Nimewahi kuwa changudoa, nimjulishe?

Nimewahi kuwa changudoa, nimjulishe?

baada ya matatizo yote ya utotoni kwa sasa nimekuwa mpole sana
nilikuwa kiongozi wa vijana kanisani ila nlilazimika kuhama baada ya MKENYA MDADA flani kuanza kuhudhuria huduma ya hapa kanisani.
BF alinishangaa kwani nahama kanisa ninaloheshimika kwa namna nlivyowaongoza vijana na mchungaji aliingilia akinitaka nisihame....mwishowe nikahama kilazima mkaanza kusali kikanisa kidogo njee ya mji....nayaona maisha yangu yoote yamejaa uongo nateseka sana
dada, Mungu akusaidie. ninaomba usipate shida hivyo, maisha yako yapo mikononi mwa Mungu si mikononi mwa mwanadamu. mwanaume bora ataletwa na Mungu sio wanadamu. wewe mwangalie Mungu, haukuwa hata na umuhimu wa kuhama kanisa, ulitakiwa kubaki tu Mungu atakusaidia, kama kuna mtu atavujisha mwache avujishe, hata katika kuvujisha huko Mungu atakusaidia tu. hayo ni maisha ya zamani. sisi sote tulikuwa malaya sana, nimelala na wanawake wengi sana na nina watoto nje ya ndoa wengi, lakini ilifika kipindi nikaamua kumrudia Mungu, nimebadilika, nikikutana na mtu aliyekuwa malaya zamani, simhukumu kwa mambo yake ya zamani.

ya kale yamepita, tazama yamekuwa mapya. unachotakiwa kufanya, rudi palepale kanisani, wewe fanya mambo mema ili matendo yako yakutetee, hata mtu akisema ulikuwa changu kwa kuona matendo yako atasema ohhh lakini amebadilika kabisa sio kama yule wa zamani. wanawake wengi wanaoolewa walishawahi kufanywa na wanaume wengi sana, tunaoa basi tu. sisi wanaume pia tumelala na machangu wengi tu. mimi binafsi nimelala na machangu rundo, nimelala na wahudumu wa hoteli rundo, nimelala na wahudumu wa migahawa rundo....machangu wa kuwalipa kabisa rundo hadi wengine nikikutana nao siwakumbuki sura, na hata kama kanisani kwangu mtu atasema nililala na mimi, nitasema ohhh really, kumbe nilishawahi kulala na wewe, lakini nitamwambie siku hizi nimeokoka siko vile tena moyo wangu umebadilika, matendo yangu yamebadilika sasaivi nina Yesu na kwakuangalia matendo yangu yeye mwenyewe hata mdomo hatafungua na hata akifungua hatakuwa na madhara yeyote kwangu. watu wote sisi tulikuwa waovu tu zamani bila neema ya Mungu tungeshakufa zamani. wewe hauko tofauti na wanadamu wengine waliokosea sana, cha muhimu tu unatakiwa kujitahidi umwombe Mungu aondoe tamaa ya uzinzi, kama tamaa ikiondoka basi, wewe ni msafi na usiwe na wasiwasi. unasikia?
 
sina namba zao na hawajui nafanya nini maana kanisani hatukuongea zaidi ya salamu ...na nilihama hili kanisa tokea siku hiyo

Then you don't have to worry, we kila siku mlilie Muumba wako, ombea ndoa yenu tarajiwa, Bwana ni mwema siku zote!!!
 
Dah!!!!!! usijaribu aisee kumwambia, yaliyopita yamepita, uhuru gani wa moyo unaotafuta bhana??????? hata akija jua kwani wana picha zako hao watoa habari???? watu wanakana hadi kaburini wakati wamekutwa ana kwa ana ije kuwa stori yakuambiwa, Kaa na lako moyoni, ndio maana wahenga wanasema "wanawake matusi mengine toka kwa waume zao wanajitakia wenyewe"



Hawa wanaume sio kabisa, ukikosa jambo huweza kukutukania hadi kuku wa nyumbani kwenu, sembuse umwambie hilo si itakuwa kama alarm ukikosa.
 
tena unaweza kukuta hawa ndio wale wadogo zangu nliowalipia ada na walikuwa wakigombana na mimi wakidhania nina akaunti ambayo mama kaniachia pesa nyingi ambazo nawabania

Exactly!!
 
kumbe ni love story nilidhani ni kweli.

