Masikitiko: Utamaduni wa wizi na kukosa uaminifu kunazuia maendeleo yetu sana!

Kamundu

Platinum Member
Nov 22, 2006
6,609
8,753
Mimi ni dispora lakini matatizo yangu ni matatizo ya wengi hata kaka yangu ambaye yuko Tanzania anapata matatizo hayo hayo.

Naomba niweke utangulizi kwamba nayoyasema hapa sio kwa 100% ya Watanzania lakini ni utamaduni ambao unaturudisha nyuma

Najua kama jamii tuna mikasa mingi sana na mimi badala ya kusema ya watu niseme yale ambayo nina uhakika nao

Diaspora tufauti wa wengi wanavyo amini ni wengi wetu ni Watanzania wa kawaida ambao tunatafuta pesa na kuinua maisha yetu. Mimi mfano nimepigika sana kwanza nimekaa hapa US kwa miaka 25. Ilinichukuwa miaka 12 bila kumuona baba yangu mzazi kuanzia 1997 mpaka 2009.

Tena bahati mbaya nimeshanunua ticket ya kwenda Tanzania miaka ile kaka yangu akafariki hivyo baada ya miaka 12 nilimkuta mzee wangu kwa masikitiko makubwa. Nimejipiga ndugu zangu sana nikafanikiwa kumaliza mpaka degee ingawa kwasababu ya kufanya kazi ilinichukuwa mpaka 2006 kukamilisha na kupata shahada ya fedha.

Nimefanya kazi za mabox za kila aina mpaka sasa nimekuwa consultant kwenye kampuni kubwa sana na nafanya kazi na hospital. Naelezea hili ili ujue kwamba watu wanatokea mbali na sio kwa kujionyesha au kulalamika. Naomba nitoe mifano michache jinsi gani uaminifu wa wetu unaturudisha nyuma:

1. Nina shamba Bagamoyo kubwa wale watu ambao wameniuzia shamba ndiyo haohao wanarudi tena na kujaribu kuwauzia wengine. Kibaya zaidi hawana uoga na wanaona ni sawa tu.

2. Kuna mzee nilimweka shambani kwangu nikamjengea nyumba, nika ajiri watu watu wamlimie eka 4, nikamnunulia pikipiki ili aweze kufanya shughuli zake lakini kwanza amekuwa akiiba bati za nyumba ambayo anakaa yeye anauza halafu anasingizia wezi. Nilikubali kutengeneza nyumba mara ya kwanza, ya pili, ya tatu na ya ya nne. Baada ya kuuza mabati mara nne nikaweka mtego na polisi wa kule bagamoyo bahati nzuri OCD alikuwa classmate watu wakamshika yule mzee akiiba mabati. Pikipiki yangu ambayo nilimpa nikakuta ameenda kuweka rehani na kapewa 100,000 wakati nilitumia 900,000 kununua.

3. Kuna fundi ambaye wamenipa nyumbani uninio anisaidie na wakaniambia ni mwaminifu lakini cha ajabu kazi ambayo ilikuwa inahitaji bati 13 aliweka bati 22 mpaka nilipouliza ndiyo akajirudi na kusema kazi inahitaji bati 13.

4. Tusisema watu wa chini tu nilipeleka kontena 2013 kwa mpango wa kufungua clinic ndogo thamani ya vitu ilikuwa $98,000 lakini nilipata kwa $20,000. Basi nikatuma list Tanzania ili nijue gharama zote za kodi kabla ya kupeleka vitu nikaambiwa hakuna kodi ni usafiri tu na storage ya siiku moja. Mzigo ukatuma ukafika Tanzania ghafla TRA haohao wakaja na kunitaka nilipe tsh 15M au wataifishe vitu vyote.

5. Mwaka jana Oct 2022 nimeenda Tanzania na nilihitaji NIDA. Yaani kwasababu jamaa nilimpa pesa kidogo ya kuifanya haraka nilipata card yangu ndani ya wiki wakati wazazi wangu nikaja kugundua walikuwa hawajapata card zao kwa zaidi ya miaka 2. Wazazi wangu ambao wanahitaji NIDA zaidi yangu walizungushwa miaka zaidi ya miwili mpaka nilivyofika Tanzania na baada ya mimi nao walipewa lakini kwasababu ya uwezo na kujuana.

