Hiyo watu hawataki kukubali, pesa unayoipata kwa ghafla ina utumwa sana na inaleta majuto kuliko ile pesa unayoipata kidogo kidogo mpaka inakuwa nyingi..
Hiyo ni saikolojia ya pesa ambayo watu wengi hawaizungumzii na hawaijui.
500M uliyoipata ndani ya mwaka mzima kidigo kidoho ni bora kuliko 500M uliyoipata ndani ya wiki moja.
Kwa sababu hii uliyoipata kwa muda mrefu inaweza kuendelea kudumu na utakuwa umeshaizoea akilini.
Ila kutoka 0 - 500M hapo kati umevuka stepu nyingi sana na hizo step lazima urudi uzipige tena kama utataka kufika hapo.
Masikini akishika 500M anakosa kabisa interest ya kuwekeza kwenye biashara itakayompa faida ya laki 3 kwa mwezi kwa sababu anaona ndogo yeye ana 500M alafu ahangaike na laki 3?
Mambo ni mengi sana mtu atafanya namna atafuja, atagawa hela, ataenjoy na watoto wakali, swhsmu za starehe na pengine hata gari ya maana asinunue, asijenge, yeye atahangaika na starehe..
Kwa sababu watoto wengi zamani tulipewa pesa pale tunapotaka kufanya starehe kama kununua pipi, kwenda disko, kununua juisi, magemu n. K, so the same mentality inatutafuna mpaka ukubwani..
Ni hatari sana mku, umenigusa sana na ile comment yako maana nina mengi ya kusema kuhusu hii mada, ila naomba niishie hapa..