Nina mpango wa kuwapandisha Meridianbet mahakamani, wamenidhulumu pesa nyingi sana. Mmiliki ambaye ni Waziri jiandae

basketball
Mimi pia mdau basketball betting uwa nadeposit mpka 2m na sijawahi pata hiyo Changamoto.
Cha kufanya nenda makao makuu yao ya meridian bet issue yako inaisha mara moja wala usiwe na wasiwasi meridian bet ni kampuni bora sana bongo kuliko zote
 
nimejisajiri mweridianbet 2017 ilikuwa ni kampuni yangu pendwa tena nikiwa mpiga debe wao kindaki ndaki.

ghafla 2019 yakaanza majanga,mara jumamosi mtandao haufanyi kazi??na ukirogwa uweke pesa siku hizo yaani jmosi,yanatokea kama ya dada mlalamikaji.

siku niliyoacha rasmi kufanya nao kazi ni pale nimeweka elfu 20 pesa hakuna ktk acc,napiga naambiwa wapigie provider wako,nawapigia voda wananambia pesa imekwenda tayari,nikawafata kwenye email nikawapasukia sana,na ahadi kwamba nakwenda kuwachafua mitandaoni,kinyonge wakarudisha pesa,nataka kuitoa pesa haitoki,napiga kuwauliza yule mpuuzi ananijibu simple tu ile sio benk ya kuhifadhia pesa,kwamba unaweka bila kubeti kisha unatoa.
kwa jeuri nikamjibu,
nikamwambia ndugu yangu mimi ni mwizi kuliko unavyodhani,naitoa hiyo pesa na faida juu subiri uone.nikachukua possible odds kama 2 hivi nikatia ile 20 ilaleta 49,nilivyowin nikamtumia mkeka inbox na kuitoa pesa yote.

baada ya wiki nalog in naambiwa umekosea password,kureset password nikaambiwa acc yako haipo,mpaka leo imebaki historia niko na akina 22bet,sportpesa wana kodi kubwa mno.

USHAURI,kesi yako iko serious zaidi ya hizi zangu,nenda ofisini kwao,kisha bod ya kamari kama wasipokuelewa.
inaonekana kuna mambo ya tamaa yameshafanyika,na watu wa huduma kwa wateja wanajua michezo ya baadhi ya staff wenzao wanafumbia kifua.
 
Nina mpango wa kuwapandisha meridianbet MAHAKAMANI, mmiliki ambae ni waziri jiandae,naomba ushauri,


HABARI WADAU;
kwa majina naitwa khadija, mtanzania na mteja wa muda mrefu wa kampuni tajwa hapo juu, kisa kilianza hivi,

mnamo tar 14 mwezi huu wa saba, nilideposit tshs mil 1, uthibitisho wa sms kutoka kampuni ya halolet nilipata kwamba pesa imekatwa,na imeenda kwa kampuni tajwa hapo juu, nikaamua kulogin kwa acc ya meridian ili niweze kuplace mkeka, nilikuwa nashida na mili 2 tu hivyo odd 2.

niliwasiliana na meridian muda huohuo wakaniomba info zangu, acc ID,sms ya uthibitisho na majina ya acc,nikawapatia wakanijibu nisubiri mnamo tar 15 wataweka pesa yangu.

tar 15 nikangalia hakuna pesa, nikasema ngoja nisubiri,tar 16 hakuna, nilikuwa naenda field nje ya dar kwa ajili ya kazi,nikasema ngoja niende nikirudi nitawapigia ,imefika tar 24 hakuna pesa,nikwasiliana nao tena , mara ya kwanza akapokea mwanamke tuliongea karibu dk 80 mimi ndio nilipiga majibu aliyonipa ni kwamba sina muamala wangu unaosubiri pesa. nilikasirika sana nikakata simu,nikapiga tena akapokea mwingine nikaongea nae eeeh ktk kueleweshana akasema kweli nimeuona,bado haujashugulikiwa, wakaniomba radhi waksema wanaweka.

nimesubiri wee,leo tar 29 nikasema isiwe case ngoja niwapigie tena, wakasema kwamba nina acc 2 zenye jina moja, hivyo waliweka kwenye hiyo acc nyingine, nikwaambia siitambui kwani nilireport acc ipi? wakakomaa kwamba wameweka kwenye acc hiyo nyingine, nikasema sawa, hiyo acc nalogin vipi? wakaniambia username yake ni namba yangu, nikwaomba paswd hawana,

lakini wakaniambia kwamba ninaweza kureset paswd kama namba ni yangu , nikafanya walivyonieleza nikalogin, nilivyologin hiyo pesa haipo na hata jina la acc ni "afg tza"

nikawapigia tena simu nikawambia mbona mnanidanganya? wakasema subiri tutakupigia hadi sasa hivi hawajapiga.

mimi nimechoka, nahitaji mwanasheria nguli, twende bodi ya michezo then mahakamani. nina imani wananitafutia utajiri wa maisha.

mwanasheria atakaekuja tutagawana nusu nusu ya pesa yote ya fidia tutakayopata.

karibuni kwa ushauri.

pia ninaomba namba za mh.waziri wa michezo kwa mwenye nazo tafadhali
Ngoja nikutumie namba ya Kibatala. Nahisi niliiona sehemu.
 
