Nimrod Mkono na Mkono Advocates watch

Dereva, konda waua abiria

Na Mwandishi Wetu (Mwananchi)

POLISI mkoani hapa wanamshikilia dereva na kondakta wake wa basi dogo la abiria aina ya Toyota Coaster kwa tuhuma za kumuua abiria, Herry Losujak Saning’o (34) aliyekuwa anadai arejeshewe chenji yake ya Sh600 baada ya kulipa nauli.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Matei Basilio, alisema baada ya kumpiga na kumuua abiria huyo, watuhumiwa hao walikamatwa wakimtupa katika eneo la makaburi ya Kaloleni jijini hapa.

Kamanda Basilio alisema, tukio hilo lilitokea juzi saa 1.30 jioni baada ya gari hilo kurejea jijini hapa likitokea Moshi mkoani Kilimanjaro, ambako hufanya safari zake za kila siku.

Wakielezea tukio hilo, ndugu wa marehemu ambao walikuwa wamesafiri naye kutoka eneo la King’ori wilayani Arumeru kuja mjini hapa, walisema ugomvi baina ya marehemu na kondakta wa basi hilo, ulianzia katika eneo la Mianzini wakati alipoanza kudai chenji yake.

William Mandaine ambaye ni shemeji wa marehemu, alisema wakiwa kwenye gari hilo, Saning’o ambaye alikuwa ameandamana na mkewe, Glory Herry, alitoa Sh2,000 kama nauli.

Mandaine alisema nauli ya kutoka King’ori hadi Arusha mjini ni Sh700 na hivyo aliomba kurejeshewa Sh600, kitu ambacho kondakta alikataa.

“Baada ya kumuomba kwa muda mrefu tulipofika Mianzini ambapo ndio mwisho wa safari yetu, tulianza kushuka na ndipo Saning’o alikumbushia kupewa Sh600 yake, na ndipo kulitokea kutoelewana baina yao. Dereva kuona hivyo, alishuka kwenye gari hilo kuingilia,” alisema Mandaine.

Alisema badala ya dereva huyo kusuluhisha ugomvi huo, naye alimuunga mkono kondakta wake kuwa kamwe hawarejeshi fedha, kwani wao ndio wanadai na hapo hapo walimbeba Saning’o na kumrejesha kwenye gari na kuondoka naye kwa kasi.

Mandaine alisema, baada ya kuondoka na Saning’o, wao walikodi teksi na kuanza kuwafuata kwa nyuma lakini kutokana na mwendo kasi ya gari hilo, walipotezana katikati ya jiji, hivyo wakaamua kwenda polisi.

Alisema wakiwa polisi, waliliona gari hilo likiwa katika makaburi ambayo yapo jirani na Kituo Kikuu cha Polisi mjini hapa na ndipo nao walipokwenda na kukuta tayari polisi wamefika.

“Mara baada ya kuwakuta polisi, ndipo tulipewa taarifa kuwa kondakta na dereva huyo wameonekana wakimtupa mtu nje ya gari na baada ya kufuatilia ndipo tulimkuta Saning’o akiwa katika hali mbaya na baadaye alifariki,” alisema.

Kwa mujibu wa taarifa ya awali ya uchunguzi wa kifo hicho, Saning’o alifariki kutokana na jeraha kubwa kichwani baada ya kupigwa na kitu kizito kilichotoboa sehemu ya kichwa.

Akizungumzia tukio hilo, Kamanda Basilio, alisema polisi bado inafanya uchunguzi ili kujua chanzo cha kifo hicho lakini taarifa ya awali inaonyesha marehemu alipigwa na kitu kizito kichwani.

“Tunaandika maelezo na yakikamilika tutawafikisha mahakamani watuhumiwa hao… hiki ni kitendo cha kinyama kamwe hatuwezi kukaa kimya,” alisema Kamanda Basilio

Marehemu huyo, ambaye ni mkazi wa kijiji cha Kiranyi, Wilaya ya Arumeru ameacha mjane na watoto wawili ambao ni Jesca anayesoma darasa la pili na Linda anayesoma shule ya awali.