80% ni true nimeficha kidogo sana kwa kuwa staki kumwingiza mama matatizoni
mama yangu ni mfanyabiashara mtata na hamna anachoogopa na kafanya mengi so....namweshimu na nitamlinda kwani amerudisha uchumi wa nyumbani juu haraka
 
siwezi kujua idadi ila ilikuwa haisumbui kupata hela kiasi nachotaka ndani ya siku chache kwa kuwa tulikuwa tumejichagua wadada wazuri na hatukukaa hoteli mmoja zaidi ya wiki so kila eneo tulionekana wapya tulipanga bei tutakayo

pls hii stori ilitakiwa ikuhuzunishe na sio kukuvutia.....nateseka sana kila nikiwaza future itakuwaje hii siri ikivuja

Ikivuja kwa nani? Kwa Mungu au hao wadada?
 
Well, ulianza vzr kama vile mtu aliyejutia ile kazi, yale maisha na consequence zake, na nikachukulia sasa umeamua kurudi kwa Mungu ki ukweli hivyo Yesu Kristo achukue adhabu yako(mshahara wa dhambi=mauti),misiba yako,aibu yako na kukubali kununuliwa kutoka jela ya shetani(kwako uchangu) kwa kulipiwa kwa Damu ya Thamani ya Yesu Kristo Mkombozi wetu. Hapo nilikupenda na nilitaka kukuombea upate msaada wa kimungu huyo uliyemkimbilia! Sasa unasema,eti ukimwambia akikumwaga, huyo aliyekushauri akutafutie mdhambi mwingine, mmmh, bado hujapona! Ushauri, jiachilie kwa Mungu wako wholy, jinyenyekeze kwake,mtumikie na kumtegemea yeye tu mbona Mungu huyu nimtumikiaye Anaweza? Yesu anasema alikuja kwa wenye dhambi ili wapate kutubu. Ukitubu kisawasawa mpaka ukawekwa huru, utaona unakuwa na ujasiri wa kutamka ulikopitia, tena sio kwa huyo mchumba tu, (ambaye kuna kazi ya kufanya ili awe wako) bali utapata ujasiri wa kupanda madhabauni na kutoa hiyo stori kama 'ushuhuda'! Kuanzia hapo, hata hao machangu wa Kenya kama bado wapo kwenye hiyo fani watakuogopa, lkn kama wameacha au wanataka kuacha, basi watakuona wewe ni shujaa, nawe utakuwa kioo kwao. Huyo njemba kama ni wako atakupenda zaidi, akiishia ujue yupo aliye wako anakuja! Lkn haya yote inategemea na kanisa unalosali, je wanaelewa maana ya 'Deliverance of the Soul'! Kama hamna, huko kwenye wazo mbadala mie siko! Mkubali Yesu na Mtumikie Mungu wa Moyo wako wote. Barikiwa mama.
kaka nimepitia maisha ya kila namna na to be honest sina chafu nifanyalo kwasasa
wana JF wengine wananikera ndio maana najikuta najibu hasira........
KAKA nimemrudia YESU ndio maana nafanya kazi na si biashar trade na sio kujiuza ..nkiamua kuwa mfanyabiashara nina back up ya kutosha kufanya kila rafu na dhuluma na ndani ya miaka mitatu naweza kumiliki hata gorofa ila staki

UKITAKA KUFANIKIWA GAFLA KIBIASHARA LAZMA UWE MTU WA SHETANI dats why nafanya kazi
 
Changudoa home Arusha, baba Mngoni, mama Mchagga

Ilikuwa hivi baba na mjomba waliwekwa korokoroni kwa kesi ya ujambazi tukiishi na kusoma arusha mimi na wadogo zangu wawili kuna siku gafla kama saa nne mama akaja shuleni (day skuli) akatuchukua (wawili, mdogo alikuwa hasomi) bila kupitia nyumbani tukaelekea tanga tukakaa hotelini for two weeks then tukaelekea Kenya Nakuru ambapo mama alinunua nyumba na gari tukaanza maisha bila ya baba na mjomba.

Wote watatu tukapelekwa boarding skuli Nairobi-Kenya, mama akarejea nakuru miaka minne baadae mama akakamatwa akarejeshwa arusha kuunganishwa kwenye kesi, mimi ndiye nlikuwa mtoto wa kwanza na woote hatukuwa tumejua kama mama kakamatwa mpaka tuliporudi nyumbani likizo.

