Melancholic
JF-Expert Member
- Oct 12, 2018
- 1,831
- 3,063
Habari za asubuhi ndugu zangu awali ya yote tumshukuru Mungu kwa kutuamsha salama.
nahitaji ushauri ndugu zangu ni hivi, Siku ya jumamosi nilitafuta hawa vijana wanaouza simu online, kuna simu niliipenda kwa bahati mbaya baada ya kumpigia muhusika nilikuta imeshatoka.
Bac muhusika akaniahidi kupiga simu ofisi ndogo ya kariakoo kwa siku ya kesho ambayo ilikuwa jumamosi ili kunichekia stool kwa bei tuliokuwa tumekubaliana. Ila yeye ofisi yake ipo makumbusho.
Ni kweli ilipofika jumamosi asubuhi muhusika alinitafuta akaniambia simu niliyokuwa nikihitaji imepatikana ila kaongea na mtu wa stool kwamba yeye ndio kanituma nimchukulie hiyo simu kwa bei ya 160k kwamba anamchukulia mdogo wake,
Tukaelewana basi akanitumia namba ya mtu wa stool tukawasiliana nikamuelekeza hivo kwamba jamaa kaniagiza simu aina flani nimpelekee makumbusho na nimpe kiasi cha 160k,
bac huyu mtu wa karikoo akakubali ila akaniambia niende na mfuko ili bosi asistukie mchezo nkamwambia poa.
Na hapo tulikubaliana wanipe fullbox kabisa.
Bac nikaenda kariakoo maeneo ya mkombozi bank tukakutana na jamaa wa stool akaniomba mfuko na hela hapo ndipo nilipofanya kosa sijui jamaa huwa wanatumia madawa au vp aisee amuwezi amini yule jamaa alinichota akili nikamkabidhi pesa yote 160k na mfuko.
Tukaenda kwenye ghorofa flani akaniambia nimsubili kwa nje baada ya dakika 5 ndio faham zinarudi kwamba nishaibiwa na kweli jamaa alivyotokomea akurudi.
Bac nikawapigia simu awakupokea wote wawili hapo nkajua tayari nishakaribishwa mjini. Bac kuna watu wakanishauri niende msimbazi polisi kuchukua rb ni kweli nikaenda msimbazi nikawaelezea jinsi tukio lilivyotokea askari wakaniambia wao awawezi kunipa rb sababu huo ni wizi wa kuaminiwa inamaana kwamba mimi nilimuamini mtuhumiwa wangu nikamkabidhi pesa hivyo niende mahakamani kufungua kesi ya madai.
Bac nikaondoka zangu ni sijamwambia mtu yoyote kuhusu hilo tukio. Ndio nimeona nililete kwenu mnisaidie ni vp naweza kuwapata watuhumiwa wangu maana awajazima simu wanapatikana muda wote ila simu yangu ndio awapokei namimi pia sijataka kuwatafuta tena na jana kuna mmoja alinipigia sikupokea coz nilikuwa mbali na simu ila baadae nikamchek akapokea halafu akasema atanitafuta ndio ajanitafuta mpaka sasa.
Mnaweza kuniona mjinga lakini kiukweli kwa muda ule fahamu zilikuwa zimefungwa sijui ni dawa au ni nini? Ila ndio hivo nahitaji ushauri wa kuwakamata hawa watu maana simu zao zinapatikana muda wote.
Ahsanteni na karibuni kwa mchango wenu.
nahitaji ushauri ndugu zangu ni hivi, Siku ya jumamosi nilitafuta hawa vijana wanaouza simu online, kuna simu niliipenda kwa bahati mbaya baada ya kumpigia muhusika nilikuta imeshatoka.
Bac muhusika akaniahidi kupiga simu ofisi ndogo ya kariakoo kwa siku ya kesho ambayo ilikuwa jumamosi ili kunichekia stool kwa bei tuliokuwa tumekubaliana. Ila yeye ofisi yake ipo makumbusho.
Ni kweli ilipofika jumamosi asubuhi muhusika alinitafuta akaniambia simu niliyokuwa nikihitaji imepatikana ila kaongea na mtu wa stool kwamba yeye ndio kanituma nimchukulie hiyo simu kwa bei ya 160k kwamba anamchukulia mdogo wake,
Tukaelewana basi akanitumia namba ya mtu wa stool tukawasiliana nikamuelekeza hivo kwamba jamaa kaniagiza simu aina flani nimpelekee makumbusho na nimpe kiasi cha 160k,
bac huyu mtu wa karikoo akakubali ila akaniambia niende na mfuko ili bosi asistukie mchezo nkamwambia poa.
Na hapo tulikubaliana wanipe fullbox kabisa.
Bac nikaenda kariakoo maeneo ya mkombozi bank tukakutana na jamaa wa stool akaniomba mfuko na hela hapo ndipo nilipofanya kosa sijui jamaa huwa wanatumia madawa au vp aisee amuwezi amini yule jamaa alinichota akili nikamkabidhi pesa yote 160k na mfuko.
Tukaenda kwenye ghorofa flani akaniambia nimsubili kwa nje baada ya dakika 5 ndio faham zinarudi kwamba nishaibiwa na kweli jamaa alivyotokomea akurudi.
Bac nikawapigia simu awakupokea wote wawili hapo nkajua tayari nishakaribishwa mjini. Bac kuna watu wakanishauri niende msimbazi polisi kuchukua rb ni kweli nikaenda msimbazi nikawaelezea jinsi tukio lilivyotokea askari wakaniambia wao awawezi kunipa rb sababu huo ni wizi wa kuaminiwa inamaana kwamba mimi nilimuamini mtuhumiwa wangu nikamkabidhi pesa hivyo niende mahakamani kufungua kesi ya madai.
Bac nikaondoka zangu ni sijamwambia mtu yoyote kuhusu hilo tukio. Ndio nimeona nililete kwenu mnisaidie ni vp naweza kuwapata watuhumiwa wangu maana awajazima simu wanapatikana muda wote ila simu yangu ndio awapokei namimi pia sijataka kuwatafuta tena na jana kuna mmoja alinipigia sikupokea coz nilikuwa mbali na simu ila baadae nikamchek akapokea halafu akasema atanitafuta ndio ajanitafuta mpaka sasa.
Mnaweza kuniona mjinga lakini kiukweli kwa muda ule fahamu zilikuwa zimefungwa sijui ni dawa au ni nini? Ila ndio hivo nahitaji ushauri wa kuwakamata hawa watu maana simu zao zinapatikana muda wote.
Ahsanteni na karibuni kwa mchango wenu.