Ningekuwa Kikwete ningekimbia Nchi

kuomba kikwete akimbie hasa kama tatizo ni la kimfumo haitasaidia badala yake hata akija Rais mwingine naye tutaomba akimbie ni bora tukaanza kufumua mfumo kwa kuanzia na katiba
 
Hakuna haja ya kukimbia kinchompasa ni kufukuza watendaji wote wanaomfanya wananchi wamchukie,anatakiwa awe mkali kama Rais na baba wa nchi aache ushkaji achape kazi kwa weledi zaidi.
 
Huyo Kikwete amewekwa na wananchi sasa unapomshauri akimbie nchi sielewi unamaanisha nini. Unaweza kufanya vizuri kama utawashauri wananchi wasiichague tena CCM 2015.

Hapana ushauri kwa wananchi si kutoichagua CCM 2015, ni kuwaambia wananchi waige Tunisia, Misri na Libya. Huko 2015 ni mbali sana na nchi itazidi kuharibika, ni bora tupigane kidogo tumuondoe JK na CCM yake ndipo tutaheshimiana.
 
Sio ushauri stahiki mkuuu Nguvumali, why should he (Mr President) run away, uliyoyazungumzia kuwa ni matatizo ni mambo madogo besides ni part and parcel ya political life. Hakuna kukimbia bana mpaka 2015 ashuhudie uchaguzi mwingine na labda chama la mafisadi liangushwe kupitia sanduku la kura though pia sidhani maana dhana ya mabadiliko haijawafikia vilivo wananchi (majority) vjjini huko! Upinzani labda wataongeza viti vya ubunge tu which will also be good!
mKWEREE sasa hivi analaumu kila mtu kuwa anamkwamisha katika utendaji wake, anawalaumu wapinzani kuwa wanamkwamisha, analaumu kina Mzee Sita , analaumu waandishi .....
kama kashindwa anaweza kwenda hata msoga atuache tuendeleze Gurudumu la maendeleo
 
Hakuna haja ya kukimbia kinchompasa ni kufukuza watendaji wote wanaomfanya wananchi wamchukie,anatakiwa awe mkali kama Rais na baba wa nchi aache ushkaji achape kazi kwa weledi zaidi.

Ndugu Mlate hilo limekwishamshinda na hana la kufanya ndiyo maana anmtanguliza Nape kama vuvuzela kwani yeye hana ujasiri hata kidogo wa kushughulikia wa chini yake. Sababu iko wazi kabisa, yeye ndiye fisadi namba moja. Anatakiwa kutimuliwa haraka sana vinginevyo nchi inaangamia.
 
mKWEREE sasa hivi analaumu kila mtu kuwa anamkwamisha katika utendaji wake, anawalaumu wapinzani kuwa wanamkwamisha, analaumu kina Mzee Sita , analaumu waandishi .....
kama kashindwa
anaweza kwenda hata msoga atuache tuendeleze Gurudumu la maendeleo
Hawezi kwenda mwenyewe bana.Toka lini?Atavuta muda tu hadi hapo atakapopokeza kijiti kwa mwenzake.

Ila wewe kusubiri aondoke ni maajabu kwangu mimi.We unadhani yeye binafsi ni nini kinampa shida hadi aamuwe kwenda Msoga?
 
Hii ndoto yako ungeipeleka kwanza kwa mganga wa kienyeji ili ujue kama ni maluweluwe, jinamizi au umeanza kupotelewa na kumbukumbu kwamba kikwete alishaapishwa hakuna kurudi nyuma hadi dr silaha kaacha kusema hamtambui kikwete
 
Hii ndoto yako ingeipeleka kwanza kwa mganga wa kienyeji ili ujue kama ni maluweluwe, jinamizi au umeanza kupotelewa na kumbukumbu kwamba kikwete alishaapishwa hakuna kurudi nyuma hadi dr silaha kaacha kusema hamtambui kikwete
Mkuu ni wananchi peke yake wanaoweza kumwondoa bila hata ya huo muda kupita.

Kuapishwa ndiyo ameapishwa,lakini haina maana kuwa wananchi hawawezi kumwondoa.

Hili la kuondoka peke yake sidhani,nasubiri mleta hoja anieleze ni yapi anadhani yanampa JK wakati mgumu yeye binafsi.

Kwani kwenye hotuba zake anaonekana kuwa anajuwa shida za wananchi na anataka kuzitatua?Na shida yetu kubwa si unajuwa ni umasikini na ufisadi?
 
JK anatakiwa kufahamu kuwa uongozi wa nchi si issue binfasi kabisa.Urais ni taasisi.

Na wananchi wanaweza kuwa dissatisfied na hiyo taasisi hata kama wanampenda JK yeye binfasi.

Ni vitu viwili tofauti.Ni kama kazi na mmwajiriwa.

Maisha binafsi ya mwajiriwa ni tofauti sana na perfomance yake kwenye kazi.Kama kuna correlation huo ni mjadala mwingine.

However mwajiriwa hupimwa kwa work perfomance na si kwa maisha yake binafsi.

Viongozi wetu wameshindwa kuweka mipaka hapo na ndiyo maana hata wakipingwa wanatake it personal.

Ndiyo hapo anajikuta anasahau kuwa mwananchi ndiyo mwajiri wake.Na kwamba matokeo ya kazi yake ndiyo yanapingwa.