Majirani walitushangaa na kuanza kutuuliza alipo mama, kwa msaada tukavunja mlango gari ilikuwepo kuna chumba ilikuwa inafungiwa nliwaambia wadogo zangu mama kaenda kumsalimu mjomba atarejea. Nikaanza misele Nakuru mjini na kiboyfriend changu, siku mmoja akaja mama fulani nlipokuwa nimepaki kigari mjini akajitambulisha ni Mtanzania mmarangu na aliongea kichagga nikazuga simsikii.

Akaniambia amenitambua kwa kuwa anaifahamu gari ya mama na anajua mama na nimefanana na mama.Akanieleza kuhusu mjomba,baba na akaniambia mama alikuwa gerezani arusha kwa kesi. Akanitaka niiuze gari na nyumba fasta kabla havijakamatwa. Akaniambia nsiwe narudi rudi kukaa muda mrefu pale nyumbani mpaka atakapoachiwa mama nlikuwa form three-Nairobi, four days baadae niliuza gari, nyumba ikagoma kwa kuwa collateral ya mkopo alichukua mama benki. Nikawaamuru Madogo tuondoke tuwahi kurudi shuleni mama anatusubiri Nairobi.

With time hata mwaka haukuisha hela ikakata nikashawishiwa na a classmate Elizabeth-Mkenya mkamba wa Nairobi
tukaanza kujiuza likizo and life ikasonga na nikawa nawalipia wadogo na mimi ada. Nilijiuza mpaka nikasoma chuo na wadogo wakaingia sekondari thank god mama aliachiwa baada ya mitatu miaka kuna wakati tuligombana sana na wadogo zangu wakiamini mama amenipa access ya akaunti zake za benki na natumia hela nyingi kivyangu huku nikiwapa wao kidogo.

Tatizo: Kwa sasa tupo Arusha nina boyfriend mmasai na kila wakati wa semina kanisani mchungaji husema ni bora wapenzi wachumba muwekane wazi kuhusu maisha yenu hata ya nyuma ili isiwagharimu baadae. Naogopa sana kumwambia jamaa kuwa niliwahi kuwa nilikuwa changudoa.

NOTE:KUNA WADADA WAKENYA AMBAO NLIJIUZA NAO WAMEHAMIA ARUSHA NA HAWANA KAZI ZA MAANA, nlilazimika kuhama kanisa ambalo mimi nlikuwa kiongozi wa vijana baada ya baadhi yao kuanza kusali pale kanisani uamuzi ambao BF na mchungaji wanaushangaa mpaka leo.Kwa sasa nasali kikanisa kidogo njee ya mji kwa kuwaogopa washirika uchangudoa wenzangu wa NAIROBI...nateseka sana kuwaza

Kwanza kabisa nakupa pole kwa machungu yote uliyopitia na vilevile nitakuwa mchoyo wa fadhira kama sito kupongeza kwa raha na uhondo uliopata kipindi hicho. Pili nmekuwa mteja wenu kwa muda mrefu sana na nashukuru kwa huduma mnayotupa....aisee mnatisha. Tatu Nakushauri acha kabsa ukaribu na wote wanaofahamu kama wewe ulikuwa mama wa barabarani au showroom[KAHABA] kwani wanaweza toa siri yako kwa mwenza wako wa sasa wakakuharibia au wakakuchukulia mwenza wako na Siri hiyo usidhubutu kumwambia mwenza wako hata iweje kwani hato weza kuvumulia ila mimi naweza kuvumilia na nikadumisha pendo as normal......Endelea na maisha hayo mapya hakika umeshinda mengi majaribu maana nyie wauzaji nkikumbuka zama zenu unaweza ukaacha ghorofa,magar,mapesa na kila kitu ndani lkn ukataka kutimiza azma yako tu ya kwenda kuwinda[KUJIUZA] Vumilia mlilie Mungun wako na utubu sana.......Ila siku ukitaka kupiga tizi usini PM nmeshastaafu kuwanunua
 
Kama tyr umejisalimisha kwa Yesu,ni bora ukayatapika yote ili uwe huru,huwezi ukawa huru ikiwa kuna kitu kipo ndani yako kinakukereketa..hicho kitakutesa na kukusababishia uwe mfungwa na mtu una hana hama,katika huduma.
Nataka nikutie moyo,hakuna aliyekuwa mkamilifu sisi ni wanadamu tu,tunapitia Mengi na kwa sabb tofautitofauti,mpk pale unapopata tumaini jipya kwa kumpata Yesu Kristo.
Hivyo mwambie tuu,kama huyu ni mume wako,atakuwa wako tu.hata kama atayapokea kwa style gani yale utakayomwambia,
kama sii wako,basi Mungu atakupa wako,
Mwekani wazi tu,
Hata afya yako mweleze ukweli
Over.
 