Kutokana na tukio hilo, chama cha wamiliki wa magari ya abiria Arusha na Kilimanjaro (Akiboa) na chama cha madereva mkoa wa Arusha (Umma) wamelaani kwa nguvu kitendo kilichofanywa na dereva huyo na kondakta wake.

Katibu Mkuu wa Akiboa, Locken Adolf, alisema jana kuwa wamepokea kwa mshituko tukio hilo na wanatoa pole kwa familia ya marehemu.

Tukio hilo limekuja siku chache baada ya dereva mwingine wa gari dogo la daladala maarufu, kama kifodi jijini hapa, kumjeruhi kwa sime askari ya kikosi cha usalama barabarani, PC Hamad.
 
Jasusi,

kwa hiyo kama ilivyokuwa Familia ya Kombe, Familia ya Mwakibete inabidi wagangamae walipwe fidia, kwani inasemekana kifo chake kilichangiwa sana na dipression aliyoipata toka apofukuzwa kazi.
 
Dereva, konda waua abiria

Na Mwandishi Wetu (Mwananchi)

POLISI mkoani hapa wanamshikilia dereva na kondakta wake wa basi dogo la abiria aina ya Toyota Coaster kwa tuhuma za kumuua abiria, Herry Losujak Saningo (34) aliyekuwa anadai arejeshewe chenji yake ya Sh600 baada ya kulipa nauli.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Matei Basilio, alisema baada ya kumpiga na kumuua abiria huyo, watuhumiwa hao walikamatwa wakimtupa katika eneo la makaburi ya Kaloleni jijini hapa.

Kamanda Basilio alisema, tukio hilo lilitokea juzi saa 1.30 jioni baada ya gari hilo kurejea jijini hapa likitokea Moshi mkoani Kilimanjaro, ambako hufanya safari zake za kila siku.

Wakielezea tukio hilo, ndugu wa marehemu ambao walikuwa wamesafiri naye kutoka eneo la Kingori wilayani Arumeru kuja mjini hapa, walisema ugomvi baina ya marehemu na kondakta wa basi hilo, ulianzia katika eneo la Mianzini wakati alipoanza kudai chenji yake.

William Mandaine ambaye ni shemeji wa marehemu, alisema wakiwa kwenye gari hilo, Saningo ambaye alikuwa ameandamana na mkewe, Glory Herry, alitoa Sh2,000 kama nauli.

Mandaine alisema nauli ya kutoka Kingori hadi Arusha mjini ni Sh700 na hivyo aliomba kurejeshewa Sh600, kitu ambacho kondakta alikataa.

Baada ya kumuomba kwa muda mrefu tulipofika Mianzini ambapo ndio mwisho wa safari yetu, tulianza kushuka na ndipo Saningo alikumbushia kupewa Sh600 yake, na ndipo kulitokea kutoelewana baina yao. Dereva kuona hivyo, alishuka kwenye gari hilo kuingilia, alisema Mandaine.

Alisema badala ya dereva huyo kusuluhisha ugomvi huo, naye alimuunga mkono kondakta wake kuwa kamwe hawarejeshi fedha, kwani wao ndio wanadai na hapo hapo walimbeba Saningo na kumrejesha kwenye gari na kuondoka naye kwa kasi.

Mandaine alisema, baada ya kuondoka na Saningo, wao walikodi teksi na kuanza kuwafuata kwa nyuma lakini kutokana na mwendo kasi ya gari hilo, walipotezana katikati ya jiji, hivyo wakaamua kwenda polisi.

Alisema wakiwa polisi, waliliona gari hilo likiwa katika makaburi ambayo yapo jirani na Kituo Kikuu cha Polisi mjini hapa na ndipo nao walipokwenda na kukuta tayari polisi wamefika.