Hakuna mtu anajali kuwa ana wake wangapia ama kala nini.Hayo ni mambo madogo ambayo kwa level ya taasisi ya urais hayatakiwi yawe issue.

Tatizo however ni pale wanapokufuru na huku nchi ni masikini na wanaowaongoza asilimia kubwa ni masikini.

Kwa kifupi wananchi wanaweza kumfuta kazi saa yoyote wanayotaka na kumtaka arudi msoga.

Na hilo siyo personal endapo hatapingana nao.
 
Huna tofauti na gazeti moja nimesoma jana linasema KAFURILA azikoromea nchi tajiri, sijui huyu mwandishi alikuwa anaota, lakini ndo taaluma yake iliishia hapo kufikiri kichwa cha kuandika. Hivi kweli Kafurila anaweza kuyakoromea mataifa tajiri. Nirudi kwako sasa hizo sababu ulizoandika hapo juu ndyo za kumkimbiza rais nchini?

Inaonekana hauna hata takwimu, hebu fuatilia kesi zilizoko mahakamani kuhusiana na ufisadi, nenda TRA upewe takwimu za jinsi tanzania inavyokusanya kodi ukilinganisha na nchi n yingine, tayari megawatt 100 zimeshaingia grid ya taifa kama ulikuwa hujui nakupa taarifa. Jakaya mbona mtamkumbuka tu na chuki binafsi zenu hizo.

Mmshukuru siku hizi mnalala milango wazi , hakuna ujambazi tena. Wale jamaa wameacha ujambazi sasa wanajifanya kuzama kwenye siasa. Huko nako watachemsha tu. JK komaa nao usichoke.

Mkuu,

Mimi nina uhakika kuna siku mtarudi humu na kukataa kula matapishi yenu!!! Nchi hii kwa sasa haina muelekeo.

KIla mtu anfanya kivyake vyake tu.
 
Badilisha kichwa cha habari chako kikwete ni jina tu wako wengi kule msoga ungeanza na Rais kikwete ili tujue kwamba ndiye yule tuliyemchagua kwenye sanduku la kura
 
kitu kama hakipo na hakiwezekani kukileta hapa naona haina maana wakati jibu ni rahisi Rais kikwete hataweza kuikimbia nchi
 
usingizie watoto bwana, wale ni malaika. wanaozomea ni wendawazimu wenu wale mnaowalipa kufanyakazi hiyo. Siasa kwli noma yaani ukishindwa hoja unaanza zile za kitoto kitoto mara ohh wazomeeni, tutawashtaki kwa wananchi nani wewe unawashtaki kwa wananchi, mara hakuna kulala mpaka kieleweke, na usilale, Jakaya yupo kikazi zaidi siyo majungu.

nyanya tupu kichwani hapo
 
kukimbia matatizo sio mwisho wa matatizo.
wakati mwingine ni bora mara mia, ndio maana Balali alikimbia matatizo yalipomzidia , hahaaah katoweka na koba limejaa mahela kisha akatangazwa kafa, hahaaaah anaishi kwa amani huko Jersey akitumbua mahela yake.
mwambieni jamaa akimbie , akifika popote atoe taarifa kuwa yoyote anaweza kujikaimisha madaraka , na kuwa rais.
 
mwambieni jamaa akimbie, akifika popote atoe taarifa kuwa yoyote anaweza kujikaimisha madaraka , na kuwa rais.
Again,like i've said,sidhani kama atakubali.Anajua kama akikimbia basi ni kukiri hayo yote,sasa undhani akikimbia kwa namna hiyo msoga ndo pa kwenda?

Hivyo atapima na ataamuwa kubaki amalizie muda wake.

Utafanya nini?
 
Haya yanayoendelea sasa katika duru za siasa hapa Tanzania bara ni aibu kwa utawala wake kama rais wa Jamhuri ya Tanzania. Rushwa imeshamiri, serikali haikusanyi kodi ipasavyo, kila mtumishi wa umma anakusanya kwa nguvu zake zote kila raslimali iliyopaswa kutumika kwa umma.
Ukija kwenye nishati hasa umeme/stima utalia, kila siku ni takwimu za Megawati lakini hatujawahi kufurahia umeme mfululizo.
Madini huko ndio aibu aibu na fedheha kubwa.

Nimshauri Bwana Kikwete, mzaliwa wa Msoga, ikiwa anahisi nchi imemtumbukia nyongo asione haya kubwaga manyanga, kama hilo pia litamnyima usingizi, achimbe kama Balali kisha tutamtangaza kama walivyomtangaza Balali, na kwakua WaTanzania ni watu wanaoamini kila jambo kirahisi wataishia kusema Rest In Peace.
Ni ushauri wangu, kama umeshindwa Kimbia mzee.


Mpaka angekuwa na ujasiri wa kuwaangalia watanzania maskini kwa AIBU kwa kuwa hajawafanyia chochote cha Maana!
Lakini ujasiri wake ni wa kuwaangalia watz kwa Tabasamu!
 
Huyo Kikwete amewekwa na wananchi sasa unapomshauri akimbie nchi sielewi unamaanisha nini. Unaweza kufanya vizuri kama utawashauri wananchi wasiichague tena CCM 2015.

Mwita25 ni kama SITTA hivi....mnafiki!!!
 
Back
Top Bottom