tatizo nimekuwa mtu wa dini na sipendi kuendelea kuwa muongo kama mama alivyonidanganya
pia kuna waschana wawili wakenya wanaishi hapa ARUSHA na tulifahamiana KENYA kwenye hotel

Kama unaona sawa basi mwambie ila usije kulia hapa.
 
Changudoa home Arusha, baba Mngoni, mama Mchagga

Ilikuwa hivi baba na mjomba waliwekwa korokoroni kwa kesi ya ujambazi tukiishi na kusoma arusha mimi na wadogo zangu wawili kuna siku gafla kama saa nne mama akaja shuleni (day skuli) akatuchukua (wawili, mdogo alikuwa hasomi) bila kupitia nyumbani tukaelekea tanga tukakaa hotelini for two weeks then tukaelekea Kenya Nakuru ambapo mama alinunua nyumba na gari tukaanza maisha bila ya baba na mjomba.

Wote watatu tukapelekwa boarding skuli Nairobi-Kenya, mama akarejea nakuru miaka minne baadae mama akakamatwa akarejeshwa arusha kuunganishwa kwenye kesi, mimi ndiye nlikuwa mtoto wa kwanza na woote hatukuwa tumejua kama mama kakamatwa mpaka tuliporudi nyumbani likizo.

Majirani walitushangaa na kuanza kutuuliza alipo mama, kwa msaada tukavunja mlango gari ilikuwepo kuna chumba ilikuwa inafungiwa nliwaambia wadogo zangu mama kaenda kumsalimu mjomba atarejea. Nikaanza misele Nakuru mjini na kiboyfriend changu, siku mmoja akaja mama fulani nlipokuwa nimepaki kigari mjini akajitambulisha ni Mtanzania mmarangu na aliongea kichagga nikazuga simsikii.

Akaniambia amenitambua kwa kuwa anaifahamu gari ya mama na anajua mama na nimefanana na mama.Akanieleza kuhusu mjomba,baba na akaniambia mama alikuwa gerezani arusha kwa kesi. Akanitaka niiuze gari na nyumba fasta kabla havijakamatwa. Akaniambia nsiwe narudi rudi kukaa muda mrefu pale nyumbani mpaka atakapoachiwa mama nlikuwa form three-Nairobi, four days baadae niliuza gari, nyumba ikagoma kwa kuwa collateral ya mkopo alichukua mama benki. Nikawaamuru Madogo tuondoke tuwahi kurudi shuleni mama anatusubiri Nairobi.

With time hata mwaka haukuisha hela ikakata nikashawishiwa na a classmate Elizabeth-Mkenya mkamba wa Nairobi
tukaanza kujiuza likizo and life ikasonga na nikawa nawalipia wadogo na mimi ada. Nilijiuza mpaka nikasoma chuo na wadogo wakaingia sekondari thank god mama aliachiwa baada ya mitatu miaka kuna wakati tuligombana sana na wadogo zangu wakiamini mama amenipa access ya akaunti zake za benki na natumia hela nyingi kivyangu huku nikiwapa wao kidogo.

Tatizo: Kwa sasa tupo Arusha nina boyfriend mmasai na kila wakati wa semina kanisani mchungaji husema ni bora wapenzi wachumba muwekane wazi kuhusu maisha yenu hata ya nyuma ili isiwagharimu baadae. Naogopa sana kumwambia jamaa kuwa niliwahi kuwa nilikuwa changudoa.

