Nimewahi kuwa changudoa, nimjulishe?

Nimewahi kuwa changudoa, nimjulishe?

MNANIUMIZA NYIE?? hivi mnataka niolewa na nyani????? nimeshawaambia uchangudoa nimeacha

Kama unaishi kwa msongo wa mawazo kwa hofu ya mpenzi uliye naye, basi ni vema ukaishi pekee yako ujipatie/uzae katoto kamoja kakukufariji. Sure
 
nkiweka wazi ntaachika tu hamna mwanaume anayekubali kuona x-changudoa
staki kuachuka kwa kuwa:

1.To be honest najihisi na najiona kama nimechoka sana kufikiri kwa ajili ya maisha yangu......ubongo kama unashrink
so naitaji mtu wa kufikiri kwa niaba yangu, mtu wa kuplan na kuweka au to monitor mikakati kwa niaba yangu as i am too tired.
Yaan nalitumia kanisa kama sehemu ya kujiburudisha na kujifariji kwa kuwa nakutana na watu wenye shuhuda mbalimbali.Wikiend naweza kwenda kanisani hata mara mbili yaan asubuhi kanisa hili then jioni kanisa lingine.

2.Nimekutana na wanaume wengi sana na kuna wakati nilifikiri siwezi kupenda ila huyu Mmasai ni right person kuwa na mimi na anafikiri, ana panga na kumonitor kwa niaba yangu.Si tajiri na sio kwamba sitongozwi na wanaume matajiri hapa ARUSHA na NAIROBI, nimependa sana na naamin nkiachika ntahangaika maisha yangu yote duniani.

3.Natakiwa niwe na mume anayejali sana kwa maana mimi ni rahisi sana kuanguka.(SI KURUDI KWENYE UCHANGUDOA BALI KUJIINGIZA KWENYE BIASHARA YEYOTE CHAFU)........kumbuka my uncle,dad and the entire circle nlliyokulia bado ipo na ipo tayari kunisaidia na wanataka niache kazi nifanye biashara.Huko kwenye biashara ndiko michezo yote michafu hiubuka.......kurushana, kudhulumiana, kuporana, kutumiana majambazi, kutekeana dili ni uchafu usioongeleka.So naitaji mwanaume wa kuwa nami kiimani na siyo wa kunikwaza nije kujikuta narudi nyuma

Hapana kubwa kabisa wewe ulifanya lini research na kugundua hakuna mwanaume anayeweza kuoa ex changudoa? Nakuomba sana tazama ukubwa wa Mungu na sio ukubwa wa tatizo ulilo nalo.

Kumbuka akija kugundua hilo hilo baadae hata kama mtakuwa mmeishafunga ndoa, akilalamika itatangazwa kwamba hiyo haikuwa ndoa maana alioa mke asiyemfahamu. Lakini hata asipolalamika ataumia sana na huenda ukazuka mgogoro mkbwa ambao utakuumiza zaidi kuachwa sasa unapoweza kupata mchumba mwingine mzuri zaidi ukimtanguliza Mungu.

Mimi nipo kwenye ndoa kwa miaka 12 sasa watoto 2, miaka 9 na 9. Migogoro ya kwenye ndoa inaanzishwa na vitu vidogo sana, sembuse hili? Bora uumie sasa lakini baadae hali itakuwa mbaya zaidi sana.
 
mh!....Kazi kweli kweli, usimwambie ulishafanya hiyo biashara,atawehuka,piga kimya tu.machangudoa wanavotumika hivo,akijua hakutakua na ndoa tena hapo!...
 
Ni heri tu umwambie,
Uangalie akiwa na hali ya utulivu useme ukweli; akiamua kukuacha ujue alikuwa hakupendi.
Vinginevyo ipo siku hao wenzio watakuumbua ukiwa umevaa shela.
 
Pole sana Marytina. Kwanza nikushukuru kwa kuwa na nia hiyo ya kutaka kumwambia boyfriend wako.