Mara baada ya kuwakuta polisi, ndipo tulipewa taarifa kuwa kondakta na dereva huyo wameonekana wakimtupa mtu nje ya gari na baada ya kufuatilia ndipo tulimkuta Saningo akiwa katika hali mbaya na baadaye alifariki, alisema.

Kwa mujibu wa taarifa ya awali ya uchunguzi wa kifo hicho, Saningo alifariki kutokana na jeraha kubwa kichwani baada ya kupigwa na kitu kizito kilichotoboa sehemu ya kichwa.

Akizungumzia tukio hilo, Kamanda Basilio, alisema polisi bado inafanya uchunguzi ili kujua chanzo cha kifo hicho lakini taarifa ya awali inaonyesha marehemu alipigwa na kitu kizito kichwani.

Tunaandika maelezo na yakikamilika tutawafikisha mahakamani watuhumiwa hao hiki ni kitendo cha kinyama kamwe hatuwezi kukaa kimya, alisema Kamanda Basilio

Marehemu huyo, ambaye ni mkazi wa kijiji cha Kiranyi, Wilaya ya Arumeru ameacha mjane na watoto wawili ambao ni Jesca anayesoma darasa la pili na Linda anayesoma shule ya awali.

Kutokana na tukio hilo, chama cha wamiliki wa magari ya abiria Arusha na Kilimanjaro (Akiboa) na chama cha madereva mkoa wa Arusha (Umma) wamelaani kwa nguvu kitendo kilichofanywa na dereva huyo na kondakta wake.

Katibu Mkuu wa Akiboa, Locken Adolf, alisema jana kuwa wamepokea kwa mshituko tukio hilo na wanatoa pole kwa familia ya marehemu.

Tukio hilo limekuja siku chache baada ya dereva mwingine wa gari dogo la daladala maarufu, kama kifodi jijini hapa, kumjeruhi kwa sime askari ya kikosi cha usalama barabarani, PC Hamad.


Wote wamefanya kosa la aina moja la kuua, lakini hawa jamaa wameongeza kosa jingine la kutaka kuficha ushahidi. Kwa hiyo hawa wanastahili adhabu kubwa zaidi ya ile ya Dito.

Kwa mfano kwa vile sheria ya mauaji adhabu yake ni kunyongwa, Dito anawewa kupunguziwa makali ya adhabu kwa kupewa nafasi ya kuchagua jinsi anavyotaka anyongwe, wakati hawa wataanza kwanza kutumikia jela kama miaka miwili au mitatu hivi kutokana na kosa na kujalibu kuficha ushahidi, halafu ndipo watanyongwa kwa staili itakayoamuliwa na mahakama yenyewe.
 
Naam aliefungua mjadala huu nadhani aliweka wazi kwamba anataka mjadala ulenge katika kuangalia nafasi ya Mkono kama wakili as well as kama mbunge mwakilishi wa wananchi.

Kuna mjadala baina wa kujadili mwenendo wa kesi nzima upo hivyo hapa ni sahihi kabisa kuweka intellectual and coherent arguments za kueleweka ili tujue sheria zetu, sometimes binafsi yangu huwa ninaelimika kwa elimu ya humu ndani at least kwa kutekenywa mawazo nikatafute zaidi.

Mzee Mwanakijiji umeraise valid points kuhusu mjadala unaoendelea bungeni kuhusu makosa ya jinai, hapa ndio unaona pana walakini mkubwa kwa kweli manake Maoni yoyote ambayo wakili mkono atayatoa akiwa ndani ya bunge yanaweza kutafsirika kama ni mpangilio wa kutaka kuvuruga kesi. Ingawa katika hali halisi hilo haliwezekani manake kesi ipo mahakamani na inaamuliwa kwa exisiting laws hii ''sheria'' inayojadiliwa bungeni bado ni muswada tu itatake time kubwa mpaka kufikia kutumika mahakamani.

