nguvumali
JF-Expert Member
- Sep 3, 2009
- 4,923
- 1,325
Haya yanayoendelea sasa katika duru za siasa hapa Tanzania bara ni aibu kwa utawala wake kama rais wa Jamhuri ya Tanzania. Rushwa imeshamiri, serikali haikusanyi kodi ipasavyo, kila mtumishi wa umma anakusanya kwa nguvu zake zote kila raslimali iliyopaswa kutumika kwa umma.
Ukija kwenye nishati hasa umeme/stima utalia, kila siku ni takwimu za Megawati lakini hatujawahi kufurahia umeme mfululizo.
Madini huko ndio aibu aibu na fedheha kubwa.
Nimshauri Bwana Kikwete, mzaliwa wa Msoga, ikiwa anahisi nchi imemtumbukia nyongo asione haya kubwaga manyanga, kama hilo pia litamnyima usingizi, achimbe kama Balali kisha tutamtangaza kama walivyomtangaza Balali, na kwakua WaTanzania ni watu wanaoamini kila jambo kirahisi wataishia kusema Rest In Peace.
Ni ushauri wangu, kama umeshindwa Kimbia mzee.
Ukija kwenye nishati hasa umeme/stima utalia, kila siku ni takwimu za Megawati lakini hatujawahi kufurahia umeme mfululizo.
Madini huko ndio aibu aibu na fedheha kubwa.
Nimshauri Bwana Kikwete, mzaliwa wa Msoga, ikiwa anahisi nchi imemtumbukia nyongo asione haya kubwaga manyanga, kama hilo pia litamnyima usingizi, achimbe kama Balali kisha tutamtangaza kama walivyomtangaza Balali, na kwakua WaTanzania ni watu wanaoamini kila jambo kirahisi wataishia kusema Rest In Peace.
Ni ushauri wangu, kama umeshindwa Kimbia mzee.