Jamii yetu haitakiwi kuwa hivi. Kuna pesa nyingi sana vitu vingi sana hatuwezi kufanya au hata kusaidia kutokana na uaminifu. Rafiki yangu Professor youko Mississippi alitaka kuleta wanafunzi wa udaktari wa chuo kikuu muhimbili kwa semina akashidwa kwasababu Professor wa muhimbili mkuu wa kitengo alimuomba pesa ambayo hakuwa nayo. Mimi hapa mwenyewe nashidwa hata kupeleka vitu tena kwasababu vitu vikifika Tanzania ni maneno mengine.

Yaani kwa ushauri wangu kusaidia nchi nunua bond/TRESURY BILLS za Tanzania na hiyo pesa itaenda kwenye miradi ya serikali na utapata 10%-12% kwa mwaka lakini kufanya miradi nchini Tanzania ni ngumu sana sana kutokana na utamaduni wa wizi na udanganyifu
 
Ndugu Kamundu , uliyoyaandika ni kweli tupu.
Kongole kwa kuamua kulisemea hili.

Uaminifu ni tatizo kubwa sana Tanzania ambalo chanzo chake kikuu ni kutotimiza wajibu kwa wazazi/walezi, serikali, viongozi wa dini pamoja na mitaala mibovu ya elimu yetu na vyombo vya kusimamia sheria vilivyo butu.

Mimi binafsi kwa kuwa nililelewa katika malezi ya kidini sana,nilikataa kufanya kazi yoyote ya kuajiriwa kwani sikuwa tayari kufanya mambo kinyume na mafunzo niliyopewa kifamilia na kidini.
 
Mimi ni dispora lakini matatizo yangu ni matatizo ya wengi hata kaka yangu ambaye yuko Tanzania anapata matatizo hayo hayo.

Naomba niweke utangulizi kwamba nayoyasema hapa sio kwa 100% ya Watanzania lakini ni utamaduni ambao unaturudisha nyuma

Najua kama jamii tuna mikasa mingi sana na mimi badala ya kusema ya watu niseme yale ambayo nina uhakika nao

Diaspora tufauti wa wengi wanavyo amini ni wengi wetu ni Watanzania wa kawaida ambao tunatafuta pesa na kuinua maisha yetu. Mimi mfano nimepigika sana kwanza nimekaa hapa US kwa miaka 25. Ilinichukuwa miaka 12 bila kumuona baba yangu mzazi kuanzia 1997 mpaka 2009.

Tena bahati mbaya nimeshanunua ticket ya kwenda Tanzania miaka ile kaka yangu akafariki hivyo baada ya miaka 12 nilimkuta mzee wangu kwa masikitiko makubwa. Nimejipiga ndugu zangu sana nikafanikiwa kumaliza mpaka degee ingawa kwasababu ya kufanya kazi ilinichukuwa mpaka 2006 kukamilisha na kupata shahada ya fedha.

Nimefanya kazi za mabox za kila aina mpaka sasa nimekuwa consultant kwenye kampuni kubwa sana na nafanya kazi na hospital. Naelezea hili ili ujue kwamba watu wanatokea mbali na sio kwa kujionyesha au kulalamika. Naomba nitoe mifano michache jinsi gani uaminifu wa wetu unaturudisha nyuma:

1. Nina shamba Bagamoyo kubwa wale watu ambao wameniuzia shamba ndiyo haohao wanarudi tena na kujaribu kuwauzia wengine. Kibaya zaidi hawana uoga na wanaona ni sawa tu.

2. Kuna mzee nilimweka shambani kwangu nikamjengea nyumba, nika ajiri watu watu wamlimie eka 4, nikamnunulia pikipiki ili aweze kufanya shughuli zake lakini kwanza amekuwa akiiba bati za nyumba ambayo anakaa yeye anauza halafu anasingizia wezi. Nilikubali kutengeneza nyumba mara ya kwanza, ya pili, ya tatu na ya ya nne. Baada ya kuuza mabati mara nne nikaweka mtego na polisi wa kule bagamoyo bahati nzuri OCD alikuwa classmate watu wakamshika yule mzee akiiba mabati. Pikipiki yangu ambayo nilimpa nikakuta ameenda kuweka rehani na kapewa 100,000 wakati nilitumia 900,000 kununua.