Mzee ES naona umejikanganya sana katika mjadala huu, ukijaribu kuelezea masuala mengi intellectually huku ukimix na conspiracy theories... sikubaliani na hoja kwamba wabunge ni watumishi wa serikali, no! kama alivyosema mwanzo hapo juu MGONJWAUKIMWI kwamba mgawanyo wa madaraka unaonesha wazi kuwa inaweza kukawa na inter-relationship lakini kamwe wabunge hawahusiani na serikali.

Mawaziri ndio the best example ya inter relation ilivyo, kwamba wao ni wabunge at the same time ni key players katika serikali, lakini then Mkono sio waziri angekuwa waziri bila shaka kazi ya uwakili ingekuwa on hold. Mzee ES wabunge kwenda nje kwac safari za kazi sio kuwa wawakilishi wa serikali kama ambavyo majaji kusafiri kwenda nje kikazi sio kuwa ni watumishi wa serikali, ndio maana Jaji Mohamed Chande wa Mahakama Kuu Mbeya yupo Israel hivi sasa akiwa anachunguza allegations za improper war conducts za Israel wakati wa mapigano yake na Hizbollah, hayupo huko kama mwakilishi wa serikali bali ni kama independent and impartial individual worthy of doing this job...

Ama kwamba Lowassa amekuwa akikaripia wabunge, I can appreciate the argument but I am not accepting it, hii ni paradox ya kichama kwamba waziri mkuu ana uwezo wa kuwaita wabunge wa chama wakakaa na kuamua hatuhoji kuhusu umeme, ni tatizo in its own right lakini haimanishi kwamba wabunge ni watu wa serikali....hii ni concept ya kwamba bunge linakaa kama chama, kama ambavyo wapinzania huamua kukacha baraza la wawakilishi kule zanzibar kwa msimamo wa pamoja, wakiamua kuhudhuria hawawi watumishi wa serikali...

Uhuru wa Mahakama? Naam upo kama hujajua hilo Mzee ES tafiti vizuri, manake umekuwepo from time immemorial manake ukiangalia tangu enzi za jaji Wolfgang Dourado kumekuwa na maamuzi mengi tu yanayokinzana na serikali:

1. Mwalimu Nyerere katika peak ya kushindwa kwake alisema wale wote wenye kumiliki mali,ni wahujumu uchumi, watu wakapitiwa majumbani wakikutwa na dawa za miswaki basi ni wahujumu, wakasekwa rumande, kesi ikaenda mahakamani, jaji akaidismiss kwamba hawana kosa la kujibu kwa vile Tanzania hakuna sheria inayohusu kuhujumu uchumi!

Nyerere akaitisha bunge haraka haraka ikatungwa sheria ya kuhujumu uchumi kesi ikarudishwa mahakamani, jaji Dourado akaidismiss tena na kuwaachia watu huru kwamba wamekamatwa wakati sheria ikiwa haiexist, the new suspect ndio watahukumiwa nao sio wale waliokamatwa awali.

Nyerere akaagiza sheria iwe backdated!

Naam mfano huo hapo juu unakupa maelezo ya namna mahakama ilivyo huru kufanya kazi zake ingawa ni kweli kuwa bado mabavu makubwa yanayotumiwa nac serikali lakini the elements and idea is there, yes wanateuliwa na rais lakini wana protection kwamba Rais akishawateua majaji hawezi kuwafuta kazi... good idea lakini kama ulivyosema tunahitaji kuona wakithibitishwa openly in a due process of the law lakini tunaona hata nchi nyingine ni waziri mkuu anaeteua majaji lakini kwa kushirikiana na jopo huru.


It can't be truer than this. Conspiracy theories ndizo zinazochochea chuki na kupotosha sheria pamoja na uelewa wa jambo husika. Hapa, kula 5.
 
