Nimewahi kuwa changudoa, nimjulishe?

Nimewahi kuwa changudoa, nimjulishe?

Hayo yalishapita ushaomba msamaha kwa muumba wako,kwa wanaume w kibongo ukimuambia ukweli siku mkikosana ndio silaha ya kukuumiza wewe utaambiwa ndio maana ulikua changudoa ,mwambie sasa utayaona tunayokuambia

Kila mtu ataandika anavyofikiria lkn ukweli ndio huuu hapa,Sisi haswa baadhiyetu ndivyo tulivyo...
 
Wakaka wepi wamekupa stress? Sikiliza ushauri unaokutaka usolve tatizo hili once and for all na sio kuliahirisha. Pia usidhani kila mwanaume anaelewa maisha wengine kula kulala hata hawajui chochote kuhusu maisha staha achilia mbali ndoa.

Nani kakudanganya kwamba mtoto analeta faraja? Je ukimpata kilema au zezeta utafarijika kweli? Wewe kiri ulikosea kutomwambia mapema lakini mwambie ili uwe huru.

HApo kwenye kilema umechemsha
 
nakuelewa..........nina makovu sana kwenye ubongo wangu ndio maana naogopa to add up a new scandal
Usiogope matokeo usiyoyajua.
Naamini kuwa wapo wateja wako enzi za uchangudoa waliokuwa wakitaka kuchukua changu lazima wakutafute kwanza wewe, wakikukosa ndio wanaangalia option nyingine, ina maana uko bomba hata mmasai kaona

Usiishi kwa kuhofia mgogoro hata kama kuna viashiria vyake kumbuka si kila mawingu hunyesha mvua.

Umeamua kuwa mpole na kuishi aina mpya kabisa ya maisha, aina hiyo ndiyo anayoijua mmasai, hiyo nyingine ni story.

Ujue kuwa zamani wewe ulikuwa mtoto, unapoolewa leo utoto wako wa enzi zile leo sii factor kwamba "eti alikuwa mtoto"

Na mwanamme (sio mwanaume) akiamua kuoa "story makandokando" huongeza hamasa ya kujipatia hatimiliki.........

Ujue changu kwa viwango ni mwanamke anayekubalika kimvuto, kipimo ni wingi na madau kutoka kwa wateja wake.

Ujue changu akiolewa hayumbishwi na mapenzi, ni rahisi kupanga mambo ya msingi pamoja naye.

Ujue changu anaheshimu sana akiamua kama unavyotuambia umeamua.

HALAFU UJUE TUMEAMBIWA KWENYE BAIBO KUWA MACHANGUDOA WATATUTANGULIA PEPONI, isije ikawa nawe umo!!!!

HALAFU PIA UJUE KUWA KWA SWALA LA KIMUNGU TUMEAMBIWA NA BAIBO KUWA "MSIFIKIRIFIKIRI MTAKACHOSEMA/MTAKACHOJIBU, ROHO MTAKATIFU ATAKUONGOZENI"

Kwa hiyo fate yako na mmasai imebebwa na time. Kuwa Optimistic inaweza kuwa swala bora sana kwako.

Kumbuka:-
Kupiga pua hutokeza damu,
Kuyasukasuka maziwa hutokeza mafuta (samli)
Na ndoto huja kwa wingi wa fikra za mchana.

Katikati ya mistari hiyo kuna majibu na ushauri unaokufaa.
 
Ukisema ukweli tu umeula wa chuyaaa,maana hata yeye kuna aliyoyafanya lakim hatakuambiaa kila mtu siri yakee we baki na yako watanzania kwenye ukweli bado hatujajifunza

Usijaribu kumwambia utakuwa umejiharibia. Maana yatafuata maswali mengi sana ni bora ukakaa kimya

Nani atakubali kuoa changu, bora ukae kimya sio kila kitu ni cha kuweka wazi hapa duniani.

Siku jamaa akijua kupitia hao wakenya utakuwaje?
1. Kumbuka mleta mada mwenyewe kashajichanganya, kahama kanisa baada ya hao wenzake wakenya kuja kusali kanisani kwao hadi mchungaji na huyo mchumba wake wakabaki njia panda..
Hamuoni kuwa siku siri zikianza kuvuja huyo mchumba wake atakuwa na ushahidi 100% na anaweza kumuuliza sbb ya kutokuwa muwazi kabla?
2. Mleta mada hakufanya ukahaba kwa kupenda... Ni mazingira yalimlazimisha.. Hamuoni kama akajieleza maelezo ya kutosha kwa bf wake jamaa Anaweza kumuelewa kama kweli ana mapenzi ya dhati na yy?