Ushauri wangu uko hivi, naomba ufuatane nami:

Mimi ni Mkatoliki, kanuni za kanisa zinasema ukienda kwa Padri au askofu ukatubu dhambi zako kwa kuzitamka moja baada ya nyingine, halafu padre akakupatia kitubio, ukafanya kitubio kwa sala kadhaa ambazo amekuagiza, ukarudi kwake kumwambia umefanya kitubio sasa Mungu akusamehe dhambi zako, basi kwa moyo mweupe kabisa ukiondoka pale....umesuuza moyo wako maana unajua Mungu amekusamehe kwakuwa umezisema dhambi zote, umeagizwa kusali baadhi ya sala na umetimiza na kisha kuomba msamaha! Kwa kupitia mchakato huo, roho yako, akili yako na generally saikolojia yako inakubali kuwa umesamehewa dhambi zako. Leo hii usingekuja kutueleza maana wewe huna dhambi tena.

Kwa kuwa dhehebu lako ni tofauti, mnaambiwa kuungama dhambi hadharani, na wewe unaona ni vigumu kwa sasa kusimama kanisani ukatamka wazi, na kwakuwa roho inakuuma kwa kuhama kanisa ulilolipenda sana, basi ni vema ukatibu mambo yote haya: kutubu dhambi, kusema ukweli, kurudi kanisani - kule ulikohama na kujenga mahusiano yako na mpenzi wako:
1. Ongea na Mpenzi wako kwamba kuna kitu unataka kuongea naye ukiwa na Mchungaji wa Kanisa Kuu (ulikohama).
2. Mweleze mpnz wako nia yako ya kuolewa naye, kama yupo tayari kufunga ndoa na wewe akueleze ni lini.
3. Kama mpnz wako yupo tayari kwa hizo hatua 1 na 2
4. Ongea na Mchungaji huyo kwamba una neno unahitaji kumwambia ukiwa na mchumba wako.
5. Panga siku ya kwenda wewe na mpnz wako kwa Mchungaji
6. Siku hiyo kuwa jasiri kusimulia kama ulivyosimulia humu ndani.
7. Hdithi yako ihitimishwe na kusema: Mpnz wangu, baada ya kuokoka, nimeona ni vema kuwa muwazi kwako na kwa mchungaji ili niwe huru, nirudi kanisani hapa na toka leo siwezi kusema uongo kwako. Mkumbatie mpnz wako, lia kidogo (najua utalia tu)
8. Ratiba itakayofuata anaifahamu Mchungaji.

N.B: Hakikisha Mchungaji ni mtu wa makamo, siyo kijana na awe ni mtu ambaye anaheshimika. Ushauri atakaoutoa Mchungaji utakuwa wa mwisho. Mpnz wako hawezi kukuacha kamwe! Ndoa itadumu, utafunguliwa kutoka minyororo ya shetani. Unajua unaweza ukawa unasali lakini dhambi ya uzinzi bado inakusumbua, ndiyo maana humo ndani nimeona unapitiwa na kusema,...."nikiharibikiwa utanitafutia mume?'" sijapenda sana hapo, maana wewe unapenda yeyote?? Lakini kwakuwa nafahamu maisha uliyopitia na maisha unayoyataka nimegundua tatizo lako. Ndiyo maana ushauri wangu nataka utue mzigo huo kwa mchungaji.

9. Weka ratiba ya kufanyia kazi ushauri ulipewa na wadau humu ndani!

Hao madada wa Kenya, hawatakudhuru kwa lolote ukifanya haya mambo. Kwanza, utakuwa wewe siyo mdhambi tena. Siyo mwongo tena. Humwogopi Mpnz wako tena. Mpnz wako ameshapewa ushauri wa kutosha na mchungaji na hawezi kukiuka, imani ya dini ni silaha tosha. Utakuwa unawachukulia kama watu wa dunia, usijichanganye nao! Wakikufuata waeleze wewe siyo wa Nairobi, you are a new born again and God fearing Lady!

May the Almighty God Bless You!
 
Unaongea kama mtu ambaye amekuja akiwa tayari anajua every possible course of action and its consequences....

Unahitaji ushauri gani? Tukupeti peti tukwambie "Its gonna be okay?"

hah
kweli mumenichoka
 
Kama unaishi kwa msongo wa mawazo kwa hofu ya mpenzi uliye naye, basi ni vema ukaishi pekee yako ujipatie/uzae katoto kamoja kakukufariji. Sure
kila wakati mama huniambia hivi hivi
tatizo ni kwamba staki kuwa kiongozi wa familia, staki tena kufikiri juu ya maisha yamgu, staki tena kupanga na to monitor naitaji mtu wa kunifanyia haya ambaye ni mume sahihi
 
Ni heri tu umwambie,
Uangalie akiwa na hali ya utulivu useme ukweli; akiamua kukuacha ujue alikuwa hakupendi.
Vinginevyo ipo siku hao wenzio watakuumbua ukiwa umevaa shela.
pana ugumu sana
hivi kaka yako akitaka kuoa x-changudoa hutamshangaa???
bora sjui anipe mimba nijilele kitoto kivyangu na maisha yangu
 
Pole sana Marytina. Kwanza nikushukuru kwa kuwa na nia hiyo ya kutaka kumwambia boyfriend wako.