3. Kuna fundi ambaye wamenipa nyumbani uninio anisaidie na wakaniambia ni mwaminifu lakini cha ajabu kazi ambayo ilikuwa inahitaji bati 13 aliweka bati 22 mpaka nilipouliza ndiyo akajirudi na kusema kazi inahitaji bati 13.

4. Tusisema watu wa chini tu nilipeleka kontena 2013 kwa mpango wa kufungua clinic ndogo thamani ya vitu ilikuwa $98,000 lakini nilipata kwa $20,000. Basi nikatuma list Tanzania ili nijue gharama zote za kodi kabla ya kupeleka vitu nikaambiwa hakuna kodi ni usafiri tu na storage ya siiku moja. Mzigo ukatuma ukafika Tanzania ghafla TRA haohao wakaja na kunitaka nilipe tsh 15M au wataifishe vitu vyote.

5. Mwaka jana Oct 2022 nimeenda Tanzania na nilihitaji NIDA. Yaani kwasababu jamaa nilimpa pesa kidogo ya kuifanya haraka nilipata card yangu ndani ya wiki wakati wazazi wangu nikaja kugundua walikuwa hawajapata card zao kwa zaidi ya miaka 2. Wazazi wangu ambao wanahitaji NIDA zaidi yangu walizungushwa miaka zaidi ya miwili mpaka nilivyofika Tanzania na baada ya mimi nao walipewa lakini kwasababu ya uwezo na kujuana.

Jamii yetu haitakiwi kuwa hivi. Kuna pesa nyingi sana vitu vingi sana hatuwezi kufanya au hata kusaidia kutokana na uaminifu. Rafiki yangu Professor youko Mississippi alitaka kuleta wanafunzi wa udaktari wa chuo kikuu muhimbili kwa semina akashidwa kwasababu Professor wa muhimbili mkuu wa kitengo alimuomba pesa ambayo hakuwa nayo. Mimi hapa mwenyewe nashidwa hata kupeleka vitu tena kwasababu vitu vikifika Tanzania ni maneno mengine.

Yaani kwa ushauri wangu kusaidia nchi nunua bond/TRESURY BILLS za Tanzania na hiyo pesa itaenda kwenye miradi ya serikali na utapata 10%-12% kwa mwaka lakini kufanya miradi nchini Tanzania ni ngumu sana sana kutokana na utamaduni wa wizi na udanganyifu
Ndio maana awo waliokuwa awampendi uncle magu,
 
Ndugu Kamundu , uliyoyaandika ni kweli tupu.
Kongole kwa kuamua kulisemea hili.

Uaminifu ni tatizo kubwa sana Tanzania ambalo chanzo chake kikuu ni kutotimiza wajibu kwa wazazi/walezi, serikali, viongozi wa dini pamoja na mitaala mibovu ya elimu yetu na vyombo vya kusimamia sheria vilivyo butu.

Mimi binafsi kwa kuwa nililelewa katika malezi ya kidini sana,nilikataa kufanya kazi yoyote ya kuajiriwa kwani sikuwa tayari kufanya mambo kinyume na mafunzo niliyopewa kifamilia na kidini.
Kwa hiyo ulianzisha dhehebu lako ili upige pesa za wajinga. Una tofauti gani na hao waajiriwa mafisadi?
 
Issue hapo ni mifumo inayotoa mwanya wa kuendelea kwa tabia ovu mkuu.

Sasa unadhani binadam unaweza wabadilisha bila mifumo inayoadhibu tabia za namna hiyo?

Hao ndugu zako ni zao lile lile la mifumo mibaya.. na wewe umekiri umekuja hapa na umetoa rushwa upatiwe nida chap na haraka.., zao lile lile, manake ungekuwa huku ungefanana na hii mifumo tu.

Pole mkuu.
 
Mimi ni dispora lakini matatizo yangu ni matatizo ya wengi hata kaka yangu ambaye yuko Tanzania anapata matatizo hayo hayo.

Naomba niweke utangulizi kwamba nayoyasema hapa sio kwa 100% ya Watanzania lakini ni utamaduni ambao unaturudisha nyuma

Najua kama jamii tuna mikasa mingi sana na mimi badala ya kusema ya watu niseme yale ambayo nina uhakika nao

Diaspora tufauti wa wengi wanavyo amini ni wengi wetu ni Watanzania wa kawaida ambao tunatafuta pesa na kuinua maisha yetu. Mimi mfano nimepigika sana kwanza nimekaa hapa US kwa miaka 25. Ilinichukuwa miaka 12 bila kumuona baba yangu mzazi kuanzia 1997 mpaka 2009.