Mzee wangu,

Warioba na Mahalu, wanayo Law Firm je umewahi kuwasikia wakitinga mahakamani kutetea wahalifu? Unafikiri ni kwa nini? Ni kwa sababu ya kuheshimu nafasi zao katika taifa letu, na kwamba wote wawili bado wanachukua pension ya serikali yetu, yaani hela za walipa kodi,

Huyu Mkono, mshahara wake wa bunge na marupurupu ambayo sijawahi kusikia ameyakataa, hulipwa na nani? Si hela za walipa kodi? Hizi hela za walipa kodi hutokea wapi, jimboni au serikalini? Wabunge wa bongo toka lini wamekuwa independent?

Mzee wangu wewe ndiye unayechanganya mambo, kwani unaongelea mambo ya US na UK, na kujaribu kuyaingiza kwetu bongo, huku ukielewa wazi kuwa hatuna hizo system bongo za Judicial independence, wala Parliament indendence, isipokuwa ni Executive tu yaani rais wetu ndiye independent, na all mighty man, au The King. Ninasema akija mgeni kusoma hapa anaweza akaupanda mkenge bure kuwa eti bongo tuna Three branches za government wakati wewe binafsi unajua hatuna ila tuna majina tuu!

Yaani kweli unadiriki kuweka mifano wa majaji kama Dourado na huyo alioko Israel, ambaye honestly sisi hatujawahi hata kumsikia as a example ya Judicial independence ya bongo? Are you serious? Hao majaji wanachaguliwa na nani? sio rais wetu, halafu wanakuwa confirmed na nani? Yaani jaji mmoja mdogo wa bongo kwenda Israel, tena mwaka 2006, yaani mwishoni mwa mwaka ndio unaweka kuwa a big deal mpaka ya kumtumia kama reference ya separation of power bongo between three branches toka tupate uhuru na pia kuhalalisha Mkono kumtetea a murdereer, kwa kweli mzee wangu I am very disappointed pamoja na kwamba mimi sio intellectual au an academic person, ila ni kalagha baho tu wa mtaani lakini hapo ndugu yangu umeniacha hoi,

Kwa sababu Mkono, anapewa nyumba na serikali yetu, kama viongozi wengine wote wa serikali yetu kwa kuwa mbunge, Mkono kama mbunge anaruhusiwa kusoma intelligence information katika kamati ya bunge kutokana na kula kiapo cha serikali, kuwa atakuwa mtiiifu kwa serikali na atatunza siri za serikali kama mfanyakazi wake, I do not need to be a professor kuelewa hilo bro, uwakili wake unatakiwa usimame inapokuja kwenye kesi nzito kama ya Blaza Dito, na bongo kama hatuna sheria ya kumsimamisha basi kuna hatari hata tukagundua kuwa Blaza Dito was right kufanya aliyoyafanya period!

Maneno yako ni mazuri sana lakini sio reality ya sheria na siasa ya bongo, bongo hatuna three branches zinazofunction equally, ndio maana Warioba alipokwenda kule NY kugombea ujaji wa Dunia katika mambo ya bahari, ni rais wetu ndiye aliyeamuru wizara ya foreign kutumia kila mbinu kuhakikisha anapita, sasa mzee wangu unategemea kungekuja kesi ya bahari ya kuhusu bongo Warioba angeamua independently against bongo?

Mambo ya majuu tusiyachanganye na mambo yetu ya uswahili ya huku bongo!
 
....Nyerere akaitisha bunge haraka haraka ikatungwa sheria ya kuhujumu uchumi kesi ikarudishwa mahakamani, jaji Dourado akaidismiss tena na kuwaachia watu huru kwamba wamekamatwa wakati sheria ikiwa haiexist, the new suspect ndio watahukumiwa nao sio wale waliokamatwa awali.

Nyerere akaagiza sheria iwe backdated!!


Hebu tupe evidence tafadhali....thats a serious allegation bro!
 
Mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania anaenda kusimama kwenye Mahakama iliyochini ya jamhuri hiyo kama wakili, kufanya utetezi katika kesi ya jinai, kesi ambayo inaletwa na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania dhidi ya aliyekuwa mmoja wa watumishi wa serikali ya jamhuri hiyo, halafu hakuna mgongano wa kimaslahi!

