Nini kilikusaidia kupata kazi?

Nini kilikusaidia kupata kazi?

Acha tu mkuu, nilienda kwenye interview moja tena benk, tumefanya round one tulikuwa kama 300 hvi, tukatokea 10 kati ya wale 300, interview ilikuwa ya round w tu ndo mana walikata kutoka 300 mpaka kumi kupunguza idadi ya wanaoenda round ya 2 ambayo ni mwisho

Tulipoenda tulikuwa wanaume 2 na wanawake 8

Interview ikaendelea, ilipofika zamu yangu wakauliza maswali mpaka ya siasa, nkajibu

Mwisho wakaniambia eti nina mwili mdogo sitoiweza nafasi nanayoiomba mana nafasi hiyo chini yake kuna watu wengine wazima na wakubwa sana kimwil hivyo hawataniheshimu

Najuta kuwa na mwil mdogo, nilitaman Mungu aniumbe upya, mpaka leo npo mtaani zaid ya 5 yrs sasa

Hao ni wapumbavu sana, eti mwili mdogo! Mbona mm nna mwili mdogo nimeajiri wenye miili mikubwa wapo chini yangu na wananiheshimu tuu! Huo ni unyanyasaji..
 
That was so unproffesional of them you applied for the job because you had the qualifications they needed. Kwenye Tangazo la kazi hawakuweka physique appearance kama moja ya vigezo vya kupata kazi (ah waliweka?) kwangu mimi huo ni unyanyapaa....and I swear nnavyopenda kucheza na sheria ninge wa sue [emoji1][emoji1] Yani ungekua na mwanasheria mzuri mbona hiyo ni kesi na wangekulipa....

Sent from my SM-G955F using JamiiForums mobile app
Hapana kwa kwel, suala la muonekano hawakuweka, sifa nyingine zote nilikuwa nazo ndo mana hata round ya kwanza nilipita kati ya watu 300, wale 10 nilikuwepo na ambao tulikuwa nao wala hawakunizid mwil kivile, naweza sema ni mmoja tu alikuwa bonge
 
Hao ni wapumbavu sana, eti mwili mdogo! Mbona mm nna mwili mdogo nimeajiri wenye miili mikubwa wapo chini yangu na wananiheshimu tuu! Huo ni unyanyasaji..
Mkuu nadhan walitafuta tu sababu, na uzuri ni kuwa walinambia hiyo sababu hapo hapo, huenda hata nisingejua na kuchukulia ni sehemu ya kukosa kama nyingine nyingi ambazo nimefanya
 
Omba Mungu sana, kuajiriwa hakuna ujanja, ni Mwenyezimungu akiamua tu unapata, kuna jamaa yangu mmoja hivi alijitolea Kinyerezi 2, miezi 10 hakupata ajira, kipindi anajitolea akaitwa tena kujitolea TPA(seap program) mwaka mzima uliisha na ajira zikitoka yupo pale lkn alikuwa hapati ajira, ingawa alikuwa analipwa 1M kwa nwezi. juzikati ajira za TBA wakaitwa watu 280 huku wakiwa wanatafuta mtu mmoja akachukuliwa yeye (Mechanical Engineer 2).

Kuna mdogo wangu kamaliza mwaka huu AUTOMOBILE ENGINEERING, kapata kazi TOTAL bila connection walienda kuomba kurecruit watu wa automobile wanamchukua kisa ana gpa nzuri, kuna jamaa humu jamii forum, nilimkonect tu mahala wanatafuta maintenance engineer haikuchukua hata week 2 akaitwa kazini, na niliwapa watu wengi email watume maombi lkn ye aliitwa faster. .

Ukisikia mtu kapata kazi wala sio ujanja wake, bali nimuda tu umefika.

Mkuu Rustem Pasha
Naomba naomba connection ya huyo jamaa wa bandari na mie nikajitolee huko au nikajishikize hata kwa vibarua vyovyote

Mtaani kugumu jamani
 
Mimi nilipata kazi kwa kuchukua email ya COO, nikamuemail sikuweka hata CV, asubhi ninaamka nakuta kaniomba CV niakamtumia, akaniambia niende ofisini kwao kesho yake. Interview tukaifanyia SLipway na haikuwa interview ilikuwa story. Training akanipa mwenyewe niliomba internship akaishia kunipa kazi na malipo mazuri.