Tena bahati mbaya nimeshanunua ticket ya kwenda Tanzania miaka ile kaka yangu akafariki hivyo baada ya miaka 12 nilimkuta mzee wangu kwa masikitiko makubwa. Nimejipiga ndugu zangu sana nikafanikiwa kumaliza mpaka degee ingawa kwasababu ya kufanya kazi ilinichukuwa mpaka 2006 kukamilisha na kupata shahada ya fedha.

Nimefanya kazi za mabox za kila aina mpaka sasa nimekuwa consultant kwenye kampuni kubwa sana na nafanya kazi na hospital. Naelezea hili ili ujue kwamba watu wanatokea mbali na sio kwa kujionyesha au kulalamika. Naomba nitoe mifano michache jinsi gani uaminifu wa wetu unaturudisha nyuma:

1. Nina shamba Bagamoyo kubwa wale watu ambao wameniuzia shamba ndiyo haohao wanarudi tena na kujaribu kuwauzia wengine. Kibaya zaidi hawana uoga na wanaona ni sawa tu.

2. Kuna mzee nilimweka shambani kwangu nikamjengea nyumba, nika ajiri watu watu wamlimie eka 4, nikamnunulia pikipiki ili aweze kufanya shughuli zake lakini kwanza amekuwa akiiba bati za nyumba ambayo anakaa yeye anauza halafu anasingizia wezi. Nilikubali kutengeneza nyumba mara ya kwanza, ya pili, ya tatu na ya ya nne. Baada ya kuuza mabati mara nne nikaweka mtego na polisi wa kule bagamoyo bahati nzuri OCD alikuwa classmate watu wakamshika yule mzee akiiba mabati. Pikipiki yangu ambayo nilimpa nikakuta ameenda kuweka rehani na kapewa 100,000 wakati nilitumia 900,000 kununua.

3. Kuna fundi ambaye wamenipa nyumbani uninio anisaidie na wakaniambia ni mwaminifu lakini cha ajabu kazi ambayo ilikuwa inahitaji bati 13 aliweka bati 22 mpaka nilipouliza ndiyo akajirudi na kusema kazi inahitaji bati 13.

4. Tusisema watu wa chini tu nilipeleka kontena 2013 kwa mpango wa kufungua clinic ndogo thamani ya vitu ilikuwa $98,000 lakini nilipata kwa $20,000. Basi nikatuma list Tanzania ili nijue gharama zote za kodi kabla ya kupeleka vitu nikaambiwa hakuna kodi ni usafiri tu na storage ya siiku moja. Mzigo ukatuma ukafika Tanzania ghafla TRA haohao wakaja na kunitaka nilipe tsh 15M au wataifishe vitu vyote.

5. Mwaka jana Oct 2022 nimeenda Tanzania na nilihitaji NIDA. Yaani kwasababu jamaa nilimpa pesa kidogo ya kuifanya haraka nilipata card yangu ndani ya wiki wakati wazazi wangu nikaja kugundua walikuwa hawajapata card zao kwa zaidi ya miaka 2. Wazazi wangu ambao wanahitaji NIDA zaidi yangu walizungushwa miaka zaidi ya miwili mpaka nilivyofika Tanzania na baada ya mimi nao walipewa lakini kwasababu ya uwezo na kujuana.

Jamii yetu haitakiwi kuwa hivi. Kuna pesa nyingi sana vitu vingi sana hatuwezi kufanya au hata kusaidia kutokana na uaminifu. Rafiki yangu Professor youko Mississippi alitaka kuleta wanafunzi wa udaktari wa chuo kikuu muhimbili kwa semina akashidwa kwasababu Professor wa muhimbili mkuu wa kitengo alimuomba pesa ambayo hakuwa nayo. Mimi hapa mwenyewe nashidwa hata kupeleka vitu tena kwasababu vitu vikifika Tanzania ni maneno mengine.