Niiteni miye mpumbavu lakini hata kipofu hahitaji kuona moto kuukimbia!
 
Mzee Es,

Uliyoyasema ndio haswa hali halisi ya siasa za Tanzania kwa sasa.
 
NANI NI MWENYEKITI?

Kamati ya uongozi?

Kamati ya katiba, sheria na utawala?

Mbunge mmoja alipokwenda Ujerumani bila kuomba ruksa alikiona cha mtema kuni, sasa vipi Mkono?

Ama kuna kaubaguzi bungeni?


Wacha
 
tafiti then jadili

Naona umeelezea vizuri what's on PAPER hapa bongo.

Mzee ES

Hapo umeweka wazi hali halisi ON-GROUND bongo. Lakini kama nimekuelewa vizuri hupingani ya Mh tafiti then jadili.

Hivyo, kimsingi nakubaliana na hoja zote 2 zinazozungumzia tofauti ya nguzo 3 za nchi. Ila sina matumaini kama katika kizazi hiki tutaweza kushuhudia Uwazi wa Nguzo hizo 3 kama ilivyo UK au USA.
 
Mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania anaenda kusimama kwenye Mahakama iliyochini ya jamhuri hiyo kama wakili, kufanya utetezi katika kesi ya jinai, kesi ambayo inaletwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania dhidi ya aliyekuwa mmoja wa watumishi wa serikali ya jamhuri hiyo, halafu hakuna mgongano wa kimaslahi!!!! Niiteni miye mpumbavu lakini hata kipofu hahitaji kuona moto kuukimbia!!!

Mheshimiwa, Hapo umekosea au mimi nimeshindwa kuelewa?
 
Tatizo ni kuwa sheria zetu hazifanyiwi marekebisho according na wakati. Worse enough hao hao wanaothibitisha sheria kutumika do you expect wajitie kitanzi? waondokane na ulaji? never on earth.

In practice Mkono hajafanya mabaya au kosa. But on moral basis he is 100% wrong.
 
Bravo wazee, kwenye la Blaza Dito ni lazima tu-digg in tena ndugu zangu tusifanye masihara, maana media ya bongo haina stomach na hii story maana inawagusa wanaowalipa,

I have no beef na mtu hapa, lakini ninasema kwamba Tanzania tunataka sheria, au heshima kwa The Rule of Law, tena now tukianzia na kesi hiii ya Blaza Dito, Mzee Mwanakijiji you are right on the money,

I have a lot of respect kwa Mbunge Mkono, hasa kutokana na mafanikio yake kimaisha na kibinafsi, na yes he is a hard working man na very royal man kwani nimeuona fisrt hand kwenye kampeni za urais kwenye kambi ya JM,

But, I have a big problem na kitendo chake cha kujiingiza kwenye hii kesi, WHY? WHY? sipati jawabu! Kweli Mbunge Mkono how do you reconcile within yourself and your soul, na issue kama hiii ya an ARROGANT GOVERNOR OF STATE, anapokwenda mchana kweupe mbele ya halaiki yaani wananchi in the public, na kutoa bastola na kumpiga nayo mwanachi ambaye ni dereva wa walalahoi?

To this day, Ditopile hajaomba msamaha hata kwa abiria waliokuwa kwenye basi lile ambao hawakuweza kufika majumbani mwao on time kwa ajili yake, mpaka leo hajaomba radhi kwa familia ya marehemu, badala yake anakaimbilia kuandika barua kwa rais, as if alipiga risasi ndege tu njiani, yaani the man is so ARROGANT kwamba hata kwenye hiyo barua ya rais hajamuomba msamaha rais kwa kumuuua raia asiyekuwa na hatia!

I do not care kuhusu sheria za serikali wala za bunge, and sitaki habari za Three branches wala legally implications, Ditopile should appologise first, kwa taifa letu, ndugu wa marehemu, na kwa familia yake pia tena NOW! Halafu Mbunge Mkono angejitoa mara moja kwenye hii kesi, it is just the right thing to do bado sio too late!