Nwy.. Kila mtu ana kitu anachokilenga... Bt for me Marytina angefunguka tu... Kama huyo bwana Mungu kampangia atamuoa tu na kama hakumpangia bila hata kujua hiyo siri huo uchumba unaweza kuvunjia kwa sabb nyingine tu ya tofauti...
Marytina my love... Binafsi niliwahi kuwa na mchumba ambae alikuwa na mtoto.. (wakati namuapproach tyr alikuw na mtt wa miaka 2) niliwahi kumuhoji akabiambia kuwa alipewa Mimba na bf wake Wa kwanza akamtelekeza...
NIKAAMINI JUST KIRAHISI...
Bt kuna siku yule dada alinitafutia muda wa kunieleza siri nzito iliyopo moyoni mwake.. Alianza kwa kuniomba msamaha kwa kunidanganya ( wakat naanza nae mahusiano hakudhani kama tungefika mbali, so hakupenda sana kuianika siri yake kwa kila mtu) bt baada ya kuona kuwa nilikuwa serious Na yy akaona bora awe muwazi..
Story ikaanza.......
Mama yake na baba yake waliwahi kutengana na baadae mama akaolewa na mwanaume mwingine ( Alikuwa kijana tofauti na umri wa baba yake) so wakawa wanaishi na huyo baba yake mdogo au baba wa kambo ambae alikuja kuishi kwa mama yake... Siku moja mama akiwa safarini yule jamaa akambaka yule binti (alikuwa na age ya Miaka 15na alikuwa form one secondary) kwa bahati mbaya akabeba mimba na shuleni akafukuzwa.. Alipomwambia mama yake muhusika wa mimba mama akabisha na akaona iwe siri (asije akajaribu Kusema Mtu yyt akamdhalilisha mume wake) kutokana na umri mdogo yule dada hakuwa Na msaada.. Akalea mimba yake akazaa...
Aliponieleza ile siri nilimwonea sana Huruma na nikampenda zaidi tofauti na matarijio yake kuwa huenda ndo ingekuwa mwisho wa mapenzi...
Nilidumu na yule dada kwenye mahusiano kwa muda wa miaka minne ila kwa bahati mbaya tukaja kuachana kwa sbb tofauti kabisa... (niliamini Mungu hakunipangia)..

SO MPENZI Marytina KUENDELEA KUFICHA HIYO SIRI

1. Kutaendelea kukutesa nafsi na kujishuku hata kama hao wenzio wa kenya hawavujisha lakini hutakuwa na ujasiri wa kuishi kimaisha.
2. Kutokuwa na uhuru wa kufanya ibada hasa kwa sbb hao wanasali kanisa ulilokuwa unaabudu
3. Hutakuwa na uwezo Wa kuongoza kanisani kwa kudhani wenzio wanakuelewaje ilhali wanakujua mwanzo mwisho....
Imagine hao wakenya wakaja kuhamia kwenye hilo kanisa ulilokimbilia, UTAHAMA TENA?

FICHUA MAMBO UWE HURU.. Tena wahi kabla jamaa hajastuka.. Akijua kabla hujamwambia wewe KWANZA UMEKWISHA... Hatakuwa na IMANI TENA NA WEWE.. ATAKUACHA VIBAYA SANA.
First Born.....
 
Last edited by a moderator:
Dada kwa sababu zifuatazo inabidi umwambie ukweli bf wako.
...Ujio wa hao Wakenya.
...Wewe kuhama kanisa.
...Mshangao ulioonyeshwa na bf wako baada ya kuhama.


Vinginevyo usingekuwa na sababu kabisa ya kumweleza. Najua baadae bf wako anaweza kuja kuitumia kama fimbo ya kukuchapia, ila huna namna kwa sasa. Ni bora kupambana na yatokanayo kuliko kuachwa kwa kashfa na dharau.
 
sikuwahi kufanya kinyume na maumbile
pia kuna wadada wakenya wako hapa AR wanaweza kuvujisha hii siri ikawa msala zaidi sjui hata nianzie wapi..

mamito..............
wewe ndo unaoujua ukweli wa maisha yako yote, na pia ndo pekee unayeweza kufeel aina ya mahusiano uliyonayo.
ushauri wangu kwako huu............

