuhitaji kuitwa madoctor
Matango Pori kabisa haya unajiamini nini kudanganya?
 
Swali niliokuwa najiuliza mfano Obama alikuwa na PHD lakini sikuwahi kuona au kusikia jina lake likianzia Dr kama ilivyo kwa Kikwete,Magufuli etc, ambao majina yao yanaanzaga na Dr
Huku kwetu ni sifa.. watu hupenda kujulikana/kujisikia kwa level ya elimu yake. Wenzetu hujitambulisha kiwango cha elimu yake pale tu inapohitajika, sisi ni sehemu ya jina..
 
Obama hajasoma level ya Ph.D, ila technically ni Juris Doctor kwa sababu ana degree ya sheria. Degree ya Sheria Marekani ni Juris Doctor (J.D)Kwa hiyo angependa maujiko angejiita Dr. Obama.

Nchi kama Marekani, si ma doctor wote wana Ph.D. Kunda ma doctor wengine wana Ed.D (Doctor of Education) au Psy.D (Doctor of Psychology)

Jamii zilizoendelea kielimu, kama mtu hayupo katika kazi za kufundisha au research, kujiita Dr. inaonekana ulimbukeni.

Watu kama Waziri wa Ulinzi wa zamani wa Marekani Robert Gates, ana Ph.D, lakini alikuwa anaitwa tu Defense Secretary, Robert Gates. Kwa sababu mtu kuwa na doctorate si kitu cha ajabu.

Watu wengine ambao wana Ph.D lakini mara nyingi husikii wakiitwa "Dr" ni Condoleeza Rice na Susan Rice.

Kuhusu tofauti ya Dr na Professor, inategemea na mfumo wa nchi.

Kwa Marekani, Professor ni mtu anayefundisha chuo Kikuu tu. Nakumbuka wakati naanza chuo, kuna Professor mmoja tulimuita Dr., tukifikiri ni Dr., akatusahihisha kwamba yeye hajafanya doctorate degree yake bado, kwa hiyo tusimuite Dr. yeye ni Profesa tu.

Lakini kwa Tanzania, nilivyoona, ni kwamba, U Profesa ni cheo fulani, kwa hiyo kuna watu wengi wenye doctorate zao ni ma Doctor so and so, lakini hawajafikia cheo cha u Profesa.
Alafu wanaopenda kushoboka kuitwa Ma-Dr wengi huwa ni vilaza...
 
Tafiti ngapi zina mfanya awe professor kamili, maana bongo kuna Associate professor na Professor sijui kama nazo ni tofauti?
Nimesema vigezo utofautiana kutoka taasisi moja kwenda nyingine. Mfano SUA, Makelele, na UDSM vina criteria tofauti.

Kikubwa kila publication ina point zake kutegemeana kama ww ni main author ama second. Pia umepublish kwenye journal yenye uzito kiasi gani.

Kikubwa kuna vigezo vya point kufikiwa ili uanzie associate kabla ya kuwa complete professor.
 
Umeliweka vizuri sana mkuu! Bravo! Kwa kuongezea kibongo ukishakuwa na PHD ili uwe Prof kuna number of research and publications unatakiwa uwe nazo na kwa chuo baada ya kuwa na phd unakuwa associate prof then prof. Pia kuna honorary phd ndio zile za JK na Marehemu Mengi...uwe una mchango fulani katika jamii...hizi ni phd za heshma na sio za kusoma.
Si sahihi, kuna vigezo rasmi vya mtu kuwa Dr. wa elimu, na pia kufikia rank ya uprofessor.

Tatizo ni wakati mwingine kwa kutokufaham watu wanaweza anza kukuvisha UDr. ama Uprofessor kwa kutokuelewa kama una vigezo.

Ni kama tu mahospitalini kuna watu wanaitwa maDr. bila kuwa na qualification ya MD. Sometimes ni nurse ama C.O, ama M.O but watu humuita Doctor fulani. Hii haimpi uhalali wa kuwa Dr. kwa maana ya qualification ya M.D.

Hivyohivyo hata kwa wanataaluma hii hutokea. But kwa kifupi kuna vigezo vya kuvishwa hizo nafasi.
 
Ni sawa na zile wakili msomi, dereva msomi, mwanajf msomi. Mganga.msomi,nyumbu msomi, n.k
Nimekusoma vizuri.

Nilichokielewa zaidi ni kwamba Kuna tofauti Kati ya nchi na nchi.

Sema Tanzania Kuna ka harufu kakupenda maujiko.
 
professor niliwahi kusikia ni yule ambae amefanya utafiti UNIQUE sana juu ya jambo fulani, ambalo halikuwahi kufanywa hapo nyuma sana

Na amevumbua jambo ambalo lililkuwa likisumbua sana watu kwa kulifanyia utafiti wa kina

mi najua kidoogo hivyo kuhusu Professor
Lipumba alifanya utafiti gani mkuu.
 
Phd in Tanzania is associated with ulimbukeni au poverty mentality. Kwa wenzetu PHD aint a big deal.
 
Huku kwa wenzetu hawapendi kujikweza, ni nadra sana mtu kutanguliza credential zake kama wanavyofanya Tz, mara nyingi utajua kutoka kwa mtu mwingine lkn sio muhusika. Niko na watz na waafrika wengi tu huku ambao ni Phds au maprofessor lkn huwezi kujua kirahisi
Nimekuelewa, but kinachonitatiza nimetolea mfano Obama ana PHD lakini sikuwahi kusikia au kusoma akiitwa Doctor.

Utofauti upo wapi?
 
Nimesema vigezo utofautiana kutoka taasisi moja kwenda nyingine. Mfano SUA, Makelele, na UDSM vina criteria tofauti.

Kikubwa kila publication ina point zake kutegemeana kama ww ni main author ama second. Pia umepublish kwenye journal yenye uzito kiasi gani.

Kikubwa kuna vigezo vya point kufikiwa ili uanzie associate kabla ya kuwa complete professor.
Hahaha kwahiyo uprofessor ni tafiti siyo PhD au nakuelewa ndivyo sivyo?! Au ndiyo doctorate degree?! Hivyo PhD holder ni sawa kujiita professor au Doctor?!
 
Doctor utamkuta anapiga watu sindano kwa zahanati.
Professor ni kame vile maji marefu yaani mganga wa jadi.
Kwa ujumla prof na doctor wote ni waganga sema mmoja anatibu vidonda mwingine anatoa majini
hatari kwelikweli!!!!
 
PhD ni Shahada ya Uzamivu, yaani mtu anabobea au kuzamia katika Kaeneo fulani kidogo kataaluma take na wanaitwa madaktari wa falsafa. Uprofesa ni daraja la juu la wanataaluma, kuanzia mhadhiri mzaidizi, hadi profesa. Na vyeo hivyo vinapanda kwa kusomea na kufanya machapisho kwenye majarida ya kisayansi
Hii inasound kuwa na ukweli fulani.Naweza kukubaliana na hiyo sababu.

Kumbee ni sisi waafrika na masifa yetu
Sio sifa mkuu, mtu amesotea PhD yake kwa nini asiitwe Dr? Ni stahili yake kabisa na huko nje wanataaluma wanapeana heshima zao, na wenzetu kama ni Prof ataanza kuandika Prof.Dr xxxy
 
Back
Top Bottom