NOTE:KUNA WADADA WAKENYA AMBAO NLIJIUZA NAO WAMEHAMIA ARUSHA NA HAWANA KAZI ZA MAANA, nlilazimika kuhama kanisa ambalo mimi nlikuwa kiongozi wa vijana baada ya baadhi yao kuanza kusali pale kanisani uamuzi ambao BF na mchungaji wanaushangaa mpaka leo.Kwa sasa nasali kikanisa kidogo njee ya mji kwa kuwaogopa washirika uchangudoa wenzangu wa NAIROBI...nateseka sana kuwaza
Pole sana kwa machungu uliyopitia na hongera kwa kufaida fursa hiyo adimu....Nakushauri usije ukathubutu ukamwambia hayo uliyo wahi kuyapitia na kaa mbali na acha ukaribu na wote wanaojua kama wewe ulikuwa mama wa road[kahaba]
 
....... kuna tofauti ya ndugu zako kujua ulikopitia na mume mtarajiwa. Ndugu hawawezi kukupiga chini na undugu haufi mtaendelea kuwa ndugu hata kama wataumia, lakini kwenye penzi linaloelekea kufunga pingu za maisha hali ni tofauti. Wanaume wachache sana wanaweza kukubali kuendelea na mipango ya ndoa wakijua mke mtarajiwa aliwahi kuuza mwili wake. Akili mkichwa Mkuu.
dah!ntamfaa nani dunia hii mie????
 
Hayo yalishapita mdada, unapoamua kuishi maisha chanya yae yote ya nyuma huwa tunayasahau na kuangalia ya mbele unless kama ungekuwa bado upo kwenye fani kidogo hata mie ningepata cha kukushauri,kila mtu ana mambo mabaya ambayo alishayafanya nyuma tofauti tu la kwako linaonekana kubwa kwa kuwa linaonekana lipo against na watu wengi na ndio maana unaona kama dhamira inakusuta lakini mbele za mungu aliekuwa changudoa, mzinzi kama ilivyo mie naweza nikawa na mke na bado natoka na wanawake wengine wote tunahesabika ni wale wale tofauti wewe ulikuwa unauza na mie nilikuwa natongoza alafu wananikubali kwa hiari yao wenyewe lakini mwisho wa siku wote tunaangukia kundi moja. Sasa iweje wewe ujione mkosaji sasa kiasi kwamba kutaka kumwambia mwanadamu mwenzako mambo ya nyuma ambayo umeachana nayo tayari

Kama ingekuwa ameambiwa na watu alafu anakuuliza wewe unasita kumwambia hapo hata mie ningekushauri umwambie lakini kwa sasa amekufuata wewe kwa kujua tabia zako njema baada ya kumrudia Mungu hivyo basi yale ya nyuma yote sahau na yatumie kama funzo katika maisha yako mapya ili yasiweze kujirudia tena si kwako wala kwa familia yako au hata sie wengine tunaokuzunguuka

Kila watu wanapotaka kuoana wangekuwa wanaambiana makosa yao ya nyuma au historia zao za nyuma, watu wanaohusika na mambo ya stationery wangebuni na kadi za kuhairisha harusi na kusogeza mbele kwa jinsi wengi wanekuwa wanaji-withdraw, hapa tu mtu amekukubali na mlikutana kila mtu alikuwa na mahusiano nyuma ukizungumzia issue kidogo tu ya mpenzi wako wa nyuma ananuna je hili la kwako

kweli kila mtu ana makosa ila yanaongeleka hili la kwangu sidhani kama kuna mwanaume atavumilia siku ukweli ukijulikana hata kama tumeshaoana...ntakuwa kimya ila wale wakenya wakijua naolewa najua patachimbika...nawajua machangudoa jaman hawapendi kabisa mwenzao aolewe
 
Nini maana ya changudoa? Kufanya na watu usiowajua in return for money? Na wanaotembea na wanaume 20 kidogo in the name of boyfriend na wanapewa "hela za matumizi" are they any better? Hawa huwa wana confess kwa wachumba wao? To me kuna different levels za "uchangudoa" from kujiuza barabarani to kubadilisha partners kila kukicha na kuhongwa pesa. Sioni kama wewe ndo mkosefu kuliko wote, kila mmoja ana lake. Wangapi wamekuwa na one night stands kibao, na wanadunda tu na leo wanaweza kuku judge wewe. Songa mbele u seem to regret thats good coz ni step ya kuomba forgiveness. Truly repent and forgive urself. Hakuna atakayekuja kukwambia umesamehewa, wewe omba msamaha to ur God and be a better person everyday. Nafsi yenye kujutia dhambi ni bora zaidi na ita heal
 
muambie tu ukweli huyo mchumba wako kama ni kweli umeamua kuokoka na huyo ndyo mwanaume ambaye mungu kakupangia nadhan atakuelewa na mtaishi kwa aman katika ndoa yenu mkiongozwa na neno la mungu.
 
Back
Top Bottom