kwasabb umeokoka basi mshirikishe sana Mungu kwanza ili Mungu akupe njia ya kutokea. kisha ukipata amani basi mweleze kwa ukimya tena iwe kama vile unampa historia ya maisha yako yote na pia umwambie msimamo awako kwasasa. Kisha chukua hatua kumfanya akuamin meaning michepuko, acha, kampani mbaya acha, tulia uwe mke, na mama wa watoto wa mumeo.

kuna machangudoa kibao wameolewa na wametulia na ndoa zinazidi kukua kukua. Uzuri ni kwamba ukisha jua tatizo lako na sasa umeamua kubadilika basi take it badilika wala usimwogope mtu eti atamwambia.

cha kufanya just be open na hata juu ya uwepo wa hao ulokuwa nao huko nairob ambao unawahofia mweleze ukweli
 
Changudoa home Arusha, baba Mngoni, mama Mchagga

Ilikuwa hivi baba na mjomba waliwekwa korokoroni kwa kesi ya ujambazi tukiishi na kusoma arusha mimi na wadogo zangu wawili kuna siku gafla kama saa nne mama akaja shuleni (day skuli) akatuchukua (wawili, mdogo alikuwa hasomi) bila kupitia nyumbani tukaelekea tanga tukakaa hotelini for two weeks then tukaelekea Kenya Nakuru ambapo mama alinunua nyumba na gari tukaanza maisha bila ya baba na mjomba.

Wote watatu tukapelekwa boarding skuli Nairobi-Kenya, mama akarejea nakuru miaka minne baadae mama akakamatwa akarejeshwa arusha kuunganishwa kwenye kesi, mimi ndiye nlikuwa mtoto wa kwanza na woote hatukuwa tumejua kama mama kakamatwa mpaka tuliporudi nyumbani likizo.

Majirani walitushangaa na kuanza kutuuliza alipo mama, kwa msaada tukavunja mlango gari ilikuwepo kuna chumba ilikuwa inafungiwa nliwaambia wadogo zangu mama kaenda kumsalimu mjomba atarejea. Nikaanza misele Nakuru mjini na kiboyfriend changu, siku mmoja akaja mama fulani nlipokuwa nimepaki kigari mjini akajitambulisha ni Mtanzania mmarangu na aliongea kichagga nikazuga simsikii.

Akaniambia amenitambua kwa kuwa anaifahamu gari ya mama na anajua mama na nimefanana na mama.Akanieleza kuhusu mjomba,baba na akaniambia mama alikuwa gerezani arusha kwa kesi. Akanitaka niiuze gari na nyumba fasta kabla havijakamatwa. Akaniambia nsiwe narudi rudi kukaa muda mrefu pale nyumbani mpaka atakapoachiwa mama nlikuwa form three-Nairobi, four days baadae niliuza gari, nyumba ikagoma kwa kuwa collateral ya mkopo alichukua mama benki. Nikawaamuru Madogo tuondoke tuwahi kurudi shuleni mama anatusubiri Nairobi.

With time hata mwaka haukuisha hela ikakata nikashawishiwa na a classmate Elizabeth-Mkenya mkamba wa Nairobi
tukaanza kujiuza likizo and life ikasonga na nikawa nawalipia wadogo na mimi ada. Nilijiuza mpaka nikasoma chuo na wadogo wakaingia sekondari thank god mama aliachiwa baada ya mitatu miaka kuna wakati tuligombana sana na wadogo zangu wakiamini mama amenipa access ya akaunti zake za benki na natumia hela nyingi kivyangu huku nikiwapa wao kidogo.

Tatizo: Kwa sasa tupo Arusha nina boyfriend mmasai na kila wakati wa semina kanisani mchungaji husema ni bora wapenzi wachumba muwekane wazi kuhusu maisha yenu hata ya nyuma ili isiwagharimu baadae. Naogopa sana kumwambia jamaa kuwa niliwahi kuwa nilikuwa changudoa.

