Napitia kipindi kigumu sana wana JF. Nahitaji msaada wenu

Status
Not open for further replies.

Hatima yangu

Member
Dec 3, 2022
7
11
Naomba kujitambulisha
Mimi ni kijana wa kiume mwenye umri wa miaka 22 kutokea mkoani Mwanza. Kwa sasa ninaishi Manzese jijini Dar es salaam. Elimu yangu ni kidato cha sita. Sina familia na wala sijawahi wazia kutokana na ugumu wa kimaisha nilionao pamoja na kukosa uelekeo wa maisha yangu

Niko mbele yenu kuwaomba kwa mwanafamilia yeyote mwenye walau nafasi ya kazi katika kampuni / super market / duka / Hotel au assets nyingine kama hizo. Au mwenye connection za kazi viwandani au mahali popote ambapo ninaweza kujishikiza na kutengeneza future yangu anisaidie. Kwa sasa maji yamefika shingoni, napitia kipindi kigumu sana cha kimaisha. Sina mbele wala nyuma. Nina mzigo mkubwa sana nyuma yangu, bado umri unakwenda, majukumu yanaongezeka, napatwa na msongo wa mawazo, nakonda, nashambuliwa na "Sonona" kila uchao. Nina hali mbaya sana ya kimaisha
man-crying.jpg
Naombeni walau nipate mahala pa kujishikiza ili kuwabeba wanaonitizama nyuma yangu, ili nami nitengeneze maisha yangu, nami nihame hapa kwa ndugu, si mnajua tena athari za kukaa kwa ndugu!

Natamani kurudi zangu nyumbani, lakini kule nitaenda kuwaongezea mzigo tu. Bora tuungane wana jamiiforums wenzangu, mnisaidie nami nipate maisha. Napitia kipindi kigumu sana cha kimaisha Kigumu mno

Nahitaji msaada. Mwenye kazi / connection yoyote walau kibarua kiwandani anisaidie

Niko tayari kufanya kazi mahali popote pale. Kuhusu kulala, hata nje nitalala. Kikubwa najua natengeneza kiasi kadhaa ambacho mwisho wa siku kitanisaidia kutengeneza maisha yangu, kupanga chumba changu, kujiendesha mwenyewe, kuwanyenyua wanaonitizama, kutengeneza future iliyo njema kwa familia yangu ijayo

Summary
Jinsia: ME
Umri: Miaka 22
Elimu: Kidato cha sita

Aina ya kazi: Yoyote ile itakayonitengenezea future yangu, hata kama ni kuwa kibarua viwandani, sawa tu

Hali ya kimaisha: Napitia kipindi kigumu sana cha kimaisha

====

UPDATES:
Niwashukuru wote mliokuwa bega kwa bega na mimi kwa mchango wenu wa hali na mawazo. Nipende kumshukuru member mmoja aliyeamua kujitolea kunipatia kazi
Shukhrani sana na Mungu awabariki
 
Naomba kujitambulisha

Mimi ni kijana wa kiume mwenye umri wa miaka 22 kutokea mkoani Mwanza. Kwa sasa ninaishi Manzese jijini Dar es salaam. Elimu yangu ni kidato cha sita. Sina familia na wala sijawahi wazia kutokana na ugumu wa kimaisha nilionao pamoja na kukosa uelekeo wa maisha yangu

Niko mbele yenu kuwaomba kwa mwanafamilia yeyote mwenye walau nafasi ya kazi katika kampuni / super market / duka / Hotel au assets nyingine kama hizo. Au mwenye connection za kazi viwandani au mahali popote ambapo ninaweza kujishikiza na kutengeneza future yangu anisaidie. Kwa sasa maji yamefika shingoni, napitia kipindi kigumu sana cha kimaisha. Sina mbele wala nyuma. Nina mzigo mkubwa sana nyuma yangu, bado umri unakwenda, majukumu yanaongezeka, napatwa na msongo wa mawazo, nakonda, nashambuliwa na "Sonona"

kila uchao. Nina hali mbaya sana ya kimaishaView attachment 2434182Naombeni walau nipate mahala pa kujishikiza ili kuwabeba wanaonitizama nyuma yangu, ili nami nitengeneze maisha yangu, nami nihame hapa kwa ndugu, si mnajua tena athari za kukaa kwa ndugu!

Natamani kurudi zangu nyumbani, lakini kule nitaenda kuwaongezea mzigo tu. Bora tuungane wana jamiiforums wenzangu, mnisaidie nami nipate maisha. Napitia kipindi kigumu sana cha kimaisha Kigumu mno

Nahitaji msaada. Mwenye kazi / connection yoyote walau kibarua kiwandani anisaidie

Niko tayari kufanya kazi mahali popote pale. Kuhusu kulala, hata nje nitalala. Kikubwa najua natengeneza kiasi kadhaa ambacho mwisho wa siku kitanisaidia kutengeneza maisha yangu, kupanga chumba changu, kujiendesha mwenyewe, kuwanyenyua wanaonitizama, kutengeneza future iliyo njema kwa familia yangu ijayo

Summary
Jinsia: ME
Umri: Miaka 22
Elimu: Kidato cha sita

Aina ya kazi: Yoyote ile itakayonitengenezea future yangu, hata kama ni kuwa kibarua viwandani, sawa tu

Hali ya kimaisha:Napitia kipindi kigumu sana cha kimaisha

Mawasiliano: 0769007007 (Normal call & WhatsApp) Au natafutamaisha@gmail.com
Eee mola
Muone mja wako .

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Naona umelenga zaidi kazi za kuajiriwa.

Labda pia ungefikiria na shughuli za kujiajiri...yaani kama kuna Mjasiriamali mahali akualike mkapige kazi...kama ni kuzalisha sabuni na kuziuza mtaani kazi iendelee.
 
Nyuzi kama hizi watu wanapitaga mbali ....ndio utajua dunia haina huruma.
Siyo dunia haina huruma.

Nchi haina mazingira rafiki ya uwekezaji. Watu wana hela zao, wakiangalia mazingira ya uwekezaji bongo wanaona bora wawekeze masoko ya kimataifa tu.

Mkuu kama mimi binafsi naamua najinyima kununua the latest BMW X7 na mambo mengine ya anasa, nakusanya sh milioni 400- 500, niamue kuwekeza kwenye kilimo hapo TZ, kitu ambacho naweza kufanya ndani ya mwaka, bila mkopo, unafikiri kuna ajira ngapi nitatengeneza hapo?

Sasa tukikusanyana watu kama mimi kumi, tukakusanya shilingi bilioni tano, mtaji wetu utaongeza ajira vipi hapo nyumbani?

Na unafikiri kwa figisu za sasa za ardhi, uraia pacha na ujinga mwingi wa serikali, mtu mwenye akili zake timamu ambaye ana paspoti ya nje lakini ni mzawa wa Tanzania anaweza kuwekeza hivyo?
 
Kama una ujuzi wa kutengeneza video za katuni; njoo upulizwe na kiyoyozi ofisini
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom