Tlaatlaah
JF-Expert Member
- May 18, 2023
- 8,173
- 11,590
Namshukuru Mungu kwa ajili ya yako na yangu, kwa wasaa huu muhimu, ambao ni zawadi kutoka kwa Mungu kwetu sisi sote.
Tumeipewa zawadi hii bure na tuitumia bure, na kwahivyo yatupasa kuitumia vizuri kadiri tuwezavyo na kwa uaminifu, huku tukimshukuru yeye pekee daima, kila wakati tunapopata wasaa wa kufanya hivyo.
Namsalimu sana mtumishi, msaidizi wangu mpendwa sana na kipenzi cha haja ya moyo wangu Lamomy popote alipo.
Namuombea kwa Mwenyezi Mungu ulinzi mkali sana wa kiroho na kimwili uambatane nae daima kila mahali anapotekeleza majukumu, kazi na mahangaiko yake ya kila siku.
Milango yangu ya kimwili na kiroho iko wazi daima kwajili yake, na saa zingine inalala wazi usiku na mchana ikitazamia ujio wake wakati wowote maishani mwangu katika Roho na kweli ya Mungu.
Namuomba Roho Mtakatifu ahuishe nafsi yake Lamomy ilainike na ipate kuskia sauti ya wito wa Mungu kwake dhidi yangu.
Afungue moyo wake uweze kutambua na kujua vema nia, haja, makusudi na madhumuni yangu mema sana kwake na yenye baraka, neema, sifa na utukufu wa Mungu daima na milele....
Lamomy katika dhiki na faraja daima na milele.
Kwa jina la Baba, Mwana na Roho Mtakatifu.
Tumeipewa zawadi hii bure na tuitumia bure, na kwahivyo yatupasa kuitumia vizuri kadiri tuwezavyo na kwa uaminifu, huku tukimshukuru yeye pekee daima, kila wakati tunapopata wasaa wa kufanya hivyo.
Namsalimu sana mtumishi, msaidizi wangu mpendwa sana na kipenzi cha haja ya moyo wangu Lamomy popote alipo.
Namuombea kwa Mwenyezi Mungu ulinzi mkali sana wa kiroho na kimwili uambatane nae daima kila mahali anapotekeleza majukumu, kazi na mahangaiko yake ya kila siku.
Milango yangu ya kimwili na kiroho iko wazi daima kwajili yake, na saa zingine inalala wazi usiku na mchana ikitazamia ujio wake wakati wowote maishani mwangu katika Roho na kweli ya Mungu.
Namuomba Roho Mtakatifu ahuishe nafsi yake Lamomy ilainike na ipate kuskia sauti ya wito wa Mungu kwake dhidi yangu.
Afungue moyo wake uweze kutambua na kujua vema nia, haja, makusudi na madhumuni yangu mema sana kwake na yenye baraka, neema, sifa na utukufu wa Mungu daima na milele....
Lamomy katika dhiki na faraja daima na milele.
Kwa jina la Baba, Mwana na Roho Mtakatifu.