Nini kilikusaidia kupata kazi?

Nini kilikusaidia kupata kazi?

nimefikiria kila mtu anayeweza kunipa connection lakini nako hakuna matumaini.
Wengi wanajifanyaga wana connections za kazi ila hawana kitu mkuu. Trust me. Wengi wao wakiona wameshindwa wanakupiga chenga badala ya kuwa wakweli.

Mtu aliyenipa kazi yangu ya kwanza mwaka 2013 mkoani Iringa mshahara take home 750,000/= alikuwa ni mtu wa kipato cha chini saaaana sema aliniomba CV yangu kisha akampa ndugu yake aliyekuwa anafanya kazi BANK.
 
Nimemaliza degree baada ya miezi 3 nikapata kashavu ka data collection.
Baada ya miezi 3 tena nikapata kazi yangu ya kwanza ( private company): hapa kulikua na some sort of connection ila niliperform interview hadi nikawaacha midomo wazi maboss( sababu ya kufany vzr ni FIELD PRACTICAL YA MWAKA WA 3). Nikapata kazi kabla ya interview kuisha na wakaniomba kama nina rafiki mweny uwezo kama wangu nimlete😀😀.
My dream work ilikua ni kufanya kazi ktk International NGOs.
Baada ya miaka 2 ya expirience kwenye hiyo private company niliaanza kufight for INGOs.
Siku niliyoitwa intetview nilijiandaa usiku na mchana kuhakikisha nafanya vizuri interview. Namshukuru Mungu nilifanikiwa kuajiriwa ktk hiyo INGO.
Hadi sasa bado napambana na development projects kupitia NGOs.

Hitimisho:
Information is power, kua na taarifa nyingi ktk secta/ professional yako inasaidia sana kuperform kwnye interview.
 
Wengi wanajifanyaga wana connections za kazi ila hawana kitu mkuu. Trust me. Wengi wao wakiona wameshindwa wanakupiga chenga badala ya kuwa wakweli.

Mtu aliyenipa kazi yangu ya kwanza mwaka 2013 mkoani Iringa mshahara take home 750,000/= alikuwa ni mtu wa kipato cha chini saaaana sema aliniomba CV yangu kisha akampa ndugu yake aliyekuwa anafanya kazi BANK.
Sasa ulimkumbka huyo mtu au ndo shukurani ya punda ni mateke😃😃
 
Wakuu hiv Ku volunteer sehem kuna impact yoyote kwenye ajira ...au unaweza poteza mda
 
Tunafahamiana? Kama hapana, nina plan yangu ninayoweza kukupatia na ukabenefit from it. We can work together and have different roles in position. Lakini nikachukua 28 percent after profit off.
mkuu karibu
 
Pole sana mdogo wangu. Nilikuwa kama wewe mwaka 2009 mpaka 2012 ila yote yamepita na imebaki kuwa historia.

Ninakuombea kwa Mungu wewe pamoja na vijana wengine wanaohangaika kupata kazi kuwa ipo siku utakuwa na pesa nyingi sana mdogo wangu.
nadhamini sana kwa mtu wako mzuri..
naomba Mungu uishi milele..
 
Back
Top Bottom