Kuna ndugu yangu alipataga kazi shirika la misaada la Japan JICA, kisa kwenye interview walipewa swali la kuandaa spread sheets unajumulisha kwa formula. yeye akawa hajui, akawa anajumlisha kawaida anaweka jibu. Mjapan aliyekuwa anasimamia akamwona, akamfuata akamuuliza kwaniniunafanya hivi mbona wajumlisha kawaida, Jamaa akamjibu hapana nimeweka formula. Mjapana kaanza kuchheka jinsi jamaa alivyokuwa kaweka sura kama kweli vile. Akacheka sana akamwambia I like you. Hivyo na kazi akapata.
Mkuu
Pls care to share email template uliyomtumia ceo
Naweza kutumia mbinu hii kwa kucrack email za ceo mbalimbali nikajaribu bahati
 
Hivi mkuu Lazima kuvaa Official ukiwa unasambaza hizi cv?
Tena uwe Makini ktk Mavazi usiende umevaa ndala au viatu vya wazi

Usiendee umenyoa kihuni
.usiende umeweka Earphones maskioni

Yaan nenda like unaingia IKULU

Coz.. hata yule anaepokea CV zako kama Ni Receptionist atakudharau kutokan na muonekano wako ila ukiend upo vzr atakuwekea Thamani flan na kuithamin hiyo Bahasha Yako.
 
Daaa! one moment nilipata kupitia mchumba bana! mchuchu sababu alikuwa na ndugu zake huko kweli nikapata nzuri yenye kipato na heshima!! kimbembe sasa kikaja amri, na matangazo kwa watu, na sharti moja unioe niwe mke wako, nikaona msela barida tu, haina shida ikawa km bado haitoshi maneno;

''kazi hii ni mimi, bila mimi pale wewe siyo kitu!! leta hela hapa! takula hiyo hela mpaka iishe, sikuona maendeleo!

bila mimi usingekuwa hivi!!

ukikakataa utasimngwa mpaka na rusha roho za kilokole!! nikaona heee! isiwe tabu!! kwa heri ya kuonana!! na kule kazini akaenda kupaka kwa ndg zake nikanyanyaswa kupitiliza! kutokupanda daraja, section za chini kabisa!! but nikakomaa! kiasi hata cha kunyimwa mshahara bila sababu!!! hapo uzalendo ukanishinda. kazi za kupewa hizo!

Daa! nikatema mzigo mpaka sasa nina mpango wa kazi mpya! na mke na mtoto. nimeacha kaolewa na jamaa mwingine. sisemi usipewe la hasha unaweza kupewa kazi but uwe makini na mtoaji offer.
 
Omba Mungu sana, kuajiriwa hakuna ujanja, ni Mwenyezimungu akiamua tu unapata, kuna jamaa yangu mmoja hivi alijitolea Kinyerezi 2, miezi 10 hakupata ajira, kipindi anajitolea akaitwa tena kujitolea TPA(seap program) mwaka mzima uliisha na ajira zikitoka yupo pale lkn alikuwa hapati ajira, ingawa alikuwa analipwa 1M kwa nwezi. juzikati ajira za TBA wakaitwa watu 280 huku wakiwa wanatafuta mtu mmoja akachukuliwa yeye (Mechanical Engineer 2).

Kuna mdogo wangu kamaliza mwaka huu AUTOMOBILE ENGINEERING, kapata kazi TOTAL bila connection walienda kuomba kurecruit watu wa automobile wanamchukua kisa ana gpa nzuri, kuna jamaa humu jamii forum, nilimkonect tu mahala wanatafuta maintenance engineer haikuchukua hata week 2 akaitwa kazini, na niliwapa watu wengi email watume maombi lkn ye aliitwa faster. .

Ukisikia mtu kapata kazi wala sio ujanja wake, bali nimuda tu umefika.

umenisisimua sana mkuu katika watu 280 waliofanya interview mimi ni miongoni mwao wakachukuliwa watu 25 kwenda oral na mie nilikuepo. Nimejifunza kitu hapa
NAOMBA NIKUFATE INBOX
 
Acha tu mkuu, nilienda kwenye interview moja tena benk, tumefanya round one tulikuwa kama 300 hvi, tukatokea 10 kati ya wale 300, interview ilikuwa ya round w tu ndo mana walikata kutoka 300 mpaka kumi kupunguza idadi ya wanaoenda round ya 2 ambayo ni mwisho

Tulipoenda tulikuwa wanaume 2 na wanawake 8

Interview ikaendelea, ilipofika zamu yangu wakauliza maswali mpaka ya siasa, nkajibu

Mwisho wakaniambia eti nina mwili mdogo sitoiweza nafasi nanayoiomba mana nafasi hiyo chini yake kuna watu wengine wazima na wakubwa sana kimwil hivyo hawataniheshimu

Najuta kuwa na mwil mdogo, nilitaman Mungu aniumbe upya, mpaka leo npo mtaani zaid ya 5 yrs sasa
Daaah! ni dhahiri hii ndugu, kweli hiyo haikuwa fair game bora wangebakia na hayo majibu kwa rejea zao siyo kukuambia wewe hapo
 
Back
Top Bottom