Nina maumivu sana jamani, nahitaji msaada wenu

Nina maumivu sana jamani, nahitaji msaada wenu

Habari zenu,

Nilikua na mpenzi ambae tumedumu kwa miezi minne sote tulipendana kwa dhati na kwa kipindi hicho yeye ndio alikua ameanza kazi hivyo mshahara alikua hajaanza kupata hivyo kila nilipokua na kidogo sikusita kumpatia.

Kilichonifanya nije hapa jamvini ni kwamba mwanaume huyu amebadilika sana, hapigi simu nikipiga hapokei, nikimtumia jumbe hajibu kiukweli hali hii inaniumiza sana nashindwa hata kula, nimekua mtu wa kulia lia kila mara.

Tafadhali naombeni msaada wenu maana maji yamenifika shingoni.
Age yako Tafadhali.
 
Ulikuwa unatoa kwa moyo au kwa masharti na masimango,wengi wenu mnatusaidia kwa masharti na masimango matokeo yake tukipata hatua ya kwanza ni kukata kamba au ulikuwa hujui kwamba jamaa hayupo serious na wewe..chagua mwenyewe
 
Ulikuwa unatoa kwa moyo au kwa masharti na masimango,wengi wenu mnatusaidia kwa masharti na masimango matokeo yake tukipata hatua ya kwanza ni kukata kamba au ulikuwa hujui kwamba jamaa hayupo serious na wewe..chagua mwenyewe
duuuh, sitaki kusikia hii kitu maana moyo wangu naupenda
huyu dada alienda more than her limitations
 
Yaani wewe dada ndani ya miezi minne tu umeshaachia moyo wako woo- o-te na kumpenda mtu kiasi hicho? Kuanzia sasa sahau kila kitu kuhusu yeye. And next time kabla ya kujiachia moyo wako umpende mtu sana angalia tabia sana ujaribu "kumsoma" kwa undani kwa kipindi kirefu sio miezi minne tu. Au labda alikuwa anakugharamia vitu vingi sasa umevimiss na alipokata mawasiliano ukaumia kwa kukosa hizo zawadi-sio kukatika kwa penzi
 
duuuh, sitaki kusikia hii kitu maana moyo wangu naupenda
huyu dada alienda more than her limitations
Sasa huko ni kuyaogopa mapenzi...na unachoogopa ndo kinakutokea...km una moyo wa kutoa we toa tu ,mapenzi hayana formula
 
Back
Top Bottom