Ushauri wangu uko hivi, naomba ufuatane nami:

Mimi ni Mkatoliki, kanuni za kanisa zinasema ukienda kwa Padri au askofu ukatubu dhambi zako kwa kuzitamka moja baada ya nyingine, halafu padre akakupatia kitubio, ukafanya kitubio kwa sala kadhaa ambazo amekuagiza, ukarudi kwake kumwambia umefanya kitubio sasa Mungu akusamehe dhambi zako, basi kwa moyo mweupe kabisa ukiondoka pale....umesuuza moyo wako maana unajua Mungu amekusamehe kwakuwa umezisema dhambi zote, umeagizwa kusali baadhi ya sala na umetimiza na kisha kuomba msamaha! Kwa kupitia mchakato huo, roho yako, akili yako na generally saikolojia yako inakubali kuwa umesamehewa dhambi zako. Leo hii usingekuja kutueleza maana wewe huna dhambi tena.

Kwa kuwa dhehebu lako ni tofauti, mnaambiwa kuungama dhambi hadharani, na wewe unaona ni vigumu kwa sasa kusimama kanisani ukatamka wazi, na kwakuwa roho inakuuma kwa kuhama kanisa ulilolipenda sana, basi ni vema ukatibu mambo yote haya: kutubu dhambi, kusema ukweli, kurudi kanisani - kule ulikohama na kujenga mahusiano yako na mpenzi wako:
1. Ongea na Mpenzi wako kwamba kuna kitu unataka kuongea naye ukiwa na Mchungaji wa Kanisa Kuu (ulikohama).
2. Mweleze mpnz wako nia yako ya kuolewa naye, kama yupo tayari kufunga ndoa na wewe akueleze ni lini.
3. Kama mpnz wako yupo tayari kwa hizo hatua 1 na 2
4. Ongea na Mchungaji huyo kwamba una neno unahitaji kumwambia ukiwa na mchumba wako.
5. Panga siku ya kwenda wewe na mpnz wako kwa Mchungaji
6. Siku hiyo kuwa jasiri kusimulia kama ulivyosimulia humu ndani.
7. Hdithi yako ihitimishwe na kusema: Mpnz wangu, baada ya kuokoka, nimeona ni vema kuwa muwazi kwako na kwa mchungaji ili niwe huru, nirudi kanisani hapa na toka leo siwezi kusema uongo kwako. Mkumbatie mpnz wako, lia kidogo (najua utalia tu)
8. Ratiba itakayofuata anaifahamu Mchungaji.

N.B: Hakikisha Mchungaji ni mtu wa makamo, siyo kijana na awe ni mtu ambaye anaheshimika. Ushauri atakaoutoa Mchungaji utakuwa wa mwisho. Mpnz wako hawezi kukuacha kamwe! Ndoa itadumu, utafunguliwa kutoka minyororo ya shetani. Unajua unaweza ukawa unasali lakini dhambi ya uzinzi bado inakusumbua, ndiyo maana humo ndani nimeona unapitiwa na kusema,...."nikiharibikiwa utanitafutia mume?'" sijapenda sana hapo, maana wewe unapenda yeyote?? Lakini kwakuwa nafahamu maisha uliyopitia na maisha unayoyataka nimegundua tatizo lako. Ndiyo maana ushauri wangu nataka utue mzigo huo kwa mchungaji.

9. Weka ratiba ya kufanyia kazi ushauri ulipewa na wadau humu ndani!

Hao madada wa Kenya, hawatakudhuru kwa lolote ukifanya haya mambo. Kwanza, utakuwa wewe siyo mdhambi tena. Siyo mwongo tena. Humwogopi Mpnz wako tena. Mpnz wako ameshapewa ushauri wa kutosha na mchungaji na hawezi kukiuka, imani ya dini ni silaha tosha. Utakuwa unawachukulia kama watu wa dunia, usijichanganye nao! Wakikufuata waeleze wewe siyo wa Nairobi, you are a new born again and God fearing Lady!

