Nini kilikusaidia kupata kazi?

Nini kilikusaidia kupata kazi?

Tena uwe Makini ktk Mavazi usiende umevaa ndala au viatu vya wazi

Usiendee umenyoa kihuni
.usiende umeweka Earphones maskioni

Yaan nenda like unaingia IKULU

Coz.. hata yule anaepokea CV zako kama Ni Receptionist atakudharau kutokan na muonekano wako ila ukiend upo vzr atakuwekea Thamani flan na kuithamin hiyo Bahasha Yako.
Haya maisha yalikuwa ya fedhea sana yani nashukuru ujio wa mitandao kwa kweli.😂😂😂
 
Kuna dogo mmoja namjua huyu hajawahi sota kitaa kabisa

Na Hana connection yoyote mjini wazazi wake walimu tu .

Ndani ya Miaka 2 kafanya kazi sehemu tatu na kote alikuwa anaacha kwa condition zake .

Na Sasa anafanya kazi Taasisi kubwa hapo dar na tayari kashaanza masters

Sent from my TECNO P703 using JamiiForums mobile app
 
That's why nikasema nenda Sehem unayoona Kuna uwezekano wa KUBAKI. Halmashauri kivyovyote lazima kutakuw na Ugumu unless Mkurugenzi akubebe.

Ni kwel Field kupata ni Kazi sana.. inahitaji Connection pia ila mie naona Wengi hawafanyi RESEARCH kabla ya kwenda kuomba FIELD.

Mfn. Kwa Mtu wa Human Resources Management.. nitamuona Mjinga akikimbilia Ktk TAASISI za kawaida badala ya kwenda ktk RECRUITING AGENCIES.. na nauhakika Wanafunzi wengi wanaomba ktk Makampuni makubwa makubwa.. na kusahau hizi RECRUITING AGENCIES... Kitu ambacho wakati nafatilia Field nilikipa KIPAUMBELE nikiwa na TARGET zangu.. ila nikapata Sehem nyingine. Class langu lilikuwa na WANAFUNZI 70 Wote ni HR hakuna HATA mmoja aliyeenda ktk RECRUITING AGENCIES Kufanya FIELD.

Umeona TATIZO lilipo..?
Wengi walienda Serikali ya Mtaa.. baada ya kukosa Ktk Makampuni makubwa.

End of the day ni kupoteza MUDA.

SO swala la Field, Internships na Ajira vyote vinahitaji RESEARCH na Evaluation kabla ya kupeleka BARUA yako.

Unatakiwa ujue UNAHITAJI nini? Na kwa wakati gani. Pia inahitaji Ujue Tija ya Hiyo Taasisi ktk Career yako.

Ntashangaa IT unaenda kuomba Field HALMASHAURI hata kama umekosa pa kufanya field ni BORA uache tu ufanye muda mwingine. Instead of kupoteza Muda hapo.
Mkuu m nachukua HR je hizo RECRUITNG AGENCY ndo nn
 
Acha tu mkuu, nilienda kwenye interview moja tena benk, tumefanya round one tulikuwa kama 300 hvi, tukatokea 10 kati ya wale 300, interview ilikuwa ya round w tu ndo mana walikata kutoka 300 mpaka kumi kupunguza idadi ya wanaoenda round ya 2 ambayo ni mwisho

Tulipoenda tulikuwa wanaume 2 na wanawake 8

Interview ikaendelea, ilipofika zamu yangu wakauliza maswali mpaka ya siasa, nkajibu

Mwisho wakaniambia eti nina mwili mdogo sitoiweza nafasi nanayoiomba mana nafasi hiyo chini yake kuna watu wengine wazima na wakubwa sana kimwil hivyo hawataniheshimu

Najuta kuwa na mwil mdogo, nilitaman Mungu aniumbe upya, mpaka leo npo mtaani zaid ya 5 yrs sasa
Dah nimecheka sana. Ila pole mkuu
 
Moja kwa moja kwenye mada...

Vijana wengi wanamaliza vyuo kila mwaka ilihali wengine bado tuko mtaani hatujui hatima ya maisha yetu.Mimi binafsi nimehitimu miaka kadhaa imepita nilipomaliza chuo nilikuwa na haraka sana ya kutafuta kazi miaka inasonga ni kama zile nguvu zimeisha nahisi uchungu kusikia mtu anaongelea mambo yanahusu kazi ilihali wengine tunahangaika sana..

Kwa kweli nimeitwa interview kadhaa lakini naona kama danganya toto tu walio na iyo kazi wapo tayari wengine tunapoteza tu muda..nimefikiria kila mtu anayeweza kunipa connection lakini nako hakuna matumaini.

Sasa wandugu wewe uliwezaje kupata kazi tupeane mbinu jamani stress zinazidi
N kumshirikisha MUNGU tuu ,, kwa kuanza ni vema kufanya kazi kwa kujitolea ata kama sio ya hadhi ya elimu yako .
 
Moja kwa moja kwenye mada...

Vijana wengi wanamaliza vyuo kila mwaka ilihali wengine bado tuko mtaani hatujui hatima ya maisha yetu.Mimi binafsi nimehitimu miaka kadhaa imepita nilipomaliza chuo nilikuwa na haraka sana ya kutafuta kazi miaka inasonga ni kama zile nguvu zimeisha nahisi uchungu kusikia mtu anaongelea mambo yanahusu kazi ilihali wengine tunahangaika sana..

Kwa kweli nimeitwa interview kadhaa lakini naona kama danganya toto tu walio na iyo kazi wapo tayari wengine tunapoteza tu muda..nimefikiria kila mtu anayeweza kunipa connection lakini nako hakuna matumaini.

Sasa wandugu wewe uliwezaje kupata kazi tupeane mbinu jamani stress zinazidi
Mbinu nilizotumia. Kwanza kabisa wakati namaliza chuo sikutaka kabisa kurudi nyumbani Arusha na nilijiwekea akilini mwangu kuwa nataka kazi yangu nitakayo ipata iwe maeneo ya posta. Nilihakikisha kila gorofa lenye ofisi hapa posta lazima niingie, napeleka barua karibia maofisi yote alafu ikishapita wiki1 narudi kwenda kuuliza majibu vipi? Sito sahau nilikua nafanya followup kwa ofisi moja kila baada ya siku2 hadi jamaa akaniambia "dogo kazi hakuna, nisijekukujibu vibaya bure we nenda" niliumia ila sikukata tamaa. Nakumbuka kuna siku nilikua geto mida ya saa3 ndio najiandaa kupeleka barua nikapigiwa simu niende ofisi flani posta nikaonane naa bosi, nikafanya hivyo kweli na nakumbuka nilianza kazi tarehe 9 August 2016. Nilifanya kazi kwa bidii sana hadi nilipo pata kazinyingine hapahapa posta. Kikubwa usikate tamaa na kusali ni muhimu zaidi. Inshort
 
Back
Top Bottom