Nina maumivu sana jamani, nahitaji msaada wenu

Nina maumivu sana jamani, nahitaji msaada wenu

mie ukiniwekea mapozi siku moja tu ya masaa 24 ndo bas !yaan sikusumbukii hata ! kha !wanaume walivyojazana namna hii nakuliliaje sasa
We mkuu kuna yule mwenza unakutana nae anakuzidi kila kitu kuanzia maufundi , midekezo hadi mkwanja ndugu usiombe yakukute utaona kila kitu hakiendi, ujanja wote unapotea sema ule uzoefu tu ndo unasaidia.
 
We mkuu kuna yule mwenza unakutana nae anakuzidi kila kitu kuanzia maufundi , midekezo hadi mkwanja ndugu usiombe yakukute utaona kila kitu hakiendi, ujanja wote unapotea sema ule uzoefu tu ndo unasaidia.



hahahahah kweli lazima ulie aisee ! ishu hapa kila mtu anaingia kwenye mapenz kwa angle yake!mie ht umenijengea nyumba ukinitibua nakisanua !
 
huyo kupata wa type yake, japo nakwambia kwa uoga.
 
Habari zenu,

Nilikua na mpenzi ambae tumedumu kwa miezi minne sote tulipendana kwa dhati na kwa kipindi hicho yeye ndio alikua ameanza kazi hivyo mshahara alikua hajaanza kupata hivyo kila nilipokua na kidogo sikusita kumpatia.

Kilichonifanya nije hapa jamvini ni kwamba mwanaume huyu amebadilika sana, hapigi simu nikipiga hapokei, nikimtumia jumbe hajibu kiukweli hali hii inaniumiza sana nashindwa hata kula, nimekua mtu wa kulia lia kila mara.

Tafadhali naombeni msaada wenu maana maji yamenifika shingoni.
Huenda mkavichukia vitu ikawa ni heri kwenu,na huenda mkavipenda vitu ikawa ni Shari kwenu,muombe mungu akuongoze,
 
Kama haupati unachopenda,penda unachopata.So mtoa mada umepata chaguo lako,njoo pm tujenge maisha.Usilazimishe unachopenda ilihali hakipo na wewe, Ukweli mchungu!!
 
Kwani ni baba yako huyo. Kazaliwa na mama mwingine tofauti kinachokuumiza ni nini hasa. Hata ikiwa ndiyo alikubikiri bado hustahili kuumiza nafsi yako. Fanya amekufa tu songa mbele na maisha acha ujinga.
 
Ukimpenda mtu unajitoa kwa moyo wako wote ila yeye anakuwa nusu nusu.Ikifika kipindi cha kukuumiza anakuumiza kweli kwa sababu yeye hakukuweka moyoni.Inabidi kupiga moyo konde na kusonga mbele make maisha bado yanaendelea.Jitahidi kumsahau na umwombe Mungu akupe anayekupenda kwa dhati ambaye ataheshimu hisia zako.Jitahidi kujichanganya,kuingia mitandaoni kama hivi yaani uwe busy utamsahau mapema tu na maumivu yataisha.Usimpigie tena na usiandike sms tena mpotezee huyo sio ndugu yako isitoshe wanaume wapo wengi asikutishe wala nini
 
miezi mi4[emoji26]
pole sana bibie , ndio ukubwa huo inabidi ukubaliane na unachokiona soma alama za nyakazi. achia ngazi dada.

nahisi ulimpenda mpaka ukaamua kuwekeza kwake. ukweli ni kwamba hakupendi...achana nae tu!

watu tuko hapa mwanaume miaka mi3 akianza kuleta longolongo narudisha mbusi bandani aisee, sina superglue mikononi mchuma ukiondoka naachia ngazi.... maisha yanaendelea!!!

He's asshole
dump him
 
Mapenzi ni pasua kichwa km utayaendekeza Sana. Hapo hata hajaafikiana km mnampango wa kuishi pamoja umepaniki hivyo! Sasa mkioana utakua kwenye hali gani!: Fikiria Kwa kina.

Jambo la msingi unalotakiwa kujua siku zote ni kwamba unataka mtu wa aina gani! Je huyo ulie naye anasifa hizo unazozitaka! Km sivyo kaa pembeni mapema. Hakuna haja ya kuumiza kichwa kumfikiria mtu ambaye ukiendlea naye atakutesa milele
 
Mi enzi za mahusiano yangu wakati bado mbichi sikuruhusu moyo wangu upende sanaaaa nilikua makini sana nikiona kuna vidalili vya kuchitiwa nasepa fastaaaaaaa sijawahi achwa nimeacha mimi. So my dear kama unaona hapaeleweki piga kimya mpk akutafuta asipokutafuta jitahidi kujikaza usimtafute huku ukiendelea kum delete taratiiiiiibu.
 
Yaani huu ambao nimeuesabu wanne wote mawasiliano c mazuri kakaangu, ni kweli nilimpenda sana sifichi. Lakini hali yake yakukaa kimya ndio inaniumiza
sasa fanyia kazi mashauli hayo ya huyo ndugu,
J huoni kma utashindwa uzalendo wa kujiongeza,


Unajua kama kweli analosema yuko sahihi,siku ukiamua kumwacha kwa hisia hizo utajiona....pale itakapogundulika kuwa kweli hakuwa na nia mbaya!!!
 
Binadamu tumeumbwa tofauti mwingine akiwa na matatizo anapenda awe mwenyewe atulize akili,,,cha msingi mpe muda na usimtumie sms za kumlaumu.Baada ya kama mwezi mtafute kwa hekima muongee,,,,kama kweli anakupenda utaona respond yake na kama hakupendi utajua
 
Nilimuuliza ktk hali ya ukali alisema kwamba anastress za kifamilia na hafkirii kuhusu mapenzi kwa sasa hivyo nimuache
Iko ni kisingizio tu, akuna aja ya kulia km kakuona wa nn nawe muone wa kazi gani, jilazimishe kukubaliana na hali maisha yaendelee
 
Back
Top Bottom