May the Almighty God Bless You!
asante sana
nitakupa updates next wiki........pls remind me hata kwa PM ikiwa ntakuwa kimya
 
Hapo kuna possibility mbili aidha jamaa awe muelewa au amdharau.Kumbuka hakufanya hivyo kwa kupenda kwasababu wapo wanaobadili wanaume kila kukicha kimaslahi tu hao nao wana tofauti gani na malaya/machangudoa au kwasababu wao hawasimami barabarani??walau yeye alifanya kwa dhiki.Tofauti ni kubwa sana kati ya anayefanya kitu kwasababu hana choice au anayefanya kitu kwa kupenda kwake.Aombe sana mungu huyo bwana awe muelewa but hio ni risk anayotakiwa aichukue.Unafikiri jamaa akiyajua hayo angali wapo ndoani na mfano washazaa itakuwaje?kutafuta kuumiza nyoyo zisizokuwa na makosa kwasababu na watoto watahusika.Amwambie sasa angali hawajaingia ndoani ili jamaa aamue kunyoa au kusuka.Heshima kama ipo ipo tu....Hakuna kitu kama perfect person kila mtu ana madudu yake...let the past stay in the past we live in the present and thats all that matters



On her own risk......Anyway I don't care who'll fall as long as I have play my part.
 
pana ugumu sana
hivi kaka yako akitaka kuoa x-changudoa hutamshangaa???
bora sjui anipe mimba nijilele kitoto kivyangu na maisha yangu

Kwa comment hii nina wasiwasi na wokovu wako! Hata kama utasema umeokoka bado hujakutana na Yesu maana unamwona huyo mchumba wako ndo kila kitu na ikimkosa huwezi kuishi, kweli??? Nimekushauri hapo juu angalia ukubwa wa Mungu na sio ukubwa wa tatizo. Pia Soma Yeremia 17:5, uielewe ili kuepuka laana.

Mbali na hayo uko tayari kuzini ili upate mtoto lakini kusema ukweli ukuweke huru hutaki.

Jihadhari na wanaokushauri ukae kimya wanakutakia matatizo makubwa zaidi huko mbele.
 
Kwa comment hii nina wasiwasi na wokovu wako! Hata kama utasema umeokoka bado hujakutana na Yesu maana unamwona huyo mchumba wako ndo kila kitu na ikimkosa huwezi kuishi, kweli??? Nimekushauri hapo juu angalia ukubwa wa Mungu na sio ukubwa wa tatizo. Pia Soma Yeremia 17:5, uielewe ili kuepuka laana.

Mbali na hayo uko tayari kuzini ili upate mtoto lakini kusema ukweli ukuweke huru hutaki.

Jihadhari na wanaokushauri ukae kimya wanakutakia matatizo makubwa zaidi huko mbele.
i am really sorry
ila wakaka hapa JF wamenipa stress zaidi
.........may be nkiwa na mtoto anaweza kunipa faraja kwa maana nimehangaika sana
 
nakuelewa..........nina makovu sana kwenye ubongo wangu ndio maana naogopa to add up a new scandal

Is telling your past a scandal, really not it is inner healing and freeing yourself instead.
 
Mie useme mwanangu akiamua kuoa changu doa,
wala sitaingilia mapenzi yao;

Usiogope hayo yote ni maisha tu,
watu wasichana waliotumika kuliko hata wewe hapo ila ni siri yao.

Kama anakupenda hatakuacha.

pana ugumu sana
hivi kaka yako akitaka kuoa x-changudoa hutamshangaa???
bora sjui anipe mimba nijilele kitoto kivyangu na maisha yangu
 
i am really sorry
ila wakaka hapa JF wamenipa stress zaidi
.........may be nkiwa na mtoto anaweza kunipa faraja kwa maana nimehangaika sana

Wakaka wepi wamekupa stress? Sikiliza ushauri unaokutaka usolve tatizo hili once and for all na sio kuliahirisha. Pia usidhani kila mwanaume anaelewa maisha wengine kula kulala hata hawajui chochote kuhusu maisha staha achilia mbali ndoa.

Nani kakudanganya kwamba mtoto analeta faraja? Je ukimpata kilema au zezeta utafarijika kweli? Wewe kiri ulikosea kutomwambia mapema lakini mwambie ili uwe huru.
 
Back
Top Bottom