Uh - Oh!

Mkuu 'khadijah Mtalame', au ni 'Khadija mtanzania'?
Utatanishi unaanzia hapo kwenye majina yako. Inawezekana huko kwenye shughuli uliyoleta hapa, pia kukawa ni matatizo tupu!

Lakini hili tuliweke pembeni.

Hii stori yako mbona ni kizungumkuti?

Hii pesa ya kuchezea inapatikana wapi siku hizi? Bila shaka ndiyo sababu hata kukawa na kampuni za kitapeli kama hiyo unayojishughulisha nayo, kwa sababu kuna pesa za kuokota hovyohovyo tu, bila ya kuvuja jasho.

Najaribu kutafuta njia ya kukupa pole, lakini nashindwa, kwa sababu naona hii pesa, Tsh milioni moja, au siyo? Huna uchungu nayo hata kidogo.

Ninachoweza kukutakia ni matokeo mema katika kutafuta hiyo pesa nyingine ya kutupa, utakayopata toka kwa hao matapeli unaonuia kuwapeleka mahakamani. Hawa watakuwa na mahela mengi tu, kwani inaonyesha wanayaokota tu kama mchanga vile toka kwa watu kama wewe.

Hebu Kwanza: Mama anaupiga mwingi kwa kuibadilisha Tanzania kuwa kama Las Vegas hivi. Hadi 2025, nchi yetu hii itakuwa imeendelea sana kutokana na mafanikio ya kazi zake hizi; na za mawaziri wawekezaji kwenye miradi muhimu kama huu wa Meridian'.

Mungu Ibariki Tanzania.
Mil 1 unaona nyingi mwenyewe ?
Hivi vitu vina wenyewe kama wewe unaona ni nyingi wenzako wanaona kama buku tu,ukiona mtu ana deposit kiasi kama iko tambua ana pesa mara 100 ya hiyo
 
Kwanini ujatushirikisha kabla ya kucheza je ungepiga hela ungetusgirikisha?
nimeshindwa kukutofautisha na nguruwe. hoja kama huna cha kusaidia funga kopo. betting ni biashara kama nyingine. jadiri hoja kama ilivyoletwa. la sivyo huna msaada jamiiforum .
 
nimeshindwa kukutofautisha na nguruwe. hoja kama huna cha kusaidia funga kopo. betting ni biashara kama nyingine. jadiri hoja kama ilivyoletwa. la sivyo huna msaada jamiiforum .
Wewe kama nani au una ID ngapi hapa jf sija coment chochote kwako
 
nimeshindwa kukutofautisha na nguruwe. hoja kama huna cha kusaidia funga kopo. betting ni biashara kama nyingine. jadiri hoja kama ilivyoletwa. la sivyo huna msaada jamiiforum .
Rudi Milembe uendelee kupata tiba!
 
Mil 1 unaona nyingi mwenyewe ?
Hivi vitu vina wenyewe kama wewe unaona ni nyingi wenzako wanaona kama buku tu,ukiona mtu ana deposit kiasi kama iko tambua ana pesa mara 100 ya hiyo
Ni wangapi watu wa namna hiyo hapa Tanzania wanafanya hivyo!

Sasa utaanza stori nyingine, lakini kama unajua maana ya mstari huo niliouweka hapo juu usingeanza hizo hadithi nyingine unazozifikiria kichwani mwako.
 
Pesa yangu fulani niliipata baada ya wiki mbili.
Jamaa wasumbufu sana.
Kuanzia usiku saa 4 huwezi kutoa pesa, hata mchana ukitoa pesa inabidi uwacheki Facebook au uwapigie ndipo waupitishe muamala wako.
Playmaster hata ukikosea kudepose wanakuwekea unakokusudia within a minute ukiwapigia tu.
Ukitoa pesa ina toka ndani ya dk 1 tu.
Halafu kule unakandia watumishi wa LGAs' huku unabet... hovyo kabisa.
 
Hawa Meridianbet wanazingua Sanaa, nishawahi weka pesa kwa kupitia airtel nikaletewa SMS hela imetoka ila kwenye meridian haikufika, kuwapigia wakasema hamna muamala kutoka airte, pesa yangu ndo ikapotea kihivyo
 
Ni wangapi watu wa namna hiyo hapa Tanzania wanafanya hivyo!

Sasa utaanza stori nyingine, lakini kama unajua maana ya mstari huo niliouweka hapo juu usingeanza hizo hadithi nyingine unazozifikiria kichwani mwako.
Unatambua kuwa watu wanatumia hadi mil 50 kwa kamali tu?
 
Back
Top Bottom