mamawatano
Member
- Jan 1, 2024
- 20
- 94
Wana jamii Forums hamjambo, hapa ni mahali pekee ambapo naweza kuongea kwa uwazi na bila kuficha chochote. Kuna muda nakuwa na mawazo nashindwa wapi pa kusemea.
Iko hivi kwa sasa nina miaka 44 sijaolewa na sina mwenza ila nina watoto ambao nilipata na mpenzi wangu, mahusiano hatufanikiwa kufunga ndoa. Nimepambana na watoto kwa sasa wamekuwa wakubwa na wote wapo chuo kikuu.
Niseme sio kuwa nakuwa proud na haya maisha ila ilibidi nifunge kibwebwe ili nilee watoto maana mzazi mwenzangu tuliachana toka mtoto wa kwanza ana miaka sita.
Napitia wakati mgumu kwa vile sina mpenzi na kuna muda kama binadamu najisikia kuwa na mwenzangu. Sasa Naomba kwenye Jukwaa hili kama kuna mwanaume ambae na yeye ana watoto na anahitaji mwanamke mtu mzima ambae hawahitaji kuzaa tena karibu. Au mwanaume mgane.
-Ninafanya kazi ila sio mwajiriwa wa serikali.
-Maoni yenu pia ni muhimu lakini usinikatishe tamaa.
-Nina haki ya kupenda tena.
Iko hivi kwa sasa nina miaka 44 sijaolewa na sina mwenza ila nina watoto ambao nilipata na mpenzi wangu, mahusiano hatufanikiwa kufunga ndoa. Nimepambana na watoto kwa sasa wamekuwa wakubwa na wote wapo chuo kikuu.
Niseme sio kuwa nakuwa proud na haya maisha ila ilibidi nifunge kibwebwe ili nilee watoto maana mzazi mwenzangu tuliachana toka mtoto wa kwanza ana miaka sita.
Napitia wakati mgumu kwa vile sina mpenzi na kuna muda kama binadamu najisikia kuwa na mwenzangu. Sasa Naomba kwenye Jukwaa hili kama kuna mwanaume ambae na yeye ana watoto na anahitaji mwanamke mtu mzima ambae hawahitaji kuzaa tena karibu. Au mwanaume mgane.
-Ninafanya kazi ila sio mwajiriwa wa serikali.
-Maoni yenu pia ni muhimu lakini usinikatishe tamaa.
-Nina haki ya kupenda tena.