Mbunge Mkono save us na hizi shallow debates za sheria zetu ambazo hazipo, za kusadikika, jitoe sasa! Na kwa wale wenye elimu za juuu msitudanganye jamani tuoneeni huruma sisi wabongo yaani ya IPTL tunayasikia tu, ya Madini pia tunayasikia, sasa hata hili la Ditopile ambalo tumeliona kwa macho nalo bado mnataka kutupandisha mkenge na lugha za kisasa, za separation of power na Three Branches,

wakati wote tunajua kwa Ditopile alishuka kwenye gari lake akaenda kwenye basi na kumuua dereva wa basi, FULL STOP!
 
Mzee Es, hata mimi ninamheshimu sana huyu Mzee Mkono!

Lakini hadi sasa hainingii akilini kwani ameamua kujiingiza katika hii kesi!

ITAMUMALIZA KISIASA, NA GRAPH YA HESHIMA YAKE INAWEZA POROMOKA VIBAYA SANA!

MAUAJI YA WAZI YALIYOFANYWA NA DITO NI YA KUTETEA KWELI. NINAKUBALIANA NA WEWE HUYO KIGOGO ALIYEMUITA MKONO AMEMUINGIZA KATIKA MKENGE, MZEE MKONO ACHANA NA HILI KOSA. LAKINI FOR SURE LITAKUSHUSHIA HESHIMA YAKO SANA!
 
Mimi kwa maoni yangu naona Mkono kaenda kujiongezea umaarufu tu,kama vile alivyofanya Mustapha Lakha kwenye kesi ya wahaini.

Kwa sababu hii kesi ikianza itakuwa ni entertainment safi sana. Lawyers wote huwa wanapenda big profile cases,and they dont come bigger than this. Kwani yeye Mkono na Tenga wamekosa nini? Si wanafanya kile walichosomea na wenye utaalam nacho?

Kwa kifupi ni kazi yao,ni sawasawa wangekuwa ni madaktari, haina maana wasingemfanyia upasuaji muuaji ambaye asipofanyiwa huo upasuaji atakufa. Maana ile ni kazi yao,na hai-specify wamfanyie nani wamuache nani.

Hii kesi ikianza itakuwa ni headline news kila siku, ina maana tutayasoma haya kila siku tupende tusipende, na hichi ndio mawakili kama hawa wanatafuta.Kama kesi ya O.J Simpson, yule wakili wake Johnnie Cochran(Mungu airehemu roho yake) alikuwa maarufu sana kutokana na ile kesi na matokeo yake ni kila celebrity kumfuata yeye.

Sasa hapa kwetu wakina Dito ndio ma-celebrity wetu.
 
Mzee Zanaki,

Heshima mbele bro!, ingekuwa hii kesi inafanyawa huko majuu ningeelewa point yako ya O.J and the likes, lakini bongo hapa ambapo watoto wa kina Mungai, Kingunge, na Rupia, hawakuhitaji kina Cochrain kuachiwa na majaji wetu supposedly, INDEPENDENT, no use ya ucelebrity if that is case,

Leo Mbunge Mkono, anataka ku-prove kitu gani mbele ya wanyonge? Heshima aliyonayo sasa hivi aliipata kwa kumtetea nani? au celebrity yupi? No guys hebu tuiangalaie hii kesi na wahusika katika context inayotakiwa, kwamba tuko katika nchi ya kusadikika ambako sheria inategemea ni nani anashitakiwa, akiwa mtoto wa mkulima, kesi ya mauaaji huchukua miaka kumi kabla ya kuamuliwa, akiwa Ditopile tayari imeshatajwa mara mbili mahakamani katika wiki tatu, sasa kwa kujiingiza katika kesi hii unategemea kupata umaarufu gani, kama sio kuonea wanyonge?