NOTE:KUNA WADADA WAKENYA AMBAO NLIJIUZA NAO WAMEHAMIA ARUSHA NA HAWANA KAZI ZA MAANA, nlilazimika kuhama kanisa ambalo mimi nlikuwa kiongozi wa vijana baada ya baadhi yao kuanza kusali pale kanisani uamuzi ambao BF na mchungaji wanaushangaa mpaka leo.Kwa sasa nasali kikanisa kidogo njee ya mji kwa kuwaogopa washirika uchangudoa wenzangu wa NAIROBI...nateseka sana kuwaza

Ufafanuzi:Natumiwa PM nyingi zikitaka ufafanuzi, hii stori ni 5% ya maisha yangu na inaeleza namna nlivyoanza na kuacha uchangudoa tu.Stori haielezi maisha ya mama wala mjomba, namna walivyokamatwa na nini hasa walichokuwa wakifanya,namna mama alivyotoroka na baadae kukamatwa.HAIELEZI namna tulivyosafiri toka ARUSHA-TANGA-NAKURU KENYA

Pole sana kwa matatizo na machungu uliyowah kupitia kama ni kweli lakini,na sito kuwa mchoyo wa fadhira kama sito kupongeza kwa utamu uliofaidi asikwambie mtu dunia ulikuwa umeiweka mfukoni, hata hivyo mimi kam mdau wa biashara hiyo kwanza kabsa nashukuru kwa huduma mnayo tupatia maana hamhitaj maongez ni kuchana wallet tu mchezo kwisha dah nyie ni noma.Sasa kwa inshu yako usidiriki kumwambia mtu yyte chini ya jua hili siri yako itafika nyumban kwako na utaharibu kila kitu hata hivyo watu wote au marafiki zako wanajua kwamba ww ulikuwa showroom{kahaba} kaa na mbali kabsa,ENDELEA kumpa huduma ya kichangu changu mshkaj hd apagawe......siku ukikumbukia mawindo usisite ni PM nachukua fastjet faster siunajua jasir aachi asili..
 
Kwani unafkr uhusiano wako umebebwa na nguzo ya kuwa hukuwa changudoa?
enh bas hata kuwa ulikuwa changudoa haitakuwa sababu ya uchumba huo kuvunjika!
itakuwa haikuwa rizki tu,na wala ukisema usitegemee saaaaana kuwa eti ndo yu will gain his trust!
so ukiamua kusema sema
ukiamua kunyamaza pig kimya!
mapenzi ni.kitu complex sana unayoamini ndo sababu ya kupendwa inaweza isiwe hiyo na unayohofia itakuwa sababu ya kuacha isiwe hiyo!

by the way mekumithiiiiiiii!
thread zako huwa lazima zinyanyue watu masikio!
Marytina at her very best!
 
Last edited by a moderator:
Madame S.... This lady is not seriousat all!... We mtu gani unapewa ushauri lkn hizo reply zake duuh!.. Ooh nikiachika utanitaftia shemeji yako, frankly speaking lijistory lake la kutungaaa, i mean huu ni urongooooooo!!!!

Yaani umeona enh nilishtuka mapemaaaaaaaa kabisa Kama hayuko serious huyu MTU
 
Last edited by a moderator:
Yaani umeona enh nilishtuka mapemaaaaaaaa kabisa Kama hayuko serious huyu MTU

Mwenyewe nilimshtukia ana taka ushauri lakini ana mawazo yake tayari. Kila ushauri anabisha kwa kuweka visabu Mara ooh sijui nini.
 
kwahiyo sasa hivi dada Marytina umeshaacha kabisa uchangudoa, naskia jasiri haachi asili? na kadri mwanamke anavyofanya ngono mara nyingi ndoyo anahitaji zaidi, kwako wewe hilo likojee?

Kuna tofauti kati ya pepo la ngono na changudoa, mwanamke wa kumwogopa ni mwenye pepo la ngono, changudoa anatafuta jinsi ya kujikimu, kama mkeo ulimkuta mzima na ametulia kwenye ndoa katoe sadaka
 
Last edited by a moderator:
Ukisema ukweli tu umeula wa chuyaaa,maana hata yeye kuna aliyoyafanya lakim hatakuambiaa kila mtu siri yakee we baki na yako watanzania kwenye ukweli bado hatujajifunza

Hata mie hujaniambia ulikuwa CD nikakuoa. Ukweli ni kwamba mtu akishazoea mihogo ya jang'ombe tena ya saizi mbalimbali kuna siku tu ataimiss aina fulani ya muhogo na atataka akumbushie.

Hata wanaume (sio wote) waliowahi kugonga vyangudoa ni vigumu sana kuacha moja kwa moja hata kama wameoa.
 
sikiliza Wimbo wa Bahati Bukuku "DUNIA HAINA HURUMA" Nadhani kama ukiiskiliza kwa upana pengine utaweza kupata maamuzi ya hikma kumfahamisha mume wako.Bila kuweka ndoa wako dosari
 
Back
Top Bottom