Binafsi ni juhudi tu katika field yangu ya kwanza, pia na Bahati naweza kusema. Field yangu nilijituma sana na kama Bahati, aliyekua assistant wa boss alikua mlevi na mzembe mno kazini kiasi kwamba jumatatu kuja kazini kwake lilikua jambo zito, either apoteze simu au aje ananuka pombe siku nzima, kupitia tabia zake nikaonekana nafaa sana, hata nilipomaliza chuo sikufanyiwa interview wala kuombwa japo CV nilipewa contract na mshahara mzuri nikiwa fresh from school....
Then baadae baada ya hiyo kampuni kufunga kazi zake TZ nikatuma CV kampuni moja kiutani tu siku hiyo hiyo nikaambiwa at my favourate time nifike ofisini kwao, nikajua interview, kufika wananimbia tunegotiate mshahara na niwambie lini nitaanza kazi, baada ya hapo tukakubaliana hadi leo Niko nao na tunategemeana....
Sijawahi fanya interview yeyote wala kuombwa cheti chochote zaidi ya kuaminiwa, na nalipwa mshahara unaojitosheleza na kazi zangu zinaheshimika. Kiufupi huwa najiona ni mwenye Bahati tu mana sijawahi kutumia utaalamu au namna yoyote zaidi ya Bahati tu.