Yaani kwa ushauri wangu kusaidia nchi nunua bond/TRESURY BILLS za Tanzania na hiyo pesa itaenda kwenye miradi ya serikali na utapata 10%-12% kwa mwaka lakini kufanya miradi nchini Tanzania ni ngumu sana sana kutokana na utamaduni wa wizi na udanganyifu
Mkuu Kamundu , nimeguswa na kisa chako, testimonials kama hizi zitasaidia wengi. Mimi pia ni Diaspora wa UK na US na nilipanga kuanzisha TV program ya Tanzania Diaspora ili kuzi tap testimonials za diaspora exposure huko walipo kulisaidia taifa letu. Diaspora wa India wanaisaidia sana nchi yao.

Diaspora wetu ni wao na familia zao tuu!. Nikiwa US nili visit UN, nikashangaa kukuta Waganda na Wakenya wengi, Watanzania wachache!. Nikaenda ubalozini kwetu UN na kupokelewa na yule shemeji yetu, wife wa mwana JF mwenzetu pale ubalozini New York, nikaomba kumsalimia Balozi, akanyanyua simu kuzungumza na mtu nikajibiwa Balozi yuko very tight hana nafasi kabisa kwa wiki hii yote labda next week!.

Next day nikahudhuria event fulani, nikamuona Balozi nikaenda kumsalimia, kumbe ananifahamu!, akanichangamkia na kuniambia Watanzania mnapofika hapa New York ni vizuri kuja kujitambulisha ubalozini, nikamwambia jana nimekuja nikaelezwa you are busy!. Balozi alishangaa!. Akasema jana yake alikuwa idle tuu!. Tukazungumza kidogo na nikamuuliza mbona hapa UN Watanzania ni wachache wakati wenzetu ni wengi?. Akanijibu Watanzania ni wavivu hawaombi kazi UN!.

Nikagundua kumbe kunapotokea opening UN, taarifa inatumwa MFA, ikifika kule inakuwa circulated serikalini tuu, kwa wenzetu Kenya na Uganda wanaichapisha kwenye local media zao hivyo wengi wanaomba, wanakuwa more compepetive wanapata wengi zaidi.

Kwa kadri wenzetu wanavyopata ndvyo wanavyo vutana!. Hebu angalia idadi ya Kenyans wenye decent jobs compared na Watanzania!. https://www.jamiiforums.com/threads...fanya-nini-cha-kuonekana-huko-walipo.2051726/

Mchakato wa TV Program ukiwa tayari, naomba utoe ushirikiano ili muutumie uzoefu wenu kulisaidia taifa na sisi wa huku tutakupa uzoefu ukitaka kuwekeza bongo lazima uwe na usimamizi madhubuti zaidi ya kutegemea ndugu tuu!.
Nimeguswa sana.

P
 
Mimi ni dispora lakini matatizo yangu ni matatizo ya wengi hata kaka yangu ambaye yuko Tanzania anapata matatizo hayo hayo.

Naomba niweke utangulizi kwamba nayoyasema hapa sio kwa 100% ya Watanzania lakini ni utamaduni ambao unaturudisha nyuma

Najua kama jamii tuna mikasa mingi sana na mimi badala ya kusema ya watu niseme yale ambayo nina uhakika nao

Diaspora tufauti wa wengi wanavyo amini ni wengi wetu ni Watanzania wa kawaida ambao tunatafuta pesa na kuinua maisha yetu. Mimi mfano nimepigika sana kwanza nimekaa hapa US kwa miaka 25. Ilinichukuwa miaka 12 bila kumuona baba yangu mzazi kuanzia 1997 mpaka 2009.

Tena bahati mbaya nimeshanunua ticket ya kwenda Tanzania miaka ile kaka yangu akafariki hivyo baada ya miaka 12 nilimkuta mzee wangu kwa masikitiko makubwa. Nimejipiga ndugu zangu sana nikafanikiwa kumaliza mpaka degee ingawa kwasababu ya kufanya kazi ilinichukuwa mpaka 2006 kukamilisha na kupata shahada ya fedha.

Nimefanya kazi za mabox za kila aina mpaka sasa nimekuwa consultant kwenye kampuni kubwa sana na nafanya kazi na hospital. Naelezea hili ili ujue kwamba watu wanatokea mbali na sio kwa kujionyesha au kulalamika. Naomba nitoe mifano michache jinsi gani uaminifu wa wetu unaturudisha nyuma:

1. Nina shamba Bagamoyo kubwa wale watu ambao wameniuzia shamba ndiyo haohao wanarudi tena na kujaribu kuwauzia wengine. Kibaya zaidi hawana uoga na wanaona ni sawa tu.