Arrogance, ya kulewa madaraka that is all I can see, na kuvinjari katika nchi isiyokuwa na sheria, sihitaji huo umaarufu, kama ni kutafuta umaarufu wa sheria nitaenda kumtetea Kagame kule France anakoshitakiwa na mahakama international, au nitachukua kesi za kule Arusha kwenye tribunal, lakini sio kuonea wanyonge hapa bongo!

Mbunge Mkono ajitoe kwenye hii kesi ni the right thing to do, morally na politically, kuendelea kwake na hii kesi ni kushusha hadhi ya rais na heshima pamoja na imani ya wananchi na serikali yao ya awamu nne waliyoichagua kwa kura 80%, sio ili waje waonewe na viongozi waliowapigia kura kwa kisingizio cha kuwa eti pia ni mawakili, pamoja na kunichugua kwenu kuwa mbunge lakini mimi siku zote ni wakili, NONESENSE Mkono, lazima tuwe na civility kidogo jamani!
 
Nimekuelewa mheshimiwa,lakini bado nasema kuwa sheria zote zinamruhusu kumuwakilisha Dito,nafikiri issue hapa ni ethics.

Tunavyoina sisi hapa hii kesi ni tofauti kabisa na mwanasheria anavyoiona. Yeye kwake ni opportunity at doing what he does best na sisi ni kuwa huyu Dito ni mnyama therefore he should rightfully be treated like one.Sawa kabisa!

Mkono kuingia kwenye hii kesi sio guarantee kuwa Dito hatafungwa,kwa kweli hio itakuwa ni miracle,kufungwa lazima atafungwa tu.

Unajua there are so many things at stake here. Mimi sidhani kama hii kesi itaathiri reputation ya Mkono au Tenga.
Tukumbuke huyu Dito alikuwa ni best man wa JK na pia dada yake Dito ni secretary wa Mkono,hilo la pili sidhani kama lina nguvu zaidi ya hilo la kwanza.

Mwanzoni hapo wengi tulisema kuwa lazima kuwa kuna mkono wa mtu humu and that might as well be that Mkono kachungulia hio dili kwa angle ya u-best man wa Dito kwa JK,therefore kwa yeye kujitumbukiza mule moja ni kujitafutia umaarufu kwa rais.

Kwa sababu tukumbuke Mkono sio mwana mtandao,infact mwishoni alikuwa kambi ya Salim Salim. Huu ni mwanya mzuri kwake yeye,(maana huyu ni creme de la creme wa lawyers hapa bongo) kujiweka vizuri na JK.

Mkono feels he deserves a ministerial post,maana if Karamagi anaweza kupata then na yeye anaona anastahili,kwao huko kafanya mengi sana,na JK anajua Musoma ni kati ya ngome zake.

Hizi zote ni personal interests,kama kilivyo kila kitu kwenye nchi hii.Sisi as wabongo tutaendelea kubishana hapa mpaka mwisho wa hii kesi,lakini ukweli ndio huo,whats at stake here for Mkono is something maybe we cannot fathom.
 
Hii Kesi ya DITO! yetu macho,

mmoja aliwahi kusema inaweza kuwa the make or demolish? of JK. Ninakubaliana naye kwa kiasi fulani, ila wabongo wengi bado wana usingizi mzito na wepesi wa kusahau, njaa kali pia huchangia

Kwa kweli kitendo cha Dito kuua kimenisiitisha sana!

Kwa hiyo ni imani yangu kuwa sheria itatenda haki na kufanya ambacho wengi wanategemea.

Hii karata ya Mkono! Lakini kama anafanya kwa kufurahisha JK huoni kuwa hiyo ni mbaya kwa mtu kama yeye?

Ninadhani hata JK alichukizwa na hicho kitendo cha Dito, historia itawahukumu kama watapindisha sheria. Si unasikia kila siku watu wanakumbuka mauaji aliyofanya kijana wa kingunge et. al!
 
Back
Top Bottom