Kwa sisi tuliosoma mpaka vyuo vikuu tuna kauelewa kidogo,ili uwe professor,unatakiwa uwe unafanya tafiti sana na kupublish journals na compendiums,na makala mbalimbali za utafiti,na kufanya mihadhara mbalimbali,kila utafiti unaoufanya na kuja na majibu yake unapitiwa na jopo la wataalamu husususani maprofessa wabobevu ambao huteuliwa kupitia findings zako,iwapo utafiti wako umekubalika kuna units una score,kuna kiwango fulani cha units, ukifikisha unapewa uasosieti professor,ukizidi kuchimba zaidi na zaidi mpaka kufikia units fulani unapewa full professor,mchakato unakuwa kama ule wa kupata PHD,kwamba unafanya coursework,unafanya research unaandika thesis kisha unaidefend thesis yako kwenye viva voce(oral exam) ukifaulu unapewa PHD,isipokuwa kwenye uprofessor hakuna coursework.Hakika ni mchakato mgumu sana ndio maana unaona wengi wanastack kwenye udoctor for a lot of years