2. Kuna mzee nilimweka shambani kwangu nikamjengea nyumba, nika ajiri watu watu wamlimie eka 4, nikamnunulia pikipiki ili aweze kufanya shughuli zake lakini kwanza amekuwa akiiba bati za nyumba ambayo anakaa yeye anauza halafu anasingizia wezi. Nilikubali kutengeneza nyumba mara ya kwanza, ya pili, ya tatu na ya ya nne. Baada ya kuuza mabati mara nne nikaweka mtego na polisi wa kule bagamoyo bahati nzuri OCD alikuwa classmate watu wakamshika yule mzee akiiba mabati. Pikipiki yangu ambayo nilimpa nikakuta ameenda kuweka rehani na kapewa 100,000 wakati nilitumia 900,000 kununua.

3. Kuna fundi ambaye wamenipa nyumbani uninio anisaidie na wakaniambia ni mwaminifu lakini cha ajabu kazi ambayo ilikuwa inahitaji bati 13 aliweka bati 22 mpaka nilipouliza ndiyo akajirudi na kusema kazi inahitaji bati 13.

4. Tusisema watu wa chini tu nilipeleka kontena 2013 kwa mpango wa kufungua clinic ndogo thamani ya vitu ilikuwa $98,000 lakini nilipata kwa $20,000. Basi nikatuma list Tanzania ili nijue gharama zote za kodi kabla ya kupeleka vitu nikaambiwa hakuna kodi ni usafiri tu na storage ya siiku moja. Mzigo ukatuma ukafika Tanzania ghafla TRA haohao wakaja na kunitaka nilipe tsh 15M au wataifishe vitu vyote.

5. Mwaka jana Oct 2022 nimeenda Tanzania na nilihitaji NIDA. Yaani kwasababu jamaa nilimpa pesa kidogo ya kuifanya haraka nilipata card yangu ndani ya wiki wakati wazazi wangu nikaja kugundua walikuwa hawajapata card zao kwa zaidi ya miaka 2. Wazazi wangu ambao wanahitaji NIDA zaidi yangu walizungushwa miaka zaidi ya miwili mpaka nilivyofika Tanzania na baada ya mimi nao walipewa lakini kwasababu ya uwezo na kujuana.

Jamii yetu haitakiwi kuwa hivi. Kuna pesa nyingi sana vitu vingi sana hatuwezi kufanya au hata kusaidia kutokana na uaminifu. Rafiki yangu Professor youko Mississippi alitaka kuleta wanafunzi wa udaktari wa chuo kikuu muhimbili kwa semina akashidwa kwasababu Professor wa muhimbili mkuu wa kitengo alimuomba pesa ambayo hakuwa nayo. Mimi hapa mwenyewe nashidwa hata kupeleka vitu tena kwasababu vitu vikifika Tanzania ni maneno mengine.

Yaani kwa ushauri wangu kusaidia nchi nunua bond/TRESURY BILLS za Tanzania na hiyo pesa itaenda kwenye miradi ya serikali na utapata 10%-12% kwa mwaka lakini kufanya miradi nchini Tanzania ni ngumu sana sana kutokana na utamaduni wa wizi na udanganyifu
Sikupingi apo ulipouziwa shamba na wenyeji wakaanza kuliuza tena
Juzi kati mzee alinambia ogopa sana watu wanyonge wakikuuzia kitu kma ivo shamba au kiwanja wanakirudia na kuuza kwa wengine hlf wala hawajali ata kma makabidhiano yapo

Mda mwingine watu wanyonge wanajidhalilisha sanaaa
 
Mkuu bado hujatuma pesa kwenu ndugu zako kabisa wakujengee nyumba ya maana, ukija kurudi tz unakuta nyumba uliyojengewa imekaa upande na haizidi sh mil 5. Wakati wewe ulituma 40mil Na huna cha kuwafanya.

Kweli diaspora mnapitia magumu sana.

Ushauri diaspora mkanunuwe viwanja wenyewe mkiwa likizo, mjenge wenyewe mkiwa likizo.hizo nyumba mpangishe pesa wapangaji walipe bank.

Au nunuweni viwanja mkiwa likizo tafuta hati mtauzaga huko baadae.

Hii ndio biashara pekee inayofaaa tofauti na hapo mtakufa kwa pressure.

Kwakweli nawaoneaga huruma sana jitihada mnazofanya ila mwisho ni maumivu.
 
Mkuu Kamundu , nimeguswa na kisa chako, testimonials kama hizi zitasaidia wengi. Mimi pia ni Diaspora wa UK na US na nilipanga kuanzisha TV program ya Tanzania Diaspora ili kuzi tap testimonials za diaspora exposure huko walipo kulisaidia taifa letu. Diaspora wa India wanaisaidia sana nchi yao.

Diaspora wetu ni wao na familia zao tuu!. Nikiwa US nili visit UN, nikashangaa kukuta Waganda na Wakenya wengi, Watanzania wachache!. Nikaenda ubalozini kwetu UN na kupokelewa na yule shemeji yetu, wife wa mwana JF mwenzetu pale ubalozini New York, nikaomba kumsalimia Balozi, akanyanyua simu kuzungumza na mtu nikajibiwa Balozi yuko very tight hana nafasi kabisa kwa wiki hii yote labda next week!.

Next day nikahudhuria event fulani, nikamuona Balozi nikaenda kumsalimia, kumbe ananifahamu!, akanichangamkia na kuniambia Watanzania mnapofika hapa New York ni vizuri kuja kujitambulisha ubalozini, nikamwambia jana nimekuja nikaelezwa you are busy!. Balozi alishangaa!. Akasema jana yake alikuwa idle tuu!. Tukazungumza kidogo na nikamuuliza mbona hapa UN Watanzania ni wachache wakati wenzetu ni wengi?. Akanijibu Watanzania ni wavivu hawaombi kazi UN!.

Nikagundua kumbe kunapotokea opening UN, taarifa inatumwa MFA, ikifika kule inakuwa circulated serikalini tuu, kwa wenzetu Kenya na Uganda wanaichapisha kwenye local media zao hivyo wengi wanaomba, wanakuwa more compepetive wanapata wengi zaidi.

Kwa kadri wenzetu wanavyopata ndvyo wanavyo vutana!. Hebu angalia idadi ya Kenyans wenye decent jobs compared na Watanzania!. https://www.jamiiforums.com/threads...fanya-nini-cha-kuonekana-huko-walipo.2051726/

Mchakato wa TV Program ukiwa tayari, naomba utoe ushirikiano ili muutumie uzoefu wenu kulisaidia taifa na sisi wa huku tutakupa uzoefu ukitaka kuwekeza bongo lazima uwe na usimamizi madhubuti zaidi ya kutegemea ndugu tuu!.
Nimeguswa sana.

P
Tuko pamoja bro
 
Hata hizi kelele unasikia watu wanalalamika kwamba wahindi ni wanyonyaji sijui wachina wanatesa waajiriwa wao watanzania ni kwa sababu sisi wabongo ni wavivu na wezi.

Tunapenda shortcut bila kufanya kazi.

Sasa imagine mtu amekopa benki amefungua mradi ameajiri vijana wafanye kazi warudishe mkopo waanze kutengeneza faida nyie mnamuibia ili ashindwe kulipa loan afilisiwe, mumkimbie kwa sababu sio tatizo lenu.

Na tatizo sio maslahi kidogo. Kuna watu wengi tu wana mishahara 3+ M na bado wanacheza madili kumuibia mwajiri wao.

Inasikitisha na kuhuzunisha sana. N bahati mbaya, wezi ndio huonekana wajanja.
 
Kwa nini hukutuma hivyo vitu mwaka 2016 - 2020 wakati mwamba Magufuli akiwa madarakani? Usingeona huo upuuzi kabisa, ndiyo maana nchi iliingia uchumi wa kati.
Usilolijua ni usiku wa giza chief. Hakuna kipind Watu wamepiga pale bandarin kama enzi ya mzee baba ndio maana kila siku alikuwa yeye na wazir mkuu haach kwenda pale.
 
Suluhisho la yote haya ni Katiba Mpya.Kukiwa na Mahakama huru Polisi huru vyombo vya habari huru uwazi na uwajibikaji wa jamii na Taasisi zake utaongezeka, hata hao wezi na wadokozi watafungwa kwasababu Mifumo itaanza kuwajibika,pia uchumi utakua hizo njaa kali zitapungua.

Pole sana Kiongozi kwa yaliyokukuta, tuunganishe nguvu kudai Katiba Mpya.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom